Uchaguzi 2020 Hoja tatu ni kwanini wapinzani hawatoshi kwenye Uchaguzi huu

Uchaguzi 2020 Hoja tatu ni kwanini wapinzani hawatoshi kwenye Uchaguzi huu

Yaani unataka Jpm achaguliwe kisa
1.Corona
2.Upinzani haujaungana
3.Majimboni hakuna jipya

Hizi ni hoja au viroja?Yaani mtu apewe miaka 5 eti kwasababu hizo?Badala mumuulize sera ya viwanda imefia wapi?Vipi ajira mil 8 atafanya muujiza gani wakati ajira mil 1 hata 1% hakufikia kwa miaka mitano iliyopita!Aeleze kwanini mzunguko wa fedha umedorora na ana plan gani kuinua uchumi wa watu wake badala ya vitu vya kuonekana pekee?Muulizeni,hatma ya sekta ya kilimo ni nini maana ndiyo inayogusa wananchi wengi zaidi nchi hii huku ikiachwa nyuma kama sio kipaumbele cha serikali yake!
Hayo ndiyo mambo ya msingi tunataka kusikia mtu akieleza sio hizi cheap politics za Corona,sijui wapinzani hawajaungana,period!
Hesabu hiyo rahis sana, moja tutazarisha Ajira kwenye tren ya mwendo kazi, titazalisha viwandani baada ya kupata umeme wa uhakika kule rufiji, kwenye meri kubwa ya mizigo ziwa Victoria, na kadhalika
 
Narudia tena kusema,upumbavu ni kipaji.
Hoja yako ya tatu umeandika kuwa ni wapinzani kushindwa kuungana.
Mkuu Benny Haraba hapo juu kakuuliza unajua sheria ya vyama vya siasa inasemaje kuhusu vyama kuungana,wewe unasema nnje ya hoja.
Kama huwezi kukumbuka kitu ulichokiandika mwenyewe muda mfupi uliopita,kuna jina zuri zaidi ya kukuita zaidi ya mpumb.v.?
Tumeshamalizana na mkuu Ben. Tumeelewana
 
Hoja pumba kabisa. Asilimia kubwa ya majibu yanapatikana katika mahojiano ya TL na ITV jana. Kaisikilize.
Mkuu, zile dakika 45 za Mh. T.A. Lissu katika kipindi cha Dakika 45 cha ITV,unaweza kuombea mkopo JPMorgan Chase & Co au Wells Fargo & Co na ukapewa bila masharti.
Pia unaweza kuandikia thesis na kupatia PhD chini ya muda uliopangwa katika vyuo vikuu vinavyotoa elimu bora,sio vinavyotoa vyeti.
 
Mkuu, zile dakika 45 za Mh. T.A. Lissu katika kipindi cha Dakika 45 cha ITV,unaweza kuombea mkopo JPMorgan Chase & Co au Wells Fargo & Co na ukapewa bila masharti.
Pia unaweza kuandikia thesis na kupatia PhD chini ya muda uliopangwa katika vyuo vikuu vinavyotoa elimu bora,sio vinavyotoa vyeti.
Residenturaaaaaaaaaaa
 
Wanajamvi,

Ninaomba nilete kwenu hoja tatu ni kwanini tusichague Upinzani. Hoja hizo ni Kama ifuatavyo:

1. Njia za kushughulikia janga la korona
2. Kushindwa kuwa mfano kwenye chama na majimbo
3. Kushindwa kuungana

Njia za kushughulikia janga la Corona

Wakati serikali ikija na mpango mkakati wa kushughulikia janga la korona, wapinzani nao walikuja na mpango wao. Serikali ilisisitiza kufuata masharti lakini watu walikuwa huru kufanya shughuli zao (there was no curfews). Kwa upande wao, wapinzani (hasa CHADEMA na ACT - Wazalendo), walisisitiza kufuata masharti lakini walitaka watu wafungiwe ndani (country lockdown).

Njia ya serikali ya CCM chini ya Rais Magufuli (akisaidiwa kwa Karibu na waziri Ummy Mwalimu) iliunganisha mambo mawili; ubunifu wa kisayansi uliozingatia mazingira yetu na kuweka imani kubwa kwa Mungu. Wapinzani walitaka kufanya "copying and pasting" pasipo kuzingatia mazingira yetu.

Unamfungiaje mtu ambaye mlo wake unategemea yeye kutoka? Watu si wangekufa njaa? CCM waliona hilo. Wananchi walipokea kwa furaha maamuzi ya Rais maana yalijaa matumaini, yalitoa Faraja na yalituvusha.

Rais Magufuli na serikali yake hawakulala. Walifanya majaribio, waliagiza NIMR na matabibu watafute suluhu. Mengi aliyoyafanya Rais Magufuli yalikuja kuthibitika baadae kuwa ni kweli na hakika ingawa wakati akiyasema alishambuliwa na maadui wa ndani na nje na kuitwa majina your mabaya.

Wakati Rais Magufuli na CCM wakichukua hatua hizo, wapinzani walikebehi, kubeza na kulaani. Walitutaka tusubiri kuokota maiti. Walienda mbali zaidi wakachukua posho halafu wakatokomea kusikojulikana, wenyewe wakiita "karantini ya kishua" huku wapiga kura wao wakihangaika kutafuta riziki zao.

CHADEMA walienda mbali zaidi kwa kutoa onyo Kali pamoja na kuwafukuza uanachama wabunge waliokataa mpango huo. Inashangaza wanajiita chama cha demokrasia.

Kwa hili tuu la ugonjwa wa Corona, ilitosha kabisa kuwakataa wapinzani na kuipa CCM kura zote.

Kushindwa kuwa mfano kwenye chama na majimbo

Ukipata nafasi unatakiwa uitumie vizuri. Wabunge wa Upinzani walitakiwa wajiongeze kwa kufanya kazi kwa bidii Sana, ubunifu wa hali ya juu na uadilifu usiotiliwa shaka. Vyama vyao vilitakiwa kuongozwa Kidemokrasia. Hii ingewasaidia sana kuwathibitishia watanzania kuwa hata wakipewa nchi wanaweza. Wanasema "Charity begins at home".

Kinyume chake, chamani na majimboni, ni "business as usual". Siku zote mchepuko unajitahidi kumfunika madhahausi. Wapinzani kwa hili mmeshindwa pakubwa. Mmeshindwa kuthibitisha kuwa mnaweza kuwa mbadala wa CCM. Endeleeni kujiandaa kwa sasa hamtoshi.

Kushindwa kuungana

Wapinzani kushindwa kuungana hasa mnapomkabili mgombea wa aina ya Rais Magufuli ni udhaifu mkubwa sana. Ni wazi kuwa hamuaminiani. Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe aliahidi ahadi hii hewa. Kama nyie binafsi hamuaminiani, sisi wananchi wa kawaida tutawaaminije?. CCM itawapiga kipigo cha mbwa koko mwaka huu. Hamna rangi mtaacha kuona.

Amani Msumari
Tanga
Ukiona mtu hamweliewi lisu au Chadema maana kuna ccm b,c,d n.k ujue huyo mtu bongo yake kuna sehemu ipo na shida
 
Upumbavu ni kipaji.
Na CCM ya sasa upumbavu ni mtaji.
Wewe ni nani wa kuwasemea Watanzania kuwa mgombea wa Rebeca 83 sio chaguo sahihi la Watanzania?
Residentura ndugu yangu. Zibeni kwanza hilo tundu lenu kwa kuweka mlango imara dhidi ya hasira, wivu, visasi na jazba. Sisi tutawasaidia kuwapa "Makufuli" imara kabisa.
 
Narudia tena kusema,upumbavu ni kipaji.
Hoja yako ya tatu umeandika kuwa ni wapinzani kushindwa kuungana.
Mkuu Benny Haraba hapo juu kakuuliza unajua sheria ya vyama vya siasa inasemaje kuhusu vyama kuungana,wewe unasema nnje ya hoja.
Kama huwezi kukumbuka kitu ulichokiandika mwenyewe muda mfupi uliopita,kuna jina zuri zaidi ya kukuita zaidi ya mpumb.v.?
Kwakifupi kuungana wapinzani kuna mitego ambayo CCM wameiweka hawatakiwi watumie akili za kuvukia barabara kama wewe unavyo lazimisha
 
Kuna factors nyingi sana zinazipelekea ufukara, ila kubwa ni mindset. Kwenye majimbo fukara,hata ukimfanya Bill gates kuwa mbunge kama wananchi hawapo tayari kutumia fursa walizonazo na zinazoletwa na Serikali yao lazima tu wawe fukara. Ila kama Chadema wangekuwa madarakani tangu uhuru, wao hata nchi wangeiuza hawa jamaa.
Safi kijana, upo vizuri kwenye kudadavua hoja sio hao wengine wapo tu kwenye mkumbo.
 
Naona umeanza kuongea kitu nilichokuwa nasema ila hujajielewa tu!
Msemo huo Roma ulipaswa umgeukie JPM mwenyewe!Kuendea miradi inayochukua fedha nyingi kwa pupa ndio kunafanya sekta kama ya kilimo inayobeba maisha ya watanzania wengi kuzorota!
Mkuu sekta ya kilimo ilikuwa na madudu mengi na pesa ilikuwa inapelekwa nyingi tu. Mambo yananyooka taratibu lakini itafika siku tutakuwa katika njia sahihi.
 

Fikiria. Unaishi Ubungo; unafanya kazi Posta mjini. Unahitaji USAFIRI kwenda/kurudi kazini kila siku. Mshahara wako ni shilingi laki 2-5. Utanunua gari au kutenga bajeti ya mwendo kasi/daladala kwa mwezi? Ndio maamuzi ya kisera yanavyofikiwa.

Watu wenye akili hatuwezi kujadili umuhimu wa ndege kama vile ambavyo hatuwezi kujadili umuhimu wa gari. Suala ni USAFIRI. Sasa kwa kipato kisichozidi shilingi milioni moja, sitakuwa sahihi kununua gari ili kunipeleka kazini kwa hoja kwamba gari ni kitu muhimu! Gharama za ununuzi, mafuta, matengenezo na maegesho, nk haviwiani na uwezo wangu. Naweza kupanda Uber/taxi mara moja moja ikitokea ulazima sana kama Lissu anavyopanda ndege ASIYOIMILIKI kwenye hiyo picha. Ikitokea CHADEMA wakanunua ndege eti kwa sababu ni muhimu nitawatambua rasmi kama wehu.

Shirika la ndege halifufuliwi kwa serikali kununua ndege kwa pesa (cash) za walipa kodi. Hayo si matumizi sahihi ya pesa za umma. Hii ni biashara inayobidi kufanywa na wawekezaji binafsi. Ikibidi serikali inaweza kuwa m’bia muhimu kwa kuweka hisa zake na usimamizi makini. Halafu, sijawahi kusikia ndege za biashara zikinunuliwa kwa cash. Inaelekea hilo shirika litaendeshewa kwa ruzuku ya serikali maisha yake yote na gharama zake zikiwekwa wazi kutakuwa na mtafutano mkubwa. Brace yourselves.
 
Wanajamvi,

Ninaomba nilete kwenu hoja tatu ni kwanini tusichague Upinzani. Hoja hizo ni Kama ifuatavyo:

1. Njia za kushughulikia janga la korona
2. Kushindwa kuwa mfano kwenye chama na majimbo
3. Kushindwa kuungana

Njia za kushughulikia janga la Corona

Wakati serikali ikija na mpango mkakati wa kushughulikia janga la korona, wapinzani nao walikuja na mpango wao. Serikali ilisisitiza kufuata masharti lakini watu walikuwa huru kufanya shughuli zao (there was no curfews). Kwa upande wao, wapinzani (hasa CHADEMA na ACT - Wazalendo), walisisitiza kufuata masharti lakini walitaka watu wafungiwe ndani (country lockdown).

Njia ya serikali ya CCM chini ya Rais Magufuli (akisaidiwa kwa Karibu na waziri Ummy Mwalimu) iliunganisha mambo mawili; ubunifu wa kisayansi uliozingatia mazingira yetu na kuweka imani kubwa kwa Mungu. Wapinzani walitaka kufanya "copying and pasting" pasipo kuzingatia mazingira yetu.

Unamfungiaje mtu ambaye mlo wake unategemea yeye kutoka? Watu si wangekufa njaa? CCM waliona hilo. Wananchi walipokea kwa furaha maamuzi ya Rais maana yalijaa matumaini, yalitoa Faraja na yalituvusha.

Rais Magufuli na serikali yake hawakulala. Walifanya majaribio, waliagiza NIMR na matabibu watafute suluhu. Mengi aliyoyafanya Rais Magufuli yalikuja kuthibitika baadae kuwa ni kweli na hakika ingawa wakati akiyasema alishambuliwa na maadui wa ndani na nje na kuitwa majina your mabaya.

Wakati Rais Magufuli na CCM wakichukua hatua hizo, wapinzani walikebehi, kubeza na kulaani. Walitutaka tusubiri kuokota maiti. Walienda mbali zaidi wakachukua posho halafu wakatokomea kusikojulikana, wenyewe wakiita "karantini ya kishua" huku wapiga kura wao wakihangaika kutafuta riziki zao.

CHADEMA walienda mbali zaidi kwa kutoa onyo Kali pamoja na kuwafukuza uanachama wabunge waliokataa mpango huo. Inashangaza wanajiita chama cha demokrasia.

Kwa hili tuu la ugonjwa wa Corona, ilitosha kabisa kuwakataa wapinzani na kuipa CCM kura zote.

Kushindwa kuwa mfano kwenye chama na majimbo

Ukipata nafasi unatakiwa uitumie vizuri. Wabunge wa Upinzani walitakiwa wajiongeze kwa kufanya kazi kwa bidii Sana, ubunifu wa hali ya juu na uadilifu usiotiliwa shaka. Vyama vyao vilitakiwa kuongozwa Kidemokrasia. Hii ingewasaidia sana kuwathibitishia watanzania kuwa hata wakipewa nchi wanaweza. Wanasema "Charity begins at home".

Kinyume chake, chamani na majimboni, ni "business as usual". Siku zote mchepuko unajitahidi kumfunika madhahausi. Wapinzani kwa hili mmeshindwa pakubwa. Mmeshindwa kuthibitisha kuwa mnaweza kuwa mbadala wa CCM. Endeleeni kujiandaa kwa sasa hamtoshi.

Kushindwa kuungana

Wapinzani kushindwa kuungana hasa mnapomkabili mgombea wa aina ya Rais Magufuli ni udhaifu mkubwa sana. Ni wazi kuwa hamuaminiani. Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe aliahidi ahadi hii hewa. Kama nyie binafsi hamuaminiani, sisi wananchi wa kawaida tutawaaminije?. CCM itawapiga kipigo cha mbwa koko mwaka huu. Hamna rangi mtaacha kuona.

Amani Msumari
Tanga
Kwanini mgombea wa ccm hastahili kupewa tena kura zetu?

Sababu za kutompa kura zetu mgombea wa ccm ni hizi zifuatazo.

1. Mauaji ya raia wasio Na hatia,

2. Umeendesha nchi kikabila na kikanda,

3. Umeshiriki katika ufisadi wa kununua ndege nk kama sio kweli tupe mikataba ya ununuzi.

4. Umewatesa sana waliokukosoa mfano hai TUNDU LISU na MDUDE CHADEMA.

5. Kutoa ajira kwa kupendelea wanaccm wenzake.

6. Kuwavunjia nyumba wakazi wa mbezi kinyume na sheria za nchi.

7. Kuuza nyumba za serikali kiholela tena kwa watu ambao hawakuwa watumishi wa serikali wakati zinauzwa.
 
Mkuu sekta ya kilimo ilikuwa na madudu mengi na pesa ilikuwa inapelekwa nyingi tu. Mambo yananyooka taratibu lakini itafika siku tutakuwa katika njia sahihi.
Miaka mitano mmeshindwa kushughulikia hayo unayoita madudu,tuwaeleweje?Sasa unasema bado mnashughulikia madudu,mpaka lini?Shame!
 
Back
Top Bottom