Hivi watu wanaanzaje kuifananisha Prison Break na Money Heist?

Hivi watu wanaanzaje kuifananisha Prison Break na Money Heist?

Kakaa umenikumbusha huyo mwamba.. Sasa huyo awekwe kwenye upelelezi wa kumtafuta huyo Professor badala ya kile kidemu chenye ujauzito, si dakika 2 tu..

Michael mwenyewe kichwa kilikua kinamuuma kwa huyu jamaa.


Sent using Jamii Forums mobile app
Mahone "aliniboa" season 2 alipomminia risasi yule dogo tozi mwizi mwenye kofia iandikwa "S" yaani stealer. Kumbuka ya Michael iliandikwa C yaani clever.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Money heist Ni takataka tupu hata robo tu ya prison break haifikii kwanza inatabilika haina matukio mengi ya kusisimua Kama PB kingine zaidi wanalazamisha story iwe ndefu wakati ubunifu umeisha.Moja ya kitu nilichokipenda kwenye prison break Ni kwamba unakuta watu wenye uadui mkubwa na pia hamuaminiani inafika kipindi mnajikuta mazingira yanawazalimisha mshirikiane hata Kama mna uhasama mkubwa mfano mzuri Ni professor Mahone kuangana na kina Michael scottfield ingawa aliwaulia baba yao mzazi, mfano mwingine Ni T-bag jamaa Ni snitch Sana lakini ilibidi Michael scottfield ashirikiane ili kupata cylla hiyo Ni sehemu tu ndogo ya ubunifu uliotumika kwenye PB atujazungumzia mambo mengine kiufupi money heist itasubiri Sana kufika ubora wa PB.
Money Heist naifananisha na blindspot. Ubunifu hafifu ila ujanja ujanja mwingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
old is gold

mimi siwezi kuingia kwenye mkumbo wa kushabikia kisa nionekane najua,nimeangalia series zote mbili na season zake zote.

kila series ina mapungufu yake na kila moja ina ubora wake sema tu PB ilitoka kipindi hakujawahi kuwa na series kama ya aina ile,na MH ipo kwenye kipindi watu washaona kitu cha aina hii wanaigiza.

tunaipenda PB sababu ya memories,ipo kichwani..sababu tunakumbuka na binadamu tuna tabia ya kusifia vya zamani.

ingawa kwa upande wangu pia PB ni favourite kuliko MH....

characters hawawezi fanana,mfano mtu hapo juu anafananisha Rio na Tbeg...Rio kwenye MH kacheza kama dogo tu mtaalamu wa IT so issue za ubabe usitegemee,alichofunzwa ni kutumia tu bunduki na vitu vingine ila kazi yake kubwa mule ndani ni issue za mitambo.

halafu kumbuka pia Michael aliwachagua watu wake kuzingatia mahitaji yake,sawa..pia wale walikua kwenye gereza la watu wahalifu wakubwa so issue za wao kuwa hard lazima sababu ni wahalifu sugu,akina Rio wameokotwa tu mtaani sababu ni watu hawana cha kupoteza ndio maama hata akiua mende anaanza kulia.

lengo la proffesa ni kuteka na kubuy time waprint mzigo kwa kufanya negotiation...

mazingira mengine yameshaandaliwa miaka kadhaa nyuma huko

Sent using Jamii Forums mobile app
Very good analysis.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengi wadandiaji tu hawajui kitu wanafata mkumbo kusifia ujinga.

Mfano kama The Wire nauhakika ni asilimia chache sana ya watu wameiona hii show. Bonge moja la show.

Money Heist haifikii hata Breaking Bad
True. Show nzuri ni zile zenye kubeba uhalisia na siyo kujaza fictions kama single movie. Mfano Breaking bad na The wire. Mambo yanaenda kinyume kabisa na tulivyozoea. Uhalifu unashindaga mamlaka mara nyingi tu lakini wametumia situations za ukweli kabisa siyo zile ideal. Kwenye the wire kuna hadi characters ambao walikuwa na zile characters in real life kama mayor na wengineo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moto wa PB haugusiki wazee... Matukio ya michael scofield yalikuwa well arranged na ye ndo organizer mkuu...
Mf;
~kwenye s1, katika hali ya kawaida ilikuwa ni ngumu kuamini kuwa jamaa angemtumia pope kiasi cha kuruhusu bro ake aachiwe

~s2 licha ya kutokufanya ubaya wa kusema ni mwenye hatia lakini alienda kutubu dhambi zake baada ya kuiba ile compas

~s3 pale sona wakati wanatoroka, wakina Bellick, T-Bag na yule kiongozi wao wakang'ang'ania kuwa wa kwanza kutoka, naye akawaruhusu... kumbe wao walikuwa chambo bana, hahaha! nilipapenda sana hapa "and this is a plan" wakati mwanzo aliwaambia umeme utakata sekunde 30 na ndo inabid watumie hizo kusepa... alijua wenye kiherehere watapatikana tu

~s4 kwny kuiba cylla, card ya general alijua lazima itajileta tu, na general akabaki anamshangaa kapata wapi kadi nyingine 5?

~s5 poseidon hakuamin mchezo aliofanyiwa na scofield, kachora macho mikononi km passcode, kamfanyia flaming ya tukio alilofanyiwaga na mwisho kapropose awekwe chumba kimoja na t-bag kule gerezan
Noma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila kwenye PB kuna character tatu zilikatizwa kibabe ila zilikuwa very emotional.

1. Yule dogo tozi mwizi. Aliuawa season 2 na Mahone.

2. Lincoln Jr a.k.a LJ Jr. Mtoto wa Lincoln.

3. Demu wa Benjamin Miles "C Note". Akikuwa "mkali" balaa ila alifanyiwa ukauzu kweli na askari wa Mahone.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila kwenye PB kuna character tatu zilikatizwa kibabe ila zilikuwa very emotional.

1. Yule dogo tozi mwizi. Aliuawa season 2 na Mahone.

2. Lincoln Jr a.k.a LJ Jr. Mtoto wa Lincoln.

3. Demu wa Benjamin Miles "C Note". Akikuwa "mkali" balaa ila alifanyiwa ukauzu kweli na askari wa Mahone.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umemsahau na yule mbabe wa T-bag ambaye alichomwa kisu na T-bag baadae akauzwa na T-bag akaenda kupigwa risasi na polisi.
 
Huyo jamaa ni mmoja ya character ninao wakubali mule,kumbuka ndo alienda kuua mke wa lincoln. Akaanza kumsaka na mtoto ili amuue.

Mwishoni akaja kuwa mtu mwema kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
..Kellerman. Jamaa alikuwa kauzu sana mwanzoni, kuua yeye haoni shida.

Baadae alivyokuja kubadilika, dah! Nikamkubali, japokuwa Sara muda wote alikuwa hamuamini mpaka anakufa.
ustv-prison-break-kellerman.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom