Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa

Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa

Siasa za Kenya siyo za kulinganisha kabisa na siasa za Tanzania

Tanzania kuna vyama vyenye defined ideology while Kenya kuna magenge ya matajiri yenye wafuasi tu.

Siasa za Kenya zinajengwa kwa misingi wa ukabila while Tanzania sivyo.

Uelewa wawakenya kwenye haki za kisiasa ni mkubwa zaidi kuliko wa watanzania.

Kenya hakuna chama kinachotawala muda mrefu hivyo hakuna aliyechokwa wakati Tanzania bado wananchi wanatafuta namna ya kuiua ccm.

Yawezekana maridhiano yakampubguzia nguvu Mbowe binafsi ila siyo Chadema na Vuguvugu la mabadiliko.

Slaa alikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa wanachadema lakini aliondoka na wakasonga mbele.

Miaka 6 iliyopo hamahama ya wanasiasa imewajenga wanachadema kuamini katika njia yao na siyo wanasiasa binafsi.
Very well
 
Hongera Mbowe umeshinda mchezo wa kisiasa.

Kwa masaa 24 nimekuwa nikierejea Hotuba ya Mh Mbowe ya jana pale Mwanza na nimekuwa nikisikiliza mapokeo ya watu nje na ndani ya Chama katika mitazamo tofautitofauti, Wengi tumeelewa na tulitarajia hotuba kama hii, lakini wapo ambao hawajang'amua hasa wale ambao kwa muda mrefu hawakubaliani na maridhiano, wanaamini Mbowe kakosea vile walivyotarajia iwe pale jukwaani. Walitaraji waone hotuba ya kimapambano ya kimnyukano nk.

Naomba nichukue fursa hii kusema Hotuba ya jana ilikuwa ni kete ya mwisho na ya hatari katika game la kisiasa Chadema vs CCM+Serikali katika mechi iliyoanza tangu Mbowe atoke jela 4 March 2022. Mbowe ameshinda!

Tangu tarehe 4 March 2022, Chadema ilianza game ya kisiasa mezani na ccm na serikali, Mbowe akiwa ameongoza upinzani akiwa na mambo kadhaa mkononi, Moja watu wetu (wanachadema) wote waliokuwa na kesi mahakamani waachiwe huru. Pili waliokuwa jela waachiwe bila masharti. Tatu haki kwa wanachama na watanzania wote waliodhuriwa na kuathiriwa katika utawala uliopita wapewa haki zao. Nne Watu wetu/wanachama walioko uhamishoni wahakikishiwe usalama warudi nchini. Tano mikutano ya hadhara iruhusiwe kwakuondolewa lile katazo haramu. Sita Katiba Mpya na Tume huru, Saba sheria mbovu za vyama vya siasa zirekebishwe/zifutwe. Nane sheria ya vyombo vya habari na sheria za mitandao zirekebishwe (uhuru wa habari). Tisa Usalama wa viongozi wa kisiasa, na Kumi ni kuondolewa Bungeni wabunge haramu (COVID19).

Sasa turudi katika hoja kwanini Mbowe jana kashinda mchezo wa kisiasa? Kwanza ifahamike maridhiano bado yanaendelea na yako katika sehemu muhimu sana sana na yatahadhari, hivyo pande zote mbili Chadema na CCM kila mtu anapokuwa jukwaani au popote anazungumza kwa tahadhari kubwa ili kutovuruga mazungumzo yanayoendelea. Katika Mazungumzo yanayoendelea, Mbowe tayari mambo muhimu 7 katika ya 10 amefanikiwa kushinda katika meza ya mazungumzo, Wanachadema wameachiwa magerezani, Haki za Lissu zimepatikani (matibabu na Usalama wake), Mikutano ya kisiasa imerejeshwa, Wanachadema waliokuwa magerezani wameachiwa, nk. Huu ni ushindi mkubwa kwa Mbowe, Lakini isingempa room ya kurejea kwenye siasa ngumu za mapambano wakati bado mambo makubwa ya kinchi hajashinda, Katiba Mpya na Tume Huru bado yako katika mazungumzo na Rais ameshaonyesha utayari wa kuanza mchakato. Hivyo tamko lololete la kimapambano jana lingevuruga maridhiano yote.

Mchezo wa jana ulikuwa ni defragmenting kwa wale wahafidhina kwanza, na kumfanya mkuu wa nchi awe confirmable na meza ya mazungumzo, katika hilo Mbowe ameshinda, Upande wa ccm wasiopenda maridhiano walitamani sana Mbowe aipige ampige kwelikweli Rais hali ambayo kwao ingekuwa ahueni na mwanya wao kisiasa kuelekea 2025, Hilo limewauma maana Mbowe amewakwepa, Upande wa Chadema wale wasiokubaliana na Maridhiano walitaraji Mbowe aipige sana serikali wakiamini uasili wa Chadema, imekuwa tofauti, Chadema iko kwenye mazungumzo kauli yoyote ya kiongozi wa Maridhiano yenye kuuumiza upande wa maridhiano ingevuruga, Hatutaki tuishie kupata mikutano ya hadhara tu, tunataka kupata Katiba Mpya na Tume huru, hilo ndio lengo mahsusi la Chadema. Diplomatic language imeshinda jana.

Kwavyovyote vile Hata keshokutwa Hotuba ya Lissu akirejea Tanzania itakuwa ya kidiplomasia yenye kupalilia mazungumzo yanayoendelea, tofauti na wahafidhina wanaojaribu kupandikiza chuki ili kuvuruga maridhiano haya. Ni Wazi, Mbowe karata zake katika meza ya maridhiano zimechangwa vizuri na ameokota kete muhimu. Kitu muhimu tunachotakiwa kukielewa Watanzania wote hasa Wanachadema na Wanaccm, Matokeo ya Maridhiano hubadili sura na aina ya siasa. Baada ya maridhiano Chadema na CCM hatutafanya siasa kama za miaka 10 nyuma, tutakuwa na aina mpya ya siasa. Na haya ndio mapokeo sahihi.

Hongera Mbowe, Karibu Lissu. Chadema kupitia nyinyi tutapata Katiba Mpya bila kumwaga Damu bali kupitia njia hii nzuri ya Maridhiano.

Na Yericko Nyerere.
View attachment 2491265
Watu hatumkosoi kuhusu maridhiano. Tunamkosoa kwa kuwachinjia baharini viongozi wenzake. Alizungumzia zaidi yeye kuambiwa amelamba asali kuliko mafanikio ya maridhiano. Hapo ndipo alipotukwaza wengine.

Amandla...
 
Kumbe hadi CDM kuna chawa? Yericko Nyerere .

Mengine muwe mnaiacha tu yanapita. Ni ngumu sana Mbowe kuendelea kuaminiwa Tena. Nami nahisi Mbowe amechoka na sio yule nilio mzoea. Sasa anatafuta ugali wa wanae kwa njia nyingine anaona njia ya Ikulu ngumu.
 
Uhalisia unakataa. Maridhiano hayo yataidhoofisha CDM na sio kinyume chake.
Kwani wewe Tindo unataka M/Kiti na CHADEMA wafanye nini ili u - appreciate kuwa they are doing fine?

Uko against kila kitu kinachofanywa na CHADEMA chini ya Freeman Mbowe Kwa Sasa Kwa hoja ambazo Mimi hata sioni uzito wake..

Na mara nyingi huwa nafuatilia mtazamo na maoni yako juu ya mwenendo wa CHADEMA chini ya Freeman Mbowe Kwa muda mrefu. You don't appreciate anything bro, why.?

Yaani kuna wakati unatamani viongozi wa chama chini ya M/Kiti Freeman Mbowe na CHADEMA Kwa ujumla siku Moja usikie wakitangaza kutumia njia ya mapambano ya kimwili (physical confrontation) dhidi ya CCM na serikali badala ya hii ya kukaa mezani kuzungumza ili kupata wakitakacho--

Mimi nasema HAPANA!!... Njia hiyo uwazayo wewe haikubaliki kwa Sasa na mpaka kesho.!!

Na ikitokea ikatumika njia hiyo uitakayo, basi tambua kuwa hata wewe hutabaki salama kiasi cha kukaa kwenye Kiti chako ukiposti haya unayoposti Kwa sababu vita au aggressiveness au physical confrontation haijawahi kuwa njia fanisi na salama kupata chochote toka Kwa mpinzani wako zaidi ya hasara na maumivu...!

Kubali kuwa, Freeman Mbowe ni miongoni mwa viongozi bora sana wa vyama vya siasa vilivyo nje ya serikali a.k.a vyama upinzani Tanzania, Afrika na duniani wa miongo hii.

CHADEMA wako vizuri na Wana akili sana na wako kwenye njia sahihi na nakuhakikishia jambo Moja, hiki chama KITAICHUKUA NCHI SIKU MOJA ISIYO MBALI NA KUONGOZA SERIKALI..!!
 
Mimi sio mtaalam wa siasa ila akitokea mtu anipe success story ya mtawala kufanya maridhiano na mpinzani na bado mpinzani akabaki na nguvu basi nitaungana na wanaosema Mbowe kafanikiwa.

Mimi nna mfano hai wa juzi tu hapa, Kenyatta na Odinga. Odinga alipoteza mvuto kwa wananchi baada ya maridhiano yao. CCM ndio wanufaika zaidi wa hayo mnayoita maridhiano yanayowa-limit kuikosoa serikali.
Bt usisahau maridhiano yamesababisha manufaa makubwa Kwa wananchi.

Mauaji ya kutisha hayakuripotiwa.
 
Watu tuna vilema hapa vya kuingia barabarani, labda useme kingine. Kuna watu tulijitoa kuwapigania wakaishia kuunga juhudi, kisha wakahongwa vyeo hivyo hivyo kwa mlango wa uani. Sasa sijui unaongea nini boss.
So sorry.

Bt pasi maridhiano ya Mandela na makaburu, Hadi Leo wangekuwa wanauana.

Wakat mwingine viongozi wajishushe Ili raia wapate manufaa.

The End justifies the means.
 
Mbowe ameshakuwa 'compromised'.
Kama Mbowe ana compromise na mwisho TUNAPATA KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA,

Aendelee na njia hiyo, bt kama wanamuingiza kingi, tumekwisha.

Maana deni la Taifa linazidi kupaa, na pesa wanazoziiba what if wakirudi nazo kuwanunua wapiga kura!!!
 
Ule ulikuwa ni ufunguzi tu, huwezi ukaanza kuhukumu au kuwa na hoja ktk kilichotokea ktk mkutano wa ufunguzi. Mimi ni mpinzani haswa wa ccm lakini sipendi siasa za fujo, siasa za matusi. Napenda kushindana kwa hoja na penye ukweli pasemwe na uongo usemwe bila kuoneana. Naimani chadema ipo vizuri na inakwenda vizuri sana na itafanikiwa sana ktk juhudi zake za kupigania haki na maendeleo ya taifa hili
Hoja zitoke wapi CHADEMA ? Usijitekenye.
 
Siasa za Kenya siyo za kulinganisha kabisa na siasa za Tanzania

Tanzania kuna vyama vyenye defined ideology while Kenya kuna magenge ya matajiri yenye wafuasi tu.

Siasa za Kenya zinajengwa kwa misingi wa ukabila while Tanzania sivyo.

Uelewa wawakenya kwenye haki za kisiasa ni mkubwa zaidi kuliko wa watanzania.

Kenya hakuna chama kinachotawala muda mrefu hivyo hakuna aliyechokwa wakati Tanzania bado wananchi wanatafuta namna ya kuiua ccm.

Yawezekana maridhiano yakampubguzia nguvu Mbowe binafsi ila siyo Chadema na Vuguvugu la mabadiliko.

Slaa alikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa wanachadema lakini aliondoka na wakasonga mbele.

Miaka 6 iliyopo hamahama ya wanasiasa imewajenga wanachadema kuamini katika njia yao na siyo wanasiasa binafsi.
CHADEMA imesonga mbele ? Kweli wewe hujui kitu kabisa.
 
Kwani wewe Tindo unataka M/Kiti na CHADEMA wafanye nini ili u - appreciate kuwa they are doing fine?

Uko against kila kitu kinachofanywa na CHADEMA chini ya Freeman Mbowe Kwa Sasa Kwa hoja ambazo Mimi hata sioni uzito wake..

Na mara nyingi huwa nafuatilia mtazamo na maoni yako juu ya mwenendo wa CHADEMA chini ya Freeman Mbowe Kwa muda mrefu. You don't appreciate anything bro, why.?

Yaani kuna wakati unatamani viongozi wa chama chini ya M/Kiti Freeman Mbowe na CHADEMA Kwa ujumla siku Moja usikie wakitangaza kutumia njia ya mapambano ya kimwili (physical confrontation) dhidi ya CCM na serikali badala ya hii ya kukaa mezani kuzungumza ili kupata wakitakacho--

Mimi nasema HAPANA!!... Njia hiyo uwazayo wewe haikubaliki kwa Sasa na mpaka kesho.!!

Na ikitokea ikatumika njia hiyo uitakayo, basi tambua kuwa hata wewe hutabaki salama kiasi cha kukaa kwenye Kiti chako ukiposti haya unayoposti Kwa sababu vita au aggressiveness au physical confrontation haijawahi kuwa njia fanisi na salama kupata chochote toka Kwa mpinzani wako zaidi ya hasara na maumivu...!

Kubali kuwa, Freeman Mbowe ni miongoni mwa viongozi bora sana wa vyama vya siasa vilivyo nje ya serikali a.k.a vyama upinzani Tanzania, Afrika na duniani wa miongo hii.

CHADEMA wako vizuri na Wana akili sana na wako kwenye njia sahihi na nakuhakikishia jambo Moja, hiki chama KITAICHUKUA NCHI SIKU MOJA ISIYO MBALI NA KUONGOZA SERIKALI..!!
Kumbe umeshamsoma [emoji1319][emoji1319][emoji1319][emoji1317][emoji1317][emoji1756][emoji1756]

Now ni kujiita kilema, kutafuta huruma, bila ushahidi ili ku- justify kile anachopigania kionekane sahihi[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Ila kwenye hiyo clip nilichoona ni kimoja tuu kwamba Mbowe saa uzee unamkaba koo kwa kasi.
Nimeona na yeye anaonge huku una mung'unya mung'unya midomo kama wale wazee vibogoyo..

Ila jamaa kama ni kazi kwa taifa hili lililojaa wapumbavu basi kafanya kazi kubwa sna..Namuheshim na namuombea kwa Mungu kuhusu hilo.

Lastly i love Change but i dnt believe in change through CDM wamepoa sana kwasasa nadhan ile misuko suko haijatuacha salamaa kabisaaa na ccm wanajua fika kwamba wametumaliza
 
Kumbe umeshamsoma [emoji1319][emoji1319][emoji1319][emoji1317][emoji1317][emoji1756][emoji1756]

Now ni kujiita kilema, kutafuta huruma, bila ushahidi ili ku- justify kile anachopigania kionekane sahihi[emoji3][emoji3][emoji3]
TINDO yupo sawa.

Wasiwasi ndio AKILI.

Chama Cha Mapinduzi Si Rahisi kuachia bila KUPINDULIWA,

Tujifunze Zanzibar, Maalim alitumia njia zote za nguvu na ustaarabu bt nn yalikuwa matokeo yake???
 
Kwani wewe Tindo unataka M/Kiti na CHADEMA wafanye nini ili u - appreciate kuwa they are doing fine?

Uko against kila kitu kinachofanywa na CHADEMA chini ya Freeman Mbowe Kwa Sasa Kwa hoja ambazo Mimi hata sioni uzito wake..

Na mara nyingi huwa nafuatilia mtazamo na maoni yako juu ya mwenendo wa CHADEMA chini ya Freeman Mbowe Kwa muda mrefu. You don't appreciate anything bro, why.?

Yaani kuna wakati unatamani viongozi wa chama chini ya M/Kiti Freeman Mbowe na CHADEMA Kwa ujumla siku Moja usikie wakitangaza kutumia njia ya mapambano ya kimwili (physical confrontation) dhidi ya CCM na serikali badala ya hii ya kukaa mezani kuzungumza ili kupata wakitakacho--

Mimi nasema HAPANA!!... Njia hiyo uwazayo wewe haikubaliki kwa Sasa na mpaka kesho.!!

Na ikitokea ikatumika njia hiyo uitakayo, basi tambua kuwa hata wewe hutabaki salama kiasi cha kukaa kwenye Kiti chako ukiposti haya unayoposti Kwa sababu vita au aggressiveness au physical confrontation haijawahi kuwa njia fanisi na salama kupata chochote toka Kwa mpinzani wako zaidi ya hasara na maumivu...!

Kubali kuwa, Freeman Mbowe ni miongoni mwa viongozi bora sana wa vyama vya siasa vilivyo nje ya serikali a.k.a vyama upinzani Tanzania, Afrika na duniani wa miongo hii.

CHADEMA wako vizuri na Wana akili sana na wako kwenye njia sahihi na nakuhakikishia jambo Moja, hiki chamari KITAICHUKUA NCHI SIKU MOJA ISIYO MBALI NA KUONGOZA SERIKALI..!!

Kwanza nashukuru kwa kunifuatilia, na kizuri zaidi kutokukubaliana na mtazamo wangu, hasa kuhusu huyo Freeman Mbowe. Napenda kusema naheshimu mtazamo wako kwani hiyo ndiyo afya ya mjadala, na zaidi hiyo ndio demokrasia.

Sasa tuje huko kwa Freeman Mbowe, nasema hivi, mimi ni muumini wa nafasi ya kiongozi wa kuchaguliwa kutokuzidi miaka 10, sasa hili ni kosa langu sio lako. Lakini ni ukweli usioacha shaka kuwa kiongozi akikaa madarakani zaidi ya miaka 10, ubora wake hupungua, na huanza kutawala kwa mizengwe, Mbowe anaangukia kwenye kundi hili. Ukitazama CDM ilipotoka na ilipotakiwa kuwa sasa hasa upande wa miundombinu, kama ofisi hata 1 moja MKOA ni vitu tofauti! Kibaya zaidi anaanza kusema kuna mabilioni yake mengi ameyatumia kwa ajili ya CDM, yaani anaonyesha CDM ni mali yake na wala sio kiongozi.


Kwa kiongozi muwajibikaji, baada ya blunder ya kumpokea Lowassa kushindwa kupata urais, Mbowe alipaswa Kujiuzulu. Ama kama aliona sio sawa, kujiuzulu baada ya kosa lile, basi hakupaswa kugombea uenyekiti tena msimu uliopita. Jambo hili halinipi ruhusa dhamira yangu kukubaliana na mwenendo huo. Hii ni haki yangu ya kidemokrasia, je nakosea kutumia haki yangu ya kidemokrasia kumkataa kiongozi ambaye nina sababu za msingi za kumkataa? Sababu hizi sio lazima ziwe za msingi kwako, lakini kwangu zina msingi, na nitazishikilia.

Huko kwenye maridhiano, kwanza mimi sio muumini wa maridhiano na hao ccm, hilo moja, lakini sipingi wenye kuamini hayo maridhiano. Japo kwa mtazamo wangu, si sahihi Mbowe kwenda mwenyewe kwenye jambo hilo. Naijua tabia ya CCM kwenye maridhiano, na mifano hai ninayo. Hapa ni mjadala mpana.

Nahitimisha kwa kusema, ni sahihi sana Mbowe kukaa pembeni, kwani ameshakaa muda wa kutosha, na sasa anaelekea kushuka chini, ni vyema akakaa pembeni akapisha wengine, labda uniambie kuwa huko CDM hakuna mwingine zaidi yake kwa nafasi ya uenyekiti.
 
Kwanza nashukuru kwa kunifuatilia, na kizuri zaidi kutokukubaliana na mtazamo wangu, hasa kuhusu huyo Freeman Mbowe. Napenda kusema naheshimu mtazamo wako kwani hiyo ndiyo afya ya mjadala, na zaidi hiyo ndio demokrasia.

Sasa tuje huko kwa Freeman Mbowe, nasema hivi, mimi ni muumini wa nafasi ya kiongozi wa kuchaguliwa kutokuzidi miaka 10, sasa hili ni kosa langu sio lako. Lakini ni ukweli usioacha shaka kuwa kiongozi akikaa madarakani zaidi ya miaka 10, ubora wake hupungua, na huanza kutawala kwa mizengwe, Mbowe anaangukia kwenye kundi hili. Ukitazama CDM ilipotoka na ilipotakiwa kuwa sasa hasa upande wa miundombinu, kama ofisi hata 1 moja MKOA ni vitu tofauti! Kibaya zaidi anaanza kusema kuna mabilioni yake mengi ameyatumia kwa ajili ya CDM, yaani anaonyesha CDM ni mali yake na wala sio kiongozi.


Kwa kiongozi muwajibikaji, baada ya blunder ya kumpokea Lowassa kushindwa kupata urais, Mbowe alipaswa Kujiuzulu. Ama kama aliona sio sawa, kujiuzulu baada ya kosa lile, basi hakupaswa kugombea uenyekiti tena msimu uliopita. Jambo hili halinipi ruhusa dhamira yangu kukubaliana na mwenendo huo. Hii ni haki yangu ya kidemokrasia, je nakosea kutumia haki yangu ya kidemokrasia kumkataa kiongozi ambaye nina sababu za msingi za kumkataa? Sababu hizi sio lazima ziwe za msingi kwako, lakini kwangu zina msingi, na nitazishikilia.

Huko kwenye maridhiano, kwanza mimi sio muumini wa maridhiano na hao ccm, hilo moja, lakini sipingi wenye kuamini hayo maridhiano. Japo kwa mtazamo wangu, si sahihi Mbowe kwenda mwenyewe kwenye jambo hilo. Naijua tabia ya CCM kwenye maridhiano, na mifano hai ninayo. Hapa ni mjadala mpana.

Nahitimisha kwa kusema, ni sahihi sana Mbowe kukaa pembeni, kwani ameshakaa muda wa kutosha, na sasa anaelekea kushuka chini, ni vyema akakaa pembeni akapisha wengine, labda uniambie kuwa huko CDM hakuna mwingine zaidi yake kwa nafasi ya uenyekiti.
Naunga mkono HOJA,

Mbowe anatakiwa apumzike,

Point ya mwisho ndo yenye UKWELI,

Ukimuondoa Mbowe sasa CDM hayupo wa kuvaa VIATU vyake,

Mfumo wa CDM haukuwahi kuwaandaa vijana wake Kwa majukumu ya mkt.

Mbowe aendelee kuwapo, bt awe chini ya UANGALIZI mkali. Naamini JASUSI YERIKO nyererere ananielewa.
 
Upuuzi mtupu,maridhiano kati ya pande 2 hasimu za kisiasa huwa yanatikana na reactions za wanachama husika na sio vinginevyo.

Speech ya Mbowe ukiisikiliza kiumakini umetokana na kukosa support ya Wananchi & Wanachadema katika mapigano ya democracy-hivyo anaona umri unakwenda bora ahangaikie alichokipoteza individuali na sio tena kupigania watu wasio thamini struggle za democracy.
 
Naunga mkono HOJA,

Mbowe anatakiwa apumzike,

Point ya mwisho ndo yenye UKWELI,

Ukimuondoa Mbowe sasa CDM hayupo wa kuvaa VIATU vyake,

Mfumo wa CDM haukuwahi kuwaandaa vijana wake Kwa majukumu ya mkt.

Mbowe aendelee kuwapo, bt awe chini ya UANGALIZI mkali. Naamini JASUSI YERIKO nyererere ananielewa.

Si kweli, kuwa Mbowe akiondoka CDM itakosa mtu. Je akifa ndio mwisho wa CDM?
 
Back
Top Bottom