#COVID19 Hizi dawa za COVID-19 ni siasa au tuna malengo gani? SUA hiki kitu gani?

#COVID19 Hizi dawa za COVID-19 ni siasa au tuna malengo gani? SUA hiki kitu gani?

Ombi langu ni moja tu! Hawa wanaouza madawa kama haya wajiheshimu. Wanatumia umaarufu wa vyuo vikuu kutapeli wananchi na kuonesha ujinga wao. Na wanasiasa kwa kutaka huruma ya wananchi kwamba kuna jambo la maana linafanyika, wanaunga mkono utapeli huu. Hii ni kulisha watu uchafu.

Na inavyoonekana, tumekuwa wazoefu tangu mzee wa Loliondo.
Hivi wewe na mkemia nani anayejua sayansi??hizo dawa za vyuo zote zimepita kwake ..unataka sayansi gani??unajua procedure za kupima japo dawa moja tu inavyofanyika au kasuku tu...kubali watu walijitoa kwa ajili ya kusaidia jamii na watu wamenufaika na hizo products punguza wivu wa baleh
 
Huo unaoita utapeli ndio umesaidia kuponya wengi kwa ushahidi kabisa...
Unaweza kuthibitisha kuwa kuna watu wamepona?
sasa wewe unaowakosoa wasomi waliotumia sayansi kupima mimea yenye kusaidia matatizo ya kupumua una msaada gani kwa jamii...
Nawakosoa kwa sababu dawa yao imekosa sifa mbili kuu za sayansi:

1.Haijajaribiwa popote pale ikaonyesha mafanikio yoyote yale.Kama kuna sehemu imejaribiwa na ikaonyesha mafanikio thibitisha.

2.Haina sifa za kuitwa dawa.Ili kitu kiitwe dawa kinapaswa kuwa na specific ingredients ambazo zina-attack specific antigens katika level ambayo ni specified.Dawa hii haina sifa hiyo.
matusi haya huwatukani Mlimani,Sua bali unatukana mpk mamlaka ya mkemia mkuu wa serikali.
Ni kweli kabisa nawatukana wote hao kwa sababu wana deserve kutukanwa.Wanadeserve kutukanwa kwa sababu badala ya kutengeneza dawa kama nilivyofafanua hapo juu wanafanya mizaha na kutengeneza vitu ambavyo havieleweki na ambavyo vinafanana na ndumba.Sasa ulitaka nisifie watu wanaofanya mizahaa tena na maisha ya watu?
 
Ni
Bosi na wewe una kipaji cha ujinga! Unategemea nchi hii upate mwanasayansi wa kukupa dawa ya Corona? Hawa wapayukaji ndo wajue sayansi?
Ushamba wenu tu , kama dawa za kawaida tu zina reaction na wameeleza kabisa unaweza kutapika kuhalisha na mengineyo sasa iweje hizo zenu za kiswahili?
 
Naona huyo jamaa alidanganyika,na kauli mbiu ya 'buy Tanzania products'...... mpe pole aiseee...
Bosi na wewe una kipaji cha ujinga! Unategemea nchi hii upate mwanasayansi wa kukupa dawa ya Corona? Hawa wapayukaji ndo wajue sayansi?
 
Kuna kipi cha kujua katika haya?Kujua kwamba wanatengeneza mizahaa badala ya dawa?
Mizaha ipi zaidi ya kutukana mamlaka za kisayansi ambazo ni za rufaa..kwa msaada km kweli ungekuwa unataka kujua namna zinazofanya kazi ungehoji juu ya reserch ya mimea iliyotumika km kwelu inauwezo wa kukabiliana na jambo hilo??mfano unapoitaja Sua unazungumzia mmea uliofanyiwa tafiti zaidi ya miaka 12 unaitwa liyungi(syanadenium glaunces pax) ingia google uone kazi zake kisayansi kwa tafiti kushirikiana na hao wazungu...wee unazungusha kanga km mwanamke wa kidigo watu wanatumia elimu zao
 
Hiyo dawa inakusaidia kusafisha tumbo lililokuwa limejaa uchafu na minyoo. Uwe mple tu, uhalishaji ukiisha utabaki na tumbo kama jipya vile!
 
Kumbe hata majukumu ya mkemia mkuu hujui kisha unataka majibu ya kisayansi..kuna sayansi bila maabara
Kwani maabara zote zinapita madawa...!!?

Kazi ya kusajili na kuthibitisha madawa ni ya TFDA. Kama Mkemia mkuu naye anafanya basi kuna muingiliano wa majukumu.
 
Kwa wasiwasi wangu, koo lilipokwaruza tu, nikajua dalili hizo. Hapa nilipo niko hoi kwa kuharisha usiku kucha. Ni uchafu gani tunauziwa na taasisi za serikali? Watu wa SUA bado munacheza na afya zetu kama enzi iliyopita?

Ni kweli hiki ndo kiwango cha utaalamu wa chuo kikuu? Na hapa ni baada ya kupigwa kichupa kingine cha chuo kikuu cha Dar ambacho chenyewe kinanukia mchai-chai. Sijui Muhimbili wana mizizi gani! Mutatuua!

Dawa zote huwa na side effects ambazo wakati mwingine ni severe kwa baadhi ya watu kama kuganda damu kwenye ubongo. Wewe kuharisha tu imekuwa noma. Jee ungeganda ubongo kwa kutumia dawa za hao wazungu ingalikuwaje? Kwa taarifa yako hiyo dawa ya SUA iliua virusi vyote vya covid 19 kwenye panya 1,000 waliokuwa infected na COVID 19. Haya, na wewe si ulipona hiyo covid 19 baada ya kuhara kama bata? SUA ni miamba ya dunia. Wanatumia panya kufanya diagnosis ya covid 19, tuberculosis na AIDS. Wanatibu covid 19 kwa kutumia dawa ya panya. Si wa mchezo. WHO haitaki kuwatambua kwa sababu ni Waafrika.
 
Kwani maabara zote zinapita madawa...!!?

Kazi ya kusajili na kuthibitisha madawa ni ya TFDA. Kama Mkemia mkuu naye anafanya basi kuna muingiliano wa majukumu.
Kwa mujibu wa sheria ya sheria ya Tiba asili na Tiba mbadala namba 23 ya 2002 maabara inayotumika kupima dawa kabla ya kusajiliwa na Baraza la Tiba asili pale wizara ya afya ni maabara ya mkemia mkuu wa serikali.Na dawa asili hupimwa kwa muongozo wa Who.sasa mnapokosoa vyema pia mkaheshimu hizi jitihada chache za Watanzania wenzenu..Hiyo TFDA unayosema ilishavunjwa toka zama za mwendazake
 
Kuna kipi cha kujua katika haya?Kujua kwamba wanatengeneza mizahaa badala ya dawa?
Mkuu behaviorist naomba nikupinge kidogo. Iko hivi . mimea hutengeneza secondary metabolites kwa Kiwango na composition kinachotofautiana kati ya mmea na mmea. Baadhi ya hizo metabolites ni flavonoids, tarpenoids, phenolics, plant sterols, saponini , alkaloids etc. Kiwango cha hizi metabolites ndizo hufanya mimea fulani kuwa na uwezo wa kutumika kama tiba kwani secondary plant metabolites zimejaribiwa kwenye maabara na kuonyesha uwezo kama antioxidants, some as antiviral, anticancer, antiglycemic ,antibacterial etc. Kwaiyo sio sahihi kubeza hizi anti covid preparation kwani hata zile zitolewazo mahospitalini kutibu kovid hazimuui virus bali ni supportive therapy.
 
Kwa wasiwasi wangu, koo lilipokwaruza tu, nikajua dalili hizo. Hapa nilipo niko hoi kwa kuharisha usiku kucha. Ni uchafu gani tunauziwa na taasisi za serikali? Watu wa SUA bado munacheza na afya zetu kama enzi iliyopita?

Ni kweli hiki ndo kiwango cha utaalamu wa chuo kikuu? Na hapa ni baada ya kupigwa kichupa kingine cha chuo kikuu cha Dar ambacho chenyewe kinanukia mchai-chai. Sijui Muhimbili wana mizizi gani! Mutatuua!

Syanadol ya Sua chupa yake nyeusi na sio transparent km hiyo..pili kwenye vitu vinavyotengeneza hakuna viambata vya siri na hakuna kinachofanya mtu kuharisha (inawezekana una shida ya tumbo usisingizie dawa)tatu acha dharau huo mmea uliobeba jina la dawa synadol(syanadenium glaunces pax)ni mmea ulitafitiwa kwa sayansi ya kutosha na Sua na Zaidi ya miaka 12 kushirikiana na nchi za scandnavia....unaweze kuwa na tatizo la jambo kabla ya kuropoka pima uzito wa jambo.Watanzania wazuri kukosoa lkn hawana njia mbadala zaidi ya mdomo
 
Back
Top Bottom