Pre GE2025 Huenda sababu ya Askofu Machumu kukamatwa ni kauli yake "...Bwana alitoa, CCM wametwaa, jina lao lilaaniwe!"

Pre GE2025 Huenda sababu ya Askofu Machumu kukamatwa ni kauli yake "...Bwana alitoa, CCM wametwaa, jina lao lilaaniwe!"

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tija ya uwekezaji wa hapo bandarini haikwepeki.

Kuweza kuielezea mara kwa mara ni kupoteza muda kwa aina ya akili zinazojaa ubishi wa kijinga tu.
Mpaka leo hii hujatambua matokeo ya upotofu huo? Utajitambulisha vipi kuwa mwerevu iwapo huwezi hata kusoma alama za nyakati!
Nilikutambua toka mwanzo kwamba uwezo wako ni mdogo, na hali haikubadilika hadi leo.
 
Yego chikaka
Mwaksyanaki na Machumu saja?
Alijaribu kupotosha waumini wake kuhusu uwekezaji mzima lakini akaumbuka kadri wataalam walivyouanika wazi huo mkataba.

Ameumbuka zaidi baada ya kugundulika kwamba serikali kuingia mkataba na DP World hakuzuii wawekezaji wengine kuwekeza katika bandari nyinginezo.
Uweke hapa huo mkataba nasi tujue kweli kuwa ni mchochezi.
 
Mpaka leo hii hujatambua matokeo ya upotofu huo? Utajitambulisha vipi kuwa mwerevu iwapo huwezi hata kusoma alama za nyakati!
Nilikutambua toka mwanzo kwamba uwezo wako ni mdogo, na hali haikubadilika hadi leo.
Kuna waendeshaji watatu hapo bandarini kulingana na mahitaji ya kiuchumi na sio mwisho watakuja na wengine wengi katika bandari zetu tofauti.

Wabongo maarifa madogo halafu tunaongea kwa umahiri utadhani tunajua kwa kina nini tunaongelea!.
 
Kwa nini ufichwe (eti wapotoshaji wasipotoshe) kama una manufaa kwa taifa huo upotoshaji utatoka wapi?

Maji na mafuta huwezi kuwaweka pamoja.
Labda ungesema wenye mali tusije tukaulaani zaidi ijapo tunailaani.
Kuna mwingine pia wa TPA na adinani Huyu mdosi.

Hutakuja kusikia chochote kuhusu huu uwekezaji taarifa zake ni nyeti ili wapotoshaji wasianze kazi ya kupotosha jamii.
 
Wabongo maarifa madogo halafu tunaongea kwa umahiri utadhani tunajua kwa kina nini tunaongelea!.
"Wabongo maarifa madogo", ni hao viongozi, siyo waTanzania. Kazi ya kuongoza nchi ni kuwawezesha wananchi wako wafanye juhudi kwa maarifa kumudu mahitaji ya kuleta maendeleo nchini mwao, siyo kila siku kuzurura duniani kwenda kutafuta watu wa kuja kukulea wewe.
Korea Kusini hawakufikia hatua waliyofikia kwa kutegemea mataifa mengine, au watu wengine toka nje kuja kuwafikisha hapo walipofikia leo.
Bandari, unakwenda kuchukuwa mkopo kuikarabati, halafu unamgawia mtu mwingine kwa miaka 30 avune hapo, na wala huna mipango yoyote ya kujiandaa kuwa na uwezo wa kuiendesha bandari baada ya hiyo miaka 30, hii ni akili matope kabisa.
Misitu, hata kuwaamini wananchi wako kupanda na kutunza misitu inabidi kwenda kutafuta watu nje...!
Mkuu, Ntamusana, wakati mwingine tuwe tunaweka ushabiki wa kisiasa pembeni na kuyatazama maswala ya nchi yetu inavyostahili kuyaona.
Kamwe hatuwezi kuwa watu wa kutegemea kuja kufanyiwa tu na watu wengine toka nje bila ya kufanya juhudi zetu wenyewe, hata kama ni kidogo, za kurekebisha tunapojiona hatuwezi. Makundi yaliyopo pale bandarini yanayokwamisha shughuli za bandari; kweli viongozi wa nchi hii hawana uwezo wa kuyashughulikia makundi kama hayo? Na siyo bandarini tu, ni kila sehemu. Hebu jaribu kidogo kufungua akili yako.
Sisemi hata mara moja kuwa uwekezaji hautakiwi, lakini uwekezaji ni njia ya kusaidia juhudi zetu sisi wenyewe, kwa lengo la kupata uwezo mkubwa kadri tunavyosonga mbele.
Hatuwezi kila mara tuwe tunazungushana tu katika mambo muhimu kama haya, kwa sababu tu za kishabiki za kisiasa; au zingine zozote zinazotufanya tuwe mashabiki. Tanzania ni muhimu zaidi ya ushabiki wa aina yoyote ile; hata uwe wa kiimani, kijinsia, kikabila ,n.k..
 
Kuna mwingine pia wa TPA na adinani Huyu mdosi.

Hutakuja kusikia chochote kuhusu huu uwekezaji taarifa zake ni nyeti ili wapotoshaji wasianze kazi ya kupotosha jamii.
Sasa hii kweli ndiyo ije iwe sifa ya kiongozi kuongoza nchi?
Mbona "upotoshaji" unashamiri sana katika maswala yanayofanyiwa gizani zaidi?
 
Huenda hotuba hii ya Askofu Mwanamapinduzi ndio chanzo cha yeye kukamatwa na Polisi.


=======

Askofu Machumu: Chini ya Serikali ya mama Samia Suluhu Hassan, yeye ndio ameamua rasmi kuiuza Tanganyika, naomba iwe wazi hiyo. Yeye ameamua rasmi kuiuza Tanganyika kuanzia bandari zake, misitu, mapori yake tena ameuza kwa waarabu.

Kama wanadai nimesema uongo, watuambie ile mikataba waliofanya kule Dubai, mikataba 39 inahusu nini?

Tumewekewa mikataba miwili, mkataba wa kwanza, mkataba wa bandari. Ule mkataba wa bandari ukiusoma, unasema kwamba bandari zinakabidhiwa kwa waarabu mpaka shughuli za bandari zitakapoisha maana yake ni kwamba mpaka Yesu arudi.

Tunauliza, ni kwa shilingi ngapi hatuambiwi. Magufuli alipoingia madarakani alikuta mkataba mmoja wa kuuza bandari ya Bagamoyo. Bandari ile ilikuwa inakabidhiwa kwa wachina kwa miaka 99 ila watajenga wenyewe.

Akasema mkataba huu, mtu yeyote anayetaka kuingia mkataba huu lazima kwanza awe chizi na mwendawazimu.

Sasa mama Samia nitafutieni jina la kumpa maana kama ni uchizi ameshazidi hapo. Ameuza bandari sio moja, ameuza bandari 54 za Tanganyika za kwenye bahari mpaka maziwa, kwa miaka mingapi hatujui, kwa shilingi ngapi hatujui!

Mimi nawaambia ukweli, mama huyu tumalizane naye safari hii, tumalizanane naye Serikali za mtaa, msichague chama chake. Mkichagua CCM atapata nguvu ya kugombea, kama amewauza kwenye awamu yake ya kwanza, awamu ya pili atawafanyaje!

Pia soma:

Singida: Baba Askofu Machumu akamatwa kwa Uchochezi
Sasa mwehu km huyu si alitakiwa ahasiwe kabisa asituzalie mipuuzi km yy
 
Tutaona idadi ya maskofu wakipanda majukwaani inaongezeka, wakishaona hijab wanaumia, wakati wa Magufuli , Mkapa hatukuona haya, tulianza wakati wa mwinyi
Kwa hiyo nchi ikiuzwa na mtu aliyevaa hijabu au KOBAZI ndiyo furaha yako? Usikute na wewe BWABWA akili za wapi hizi?
 
Huyu naye ni boga tu, anapewa umaarufu wa bure.....

Huyu alikuwa anakaanga samaki sokoni, akajua vifungu viwili vya biblia kawa askofu.

Na ile misuti yake ya kushona kwa fundi mwanzalima chini ya muembe, hovyo kabisa
Hahahaaaaaa, alikuwa wapi? CDM wanampamba kuwa ni shujaa wao ila dola ikimfanyia kazi ataanza kujiliza na kutaka aonewe huruma kama Mwakipesile.
 
Ila wewe ndio hovyo kabisaa watu kama hawa nawa appriciate sana wee kama unawaona wa hovyo utajiju
 
Kwa nini ufichwe (eti wapotoshaji wasipotoshe) kama una manufaa kwa taifa huo upotoshaji utatoka wapi?

Maji na mafuta huwezi kuwaweka pamoja.
Labda ungesema wenye mali tusije tukaulaani zaidi ijapo tunailaani.
DP wanaanza kazi hapo bandarini na tuone kama mapato yatakayoongezeka hayatawasaidia ndugu zake huyu askofu mchochezi na mbaguzi aliyejaa udini.
 
"Wabongo maarifa madogo", ni hao viongozi, siyo waTanzania. Kazi ya kuongoza nchi ni kuwawezesha wananchi wako wafanye juhudi kwa maarifa kumudu mahitaji ya kuleta maendeleo nchini mwao, siyo kila siku kuzurura duniani kwenda kutafuta watu wa kuja kukulea wewe.
Korea Kusini hawakufikia hatua waliyofikia kwa kutegemea mataifa mengine, au watu wengine toka nje kuja kuwafikisha hapo walipofikia leo.
Bandari, unakwenda kuchukuwa mkopo kuikarabati, halafu unamgawia mtu mwingine kwa miaka 30 avune hapo, na wala huna mipango yoyote ya kujiandaa kuwa na uwezo wa kuiendesha bandari baada ya hiyo miaka 30, hii ni akili matope kabisa.
Misitu, hata kuwaamini wananchi wako kupanda na kutunza misitu inabidi kwenda kutafuta watu nje...!
Mkuu, Ntamusana, wakati mwingine tuwe tunaweka ushabiki wa kisiasa pembeni na kuyatazama maswala ya nchi yetu inavyostahili kuyaona.
Kamwe hatuwezi kuwa watu wa kutegemea kuja kufanyiwa tu na watu wengine toka nje bila ya kufanya juhudi zetu wenyewe, hata kama ni kidogo, za kurekebisha tunapojiona hatuwezi. Makundi yaliyopo pale bandarini yanayokwamisha shughuli za bandari; kweli viongozi wa nchi hii hawana uwezo wa kuyashughulikia makundi kama hayo? Na siyo bandarini tu, ni kila sehemu. Hebu jaribu kidogo kufungua akili yako.
Sisemi hata mara moja kuwa uwekezaji hautakiwi, lakini uwekezaji ni njia ya kusaidia juhudi zetu sisi wenyewe, kwa lengo la kupata uwezo mkubwa kadri tunavyosonga mbele.
Hatuwezi kila mara tuwe tunazungushana tu katika mambo muhimu kama haya, kwa sababu tu za kishabiki za kisiasa; au zingine zozote zinazotufanya tuwe mashabiki. Tanzania ni muhimu zaidi ya ushabiki wa aina yoyote ile; hata uwe wa kiimani, kijinsia, kikabila ,n.k..
Lengo la DP World ni kurahisisha ufanisi wa kazi hapo bandarini na kuongeza tija.

Hizi riwaya ndefu kila mtanzania anaweza kuziandika hata hao wanaofanya shughuli haramu za kupora viwanja vya watu wanaweza kuzifanya.

Sio kazi rahisi kujitegemea kwa mujibu wa ngonjera zetu.

Kwanza tuelewe bandari zinafanya vipi kazi ili kuweza kuelewa maana ya kinachofanyika hapo bandarini.
 
Of course ndicho alichokuwa anakitafuta. na wakifanya hivyo wamempiga teke chura. siasa ni timing tu.
Hakuna timing hapo… kwanza anadhalilisha ukristu, pili anadhalilisha chadomo, wanaruhusuje mtu wa hovyo hivi jukwaani kwao?
 
Back
Top Bottom