mwanamabadiliko
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 938
- 1,540
- Thread starter
-
- #101
Hiyo sehemu ni hatari mno, ukimaliza Kona unasali na kushukuru MunguNyagoro( Iringa- dodoma ) , ni shida, kile kipande kina kilometers kaa 28 toka unapozianza zile kona hadi unapozimaliza , na inasemekana zile kona zipo kaa 300. Nanikona za bampa to bampa kweli .
Basi kuna jamaa anaitwa ustadhi ( dereva fuso tandam ) huyu mjomba huwa inazila zile kona speed ikisoma 60 km / h kwenye dash board mi hupaki tu nimeshikilia roho yangu .
Kote mpaka Malawi ni balaa Ikwendeni,Chitipa(Malawi)!Ungesema mbeya kuelekea Tukuyu mzee
Unakutana na Chakito Longway au Shambalai Apache zinashuka speed ziwahi abiria Mombo. Hiyo Chakito ni Fuso body za kuchonga anavyoshuka unajiuliza mwamba anajihamini nini?Hata mimi niliuliza kuwa hapa ajari zitakuwa nyingi wakasema ni nadra sana kutokea maana wakimbiaji wa ile barabara ni wenye private wazoefu na mabasi kama kina side, burdan, maning nice n.k ule mlima ukiwa mgeni unaweza kuogopa hata ushuke upande kwa mguu, na bondeni kule ni mbali sana na barabara ni nyembamba gari kubwa zinasubiriana zipishane, halafu kuna vile vikaravati na kona papo kwa papo dah
Aisee sijapita hii njia na wala siwish kuipita😀 mambo ya kuminya breki kama mimi ndiye dereva sitaki😀Zile Kona za mtera ni kufuru[emoji23]
Halafu haziishi haraka tofauti na kitonga dk chache tu pameisha.
Zile nusu saa inaisha bado hazijaisha na hapo gari ipo speed Sana.
Zile Kona ilifika mahala nikazizoea,,Kama hujakaa siti ya dirishani unaweza kudondoka aisee[emoji1787][emoji1787][emoji1787].
Nazo ziko kama kitonga,pembeni korongo.
Hatari sana na kujishikilia kwenye kiti kwa nguvu huku ukiminya breki😀😀😀 maisha ni matamu haya jamani ijapokua tunalalamika hamna pesa maisha magumu ila when it comes to uhai mmh full mabreki kama dereva😀🙌[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
Hizi breki za miguu kumbe tupo wengi [emoji1787][emoji1787]
Kawetere ni namba moja ni vile haipo busy sana wewe ile kona ni kiboko pale juu mile tano...Kona namba moja ilipaswa kuwa nyang'oro , kutoka mtera kwenda iringa.
Na namba mbili ilipaswa kuwa lipumburu, kutoka njombe kwenda songea
Na namba 3 ilipaswa kuwa kawetere
hizi ni noma sana mkuu...pengine nyanda za juu kusini kunaongoza kwa kona kali na milima1. Kona za Iyovu - ukitoka tu mikumi kuelekea iringa utaziona Kona hizi, ni Tamu Sana
Jamaa yangu alikuwa hajawahi kupita Goba road. Siku katoka na Washkaji wakapita njia hii pale kwenye kilima Cha Mount Kibo Primary mpaka Kayuni gari yake Nissan March ilikosa nguvu akapanda kibishi.Kuna milima na kona za hatari huku goba...
Zile siyo mchezo, ni balaa tupu. Acha kabisa.Mkuu funga safari utoke iringa kwenda dodoma au dodoma kwenda iringa via Mtera utakuja kuelezea hiyo kitonga ni cha mtoto
Kona ya kutoka Sebuleni kuelekea chooni...
Sababu ile ni njia ya pembezoni hivyo magari ni machache tofauti na Kitonga ambayo nikm geti la kuingilia nyanda za juu kusini na nchi jiraniMi nashangaa watu wanafananisha eti na mburu kusiko hata na maporomoko,
Burdani anapitaga na mpaka 90kmph usiku, Madereva Wageni wengine wakifika Mombo wanaomba Mwenyeji awasaidie kupandisha, No chance for mistakes juu kuna jabali, chini kuna falls kati hapatoshi.
Cha kushangaza Sijawahi sikia ajali njia ilee.