Huenda kuanzia mwaka 2034 nchi itakuwa na vilaza watupu

Tuende na wakati
 
Wewe ni pumbavu kabisa.
 
Kisa wewe ulisoma mambo magumu advance haimaanishi utawazidi wengine kwenye ujuzi ama ndo mtaala sahihi
 
Hii ndio nature Mkuu, huwezi kupuuzia nadharia ,ukaenzi vitendo pekee, hivi vitu vinategemeana. Kimoja kunaanziasha kingine. Kifalsafa na kisayansi elimu ya nadharia ndio chanzo cha elimu ya vitendo. Vitu vyote vinavyoonekana kwa macho husnzia kwenye akili ya mwanadamu ambayo ndio nadharia yenyewe.
 
Hata mimi nimeona. Halafu wanaponda sana A level.
Sio kweli kwamba tunaoponda A level wengi hatukupita huko, ni kuwa tunaona tu kuwa haina impact kwa maendeleo ya mtoto, sana ni kumpotezea mtotp mda wake wa kusoma na kufanya kazi.

Mfumo wa 6-4-4 badala ya 7-4-2-3(4) unafaa zaidi.
 
It's not about the number of classes, It's about the quality of the education. Elimu yetu haina ubora na haimuandai mtu kukabiliana na changamoto halisi za mazingira yake na dunia ya sasa. Kingine kwenda shule sio kuwa na akili. Hizo shule ndo zinazalisha vilaza wengi watu waliokuwa brain washed wanaodhani ujuzi ni kukariri misamiati ya kiingereza
 
Sawa ila sisi wabongo tumeweka nadharia mbele yani unakuta mtu anajua misamiati balaa ila vitendo zero. Tunatengeneza taifa la wapiga midomo na sio la wafanya kazi
 
Kwani kwenye Engineering mathematics hamna hizo differential na complex number
 
Una maana gani kusema kuanzia 2034, wewe hebu angalia pale mjengoni, wote wamekubali kuuza rasimali ya nchi (Bandari zote za Tanganyika), hivi wale tuwaitaje kama sio hao uliowataja, yaani kweli wanashindwa kujua kuwa nchi inauzwa?
 
Tanzania ina watu wengi ambao hawapaswi soma mfumo rasmi.

Kwa sasa sera ya elimu bure maana yake inalazimisha watu waende shule pamoja na kuwa wengi wao wana uwezo mdogo, wanaenda ili kulinda wazazi wao wasikamatwe na polisi
 
Mkuu uko sahihi sana.Tuna kizazi kinachoamini kwenda Chuo cha kati ni kufeli. Mimi nimepita advance, sijui huko nilikua natafuta nini hahahahhah. Mwanangu Katu hata fuata ujinga wa Advance labda nife.
Ni ujinga wa hali ya juu kudhani kuingia form five na six ni kiwango cha uwezo wa mwanafunzi. Nakumbuka siku za nyuma tulipokuwa tunajiunga na form five na six tulikuwa tunajiona superior sana. Baada ya kwenda chuo kikuu ndio nilijua niliishia kupoteza muda. Walikuja watu waliokuwa vyuo vya kati wakiwa na ujuzi ambao sisi ndio tulikuwa tunaanza, na walitupiga bao.

Hata ukienda huko makazini sio lazima kwenye ajira, utakuta watu wa vyuo vya kati wengi ndio wenye tija. Watu wengi waliotoka vyuo vikuu hawana uwezo mkubwa wa kazi, na wamejaa majigambo, ndio wanaojifanya wajuaji, kazi yao kubwa ni kusimamia kuliko kutenda. Kwa sisi wenye miradi kadhaa hatupendi kuchukua watu toka vyuo vikuu, bali huchukua watu toka vyuo vya kati ili kupata ufanisi katika vitega uchumi vyetu.
 
Huko mbali sana
 
Sema Kuna Wana watakupinga ila Kwa kiasi Fulani umeongea kweli tupu.
Mfano mzizi wa engineering na engineering sciences ni Hesabu, ambazo hufundishwa zaidi Advance na Kwa kuzijua hizo Hesabu unaweza fanya ugunduzi mkubwa katika fani ya Uhandisi, ila vyuoni it's just unafundishwa stadi za kazi na sometimes malecturers wanaignore sana Hesabu na kuwafanya watu wanaotoka pale kuwa craming oriented ila sio critical thinking or creative thinking oriented.
Wagunduzi wote duniani wengi walipitia High schools, ni wachache ambao hawajapitia huku sababu kuu ni IQ za 200-250.
Anyway let's everybody decide what he/she likes and his/her fate.
 
Haya yote inategemea pia chuo unaenda kusoma nini,
course niliyosoma requirements advanced math and physics lazima, ukisoma hizo diploma sijui vigezo vyao hata sikumbuki, ila inshort hakuna mtu wa namna hiyo tulisoma naye.
Haya mambo ya kukalilishana eti kwenye field wapo vizuri ni umburula tu...wengi ni vilaza kama wengine na hata Kwenye Miradi sijawai kuona wakiongoza zaidi ya kuwa assistant..
 
Sawa ila sisi wabongo tumeweka nadharia mbele yani unakuta mtu anajua misamiati balaa ila vitendo zero. Tunatengeneza taifa la wapiga midomo na sio la wafanya kazi

Mkuu uko sahihi sana, unakuta mtu ana degree mfano ya IT, lakini hata ukimwambia abane RJ45 kwake ni mtihani. Lakini kwenye kutamka mambo kwa kiingereza hajachacha. Ukimchukua mtu aliyesoma VETA anafanya kwa usahihi bila majidai ya kijinga.

Na hatari nyingine kubwa tunayopata toka kwa waliosoma vyuo vikuu, wengi ni wapiga blabla, na ndio kundi kubwa la wezi wa kalamu. Hizi ripoti za CAG ukifuatilia vizuri, utakuta vinara wa huo wizi ni wenye elimu ya vyuo vikuu. Na sababu ya tabaka hili kujaza wezi ni ili kupata fedha nyingi zikidhi hadhi ya elimu yao ya chuo kikuu. Mimi kwenye vijimiradi vyangu ni marufuku kuchukua mtu mwenye elimu ya chuo kikuu, kwani ataishia kuwa mwizi, bushlawyer wa kumobilize wengine walete madai yasiyoendana na uhalisia wa anachokizalisha.
 
Sasa hao wenye cognitive ability,wamefsnya Nini?
Je watu kama msukuma,diamond,wapo humo,au la maana wame fanikiwa sana,bila ya kupitia huko kwenye cognitive ability,
Weka kitu kimoja alichofanya huyo mwenye cognitive behaviour,
Je wale madokta pale Benjamin udom,waliofanya upandikazji wa uume wapo kundi Hilo?je Dr Ben Carson bingwa wa kutengsnisha joined twins,yupo humo?yeye hakusoma hiyo six Yako.
Wachina wanotujengea na madaraja wapo humo?

Wanaopigia chapuo six,ni sawa na vijana wa bongo,kipato chake chini ya 1Moja,lakini anadunduliza kununua macho matatu,sio kwamba anataka simu imfanyie Nini!Bali watu wamuone na yeye yumo,apps anwzotumia ni za kuangalia vikatuni na video insta.
Kenya,hawana six,lakini katika AFRIKA,they are the most well educated people,wanakimbiza balaa.
Pale DIT,mkiwa diploma,na vijana waliotoka six,wanachowazidi ni hesabu TU,wakati huo,tunapiga ADE,six walikuwa hawawezi kujoin ADE kusoma kozi zaidi ya telekom,Kuna Mmoja,alikomaa asome ADE na waliotoka ftc,aliomba Po!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…