Hizi ni tabia za kukosa ustaarabu na kishenzi (uncultured) kwa sisi madereva tukiwa barabarani, tubadilike

Hizi ni tabia za kukosa ustaarabu na kishenzi (uncultured) kwa sisi madereva tukiwa barabarani, tubadilike

Huo ushenzi namba 3 unanihusu 100%...😜😜
 
Madereva wa gari ndogo ndo huwa wanakaza kindezi tu.
Wengi hawana zile fair play za road, wao ni kukaza tu. Akiwa mdada ndo kabisaaa ila wao wanataka kuonewa huruma.
Na wewe kwa nini ulazimishe. Ni ushenzi na ujuha.
 
Kuna tabia za ajabu sana za madereva wengi Tanzania ambazo mimi nazijumlisha na kuwa mambo mawili makubwa, ushenzi na kukosa ustaraabu. Natoa wito madereva tubadilike, kwa sababu kwa na tabia hizi barabarani ni kuonyesha ubinafsi, pupa, ushenzi, kukosa ustaarabu nk!

Hizi ni mojawapo, kama unafahamu tabia mbaya kama hizi tafadhali ongeza
  1. Dereva anataka kuingia barabarani toka barabara ndogo, au kukatisha barabara, na wewe hutaki kumruhusu au kusimama ili aingie au kukatisha barabara.
  2. Unaruhusiwa kuingia barabarani au kukatisha na dereva mwingine, na wewe hutoi shukurani kwa ishara ya taa au hata kupunga mkono wa asante au thumbs up, umekaza uso tu kama vile barabara ni ya baba yako. Kukosa kuonyesha shukurani ni tabia ya kishenzi
  3. Mtu anataka kuku-overtake na wewe unaongeza spidi ili asiku-overtake, au asiingie mbele yako, japo ulikuwa unaenda taratabu
  4. Una-overtake kwenye jam, na upapoona kuna gari zinakuja mbele yako na kulazimisha kurudi kwenye line kwa ku-bully gari ndogo au za gharama kubwa bila hata kuomba kuingia
  5. Una-overtake kwenye Zebra crossing, au unaona kuna group la watu wanataka kuvuka barabara kwenye Zebra crossing, na wala hujali kuwapa nafasi.
  6. Kuna trafic jam, na sasa upande wa jam wanatengeneza lane mbili na kuwaachia upande wa pili nafasi kidogo ili wapite. Wewe unaamua kutengeneza lane yako ya tatu na ku-block magari yanayokuja, japo tayari tumelazimisha kuwa na lane mbili na kuwaachia nafasi kidogo. Huu ni ushenzi, wewe unataka wao wapite wapi?
Hizi ni tabia mbovu tano kama wewe ni dereva na unazifanya wewe huna ustaarabu na una tabia za kishenzi - you are uncultured. Acha tabia hizi.
Kwakweli halafu unakuta mtu mwingine ame overtake vibaya ghafla anakutana na jam anarudi lane yake ghafla ww unatoka barabarani, ni ushenzi!
 
Hiyo namba 3 madereva daladala na kaka zao wa mabasi ya masafa hawaji kuacha kamwe.
Madaladala ya Papafololo ya Mburahati Posta na daladala za Nangaboy Segerea Mnazi mmoja.
Nadhani hizi ni za vigogo fulani.
Mungu yupo
 
Mkimalizana na madereva wa magari tuhamie kwenye kikao cha kuwajadili untouchable group on the road a.k.a BODA BODA,wananikera sana na masauti yao ya piki piki (noise pollution) imekuwa kama fashen sasa hivi yaani mtu Yuko umbali wa kama kilometa 4 ila unaanza kusikia sauti kali ya piki piki na hapo hajafika ulipo.Hawa watu wadhibitiwe aisee maana imekuwa kero japo wao wanaona ndio ujanja na sifa
 
Aisee;..

1. Kuhusu kuingia barabarani: Siyo jukumu la dereva wa barabara kubwa kusimama, isipokuwa ni wajibu wa dereva wa barabara ndogo kuhakikisha kwamba kwenye barabara kubwa hakuna gari iliyokaribu na ama ni salama kuingia bila kusababisha usumbufu ama ajali.

2. Kuhusu kutoa shukrani; siyo lazima na haswa ikiwa kufanya hivyo si salama. Mfano unakuta gari ina mzigo mkubwa na barabara imekaa vibaya kiasi kwamba dereva anayeingia anapaswa kuzidisha umakini kuliko kuanza kuchanganyw mambo kwa kutoa shukrani wakati namba moja (1) hapo juu inajulikana kwamba kuingia barabarani ni wajibu wa anayeingia kulinda usalama.

3. Ni wajibu kwa anaye-overtake kuhakikisha kwamba ni salama kufanya hivyo, ikiwemo kutoa taarifa kwa madereva wengine kwamba anataka kufanya hivyo. Siyo kuvizia vizia na kuchomoka. Dereva wa mbele hana wajibu wa kupunguza ili upite isipokuwa wewe unayetaka kumpita ndiye unatakiwa ujipime iwapo unaweza kumpita salama.

4. Namba nne inajibiwa na namba 3. Kwamba wajibu wa anaye-overtake kuchukua tahadhari na siyo kuruka ruka na kukurupuka.

5. Ni wajibu wa mtembea kwa miguu kuhakikisha kwamba gari zimesimama, ndiyo avuke kwenye zebra. Wajibu wa dereva ni kupunguza mwendo ili kuhakikisha kwamba hakuna mvukaji. Hivyo, kwenye kuvuka, ni wajibu wa mvukaji kuzingatia usalama na siyo dereva. Hii haihusishi zebra àmbazo zimewekwa alama ya STOP ambapo no sharti dereva kusimama kwa muda halafu ndiyo apite.
Hapa hatuongelei sheria, tunaongelea ustaarabu, sasa kama wewe unafanya ushenzi na kukosa ustaarabu kwa sababu hakuna sheria inakutaka ufanye tofauti basi una tatizo.

Hakuna sheria inasema unapokuwa na watu mnakula chakula pamoja acha kuongea ukiwa unatafuna chakula mdomoni - lakini ukiwa na tabia ya kufanya hivyo wewe ni mshenzi na huna ustaarabu.

Kuna mtu alitoa post humu kuhusu watu kula ugali pamoja huku kila mara wanajiramba vidole na kuendelea kula - huo ni ushenzi na kukosa ustaarabu, lakini hakuna sheria juu ya hilo.

Sasa wewe unaona wazi magari yako main road bumper to bumper hakuna nafasi ya mtu kuingia na humwachii mtu anaetaka kuingia kwa sababu sheria inasema asubiri kuwe hakuna gari - huo ni ushenzi na kukosa ustaarabu!
 
Ukipita Old Bagamoyo road huko Daslama kwenu ndo hizi tabia ulizosema mleta sledi
 
Hapa hatuongelei sheria, tunaongelea ustaarabu, sasa kama wewe unafanya ushenzi na kukosa ustaarabu kwa sababu hakuna sheria ainakutaka ufanye tofauti basi una tatizo.

Hakuna sheria inasema unapokuwa na watu mnakula chakula pamoja acha kuongea ukiwa unatafuna chakula mdomoni - lakini ukiwa na tabia ya kufanya hivyo wewe ni mshenzi na huna ustaarabu.

Kuna mtu alitoa post humu kuhusu watu kula ugali pamoja huku kila mara wanajiramba vidole na kuendelea kula - huo ni ushenzi na kukosa ustaarabu, lakini hakuna sheria juu ya hilo.

Sasa wewe unaona wazi magari yako main road bumper to bumper hakuna nafasi ya mtu kuingia na humwachii mtu anaetaka kuingia kwa sababu sheria inasema asubiri kuwe hakuna gari - huo ni ushenzi na kukosa ustaarabu!

Hili povu jingi sana. Pole!
 
Aisee;..

1. Kuhusu kuingia barabarani: Siyo jukumu la dereva wa barabara kubwa kusimama, isipokuwa ni wajibu wa dereva wa barabara ndogo kuhakikisha kwamba kwenye barabara kubwa hakuna gari iliyokaribu na ama ni salama kuingia bila kusababisha usumbufu ama ajali.

2. Kuhusu kutoa shukrani; siyo lazima na haswa ikiwa kufanya hivyo si salama. Mfano unakuta gari ina mzigo mkubwa na barabara imekaa vibaya kiasi kwamba dereva anayeingia anapaswa kuzidisha umakini kuliko kuanza kuchanganyw mambo kwa kutoa shukrani wakati namba moja (1) hapo juu inajulikana kwamba kuingia barabarani ni wajibu wa anayeingia kulinda usalama.

3. Ni wajibu kwa anaye-overtake kuhakikisha kwamba ni salama kufanya hivyo, ikiwemo kutoa taarifa kwa madereva wengine kwamba anataka kufanya hivyo. Siyo kuvizia vizia na kuchomoka. Dereva wa mbele hana wajibu wa kupunguza ili upite isipokuwa wewe unayetaka kumpita ndiye unatakiwa ujipime iwapo unaweza kumpita salama.

4. Namba nne inajibiwa na namba 3. Kwamba wajibu wa anaye-overtake kuchukua tahadhari na siyo kuruka ruka na kukurupuka.

5. Ni wajibu wa mtembea kwa miguu kuhakikisha kwamba gari zimesimama, ndiyo avuke kwenye zebra. Wajibu wa dereva ni kupunguza mwendo ili kuhakikisha kwamba hakuna mvukaji. Hivyo, kwenye kuvuka, ni wajibu wa mvukaji kuzingatia usalama na siyo dereva. Hii haihusishi zebra àmbazo zimewekwa alama ya STOP ambapo no sharti dereva kusimama kwa muda halafu ndiyo apite.


...............,............

Fungo Augustus ▶ ‎RSA TANZANIA(Road Safety Ambassadors)

JE NI WAKATI GANI NISIMAME KWENYE ZEBRA CROSSINGS AU JE NI AMRI KUSIMAMA KWENYE ZEBRA HATA KAMA HAKUNA MWENDA KWA MIGUU ANAYEVUKA?
Sheria inasemaje?
Sheria ya usalama barabarani kifungu cha 65 kinahusu vivuko vya waenda kwa miguu, yaani pedestrian crossings.

Kifungu cha 65(1) kinamtaka mhandisi mkuu kusimika alama za vivuko vya waenda kwa miguu mahali panapofaa barabarani.

Kifungu cha 65(2) kinatamka kwamba mahali popote ambapo alama itakuwa imewekwa itachukuliwa kuwa imewekwa kihalali na itakuwa halali isipokuwa kama itakanushwa au kuthibitishwa vinginevyo.

Kifungu cha 65(6) kinamtaka kila anayetumia kivuko cha waenda kwa miguu kufanya hivyo kwa tahadhari kubwa na atumia kivuko hicho kuvuka barabara. Aidha kifungu cha 65(7) kinamtaka mtumiaji kivuko huyo kutokanyaga barabara ili avuke bila kuzingatia umbali na spidi ya magari yanayokuja
Kifungu cha 65(10) kinasema itakapotokea mtembea kwa miguu anatumia au anataka kutumia kivuko cha waenda kwa miguu, dereva wa gari atasimama kabla ya kivuko hicho ambacho hakiongozwi na taa za barabarani, ishara za barabarani au askari.

[Hivi vivuko vinavyokuwa vimechorwa barabarani kwa mistari ya pundamilia ambapo mtu anavuka bila usimamizi wa askari au maelekezo ya taa].
Dereva ataendelea tu na safari ikiwa atajiridhisha kuwa hakuna mtembea kwa miguu anayetumia(anayevuka) au anakusudia kuvuka barabara.

KWA MINAJILI YA REJEA KIFUNGU CHENYEWE CHA 65(10) Kinasema hivi katika lugha yake asili "(10) Where a pedestrian is using or is about to use a pedestrian crossing, a driver of a vehicle shall stop before a pedestrian crossing on a carriageway which is not regulated by traffic lights, traffic signals or by a police officer."

HIVYO BASI, JIBU NI KWAMBA sio lazima dereva asimama kwenye kila zebra crossings hata kama hakuna anayevuka, dereva atapunguza mwendo na kuangalia iwapo kuna mtu anavuka au ananuia kuvuka, kama hakuna ataendelea na safari.

Kwa hiyo, dereva asimama kwenye eneo kabla ya zebra crossing pale wakati wote ambapo kuna mtu au watu wanavuka au wanakusudia kuvuka.


Ni matumaini yangu tumeelewana. Mwelimishe na mwenzio.


ZINGATIA: Maelezo haya hayahusishi zile ZEBRA crossings ambazo kabla yake kunakuwa na mchoro chini au alama ya amri iliyoandikwa kabisaaa STOP. Hapa utatakiwa kusimama hata kama hakuna anayevuka.
No. 3. Mara kadhaa nimekutana na situation ya gari mbele yangu likienda taratibu muda mrefu. Fursa ikitokea ukawasha kiashirio cha kulia na kuanza kupita (overtake) ndio kama umemuamsha mtu anaanza kuongeza mwendo mpaka unashangaa.

Kizuri huwa na naangalia magari ya kuendelea ku-overtake na ya kuachia ikitokea hali kama hiyo. Huwa sipendi kukanyaga sana - hadi nilazimike. I have my ideal speed.

Lakini kama alivyosema mleta mada si ustaarabu kabisa. Ukiamua kwenda mwendo mdogo na nyuma yako kuna magari yanakusanyika acha yapite. Vinginevyo, ukiona yanakaribia na wewe hutaki kupitwa basi ongeza mwendo kabla yasifikirie kikupita. Lazima uwe consistent barabarani. ‘usiendeshwe’ na watu wengine wakati kila mtu ana safari yake.

Kero nyingine uko kwenye barabara kuu, mbele jirani gari tokea njia ya pembeni linakuja na kuingia mbele yako kwa kasi hadi unalazimika kukanyaga breki za ghafla. Halafu sasa linaendelea na kasi ndogo tofauti na liliyoingia. Ukilipita unakuta dereva anaongea na simu ame-relax kabisa kama yuko kibarazani kwake!

Haya mambo hapa kwetu hayana sheria lakini ustaarabu barabarani ni kitu muhimu sana. Siku hizi gari ni kitu cha kawaida sana; halitakiwi “kumpanda mtu kichwani”.
 
Ukipita Old Bagamoyo road huko Daslama kwenu ndo hizi tabia ulizosema mleta sledi
Yaani Old Bagamoyo ndio hakufai kabisa! Kule kila mtu ni kingunge, mtoto wa kingunge au usalama wa taifa - anataka aachiwe barabara!
 
No. 3. Mara kadhaa nimekutana na situation ya gari mbele yangu likienda taratibu muda mrefu. Fursa ikitokea ukawasha kiashirio cha kulia na kuanza kupita (overtake) ndio kama umemuamsha mtu anaanza kuongeza mwendo mpaka unashangaa.

Kizuri huwa na naangalia magari ya kuendelea ku-overtake na ya kuachia ikitokea hali kama hiyo. Huwa sipendi kukanyaga sana - hadi nilazimike. I have my ideal speed.

Lakini kama alivyosema mleta mada si ustaarabu kabisa. Ukiamua kwenda mwendo mdogo na nyuma yako kuna magari yanakusanyika acha yapite. Vinginevyo, ukiona yanakaribia na wewe hutaki kupitwa basi ongeza mwendo kabla yasifikirie kikupita. Lazima uwe consistent barabarani. ‘usiendeshwe’ na watu wengine wakati kila mtu ana safari yake.

Kero nyingine uko kwenye barabara kuu, mbele jirani gari tokea njia ya pembeni linakuja na kuingia mbele yako kwa kasi hadi unalazimika kukanyaga breki za ghafla. Halafu sasa linaendelea na kasi ndogo tofauti na liliyoingia. Ukilipita unakuta dereva anaongea na simu ame-relax kabisa kama yuko kibarazani kwake!

Haya mambo hapa kwetu hayana sheria lakini ustaarabu barabarani ni kitu muhimu sana. Siku hizi gari ni kitu cha kawaida sana; halitakiwi “kumpanda mtu kichwani”.
Well said Mkuu!
 
Hili povu jingi sana. Pole!
Ujumbe umefika lakini? Badilika bwana. Tunataka tuendeshe IST zetu na kufurahi kuwa nazo barabarani, sio kupata ugonjwa wa pressure kwa hofu za kila wakati au hasira kunakosababishwa na madereva wengine washenzi na wasio wastaarabu.
 
Back
Top Bottom