Rafiki yangu sikujua kama Utani wangu huu juu ya hao Wasafiri 48 Wewe kama mwana Yanga SC ungeupokea kwa Machungu na Hisia Kali hivi.
Nichukue nafasi hii Kukuomba Radhi na pia kuwaomba Radhi na wana Yanga SC Wengine hapa kama nao Wamekwazika ila kiukweli huwa napenda mno Utani na Kuchangamshana hapa.
GENTAMYCINE leo kuwatania hivi Yanga SC mmeonyesha Kuchukia hadi kusema kuwa Nadhalilisha Watu ila wana Yanga SC hapa JamiiForums Kutwa wakiwa Wanatudhalilisha wana Simba SC ( GENTAMYCINE nikiwemo ) huwa hamuoni na haliwaumi tena huenda pia huwa Mnafurahi sana.
Kunya anye Kuku ila akinya Bata basi jua Kaharisha. Hakuna Kitu nakichukia kama UNAFIKI, UBINAFSI na UPUMBAVU uliotukuka.