Hongera Diamond kwa kununua ndege na helicopter. Wasafi Airlines itazalisha ajira

Hongera Diamond kwa kununua ndege na helicopter. Wasafi Airlines itazalisha ajira

Kaa hapo hapo utazame show ya mtoto wa Tandale. Si mlisema hawezi nunua ndege sasa kaleta ndege na helicopter mbili na huu ni mwanzo tu.

Chakufanya mkuu edit CV yako yenye GPA first class nikuconnect ukale shavu kwa Chibu. Hasira hazijawai kuwa dawa.
We mwenyewe huna ajira, andaa CV yako niku connect ukaogeshe wazee america
 
Natoa pongezi kwa msanii namba moja Afrika kwa sasa Diamond Platnumz kwa kununua vyombo vya anga. Biashara yake mpya anayokuja nayo ya Wasafi airlines itafungua milango ya ajira nyingi sana Tanzania na duniani kwa ujumla.

Watu tutaacha kupanda emirates na klm tutaanza kupanda ndege za kijana wa Tandale. Nitoe wito kwa vijana majobless kuanza kuandaa CV badala ya kushinda mnatukana mafanikio ya tajiri huyu mwenye umri kama wenu.

Hii biashara itaenda kuajiri marubani, hostess mpaka mainjinia mlio na madegree. Ili ni somo kwa vijana tuendelee kupambana kuzifikia ndoto zetu na tuheshimu talent. Hakuna kinachoshindikana. Hasira za kuyakosea maisha kuzishushia kwa Diamond wala sio dawa ya kutusogeza kimaisha.

Kwa biashara zote anauwezo wa kuzianzisha lakini hapa kwenye usafiri wa anga hananuwezo huo, huku ni maji marefu munoooo!!!
 
Ila raha sana kutimiza ndoto na kutimiza kila unachotaka 😀😀😀 kula ma pisi yote makali ambayo ulikuwa unaya admire
Eeh sahizi jamaa yuko kwenye ile level ambayo kiuchumi tunaita economic freedom.

Anaweza lipa Air Tanzania izunguke angani wakati anafanya birthday party yake hata kwa masaa kadhaa 😂😂😂! Ni burudani ilioje hela inaingia kila sekunde kila dakika kila saa deals zinaingiza mtonyo.

Bado investments kibao Wasafi bet, Wasafi Tv, Wasafi Fm, Online Streaming yani mihela ni back to back inaingia. Branding ndio kila kitu biasharani.
 
Sasa ndege moja ndio itaanzisha Airlines😂😂😂 hebu acheni upuuzi jamani. Hio ndege yeye auzie sura tu basi inatosha
Boss, sijawahi kuwa mshabiki wa maigizo ya maisha ya hawa waitwao "maarufu wetu"

Kweli akanunue helicopter ilhali hana pa kulala?
 
Zamani humu jamiiforums miaka ya 2013-14 kulikuwa na kifesi(yule mpiga pich wa zamani wa Diamond) aisee alikuwa anadondosha mapambio humu kwa diamond sijui siku hizi yupo wapi siku hizi,huyu tulikuwa tunajua ana maslahi na WCB sijui kwa mleta mada,halafu kule upande mwingine wa king alikuwepo mtu anaitwa shadcole na yeye alikuwa mpiga mapambio wa Kiba sijui kafia wapi na yeye,Dar es salaam vijana huwa hawana kazi kabisa aisee
 
Eeh sahizi jamaa yuko kwenye ile level ambayo kiuchumi tunaita economic freedom.

Anaweza lipa Air Tanzania izunguke angani wakati anafanya birthday party yake hata kwa masaa kadhaa 😂😂😂! Ni burudani ilioje hela inaingia kila sekunde kila dakika kila saa deals zinaingiza mtonyo.

Bado investments kibao Wasafi bet, Wasafi Tv, Wasafi Fm, Online Streaming yani mihela ni back to back inaingia. Branding ndio kila kitu biasharani.
Narudia tena kote huko ni sawa anauwezo nako, lakini kwenye hili jitu linaloitwa usafiri wa anga ni jitu jingine!!hana uwezo nako kabisa!!halafu unaweza kukuta BABA LEVO, na yule mzee wa za ndaniii, ndio wanamwambia jilipue tu sisi ndio ma CEO'S wako!!etihad, emirates, klm , athiopian, waweze sisi lazima tutoboe tu!!
 
Natoa pongezi kwa msanii namba moja Afrika kwa sasa Diamond Platnumz kwa kununua vyombo vya anga. Biashara yake mpya anayokuja nayo ya Wasafi airlines itafungua milango ya ajira nyingi sana Tanzania na duniani kwa ujumla.

Watu tutaacha kupanda emirates na klm tutaanza kupanda ndege za kijana wa Tandale. Nitoe wito kwa vijana majobless kuanza kuandaa CV badala ya kushinda mnatukana mafanikio ya tajiri huyu mwenye umri kama wenu.

Hii biashara itaenda kuajiri marubani, hostess mpaka mainjinia mlio na madegree. Ili ni somo kwa vijana tuendelee kupambana kuzifikia ndoto zetu na tuheshimu talent. Hakuna kinachoshindikana. Hasira za kuyakosea maisha kuzishushia kwa Diamond wala sio dawa ya kutusogeza kimaisha.

Anafanya vzr,hatuna wivu nae,lakini wapo ma injinia wenye mpunga mrefu,wasafi wanasubili,
Mmiriki wa molel electrical,ndie anaemiriki majengo zilipo ofc za voda na Tigo,ndie mwenye kiwanda Cha kutengeneza nguzo za zege,
Mond utajiri wake ni bilioni 23.3!!
Molel electrical ana mara kumi ya hizo,
Je umemsikia Yule kijana wa Tanzania,asimwe kabunga aliyewekeza bilioni 90+!,kwenye kiwanda Cha madini!!?
Wasomi wapo wengi tu wenye pesa ndefu,
Avumae baharini ni papa,lakini wengine wapo,Umemsikia Fernandes wa NARA?
Je Yule kijana anayemiriki kampuni ya IT,iliyoajiri CEO kutoka Kenya?
Usisahau mmiriki wa huu mtandao,JF,ni msomi sana,Tena injinia,
Kwa kijana kutoka "tandale"kutoka kwenye maisha ni long game,acha kabisa, wako wapi Juma nature,dudu bata,tmk wanaume,Marrow,Mr nice,twenty percent,YP na Ydash,sister P,Rah P,ZeY B,
Ila kwa msomi,unakuwa umepewa ngazi ya kuanzia.
 
Back
Top Bottom