Huku ni kukomoana, sijawahi kuona wala kusikia kama hili duniani, TRA mjiangalie

Huku ni kukomoana, sijawahi kuona wala kusikia kama hili duniani, TRA mjiangalie

Ni kweli mkuu RRONDO ila afisa alipaswa kumpa elimu sahihi na njia ya kutoka hapo. Naamini hili lingetokea asingekuja mitandaoni.

Raia tuna udhaifu na maafisa wana udhaifu matokeo yake ndo haya. Kuviziana na kukomoana. TRA anakosa kodi na mfanyabiashara ninakosa uhuru wa kufanya biashara
Yaani ni kuviziana na kukomoana. Umesahauvku file kikodi cha 500,000/- utapigiwa hesabu na interest tangu 2015 uliyisahau ku file. Sasa huu kama sio uchawi ni nini? Yaani nikiona hawa watu najisikia kutapika kabisa.
 
Pamoja na umachinga wangu, bado nikasema nisaidie nchi yangu kwa kulipa kodi, nimechukua tin namba nikakata leseni nikafungua kiosk, nikakadiriwa nilipe laki nne kwa mwaka, kila miezi mitatu 100,000/=.

Nimelipa vizuri mara tatu, mara ya nne nimechelewa kwasababu zilizo nje ya uwezo wangu ikiwemo biashara kuchechemea,

Wiki iliyopita nikakopa ili nilipe deni la serikali nakuta kuna 100,000/= principal,
1500/= riba na 150,000/= adhabu au faini ajili ya kuchelewa kulipa,

Hivi kweli mimi nitafanya biashara halali tena?

Serikali na nyie tra mjiangalie sasa
Hivi mnadhani wanapojisifu kuvuka lengo la makusanyo inakuwaje? ni kukamua haswa na kudhurumu ndani kwa ndani ,yaani punda afe mzigo ufike
 
Kwa nini ufunge biashara? Hapa kilichotokea ni kukiuka sheria kwa kutolipa tarehe husika. Hesabu hiyo ni hasara lipa hiyo fine pamoja na wanachostahili.

Cha kukushauri kwa kuwa tayari una faini kwa kuwa umevusha mwezi Unaweza amua kuizungusha hiyo pesa mpaka tarehe 28 huko ndio uwalipe pmoja na fine ila usivushe kwenda mwezi wa pili utakutana na penalty nyingine. Huenda ndani ya wiki mbili inaweza kuwa imekuletea hata 40,000 au zaidi ikitegemea biashara yako.

Kufunga biashara kwa changamoto ya siku moja utakuwa uzembe wa hali ya juu.
Nafunga biashara kihalali, naenda kufanya biashara kitaalamu kama wafanyavyo wengi halafu tuone nani atapata na nani atakosa, hii tra imezidi sana kuonea wanyonge,

Nilienda mwenyewe tra na kurasimisha biashara ya mtaji wa mil saba ndio nipigwe faini kubwa kuliko deni?
Uzalendo huo umenishinda

Asante kwa ushauri
 
Nafunga biashara kihalali, naenda kufanya biashara kitaalamu kama wafanyavyo wengi halafu tuone nani atapata na nani atakosa, hii tra imezidi sana kuonea wanyonge,

Nilienda mwenyewe tra na kurasimisha biashara ya mtaji wa mil saba ndio nipigwe faini kubwa kuliko deni?
Uzalendo huo umenishinda

Asante kwa ushauri
Sawa kila la heri ila kuna level ukifika tu utajikuta uko mikononi mwao
 
Yaani ni kuviziana na kukomoana. Umesahauvku file kikodi cha 500,000/- utapigiwa hesabu na interest tangu 2015 uliyisahau ku file. Sasa huu kama sio uchawi ni nini? Yaani nikiona hawa watu najisikia kutapika kabisa.
Hahaha
 
Mkuu pole sana.
Umejaribu kulima mahindi kijijini?
Kule hakuna kodi za mjini.
 
Ccm wezi, wafanyakazi wa serikali wezi, wafanyakazi wa TRA ndio majizi makubwa unawalipa kodi ya nini hao wangese, dawa ni kukwepa mpaka wakukamate...
 
Je, ilitoka Taarifa Kwa mamlaka husika juu ya Madhira yako ya kiuchumi na mategemeo yako ya uchelewaji Wa ulipwaji Wa Deni???

Sasa umepangwa nyumba ya Mtu, Mda Wa kulipa na tarehe zinakaribia Mpaka zimepita umwvunga Tu kana Kwamba nyumba ni Yako, mwenye nyumba kaamua kukurushia Vitu nje unaanza kulalamika kuwa ni mbaya.

Watanzania tunatabia ya kuchukulia Vitu poapoa...

Tanzania ni nchi salama Kwa Uwekezaji, Biashara na ujasiliamali tena Kwa Kodi nafuu.

Nchi zingine za watu, Sasa hivi ungekuwa unaangaika na kutafuta mawakili. Na wakati huo Kodi ni 35% bado mapenati.

Tusikimbilie Tu kulalamika, Je, tulijaribu kutimiza wajibu itupasvyo??
 
Shida ni kujazana ujinga, mada za kodi zinataka uelewa wa sheria za kodi.

TRA awawezi amka asubuhi na kuamua wanakudai kiasi gani, sheria lazima itasema ukichekewa kulipa how much they can charge you.

Laki nne kwa mwaka, wewe ni mlipa kodi wa aina gani?

Kodi zipo tofauti VAT na income tax.

VAT Tanzania ulipi kama una mauzo ya tsh 200 million. Income Tax uwezi pangiwa it’s based on percantage.

Mada ni hadithi tupu.

Labda elezea hiyo kodi gani ambayo TRA wanaweza panga.

Uongo mtupu
 
Hii taasisi for the most part inaendeshwa ki unprofessional sana. Kuna mwaka nilienda kumsajilia jamaa yngu biashara yake. Nikafika nikawaelezea vizuri kabisa hawa maafsa mchongo nao wakajidai wamenielewa. Sasa baada ya kuwakabidhi nyaraka zote za mshkaji wakaziingiza kwenye system dakika za mwisho wakaniambia sasa unatakiwa uweke kidole gumba hapo mimi nikashangaa sana!
Nikawauliza hii inakuwaje taarifa za mtu mwingine then mimi niweke biometric zangu si italeta shida? Wakasema hapana haina shida kuthibitisha akaniita kwenye screen kabisa kunionyesha taarifa za jamaa kila kitu kimekamilika..... Kishingo upande nikapunch japo nilikuwa na mashaka sana akilini WTF mistake??
Siku naenda kufungua tin yangu sasa nikiwa wilaya nyingine kabisa ofsa anaangalia kwenye system akaniambia wewe kupata tin kuna changamoto mfumo unakataa namuuliza sababu nini akasema ata yeye hajui. Hangaika sana pale ikabidi nimweleze ile scenario miaka kadhaa nyuma ya jamaa yangu akaniambia nimtajie hiyo tin ya jamaa yalaaaah!.... System inaonesha picha yangu na fingerprint ila majina na taarifa zingine zote za jamaa dah nikasema hii nilijua tu ni bomu hili ila ms*nge yule dada nikamwambia akajifanya hamna tatizo lolote we punch tu kumbe wakati napanch akanipiga na picha aisee

Wenzetu mbele taasisi kama hizi zina WELEDI sana nashangaa huku kwetu sijui ni kama tumerogwa vile... Hii kitu imeniletea shida sana dah sitamani kabisa kukumbuka.
 
Back
Top Bottom