Hivi wenye magari wote tukaamua Mei 4 tupaki magari, itakuwaje?

Ukiona mafuta ni bei paki huo mkweche wako tembea pekeako kwa miguu. Guys bei ya mafuta ni affordable. Ukiona ni gharama basi ujue umeshindwa kujikwamua kutoka ktk umasikini.
Unakimbia kununua petrol kwa 3,100 unakimbilia kupanda public transport kwa siku unatumia zaidi ya 3,000 unapoteza na muda, hizo ni akili au matope
 
Gharama ya kupoteza muda wengi huwa hawaifikirii
 
Mwigulu Nchemba, Ndugai na wabunge wenzao wanamiliki vituo vya mafuta. Huu ndo muda wao wa kupata pesa !
Kwa Akili yangu ilipoishia, naona ni vile vile tu sababu wenye Vituo wakipandisha basi na wanaponunua wamepandishiwa..... ilikua Lita moja ananunua 1500 yeye akauza 1600 basi nafikiri akiwa anauza 1700 basi jua ananunua 1600 shilingi 100 yake ipo pale pale, kwa navyofikiria lakini
 
Nimepaki gari leo, na itakuwa hivyo hadi kieleweke
 
Unatumia lita1 au sio?
 
Kenya waliwahi kutumia hii mbinu na walifanikiwa. Kitu kikipanda bila sababu za msingi hawanunui.
Hii mbinu inasaidia sana

Tatizo wabingo hatuna tofauti na watumiaji wa madawa ya kulevya

Tunaishia kulalamika bila kuchukua hatua

Ova
 
Eti kisa dada kaenda marekani kakuta bei ya mafuta ipo juu zaidi ya huku nae kaamua kuongeza tena
 
Eti kisa dada kaenda marekani kakuta bei ya mafuta ipo juu zaidi ya huku nae kaamua kuongeza tena
Daah, ndicho alichojifunza hicho, hajui pato la raia wa huko ni mara 40 ya raia wa huku?
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…