Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa

Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa

Mimi nampongeza sana Mbowe kwa kumsifu Mama Samia kwenye mkutano wa chama chake. Jana ni kwa mara ya kwanza Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani kumsifia mwenyekiti wa chama tawala kwenye jukwaa la chama chake. Mbowe anaungana na hayati Mrema kwenye rekodi za wenyeviti wa upinzani waliowahi kumsifu mwenyekiti wa CCM hadharani. Ikumbukwe kwenye uchaguzi wa 2020, Hayati Lyatonga alimsapoti Hayati Magufuli. Tofauti ya Mbowe ni kuanza kumsapoti Mama Samia kabla ya uchaguzi 2025.
 
9
Mambo yote huwa ayapatikani kwa wakati mmoja, kama kuna juhudi hata kidogo za kutufikisha huko tusizibeze. Tuonyeshe sapoti. Sasa nyie mnaobeza mna taka nini? Njooni na suluhisho sio kubeza tu
Tatizo huwa mnatawaliwa na mihemko! Je, wakati wa JK kwanini ilikwama? Katiba Mpya huwa haitayarishwi na wawania madaraka! Maoni yangu ni kuwa Tusubiri hadi Samia wakati Anang’atuka siyo wakati akitegemea kuwania madaraka!
 
Sasa turudi katika hoja kwanini Mbowe jana kashinda mchezo wa kisiasa?

Wananchi wamejibu hoja hii nzito mjini Musoma leo na tutaendelea kufuatilia ujio huu mpya wa siasa za ushindani wa vyama vya siasa na mapokeo yake nchi nzima wakati CHADEMA ikizunguka nchi kusalimia baada ya kifungo haramu cha kufanya siasa kwa takribani miaka 7 kutenguliwa


22 January 2023
Musoma, Tanzania

LIVE: Mkutano wa CHADEMA Musoma uwanja wa Mkendo



Source : The Chanzo

N.B
TAKWIMU muhimu kuhusu mji wa Musoma mkoani Mara nchini Tanzania :
Idadi ya Watu = 134327 soma zaidi Source : Takwimu
 
Tatizo huwa mnatawaliwa na mihemko! Je, wakati wa JK kwanini ilikwama? Katiba Mpya huwa haitayarishwi na wawania madaraka! Maoni yangu ni kuwa Tusubiri hadi Samia wakati Anang’atuka siyo wakati akitegemea kuwania madaraka!
Kwahiyo ushauri wako unataka kwasasa tukae kimya tusubili mpaka Samia hatakapokuwa hana nia ya kugombea urais?
 
Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa.

Kwa masaa 24 nimekuwa nikierejea Hotuba ya Mh Mbowe ya jana pale Mwanza na nimekuwa nikisikiliza mapokeo ya watu nje na ndani ya Chama katika mitazamo tofautitofauti, Wengi tumeelewa na tulitarajia hotuba kama hii, lakini wapo ambao hawajang'amua hasa wale ambao kwa muda mrefu hawakubaliani na maridhiano, wanaamini Mbowe kakosea vile walivyotarajia iwe pale jukwaani. Walitaraji waone hotuba ya kimapambano ya kimnyukano nk.

Naomba nichukue fursa hii kusema Hotuba ya jana ilikuwa ni kete ya mwisho na ya hatari katika game la kisiasa Chadema vs CCM+Serikali katika mechi iliyoanza tangu Mbowe atoke jela 4 March 2022. Mbowe ameshinda!

Tangu tarehe 4 March 2022, Chadema ilianza game ya kisiasa mezani na ccm na serikali, Mbowe akiwa ameongoza upinzani akiwa na mambo kadhaa mkononi, Moja watu wetu (wanachadema) wote waliokuwa na kesi mahakamani waachiwe huru. Pili waliokuwa jela waachiwe bila masharti. Tatu haki kwa wanachama na watanzania wote waliodhuriwa na kuathiriwa katika utawala uliopita wapewa haki zao. Nne Watu wetu/wanachama walioko uhamishoni wahakikishiwe usalama warudi nchini. Tano mikutano ya hadhara iruhusiwe kwakuondolewa lile katazo haramu. Sita Katiba Mpya na Tume huru, Saba sheria mbovu za vyama vya siasa zirekebishwe/zifutwe. Nane sheria ya vyombo vya habari na sheria za mitandao zirekebishwe (uhuru wa habari). Tisa Usalama wa viongozi wa kisiasa, na Kumi ni kuondolewa Bungeni wabunge haramu (COVID19).

Sasa turudi katika hoja kwanini Mbowe jana kashinda mchezo wa kisiasa? Kwanza ifahamike maridhiano bado yanaendelea na yako katika sehemu muhimu sana sana na yatahadhari, hivyo pande zote mbili Chadema na CCM kila mtu anapokuwa jukwaani au popote anazungumza kwa tahadhari kubwa ili kutovuruga mazungumzo yanayoendelea. Katika Mazungumzo yanayoendelea, Mbowe tayari mambo muhimu 7 katika ya 10 amefanikiwa kushinda katika meza ya mazungumzo, Wanachadema wameachiwa magerezani, Haki za Lissu zimepatikani (matibabu na Usalama wake), Mikutano ya kisiasa imerejeshwa, Wanachadema waliokuwa magerezani wameachiwa, nk. Huu ni ushindi mkubwa kwa Mbowe, Lakini isingempa room ya kurejea kwenye siasa ngumu za mapambano wakati bado mambo makubwa ya kinchi hajashinda, Katiba Mpya na Tume Huru bado yako katika mazungumzo na Rais ameshaonyesha utayari wa kuanza mchakato. Hivyo tamko lololete la kimapambano jana lingevuruga maridhiano yote.

Mchezo wa jana ulikuwa ni defragmenting kwa wale wahafidhina kwanza, na kumfanya mkuu wa nchi awe confirmable na meza ya mazungumzo, katika hilo Mbowe ameshinda, Upande wa ccm wasiopenda maridhiano walitamani sana Mbowe aipige ampige kwelikweli Rais hali ambayo kwao ingekuwa ahueni na mwanya wao kisiasa kuelekea 2025, Hilo limewauma maana Mbowe amewakwepa, Upande wa Chadema wale wasiokubaliana na Maridhiano walitaraji Mbowe aipige sana serikali wakiamini uasili wa Chadema, imekuwa tofauti, Chadema iko kwenye mazungumzo kauli yoyote ya kiongozi wa Maridhiano yenye kuuumiza upande wa maridhiano ingevuruga, Hatutaki tuishie kupata mikutano ya hadhara tu, tunataka kupata Katiba Mpya na Tume huru, hilo ndio lengo mahsusi la Chadema. Diplomatic language imeshinda jana.

Kwavyovyote vile Hata keshokutwa Hotuba ya Lissu akirejea Tanzania itakuwa ya kidiplomasia yenye kupalilia mazungumzo yanayoendelea, tofauti na wahafidhina wanaojaribu kupandikiza chuki ili kuvuruga maridhiano haya. Ni Wazi, Mbowe karata zake katika meza ya maridhiano zimechangwa vizuri na ameokota kete muhimu. Kitu muhimu tunachotakiwa kukielewa Watanzania wote hasa Wanachadema na Wanaccm, Matokeo ya Maridhiano hubadili sura na aina ya siasa. Baada ya maridhiano Chadema na CCM hatutafanya siasa kama za miaka 10 nyuma, tutakuwa na aina mpya ya siasa. Na haya ndio mapokeo sahihi.

Hongera Mbowe, Karibu Lissu. Chadema kupitia nyinyi tutapata Katiba Mpya bila kumwaga Damu bali kupitia njia hii nzuri ya Maridhiano.

Na Yericko Nyerere.
View attachment 2491265
Umeweka vizuri mambo, hongera kwa Chadema na mwenyekiti Mbowe!
 
Mbowe amefundishwa na Magufuli kwa vitendo kuwa dunia ya leo haihitaji siasa za matusi lest utapambana na mkono halisi wa dola. Kongole kwake.
 
Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa.

Kwa masaa 24 nimekuwa nikierejea Hotuba ya Mh Mbowe ya jana pale Mwanza na nimekuwa nikisikiliza mapokeo ya watu nje na ndani ya Chama katika mitazamo tofautitofauti, Wengi tumeelewa na tulitarajia hotuba kama hii, lakini wapo ambao hawajang'amua hasa wale ambao kwa muda mrefu hawakubaliani na maridhiano, wanaamini Mbowe kakosea vile walivyotarajia iwe pale jukwaani. Walitaraji waone hotuba ya kimapambano ya kimnyukano nk.

Naomba nichukue fursa hii kusema Hotuba ya jana ilikuwa ni kete ya mwisho na ya hatari katika game la kisiasa Chadema vs CCM+Serikali katika mechi iliyoanza tangu Mbowe atoke jela 4 March 2022. Mbowe ameshinda!

Tangu tarehe 4 March 2022, Chadema ilianza game ya kisiasa mezani na ccm na serikali, Mbowe akiwa ameongoza upinzani akiwa na mambo kadhaa mkononi, Moja watu wetu (wanachadema) wote waliokuwa na kesi mahakamani waachiwe huru. Pili waliokuwa jela waachiwe bila masharti. Tatu haki kwa wanachama na watanzania wote waliodhuriwa na kuathiriwa katika utawala uliopita wapewa haki zao. Nne Watu wetu/wanachama walioko uhamishoni wahakikishiwe usalama warudi nchini. Tano mikutano ya hadhara iruhusiwe kwakuondolewa lile katazo haramu. Sita Katiba Mpya na Tume huru, Saba sheria mbovu za vyama vya siasa zirekebishwe/zifutwe. Nane sheria ya vyombo vya habari na sheria za mitandao zirekebishwe (uhuru wa habari). Tisa Usalama wa viongozi wa kisiasa, na Kumi ni kuondolewa Bungeni wabunge haramu (COVID19).

Sasa turudi katika hoja kwanini Mbowe jana kashinda mchezo wa kisiasa? Kwanza ifahamike maridhiano bado yanaendelea na yako katika sehemu muhimu sana sana na yatahadhari, hivyo pande zote mbili Chadema na CCM kila mtu anapokuwa jukwaani au popote anazungumza kwa tahadhari kubwa ili kutovuruga mazungumzo yanayoendelea. Katika Mazungumzo yanayoendelea, Mbowe tayari mambo muhimu 7 katika ya 10 amefanikiwa kushinda katika meza ya mazungumzo, Wanachadema wameachiwa magerezani, Haki za Lissu zimepatikani (matibabu na Usalama wake), Mikutano ya kisiasa imerejeshwa, Wanachadema waliokuwa magerezani wameachiwa, nk. Huu ni ushindi mkubwa kwa Mbowe, Lakini isingempa room ya kurejea kwenye siasa ngumu za mapambano wakati bado mambo makubwa ya kinchi hajashinda, Katiba Mpya na Tume Huru bado yako katika mazungumzo na Rais ameshaonyesha utayari wa kuanza mchakato. Hivyo tamko lololete la kimapambano jana lingevuruga maridhiano yote.

Mchezo wa jana ulikuwa ni defragmenting kwa wale wahafidhina kwanza, na kumfanya mkuu wa nchi awe confirmable na meza ya mazungumzo, katika hilo Mbowe ameshinda, Upande wa ccm wasiopenda maridhiano walitamani sana Mbowe aipige ampige kwelikweli Rais hali ambayo kwao ingekuwa ahueni na mwanya wao kisiasa kuelekea 2025, Hilo limewauma maana Mbowe amewakwepa, Upande wa Chadema wale wasiokubaliana na Maridhiano walitaraji Mbowe aipige sana serikali wakiamini uasili wa Chadema, imekuwa tofauti, Chadema iko kwenye mazungumzo kauli yoyote ya kiongozi wa Maridhiano yenye kuuumiza upande wa maridhiano ingevuruga, Hatutaki tuishie kupata mikutano ya hadhara tu, tunataka kupata Katiba Mpya na Tume huru, hilo ndio lengo mahsusi la Chadema. Diplomatic language imeshinda jana.

Kwavyovyote vile Hata keshokutwa Hotuba ya Lissu akirejea Tanzania itakuwa ya kidiplomasia yenye kupalilia mazungumzo yanayoendelea, tofauti na wahafidhina wanaojaribu kupandikiza chuki ili kuvuruga maridhiano haya. Ni Wazi, Mbowe karata zake katika meza ya maridhiano zimechangwa vizuri na ameokota kete muhimu. Kitu muhimu tunachotakiwa kukielewa Watanzania wote hasa Wanachadema na Wanaccm, Matokeo ya Maridhiano hubadili sura na aina ya siasa. Baada ya maridhiano Chadema na CCM hatutafanya siasa kama za miaka 10 nyuma, tutakuwa na aina mpya ya siasa. Na haya ndio mapokeo sahihi.

Hongera Mbowe, Karibu Lissu. Chadema kupitia nyinyi tutapata Katiba Mpya bila kumwaga Damu bali kupitia njia hii nzuri ya Maridhiano.

Na Yericko Nyerere.
View attachment 2491265


Nilisha sema Mbowe yuko strategic. Katiba mpya ndiyo lengo kuu hapa. Kuongelea bei ya mahindi na mchele ni kazi ya wengine.
 
Ukweli hata mimi mbowe sikumuelewa ila kupitia hili bandiko nimemuelewa[emoji120][emoji120]

Hata demu ukiwa unamtaka....... Katika hatua za mwanzo lazima uwe mpole ujifanye fala ili siku za mbele uje umpelekee moto vizuri[emoji1787][emoji1787]
 
Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa.

Kwa masaa 24 nimekuwa nikierejea Hotuba ya Mh Mbowe ya jana pale Mwanza na nimekuwa nikisikiliza mapokeo ya watu nje na ndani ya Chama katika mitazamo tofautitofauti, Wengi tumeelewa na tulitarajia hotuba kama hii, lakini wapo ambao hawajang'amua hasa wale ambao kwa muda mrefu hawakubaliani na maridhiano, wanaamini Mbowe kakosea vile walivyotarajia iwe pale jukwaani. Walitaraji waone hotuba ya kimapambano ya kimnyukano nk.

Naomba nichukue fursa hii kusema Hotuba ya jana ilikuwa ni kete ya mwisho na ya hatari katika game la kisiasa Chadema vs CCM+Serikali katika mechi iliyoanza tangu Mbowe atoke jela 4 March 2022. Mbowe ameshinda!

Tangu tarehe 4 March 2022, Chadema ilianza game ya kisiasa mezani na ccm na serikali, Mbowe akiwa ameongoza upinzani akiwa na mambo kadhaa mkononi, Moja watu wetu (wanachadema) wote waliokuwa na kesi mahakamani waachiwe huru. Pili waliokuwa jela waachiwe bila masharti. Tatu haki kwa wanachama na watanzania wote waliodhuriwa na kuathiriwa katika utawala uliopita wapewa haki zao. Nne Watu wetu/wanachama walioko uhamishoni wahakikishiwe usalama warudi nchini. Tano mikutano ya hadhara iruhusiwe kwakuondolewa lile katazo haramu. Sita Katiba Mpya na Tume huru, Saba sheria mbovu za vyama vya siasa zirekebishwe/zifutwe. Nane sheria ya vyombo vya habari na sheria za mitandao zirekebishwe (uhuru wa habari). Tisa Usalama wa viongozi wa kisiasa, na Kumi ni kuondolewa Bungeni wabunge haramu (COVID19).

Sasa turudi katika hoja kwanini Mbowe jana kashinda mchezo wa kisiasa? Kwanza ifahamike maridhiano bado yanaendelea na yako katika sehemu muhimu sana sana na yatahadhari, hivyo pande zote mbili Chadema na CCM kila mtu anapokuwa jukwaani au popote anazungumza kwa tahadhari kubwa ili kutovuruga mazungumzo yanayoendelea. Katika Mazungumzo yanayoendelea, Mbowe tayari mambo muhimu 7 katika ya 10 amefanikiwa kushinda katika meza ya mazungumzo, Wanachadema wameachiwa magerezani, Haki za Lissu zimepatikani (matibabu na Usalama wake), Mikutano ya kisiasa imerejeshwa, Wanachadema waliokuwa magerezani wameachiwa, nk. Huu ni ushindi mkubwa kwa Mbowe, Lakini isingempa room ya kurejea kwenye siasa ngumu za mapambano wakati bado mambo makubwa ya kinchi hajashinda, Katiba Mpya na Tume Huru bado yako katika mazungumzo na Rais ameshaonyesha utayari wa kuanza mchakato. Hivyo tamko lololete la kimapambano jana lingevuruga maridhiano yote.

Mchezo wa jana ulikuwa ni defragmenting kwa wale wahafidhina kwanza, na kumfanya mkuu wa nchi awe confirmable na meza ya mazungumzo, katika hilo Mbowe ameshinda, Upande wa ccm wasiopenda maridhiano walitamani sana Mbowe aipige ampige kwelikweli Rais hali ambayo kwao ingekuwa ahueni na mwanya wao kisiasa kuelekea 2025, Hilo limewauma maana Mbowe amewakwepa, Upande wa Chadema wale wasiokubaliana na Maridhiano walitaraji Mbowe aipige sana serikali wakiamini uasili wa Chadema, imekuwa tofauti, Chadema iko kwenye mazungumzo kauli yoyote ya kiongozi wa Maridhiano yenye kuuumiza upande wa maridhiano ingevuruga, Hatutaki tuishie kupata mikutano ya hadhara tu, tunataka kupata Katiba Mpya na Tume huru, hilo ndio lengo mahsusi la Chadema. Diplomatic language imeshinda jana.

Kwavyovyote vile Hata keshokutwa Hotuba ya Lissu akirejea Tanzania itakuwa ya kidiplomasia yenye kupalilia mazungumzo yanayoendelea, tofauti na wahafidhina wanaojaribu kupandikiza chuki ili kuvuruga maridhiano haya. Ni Wazi, Mbowe karata zake katika meza ya maridhiano zimechangwa vizuri na ameokota kete muhimu. Kitu muhimu tunachotakiwa kukielewa Watanzania wote hasa Wanachadema na Wanaccm, Matokeo ya Maridhiano hubadili sura na aina ya siasa. Baada ya maridhiano Chadema na CCM hatutafanya siasa kama za miaka 10 nyuma, tutakuwa na aina mpya ya siasa. Na haya ndio mapokeo sahihi.

Hongera Mbowe, Karibu Lissu. Chadema kupitia nyinyi tutapata Katiba Mpya bila kumwaga Damu bali kupitia njia hii nzuri ya Maridhiano.

Na Yericko Nyerere.
View attachment 2491265
Nenda kachukue posho yako kwa Sophia Mjema (Mbowe)
 
Mbowe amesoma hofu ya CCM juu y katiba mpya na kuielewa hofu na kujua namna ya kudeal nayo.

Viongozi wengi wa CCM wanahofia sana hatima yao na maslahi yao baada ya katiba mpya('ya warioba'),.Anachofanya Mbowe ni kutumia diplomatic plus compromised means ili mambo yafanikiwe.

Ndio maana kuna usiri maana jambo kubwa hakikisho la hatima ya viongozi wa CCM na maslahi yao binafsi.

Hili ni kama suala la Mandela na future ya weupe wachache,hawa makaburu wlipokubaliana sirini way forward ya maslahi yao hawakuona tena haja ya kuendelea kumshikiria Mandela ivyo uhuru ukapatikana na Mandela akawa Rais(ndio walichotaka blacks) na weupe wakabakia na nguvu za kiuchumi walizotaka.

Mbowe na baadhi ya viongozi wa upinzani wanaweza kufanikisha katiba mpya na uwepo wa tume huru n kuishia hapo tu,ni jukumu la kizazi kijacho kutumia uwepo wa katiba na tume huru kuiadhibu CCM na makundi maslahi yake kwa kuwaondoa madarakani na kusimamisha zama mpya.

Ikumbukwe kuwa Musa alianzisha safari ya kwenda Kaanani lakini yeye hakufika Kanaani ila Joshua mtu wake wa karibu ndie aliehitimisha safari hiyo.

Hongera CDM na viongozi wake lakini ni jukumu letu sasa kumalizia panapokwama ktk kuleta mabadiliko kmili ya kiutawala na ukombozi kamili wa wengi wasionacho dhidi na wachache walionacho.
 
Siasa za Kenya siyo za kulinganisha kabisa na siasa za Tanzania

Tanzania kuna vyama vyenye defined ideology while Kenya kuna magenge ya matajiri yenye wafuasi tu.

Siasa za Kenya zinajengwa kwa misingi wa ukabila while Tanzania sivyo.

Uelewa wawakenya kwenye haki za kisiasa ni mkubwa zaidi kuliko wa watanzania.

Kenya hakuna chama kinachotawala muda mrefu hivyo hakuna aliyechokwa wakati Tanzania bado wananchi wanatafuta namna ya kuiua ccm.

Yawezekana maridhiano yakampubguzia nguvu Mbowe binafsi ila siyo Chadema na Vuguvugu la mabadiliko.

Slaa alikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa wanachadema lakini aliondoka na wakasonga mbele.

Miaka 6 iliyopo hamahama ya wanasiasa imewajenga wanachadema kuamini katika njia yao na siyo wanasiasa binafsi.
Kweli !
 
Naunga mkono hoja, wengi wanaopinga maridhiano ni waoga, wanaoendekeza siasa za kuviziana, wanaishi kwa hofu, na kutojiamini,

Mbowe ameshinda mchezo, ametumia uwanja wa maridhiano kupata alichopigania, anastahili kupongezwa, ajabu wapo wahafidhina waliokariri kwao siku zote siasa ni harakati, wanamuona Mbowe amekosea..
 
Najaribu kuelewa ndugu JASUSI,

Bt ilikuwa lazima kutumia kilevi kuzisukuma kete ulizozitaja?
 
Siasa zinabadilika kulingana na mahitaji halisia, kwa kipindi kirefu siasa za kiuana harakati zimeshindikana zaidi ya watu kuumizwa kufungwa na kufilisiwa. Hata Mandela alibadili mfumo wa kukabiliana na makaburu akaanza majadiliano na kisha Nyerere akapinga akisema haamini kama makaburu watabadilika kwa majadiliaon, hakuwaamini lakini ndivyo hivyo majadiliano na diplomasia ilileta uhuru na kufunguliwa jela Mandela.
 
Back
Top Bottom