#COVID19 Hoja za Askofu Gwajima wameshindwa kuzijibu

Mzee summarize. Ongea kwa bullet points. You are using too much energy
 
Hoja mamba 5: Hazard pay hio.

Namba 6: Wasanii wanatumika kutokana na dharula ya ugonjwa wenyewe. Wana ushawishi kwa jamii; mbona tunawatumia kwenye promotion kama za kukomesha malaria?

Namba 7: Nguvu inatokana na dharula ya ugonjwa. Wangapi unataka wafariki?

Namba 8: Magufuli alipinga chanjo, Mama Samia anaunga mkono chanjo. Hio ndio sababu ya chanjo kupata nguvu.

Namba 9: ugonjwa ulikuwepo wakati wa Magufuli lakini alikataza kuripotiwa.

Namba: 10 Msimamo upi? Mara ngapi Mama kasema kwamba gonjwa lipo tuchukue tahadhali na tume iliundwa kufanya utafiti zaidi .
 
Mbona daktari akiniandikia panadol au akitaka kunipima maralia huwa hamna sehemu naweka saini ?🤣🤸🐒
 
C-19 haina udharura wowote,it is a plandemic,not a pandemic.Magomjwa ya Moyo,Cancers,Sukari etc.
yanaua watu zaidi,danganyeni wengine sio mimi.Infact it is non existent.Matatizo ni mengine,wanasingizia Corona.Mr.Global ni mshenzi sana.Kweli nimeamini wajinga ndio waliwao.

Kwanza utachanjaje watu vaccine ambayo ni ya majaribio,ni ajabu sana.Hivi Watanzania tumekuwa mazuzu kiasi hicho,eti chanjo iliyokuwa developed in 18 months tunawachanja watu wetu!Ni uzuzu wa kupindukia huu frankly dah,inauma sana.
 
Mkuu naona unachanganya madesa, consent form ya kwenye upasuaji na ya chanjo ni wapi na wapi unaulizwa kuhusu chanjo na hakuna chanjo ambayo anachanjwa binadamua anaambiwa ajaze consent form, jibuni hoja hayo mambo ya kusema sijui chanjo ya TB hatukuuliza kwani chanjo ya TB ilitengenezwa na kufanyia majaribiok kwa miezi sita?
 
Magonjwa ya moyo na kisukari yanatokana na life style ya mtu ukitoa kisukari type 1. Je ni magonjwa ya mlipuko kama COVID-19?

Tunajua nini cha kufanya kuepukana na magonjwa ya moyo na kisukari type 2. Kama nina ugonjwa wa moyo, kisukari au cancer nikimtembelea mtu si wezi ku muambukiza.

Chanjo walioitengeneza ndio walio anza kuitumia kwa watu wao kutokana na watu waliofariki kwa mda mchache. Ndio imetengenezwa kwa mda mfupi kutokana na watu walikuwa wanafariki wengi kwa mda mchache.

Hivi unafikiri hili gonjwa lingekuwa nchi za Afrika tu leo hii tungekuwa na chanjo?
 
Utapoteza muda unamjibu Askofu mpiga miti?
 
Huyo yunus mgaya katengeneza ipi mpaka apinge za watu au ndio yale ma juice walioamua kutumia short cut na kuungana na akina matunge kutulisha malimao na mapilipili na kuyaita COVIDOL?

Maajabu ni kwamba hayo “malimao na mapilipili “(naomba niongeze matangawizi na mavitunguu maji + swaum) yamekukuza na leo uko na kibesi!!!

Life is just too funny!

Whoever said God is a Comedian, give them a medal!!!
 
Tafiti ngapi zimefanywa na nchi zetu kabla ya kukubali hizi chanjo?

Let's say hata kufanya test ndogo tu ya mtu mwenye chanjo na kumuweka karibu na mgonjwa wa Corona ili kujua Kinga hyo inafanya kazi vipi tumeshindwa?

Corona anaweza kupata mtu na kupona, kwa hyo kufanya test ya mtu kukaa karibu na mgonjwa ni kitu cha kawaida kabisa kupata matokea sahihi ya chanjo.

Kupokea chanjo ambayo hujatupa taarifa vizuri na wakati huo huo Kuna nchi zimeleta madhara ni tatizo.

Lakini pia, hii chanjo imetengenezwa na nini ambacho nchi yetu imeshindwa kuomba kibali na kutengeneza ndani baada ya sisi kujiridhisha kimaabara?

Nakumbuka wakati wa JPM watu waligomea barakoa kwa sababu zilikua imported kutoka nje lakini baada ya viwanda vyetu kuanza kufyatua barakoa kwa amri yake hakuna mtu anakataa barakoa tena.

Tuna Imani na vya kwetu kuliko misaada ambayo hupewi muda wa kuifanyia tafiti.

Kwenye dunia ya sasa ya vita ya kiuchumi na kudhoofishana lolote linaweza kutokea, tusipuuze wapiga kelele.

China hawezi kupokea msaada wa kitu sensitive kama chanjo akaenda kudunga watu wake bila tafiti.

Tafiti ya hii chanjo kwa Tanzania report yake iko wapi?
 
Naona sehemu kubwa anaongea kwa mihemko tu. Yeye si mwanasayansi
 
Atafiti maandiko kutoka wanasayansi. Kuna tafiti zimefanyika kutokana na gonjwa lenye tabia kama za kkrona. Asome pia jinsi dawa inavyoingia na kufanya kazi.
 
Wake up Aficans. Tuache lawama
 
Nondo za Gwajiboy wamezishindwa

Gwajima amehoji hoja za msingi sana haikufaa kumpiga biti ili kutetea ugali walifaa kujibu kwa hoja.

Fundamental questions:
1. Nikichanjwa naacha kuvaa barakoa?
WHO: Lazima uvae

2. Nikichanjwa sitaambukizwa?
WHO: Unaweza kuambukizwa

3. Nikichanjwa siwezi kuugua?
WHO: Utaugua

4. Nikichanjwa siwezi kufa?
WHO: Unaweza kufa

5. Nikichanjwa ikija Corona ya design nyingine siwezi ambukizwa?
WHO: Unaweza kuambukizwa.

Sasa Gwajima anahoji hii chanjo tunachanja ya nini???

Hili swali ndo inatakiwa wamjibu kwa niaba ya watanzania badala ya kumpiga biti.

Hoja hushindwa na hoja.
 
Mkuu, taratibu ndugu yangu. Gwajima huyuhuyu aliyekuwa anahusisha 5G Network na Covid ndio hero wako? Really? Huyu Mchungaji, ambae amegeuka mwanasiasa na ambae akiumwa leo anahudumiwa na Bima ya Serikali? Huyu ndie unamuamini kwamba maelezo yake kuhusu madhara ya Covid 19 Yana make sense kuliko wanasayansi bingwa duniani? Pengine wewe ni mfuasi wa kanisa lake ndio maana unamigia tarumbeta.

Pamoja na elimu yangu ndogo niliyonayo, kamwe Gwajima hawezi kuwa source of information kuhusu haya maradhi. Hata kidogo. Kama angekuwa anaamini anachikisema, angejiondoa CCM ili aendeleze mapambano yake dhidi ya corona. Lakini namuona ameanza kubadilisha kauli zake. Anapenda attention na power. Hana lolote

Hakuna dawa isiyokuwa na madhara. Tumekunywa sana Cloroquine hapo zamani kutibu Malaria. Wengi tulipona, lakini wapo wachache ambao walifariki au kuwa vichaa as side effects. Wengine waliwashwa mwili mzima mpaka wanatia huruma. Waulize watu wanaotibiwa Cancer kwa kutumia chemotherapy watakueleza madhara yake. Kuwashauri watu kwamba afadhali ufe kwa corona kuliko kuchanjwa sio ubinadamu hata kidogo. Haswa ushauri huo unapotolewa na mtu mwenye uwezo kama Gwajima.

Binafsi simuhitaji mhubiri na mpenda sifa kama Gwajima kuamua kama ntachanjwa au la. Ninachojuwa ni kwamba Corona ipo na imeua watu wengi sana. Dada yangu anafanyakazi kwenye nyumba za kuhudumia wazee huko Canada. Ananiambia kwamba kati ya mwezi March na August mwaka Jana, zaidi ya wazee elfu 10 walifariki kwa Corona. Mortuary ziliishiwa na nafasi kutokana na wingi wa vifo.

Chanzo zilipofika wakaanzwa hao wazee (the most vulnerable). Sasa hivi vifo vimepungua kwa asilimia 99. Upo uwezekano mkubwa kwamba chanjo za corona zikawa na madhara, lakini ni dhahiri kwamba hii chanjo inatibu.

Gwajima Hana tofauti na wale masheikh njaa kule Nigeria waliokuwa wanawahamasisha waumini wao kuwadhuru manesi waliokuwa wanaenda vijijini kutoa chanjo ya Polio. Bahati nzuri, Dola (Central Government) ya Tanzania ipo imara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…