Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria?

Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria?

Nakuombe kauteuzi hivi karibuni
Ni mawazo finyu kudhani kila mtu anayeisifia serikali ni anatafuta uteuzi!. Mimi nimeisha hudumu kwenye media kwa zaidi ya miaka 30 hivyo kama ni kuisaidia nchi, nimeisha sana bila hata ya uteuzi.

Mama akirudisha mazingira ya kabla 2015, https://www.jamiiforums.com/threads...ika-sasa-ni-zamu-ya-media-ina-suffer.1518514/ watu kama sisi hatuhitaji uteuzi wowote na tutamsaidia Mama kuwalipa mishahara ma DC wake 3, RC 2 na Mkurugenzi mmoja.
Na Ile laana ya JPM iishe
It's true kuna kauli zina powers hivyo zinaumba!, ukiitwa njaa, njaa inakutembelea kweli!, ila pia kuna watu sio mchezo!, ukiwatibua tuu... https://www.jamiiforums.com/threads...nani-kati-yake-na-aliyetoa-kauli-hii.1328562/

Hivyo mimi nami ... https://www.jamiiforums.com/threads...na-kauli-umba-ambazo-huumba-shuhudia.2013308/

Mwisho wa siku, he laughs last, laughs most!.
P
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo ni kuhusu umuhimu wa viongozi wetu na haswa wakuu wa Mihimili lazima sio tuu wawe wasomi, weledi na wachapakazi, bali lazima wawe Bright, brilliant na wabobezi wa fani husika.

Niko mahali nafuatilia Bunge Live, kiukweli kabisa nimekuwa very impressed na jinsi Madam Spika Dr. Tulia Akson anavyoliongoza Bunge.

Juzi aliifanua vizuri Ripoti ya CAG na kuifafanua ile kauli ya hasira ya Mama ya stupid na "Watupishe", ni walioongeza "cha juu" kwenye ununuzi wa ndege ya mizigo, na sio wote waliotajwa kwenye ripoti ya CAG.

Leo Mbunge wa Liwale kaibua kubwa kuliko Bungeni kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere, JNHPP japo liko Rufiji, bwawa hilo liko wilaya ya Liwale mkoani Lindi, na sio Mikoa ya Pwani na Morogoro, hivyo wilaya ya Liwale inastahili asilimia 60% ya mgao wa fedha za CSR ya JNHPP, lakini Liwale haikupata hata senti 5!.

Spika Tulia akaingilia kati kwa kumuuliza Mhe. Mbunge athibitishe Bwawa la JNHPP liko Liwale, Mbunge akasema lipo Liwale!.

Dr. Tulia akafafanua tofauti ya mahali Bwawa lilipo na the catchment area maji ya kulijaza bwawa yanakotoka!. Mhe. Mbunge akang'ang'ana bwawa liko Liwale!.

Dr. Tulia akamwambia Mhe Mbunge kuwa yeye na wabunge wamekwenda lilipo na hadi kubonyeza kitufe kukajaza maji, bwawa liko Rufiji na sio Liwale, hivyo akamwambia mbunge akae kwanza.

Kisha akauliza wahusika kama wapo waeleze Bunge bwawa la JNHPP liko wapi, ndipo akasimama Naibu Waziri wa Nishati, Byabato, akasema kwa mujibu wa ramani zao, bwawa la JNHPP liko Rufiji na Morogoro, ila kama Mbunge anayo ramani yake inayoonyesha bwawa liko Liwale, ailete na kuwaelimisha wengine tuko tayari kujifunza!.

Mbunge mwingine akasimama kuchangia kuwa bwawa liko Rufiji ila the catchment area ya maji ya bwawa hilo yanatoka Liwale.

Ndipo Spika Tulia akampiga darasa Mbunge huyo kuwa bwawa la JNHPP liko Rufiji ila maji ya kulijaza yanaweza kutiririka kutoka popote na kumruhusu kumalizia kuchangia.

Hii ndio faida ya kuwa na Spika msomi wa sheria, natumaini wengi unakumbuka uendeshaji wa Bunge enzi za Spika Sitta pia alikuwa ni msomi wa sheria.

Kwa vile mimi ni mtu wa mastori mastori
Ngoja niwape mastori ya Mimi na Dr. Tulia Akson, kwa msiopenda mastori jump kule chini

Tanzania tunakwama baadhi ya maeneo kwasababu tuna viongozi vilaza!. We can afford kuwa na wabunge vilaza, ndani ya Bunge la JMT but we can't afford kuwa na wabunge vilaza kwenye Bunge la EALA! Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo

Ili Tanzania tuweze kupata viongozi bora,, the best of the best, hatuwezi kuuendeleza ule ujinga uliochomekewa ndani ya katiba yetu kiubatili, kuwaachia kakikundi ka watu wachache kuamua huyu ni wenzetu mpe uongozi, hata kama ni vilaza!, na huyu sii wenzetu kata jina tupa kule, hatumuhitaji, hata kama ni the best bright and Brilliant

Kwa maoni yangu, nashauri Spika asitokane na ukanda wa chama cha siasa, Spika Dr. Tulia huyu, tunayemsifu leo, kuwa anakwenda kuwa Spika bora ndio Dr. Tulia yule yule aliye naibu Spika chini ya bora Spika, na alinyamaza kimya wakati katiba yetu ikikanyagwa Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?

Hitimisho,
Nahitimisha kwa lile swali, la msingi la makala hii, kufuatia Spika Sitta na Spika Dr. Tulia Akson, ambao ni wanasheria, kuwa so good kwenye uendeshaji wa Bunge la JMT, kwasababu, they are smart, bright & brilliant! kuna haja sasa, kuanzia sasa kuhakikisha MaSpika wetu wote lazima wawe wanasheria?.

Wasalaam

Paskali
Umejitahidi sana, inabidi akuone!! ulijitahidi sana pia kwa top wa awamu ya tano lakini bahati mbaya kabla hajakuona akawa amemaliza kazi na kupimzika!!
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo ni kuhusu umuhimu wa viongozi wetu na haswa wakuu wa Mihimili lazima sio tuu wawe wasomi, weledi na wachapakazi, bali lazima wawe Bright, brilliant na wabobezi wa fani husika.

Niko mahali nafuatilia Bunge Live, kiukweli kabisa nimekuwa very impressed na jinsi Madam Spika Dr. Tulia Akson anavyoliongoza Bunge.

Juzi aliifanua vizuri Ripoti ya CAG na kuifafanua ile kauli ya hasira ya Mama ya stupid na "Watupishe", ni walioongeza "cha juu" kwenye ununuzi wa ndege ya mizigo, na sio wote waliotajwa kwenye ripoti ya CAG.

Leo Mbunge wa Liwale kaibua kubwa kuliko Bungeni kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere, JNHPP japo liko Rufiji, bwawa hilo liko wilaya ya Liwale mkoani Lindi, na sio Mikoa ya Pwani na Morogoro, hivyo wilaya ya Liwale inastahili asilimia 60% ya mgao wa fedha za CSR ya JNHPP, lakini Liwale haikupata hata senti 5!.

Spika Tulia akaingilia kati kwa kumuuliza Mhe. Mbunge athibitishe Bwawa la JNHPP liko Liwale, Mbunge akasema lipo Liwale!.

Dr. Tulia akafafanua tofauti ya mahali Bwawa lilipo na the catchment area maji ya kulijaza bwawa yanakotoka!. Mhe. Mbunge akang'ang'ana bwawa liko Liwale!.

Dr. Tulia akamwambia Mhe Mbunge kuwa yeye na wabunge wamekwenda lilipo na hadi kubonyeza kitufe kukajaza maji, bwawa liko Rufiji na sio Liwale, hivyo akamwambia mbunge akae kwanza.

Kisha akauliza wahusika kama wapo waeleze Bunge bwawa la JNHPP liko wapi, ndipo akasimama Naibu Waziri wa Nishati, Byabato, akasema kwa mujibu wa ramani zao, bwawa la JNHPP liko Rufiji na Morogoro, ila kama Mbunge anayo ramani yake inayoonyesha bwawa liko Liwale, ailete na kuwaelimisha wengine tuko tayari kujifunza!.

Mbunge mwingine akasimama kuchangia kuwa bwawa liko Rufiji ila the catchment area ya maji ya bwawa hilo yanatoka Liwale.

Ndipo Spika Tulia akampiga darasa Mbunge huyo kuwa bwawa la JNHPP liko Rufiji ila maji ya kulijaza yanaweza kutiririka kutoka popote na kumruhusu kumalizia kuchangia.

Hii ndio faida ya kuwa na Spika msomi wa sheria, natumaini wengi unakumbuka uendeshaji wa Bunge enzi za Spika Sitta pia alikuwa ni msomi wa sheria.

Kwa vile mimi ni mtu wa mastori mastori
Ngoja niwape mastori ya Mimi na Dr. Tulia Akson, kwa msiopenda mastori jump kule chini

Tanzania tunakwama baadhi ya maeneo kwasababu tuna viongozi vilaza!. We can afford kuwa na wabunge vilaza, ndani ya Bunge la JMT but we can't afford kuwa na wabunge vilaza kwenye Bunge la EALA! Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo

Ili Tanzania tuweze kupata viongozi bora,, the best of the best, hatuwezi kuuendeleza ule ujinga uliochomekewa ndani ya katiba yetu kiubatili, kuwaachia kakikundi ka watu wachache kuamua huyu ni wenzetu mpe uongozi, hata kama ni vilaza!, na huyu sii wenzetu kata jina tupa kule, hatumuhitaji, hata kama ni the best bright and Brilliant

Kwa maoni yangu, nashauri Spika asitokane na ukanda wa chama cha siasa, Spika Dr. Tulia huyu, tunayemsifu leo, kuwa anakwenda kuwa Spika bora ndio Dr. Tulia yule yule aliye naibu Spika chini ya bora Spika, na alinyamaza kimya wakati katiba yetu ikikanyagwa Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?

Hitimisho,
Nahitimisha kwa lile swali, la msingi la makala hii, kufuatia Spika Sitta na Spika Dr. Tulia Akson, ambao ni wanasheria, kuwa so good kwenye uendeshaji wa Bunge la JMT, kwasababu, they are smart, bright & brilliant! kuna haja sasa, kuanzia sasa kuhakikisha MaSpika wetu wote lazima wawe wanasheria?.

Wasalaam

Paskali
Masikitiko makubwa sana kwa wakazi wa Liwale kuwa na Mbunge mjinga kama huyu.
 
Nikikumbuka hila Na ghilib za watu wengine jinsi wanavyoupata ubunge huwa nawakinahi watu hao Na kuwakifu hata wafanye jema kiasi gani!

I am sorry to say that!

Sijui sababu ni mwana wa Mungu?!

Yaani huwa napendezwa na haki mno kuliko udhalimu , uzandiki, hila , udanganyifu, ghilib na vya kufanana na hayo!
 
Tuwe na shukrani kwa madogo ili tuweze kupatiwa makubwa!. Kipindi cha Spika Makinda na Spika Ndugai uliwahi ona spika anamkosoa na kumnyoosha mbunge wa CCM?. Huu ni mwanzo mzuri, hatutaki ujinga Bungeni uwe wa CCM au wapinzani ni kunyoroshwa!.

Huu ndio Umuhimu mkubwa wa Spika msomi wa sheria!. Hili nimeliandikia sana!. Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?
P



Shukrani hiyo vipi?

Kwani ni hisani au yupo pale kuwajibika na kulipwa kodi ?
 
Leo tena Spika Dr. Tulia Akson, ameonyesha tena ubobevu wa sheria Bungeni, mbunge mmoja wa viti maalum Hanang, amelalamikia mkataba wa mkopo wa matrekta ya Asus katika mkataba na NDC uliohisisha wakulima kukopeshwa matrekta na vipuri

Wakulima wamekopeshwa matrekta lakini hayana vipuri hivyo matrekta yameharibika yako grounded na kushindwa kulipa deni, wanakuwa harassed sana.

Spika akautisha mkataba hapo hapo akaufafanua kisheria, kisha akamuuliza Waziri wa Ulinzi, Innocent Bashungwa atoe maelezo kwasababu matrekta ya Asus yanakopeshwa na Kampuni ya Suma JKT.

Ndipo Waziri Bashungwa akakiri kampuni Mama ya matrekta ya Asus ni muflis hivyo hakuna vipuri. Hivyo Spika akauliza umkopeshe mtu matrekta bila vipuri, trekta limeharibika huyo mkulima atalipa vipi mkopo huo?.

Akamshauri mbunge alipeleke jambo hilo kwenye kamati ili kamati imletee rasmi atoe maelekezo serikalini.

Hili sasa ndio Bunge linaloisimamia serikali,
Hongera sana Spika Madam Dr. Tulia Akson.
P
 
Spika ni mwasheria kwa kiwango cha shahada ya uzamivu, it was too low kwake kujadili hoja dhaifu kama hizo. Tunataka tuone mchango wake wakati sheria zinletwa bungeni.

Asanteee
 
Pascal Mayalla , je haudhani kwamba Ili tuwe na maspika wa vigezo hivyo tunahitaji kufanya mabadiliko Ili spika asiwe lazma mbunge. Mfano pale mbeya spika akishindwa kutetea nafasi yake atashindwa kuwa spika. Kuna watu wazuri sana wenye vigezo ulivyotaja ambao wanaoweza kuwa viongozi Bora na wanaoweza KUONGOZA taasis na mihimili vizuri tu, lakini watu hao sio wanasiasa. It's high time tukubali mabadiliko, maspika na mawaziri sio lazma wawe wabunge, wagombee hizo nafasi
 
Spika Tulia amtuliza Dr. Dorothy Gwajima na kumshushua kiungwana na kistaarabu baada ya Waziri Gwajima kuomba muongozo wa Spika na kuruhusiwa akamtaka Mbunge kuondoa maneno ya KE na ME ni maneno ya udhalilishaji wa kijinsia, Spika akaingilia kati kuwa hakuna udhalilishaji wowote na hakutumia kifungu sahihi cha kuomba muongozo wa kumtaja mbunge afute kauli na kumtaka mbunge aendelee kuchangia.

Ukimuondoa Spika Sitta ambaye ni mwanasheria, Spika Tulia ndie Spika wa pili kumkalisha chini Waziri, Spika Tulia pia ni mwanasheria.
P.
 
Pascal Mayalla , je haudhani kwamba Ili tuwe na maspika wa vigezo hivyo tunahitaji kufanya mabadiliko Ili spika asiwe lazma mbunge. Mfano pale mbeya spika akishindwa kutetea nafasi yake atashindwa kuwa spika. Kuna watu wazuri sana wenye vigezo ulivyotaja ambao wanaoweza kuwa viongozi Bora na wanaoweza KUONGOZA taasis na mihimili vizuri tu, lakini watu hao sio wanasiasa. It's high time tukubali mabadiliko, maspika na mawaziri sio lazma wawe wabunge, wagombee hizo nafasi
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100% chini ya 100% na niliwahi kushauri https://www.jamiiforums.com/threads...u-kuna-haja-spika-asitokane-na-vyama.1560625/
P
 
Hivi mtu akifanya jambo lolote zuri, no matter how big or small, mtu huwezi kumsifia mtu bila kuitwa chawa?. Huyu ni Mwalimu wangu wa 1st Year, nikamtabiria atakuwa spika, amekuwa Spika!. Kuna ubaya kumsifu?.
Hivyo ilipotokea wewe ni Mwanafunzi umekutana na Mwalimu wako mambo yanakuwa hivi
Kuna ubaya?.
P

Huo ni uchawa tu by any other name!!
 
Wanabodi,

Niko mahali nafuatilia Bunge Live, kiukweli kabisa nimekuwa very impressed na jinsi Madam Spika Dr. Tulia Akson anavyoliongoza Bunge.
Paskali
Nina imani sana na Spika, Dr. Tulia Akson, leo huyu Dada, ataonyesha uwezo mkubwa alionao katika kuongoza mjadala muhimu sana wa Bunge letu kujadili mkataba wa HGA kati ya serikali yetu na kampuni ya DP World ya Mwarabu wa Dubai.

Mijadala kama hii ndio itatufungua macho Watanzania, kwanini Spika Sitta alikuwa Spika bora, na sasa Spika Tulia Akson ni Spika bora!.

Kwa maneno ya rafiki William Malecela (RIP), huwezi kuacha hoja nzito kama za mkataba wa kimataifa wa rasilimali zetu, ukaongozwa na mbululaz!.

Wish all the best Madam Spika, ni maslahi ya taifa mbele!.
P
 
Nina imani sana na Spika, Dr. Tulia Akson, leo huyu Dada, ataonyesha uwezo mkubwa alionao katika kuongoza mjadala muhimu sana wa Bunge letu kujadili mkataba wa HGA kati ya serikali yetu na kampuni ya DP World ya Mwarabu wa Dubai.

Mijadala kama hii ndio itatufungua macho Watanzania, kwanini Spika Sitta alikuwa Spika bora, na sasa Spika Tulia Akson ni Spika bora!.

Kwa maneno ya rafiki William Malecela (RIP), huwezi kuacha hoja nzito kama za mkataba wa kimataifa wa rasilimali zetu, ukaongozwa na mbululaz!.

Wish all the best Madam Spika, ni maslahi ya taifa mbele!.
P
Tatizo lako P unajifanya huwajui wabunge wa CCM na speaker wao hasa kweny masuala ya kupitisha miswada bungeni!! Utasubir san kama unategemea kwenda kinyume pasi kupitisha azimio husika!
 
Nina imani sana na Spika, Dr. Tulia Akson, leo huyu Dada, ataonyesha uwezo mkubwa alionao katika kuongoza mjadala muhimu sana wa Bunge letu kujadili mkataba wa HGA kati ya serikali yetu na kampuni ya DP World ya Mwarabu wa Dubai.

Mijadala kama hii ndio itatufungua macho Watanzania, kwanini Spika Sitta alikuwa Spika bora, na sasa Spika Tulia Akson ni Spika bora!.

Kwa maneno ya rafiki William Malecela (RIP), huwezi kuacha hoja nzito kama za mkataba wa kimataifa wa rasilimali zetu, ukaongozwa na mbululaz!.

Wish all the best Madam Spika, ni maslahi ya taifa mbele!.
P
Nakumbuka uliwahi kumsifia Ndugai kuwa ni spika bora kuwahi kutokea.

Sasa naona umemruka!
 
Back
Top Bottom