#COVID19 Hoja za Askofu Gwajima wameshindwa kuzijibu

#COVID19 Hoja za Askofu Gwajima wameshindwa kuzijibu

Ninashangazwa sana na hawa watu wanaopinga chanjo bila kuwekea madhara yake kwamba tukichanja tutapatwa na madhara yepi
Na je wameingia maabara zipi kuthibitisha haya

kwa sababu ninachokiona kwa hawa ni uchonganishi wanaowafanyia wananchi dhidi ya kiongozi wao mkuu na ambaye ndiye Rais wa nchi kwa sababu yeye Rais anahamasisha chanjo kwamba raia wake wote wachache na hivyo hiyo ndiyo namna ya kupambana na korona na anawahakikishia na kuwashawishi kwamba kwa kufanya hivyo itawazuia kufa kwa Korona na kwa sababu yeye ndiye was kiongozi mkuu wengi wa wananchi watamwelewa na kuchanja ama kunao watakao kataa kuchanja kwa sababu kwamba wao wamewasikiliza watu wao wanaowaamini

lakini wakati ambao Rais na viongozi wengine wa serikali wakihasisha kuchanja anaibuka mtu mwingine ambaye anayo madaraka yake kwa kikundi ama kundi flani la watu naye anapingana na Rais na kusema kwamba tusichanje kwa sababu chanjo inayo madhara ambayo hayajaorodheshwa wala kutajwa kwenye mikutano ama matamasha wanayoyatumia katika kupingana na Rais na viongozi wengine wenye kuungana na Rais kwenye ushawishi wa kuchanja

sasa hapa kaswali kangu kadogo tu ni kwamba je hawa wapingaji wa chanjo siyo kwamba wanamchonganisha rais na wananchi wake? hapa kwa tafsiri nyepesi tu ni kwamba anawaambia wananchi ya kwamba rais anataka wananchi wafe ndiyo maana anawahamasisha wakachanje ili wafe je hii siyo hujuma na kukosa utii?

nashauri watu wa namna ya kina Gwajima vyombo vya ulinzi na usalama vinapaswa kuhangaika nao kwa kuwashughulikia maana kwa sababu chanjo ni hiari ikiwa wao hawataki na wala hawamini ktk chanjo walipaswa kukaa kimya maadamu hawajalazimishwa kuchanja na wala kama siyo uchonganishi hawakupaswa kuwashawishi tena kwa waziwazi watu wengine kwamba wasichanjwe

wanapaswa kuyaheshimu madaraka ya Urais kwani Urais hauna mipaka katika kuongoza kwake

na pia nashauri ni wakati wa vyombo vya usalama kushughulika na hawa watu wa namna ya Gwajima kuwaelewesha ama kwa taratibu au kwa namna yeyote ya kwamba hawaruhusiwi kulitolea ufafanuzi wala tafsri ya kupingana ktk hili swala la kupambana na kuizuia korona na kwamba waelewe serikali haijasema kwamba imefungua mjadala wa chanjo ya Korona na kwa hivyo wao kama wao hawaruhusiwi kuliongelea kwa namna ya tofauti ama namna inayokinzana na Serikali katika swala hili na kwa yeyote atakayebainika akitoa tafsri yenye kupotosha kuchanjwa Korona atachukuliwa hatua kali za sheria

nakaa sana nawatafakari hawa watu najiuliza je wanayo nia gani? Kwa nini wanafanya haya?

napata jibu kwamba ni watu wenye tamaa mbaya za kimadaraka watu wasijali wenzao wala maisha ya wenzao na hapa ni kwamba wanatafuta tu kujulikana kwa ajili ya maslahi yao binafsi ya kisiasa siku za baadaye kwani kwa kupingana huku kwao pia kuko ktk hali ya kubahatisha na kama upigaji ramli kwamba ikiwa kama gonjwa halitakuwa na mlipuko kama tunavyoelezwa basi nao watajitokeza sasa na kusema kuwa wao ni manabii na walitabiri na sasa watu hawajakufa kama walivyotangaziwa wao watu wenye kufahamu mambo mengi na kumbe watu wakifa haina madhara kwao kwa sababu waliopaswa kuwahoji walishafariki

kwani nini wasituambie madhara yake kisayansi?

naomba serikali ije na mwarubaini kwenye hili swala.
Itoe onyo kali na ipige marufuku kabisa kwa vyombo ambavyo havina dhamana ya kusimamia afya za wanachi kuongelea ama kutafsri kwa njia ya tofauti na ile inayopendekezwa na kusimamiwa na serikali

na pia kwa sababu mtu kama Gwajima pengine kwa sababu zake za kimaslahi ndizo zilizopelekea yeye kuwepo kwenye siasa na hatimaye bungeni akiamini kwamba kunazo pesa nyingi zaidi ya alizokuwa anapata kwenye kuhubiri kwake na sana amegundua kwamba ni tofauti na alivyotegemea kwani kanisani ndiko kwenye pesa na sasa anataka kujiondoa kwenye siasa ili arejee kwenye kuhubiri kwa namna hii anakosa njia nzuri ya kujiondoa hivyo anaamua kujilipua kwa namna hii akitafuta kugombana na serikali ili serikali umuondolee hadhi ya ubunge
Namshauri mwenyekiti wa ccm ashauriane na uingozi wa chama ngazi za juu awashawishi wamkubali kumnyang’anya kadi ya ccm Gwajima na kumfukuza uanachama wa ccm hivyo kwamba apoteze sifa ya kuwa mbunge kwa sababu atakuwa hana chama na hivyo kuondokana naye ili aweze kurudi vizuri kwenye kazi yake ya mwanzo ambayo ni uchungaji
Naomba kwa leo niishie hapa kwanza.
Mzee summarize. Ongea kwa bullet points. You are using too much energy
 
Nyomgeza:
5.Kwa nini wahudumu wanaochanja wanalipwe Sh.2,000,000 tofauti na chanjo zingine,na Marekani kila anayechanjwa anapata dollar 100?
6.Kwa nini wasanii watumike kuhamasisha tofauti na chanjo zingine?
7.Kwa nini nguvu kubwa sana inatumika?
8.Kwa nini chanjo imepata nguvu baada ya Magufuli?
9.Kwa nini ugonjwa umeibuka kwa nguvu baada ya Magufuli?
10.Kwa nini serikali isiwaambie wananchi imebadili msimamo badala yake inafanya mambo kinyemela?

Na mimi kama maswali hayo hayakupata majibu,nipo upande wa Magufuli kwa kuwa nao ni msimamo wa serikali.
Hoja mamba 5: Hazard pay hio.

Namba 6: Wasanii wanatumika kutokana na dharula ya ugonjwa wenyewe. Wana ushawishi kwa jamii; mbona tunawatumia kwenye promotion kama za kukomesha malaria?

Namba 7: Nguvu inatokana na dharula ya ugonjwa. Wangapi unataka wafariki?

Namba 8: Magufuli alipinga chanjo, Mama Samia anaunga mkono chanjo. Hio ndio sababu ya chanjo kupata nguvu.

Namba 9: ugonjwa ulikuwepo wakati wa Magufuli lakini alikataza kuripotiwa.

Namba: 10 Msimamo upi? Mara ngapi Mama kasema kwamba gonjwa lipo tuchukue tahadhali na tume iliundwa kufanya utafiti zaidi .
 
Kuhusu concent form ni utaratibu wa kimataifa wa matibabu. Kabla hujamgusa mgonjwa intakiwa umfahamishe ni kwanini unamgusa.

Unampo mpa dawa mgonjwa ni lazima umfahamishe ni dawa gani unampa na ni kwasababu gani.

Katika tiba inayohusu sindano na upasuaji consent inabeba uzito mkubwa zaidi. Mgonjwa ana paswa kuelezwa faida na hasara na kama ana akili timamu na ameelewa maelezo lakini ameamua kukataa tiba ni haki yake hatakiwi kulazimishwa.

Kuhusu watu kulazimishwa chanjo, hii chanjo ni sehemu ya jitihada ya dunia kupambana na ugonjwa ambao ni mpya na unaua. Tukiwa kama sehemu ya dunia ni lazima tu hamasishe watu wapate kinga na tiba ili kukomesha ugonjwa usienee au kupunguza makali. Hakuna aliyelazimshwa kwani Askofu Rashid ana data za watu wakiowekwa ndani kwa kukataa chanjo?
Mbona daktari akiniandikia panadol au akitaka kunipima maralia huwa hamna sehemu naweka saini ?🤣🤸🐒
 
Hoja mamba 5: Hazard pay hio.

Namba 6: Wasanii wanatumika kutokana na dharula ya ugonjwa wenyewe. Wana ushawishi kwa jamii; mbona tunawatumia kwenye promotion kama za kukomesha malaria?

Namba 7: Nguvu inatokana na dharula ya ugonjwa. Wangapi unataka wafariki?

Namba 8: Magufuli alipinga chanjo, Mama Samia anaunga mkono chanjo. Hio ndio sababu ya chanjo kupata nguvu.

Namba 9: ugonjwa ulikuwepo wakati wa Magufuli lakini alikataza kuripotiwa.

Namba: 10 Msimamo upi? Mara ngapi Mama kasema kwamba gonjwa lipo tuchukue tahadhali na tume iliundwa kufanya utafiti zaidi .
C-19 haina udharura wowote,it is a plandemic,not a pandemic.Magomjwa ya Moyo,Cancers,Sukari etc.
yanaua watu zaidi,danganyeni wengine sio mimi.Infact it is non existent.Matatizo ni mengine,wanasingizia Corona.Mr.Global ni mshenzi sana.Kweli nimeamini wajinga ndio waliwao.

Kwanza utachanjaje watu vaccine ambayo ni ya majaribio,ni ajabu sana.Hivi Watanzania tumekuwa mazuzu kiasi hicho,eti chanjo iliyokuwa developed in 18 months tunawachanja watu wetu!Ni uzuzu wa kupindukia huu frankly dah,inauma sana.
 
Consent form....

GWAJIMA anaulizia consent form....

Inaonekana hana mtu wa karibu aliyewahi kupelekwa CHUMBA CHA UPASIAJI....pia iko hiyo "consent form"....anajaza mgonjwa Mwenyewe na ikishindikana wanajaza watu wake wa karibu.....

Na hili pia ALIHOJI.....

Chanjo hizi ni mpya.....hazina muda mrefu toka ZIZINDULIWE....

Gwajima hebu afunge macho na kufikiri ,TB na magonjwa mengine ya mlipuko yalipokuwa yanatokea na chanjo kuanza kutolewa je "KIPINDI HICHO" nako kulikuwa na "consent forms" pale ilipotolewa kwa JAMII(massive vaccination)?!!!

Kipindi hicho kulikuwepo na haya MAENDELEO MAKUBWA ya HAKI ZA BINADAMU na kuheshimu mawazo ya WAGONJWA (informed consent) ?!!

Anyway ,Gwajima anataka TUUACHE UGONJWA KWA MIAKA 10 bila ya chanjo yoyote na wataokufa wafe na watakaobaki WAENDELEE kuishi(natural selection) ?!!!😲😲

Aakofu Gwajima amekuwa "CHARLES DARWIN"?!!

#TujitokezeKuchanjwa
#ChanjoNiBoraKulikoTiba
#SiempreJMT
#KaziInaendelea
Mkuu naona unachanganya madesa, consent form ya kwenye upasuaji na ya chanjo ni wapi na wapi unaulizwa kuhusu chanjo na hakuna chanjo ambayo anachanjwa binadamua anaambiwa ajaze consent form, jibuni hoja hayo mambo ya kusema sijui chanjo ya TB hatukuuliza kwani chanjo ya TB ilitengenezwa na kufanyia majaribiok kwa miezi sita?
 
C-19 haina udharura wowote,it is a plandemic,not a pandemic.Magomjwa ya Moyo,Cancers,Sukari etc.
yanaua watu zaidi,danganyeni wengine sio mimi.Kwanza utachanjaje watu vaccine ambayo ni ya majaribio,ni ajabu sana.Hivi Watanzania tumekuwa mazuzu kiasi hicho,eti chanjo iliyokuwa developed in 18 months tunawachanja watu wetu!Ni uzuzu wa kupindukia huu frankly dah,inauma sana.
Magonjwa ya moyo na kisukari yanatokana na life style ya mtu ukitoa kisukari type 1. Je ni magonjwa ya mlipuko kama COVID-19?

Tunajua nini cha kufanya kuepukana na magonjwa ya moyo na kisukari type 2. Kama nina ugonjwa wa moyo, kisukari au cancer nikimtembelea mtu si wezi ku muambukiza.

Chanjo walioitengeneza ndio walio anza kuitumia kwa watu wao kutokana na watu waliofariki kwa mda mchache. Ndio imetengenezwa kwa mda mfupi kutokana na watu walikuwa wanafariki wengi kwa mda mchache.

Hivi unafikiri hili gonjwa lingekuwa nchi za Afrika tu leo hii tungekuwa na chanjo?
 
Askofu Gwajima alitoa hoja nzito na anaendelea kutoa hoja nzito.

Akina Kigwangala na wenzake wanakuja na hoja nyepesi. Wengine wanakuja na hoja za kitoto eti Gwajima afukuzwe oh! Auliwe. Ni upuuzi.

1. Hoja ya kwanza kwanini chanjo zingine hazina fomu ya kujaza. Lakini chanjo ya korona unajaza fomu!?

2. Serikali ilisema ni hiari, kwanini sasa wanalazimisha watu kuchanja!?

3. Ni effects zipi za muda mfupi na muda mrefu zitakazotokea baada ya kuchanjwa!?

4. Hizi chanjo hazizuii korona mpaka uchanje mara kibao.

MIMI NITASIMAMA NA GWAJIMA.
Utapoteza muda unamjibu Askofu mpiga miti?
20210731_213506.jpg
 
Huyo yunus mgaya katengeneza ipi mpaka apinge za watu au ndio yale ma juice walioamua kutumia short cut na kuungana na akina matunge kutulisha malimao na mapilipili na kuyaita COVIDOL?

Maajabu ni kwamba hayo “malimao na mapilipili “(naomba niongeze matangawizi na mavitunguu maji + swaum) yamekukuza na leo uko na kibesi!!!

Life is just too funny!

Whoever said God is a Comedian, give them a medal!!!
 
Tafiti ngapi zimefanywa na nchi zetu kabla ya kukubali hizi chanjo?

Let's say hata kufanya test ndogo tu ya mtu mwenye chanjo na kumuweka karibu na mgonjwa wa Corona ili kujua Kinga hyo inafanya kazi vipi tumeshindwa?

Corona anaweza kupata mtu na kupona, kwa hyo kufanya test ya mtu kukaa karibu na mgonjwa ni kitu cha kawaida kabisa kupata matokea sahihi ya chanjo.

Kupokea chanjo ambayo hujatupa taarifa vizuri na wakati huo huo Kuna nchi zimeleta madhara ni tatizo.

Lakini pia, hii chanjo imetengenezwa na nini ambacho nchi yetu imeshindwa kuomba kibali na kutengeneza ndani baada ya sisi kujiridhisha kimaabara?

Nakumbuka wakati wa JPM watu waligomea barakoa kwa sababu zilikua imported kutoka nje lakini baada ya viwanda vyetu kuanza kufyatua barakoa kwa amri yake hakuna mtu anakataa barakoa tena.

Tuna Imani na vya kwetu kuliko misaada ambayo hupewi muda wa kuifanyia tafiti.

Kwenye dunia ya sasa ya vita ya kiuchumi na kudhoofishana lolote linaweza kutokea, tusipuuze wapiga kelele.

China hawezi kupokea msaada wa kitu sensitive kama chanjo akaenda kudunga watu wake bila tafiti.

Tafiti ya hii chanjo kwa Tanzania report yake iko wapi?
 
Hoja za kiswahili hizo anasoma kwenye viblog vya udaku.

Anatakiwa kwanza asome vizuri molecular biology aijue vizuri DNA na RNA jinsi zinavyoreplicate

Anatakiwa ajifunze vizuri amuelewe VIRUS na tabia zake na hinsi anavyoweza kutumia mwili wa host kuzsliana huku akulipua seli za host

Anatakiwa ajue chanjo zinazotengenezwa na MESSENGER RNA zinafanyaje kazi. Sio kila kitu kujifanya anajua wakati hajui na hawezi kujua tatizo kapata waumini mazezeta wanashangilia tu maujinga anayoongea
Naona sehemu kubwa anaongea kwa mihemko tu. Yeye si mwanasayansi
 
Consent form....

GWAJIMA anaulizia consent form....

Inaonekana hana mtu wa karibu aliyewahi kupelekwa CHUMBA CHA UPASIAJI....pia iko hiyo "consent form"....anajaza mgonjwa Mwenyewe na ikishindikana wanajaza watu wake wa karibu.....

Na hili pia ALIHOJI.....

Chanjo hizi ni mpya.....hazina muda mrefu toka ZIZINDULIWE....

Gwajima hebu afunge macho na kufikiri ,TB na magonjwa mengine ya mlipuko yalipokuwa yanatokea na chanjo kuanza kutolewa je "KIPINDI HICHO" nako kulikuwa na "consent forms" pale ilipotolewa kwa JAMII(massive vaccination)?!!!

Kipindi hicho kulikuwepo na haya MAENDELEO MAKUBWA ya HAKI ZA BINADAMU na kuheshimu mawazo ya WAGONJWA (informed consent) ?!!

Anyway ,Gwajima anataka TUUACHE UGONJWA KWA MIAKA 10 bila ya chanjo yoyote na wataokufa wafe na watakaobaki WAENDELEE kuishi(natural selection) ?!!![emoji44][emoji44]

Aakofu Gwajima amekuwa "CHARLES DARWIN"?!!

#TujitokezeKuchanjwa
#ChanjoNiBoraKulikoTiba
#SiempreJMT
#KaziInaendelea
Atafiti maandiko kutoka wanasayansi. Kuna tafiti zimefanyika kutokana na gonjwa lenye tabia kama za kkrona. Asome pia jinsi dawa inavyoingia na kufanya kazi.
 
Haya tueleze wewe basi mtaalamu wa hiyo sijui molecular biology!!

Shida ya madaktari uchwara wa bongo ni kujitia ujuaji mwiiiingii.... kukariri kariri tu hovyooo... oohhh molecular biology, ascomycetes thrombosis....

TENGENEZA CHANJO, acha uhuni.

Hayo mamisamiati hata mimi naweza kukariri. THROMBOCYTES SALMONELLA sijui nini.... blah blah...

We need results, sio hayo matakataka ya misamiati ya kigiriki.
Wake up Aficans. Tuache lawama
 
Nondo za Gwajiboy wamezishindwa

Gwajima amehoji hoja za msingi sana haikufaa kumpiga biti ili kutetea ugali walifaa kujibu kwa hoja.

Fundamental questions:
1. Nikichanjwa naacha kuvaa barakoa?
WHO: Lazima uvae

2. Nikichanjwa sitaambukizwa?
WHO: Unaweza kuambukizwa

3. Nikichanjwa siwezi kuugua?
WHO: Utaugua

4. Nikichanjwa siwezi kufa?
WHO: Unaweza kufa

5. Nikichanjwa ikija Corona ya design nyingine siwezi ambukizwa?
WHO: Unaweza kuambukizwa.

Sasa Gwajima anahoji hii chanjo tunachanja ya nini???

Hili swali ndo inatakiwa wamjibu kwa niaba ya watanzania badala ya kumpiga biti.

Hoja hushindwa na hoja.
 
Public health personnel? Kwani wao wanatengeneza chanjo? Gwajima ameifanya kazi ya Mungu ya kueleza ukweli! Hoja kuu mbili za Gwajima pamoja na wanasayansi wote duniani wanaojitambua hizijibiki kabisa kwa sasa kwa sababu huwa zinajibiwa pale tu mtiririko wahatua za kutengeneza chanjo salama na bora zinazofuata! Salama kwa maana leo na baadae! Na bora kwa maana ya kukinga ugonjwa na maambukizi husika! Sasa hizi chanjo zote zinazochanjwa kwa covid-19 zimeshajipambanua kuwa na madhara ya muda mfupi na hatujui ya muda wa baadae maana hiyo inasubiri matokeo ya panya binadamu waliochanjwa! Hivyo kwenye usalama kuna sintofahamu nyingi sana! Kwenye ubora napo zimeshindwa kuzuia maambukizi na ugojwa kuwapata waliochanjwa na hivyo ubora wake kutiliwa shaka! Hii imetokana na kujibadiribadiri kwa kirusi chenyewe! Kwa majumuisho kwa mtazamo wangu na wanasayansi wote duniani wanaojitambua, covax siyo salama na pia siyo bora!
Gwajima pamoja na kuwa ni msomaji na mfuatiliaji wa mambo mzuri, anapata consultation za kitaalamu na hivyo kumfanya kustahili kuhoji kama anavyoendelea kuhoji!
Mkuu, taratibu ndugu yangu. Gwajima huyuhuyu aliyekuwa anahusisha 5G Network na Covid ndio hero wako? Really? Huyu Mchungaji, ambae amegeuka mwanasiasa na ambae akiumwa leo anahudumiwa na Bima ya Serikali? Huyu ndie unamuamini kwamba maelezo yake kuhusu madhara ya Covid 19 Yana make sense kuliko wanasayansi bingwa duniani? Pengine wewe ni mfuasi wa kanisa lake ndio maana unamigia tarumbeta.

Pamoja na elimu yangu ndogo niliyonayo, kamwe Gwajima hawezi kuwa source of information kuhusu haya maradhi. Hata kidogo. Kama angekuwa anaamini anachikisema, angejiondoa CCM ili aendeleze mapambano yake dhidi ya corona. Lakini namuona ameanza kubadilisha kauli zake. Anapenda attention na power. Hana lolote

Hakuna dawa isiyokuwa na madhara. Tumekunywa sana Cloroquine hapo zamani kutibu Malaria. Wengi tulipona, lakini wapo wachache ambao walifariki au kuwa vichaa as side effects. Wengine waliwashwa mwili mzima mpaka wanatia huruma. Waulize watu wanaotibiwa Cancer kwa kutumia chemotherapy watakueleza madhara yake. Kuwashauri watu kwamba afadhali ufe kwa corona kuliko kuchanjwa sio ubinadamu hata kidogo. Haswa ushauri huo unapotolewa na mtu mwenye uwezo kama Gwajima.

Binafsi simuhitaji mhubiri na mpenda sifa kama Gwajima kuamua kama ntachanjwa au la. Ninachojuwa ni kwamba Corona ipo na imeua watu wengi sana. Dada yangu anafanyakazi kwenye nyumba za kuhudumia wazee huko Canada. Ananiambia kwamba kati ya mwezi March na August mwaka Jana, zaidi ya wazee elfu 10 walifariki kwa Corona. Mortuary ziliishiwa na nafasi kutokana na wingi wa vifo.

Chanzo zilipofika wakaanzwa hao wazee (the most vulnerable). Sasa hivi vifo vimepungua kwa asilimia 99. Upo uwezekano mkubwa kwamba chanjo za corona zikawa na madhara, lakini ni dhahiri kwamba hii chanjo inatibu.

Gwajima Hana tofauti na wale masheikh njaa kule Nigeria waliokuwa wanawahamasisha waumini wao kuwadhuru manesi waliokuwa wanaenda vijijini kutoa chanjo ya Polio. Bahati nzuri, Dola (Central Government) ya Tanzania ipo imara.
 
Back
Top Bottom