Huu mdahalo lengo ni nini? Mdahalo unaitwa “Jesus and Mohammed”

Huu mdahalo lengo ni nini? Mdahalo unaitwa “Jesus and Mohammed”

Mimi nakufuatisha wewe uliyesema kwamba Yesu sio Mungu kwa kutumia mstari wa MATHAYO 6:9 ambapo katika huo mstari Yesu anawaagiza watu wamwite Mungu "Baba". Nimekuuliza kama Yesu ni muislamu kwa nini anaagiza watu wamwite Mungu "Baba" wakati Quran inakataza ? Sasa usiniulize kama nina uhakika hayo maneno alitamka Yesu wakati huo mstari umeuleta wewe.

Labda useme umekosea kuuleta huo mstari, ungeleta mstari unaouamini kutoka Quran. Unashindwa kujibu swali langu badala yake unazusha maswali ambayo ulitakiwa kujibu mwenyewe uliyeleta hiyo verse. Ni hivi;
1. Ama Yesu sio muislamu na Quran sio kitabu cha kuaminika
2. Au Yesu ni muislamu na Biblia sio kitabu cha kuaminika

Vinginevyo ukinikuu mstari wowote kutoka Biblia kujenga hoja, assumption ni kwamba unakubaliana na hicho kitabu from which you quoted the verse.

Kwa mtazamo wa Quran, monotheism ni muhimu sana. Inaonekana kwamba kwa mtazamo wa Quran, kama watu watamwita Mungu "Baba', wanaweza kuanguka katika aina ya mawazo ya kuchanganyikiwa kwamba Baba ni baba wa Yesu, kwa maana halisi ya mwana na baba kama walivyofikia wakristo kumwita Yesu kuwa ni mwana wa Mungu.

Ikiwa Yesu ni mwana wa Mungu, kwa maana halisi, basi lazima awe kama Mungu na labda anastahili kuabudiwa pia.

Ili kuepuka mkanganyiko wa aina hii, Qur'an inachora mstari ulio wazi na kumtaja Mungu kama Rabb na kama Mola pekee.

Ingawa hakuna maelekezo ambayo yanasema kwamba Muislamu hawezi kumwita Mungu "Baba", Quran inaelezea wale wanaosema, "sisi ni watoto wa Mungu". Qur'an inauliza swali na kuuliza, "Kwa nini Mungu awaadhibu ikiwa nyinyi ni watoto wake?"

Utamaduni miongoni mwa Waislamu uliendelezwa kwa njia hii, ili tusimrejelee Mungu kama "baba".

Tunamwita yeye kama Bwana na Muumba. Hatusemi Ab, lakini tunasema, Rabb, Mtunzaji wetu. Yeye ni wa mwisho na wa mwisho. Ikiwa tutaanza kumfikiria kama Baba, basi hii inaweza kuleta fikra kama sisi ni watoto wa Mungu na tuna haki juu yake.
 
Zakir Naik anatembeleaga nchi nyingi sana mkuu hata ukiwa unascroll youtube one time moja lazima ukutane nae, wewe achana na kina mazinge mkuu fika kwenye tarehe hizo. Unasemaga fulani hajakutana na wewe. Sasa huyu sheikh katoka huko kaja bongo kaka. Mambo yasiwe mengi fika na maswali yako, mimi ntafatilia kwa makini sana nisikie majibu


View: https://x.com/jaliluzaid/status/1871401246114115996


Kila la kheri

Hana majibu yoyote huyo .....maswali yangu nikiyauliza hadi huyo niliye muuliza huanza kutilia shaka alicho kiamini toka mdogo na kupoteza amani ya dini yake mwenyewe
 

1735490970993.jpeg
 
D
Hata Sheikh wetu nchini Tanzania, mwanazuoni Sheikh Abuu Iddi ambaye ni Msaidizi wa Mufti wa Tanzania aliwahi kuonya juu ya dhehebu moja kuanza fitna, misuguano, kutishiana n.k dhidi la dhehebu jingine, wakati wote ni dini moja ya ki-Islamu..

19 January 2023
Dar es Salaam, Tanzania

SHEIKH ABUU - HATARI INAKUJA TUSIPOTOA TAHADHARI KWA HAYA YANAYOENDELEA



Sheikh Abuu Iddi ambaye ni Msaidizi wa Mufti wa Tanzania ametoa tahadhari hiyo kwa kuwa inaweza kupelekea amani kuvunjika nchini Tanzania.

Sheikh Abuu Iddi CV (wasifu) yake imesheheni nyadhifa kadha wa kadha sawia na maktaba yake binafsi iliyosheni mabuku juu ya mabuku ya elimu duniya na ilm ya dini pia ktk utumishi ulitukuka kwa dini na jamii.

Pia sheikh Abuu Iddi ni imamu mkuu msikiti wa Masjid Mnyamani Buguruni jijini Dar es Salaam. Pia kwa miaka 16 amekuwa akiendesha kipindi ktk kituo cha televisheni cha Channel Ten kutoa daawa na darsa, mratibu Al Risala Foundation, Mratibu wa Kudumisha Amani katika mkoa wa Dar es Salaam, Mwandishi wa kitabu kinachokwenda kwa jina Misingi 15 ya amani, mwandishi wa makala katika gazeti kubwa la Mwananchi pia ni Mshauri wa dini na jamii wa Mufti Mkuu wa Tanzania.

Sheikh Abuu Iddi ameelekeza tahadhari hii hususan kwa madhehebu ya Sunni Saudia na Shia linaloegamia Iran, Pakistani, India yanayo shambuliana kupitia propaganda kutoka maeneo mbalimbali ya dunia ya mitandao ya kijamii wakiongozwa na viongozi wao wenye ushawishi wa kisiasa wa ndani na nje ya nchi kuchochea misuguano

Madhehebu ya kiislamu na Madhehebu ya kikristo yote ni dini moja kwa sababu dhehebu maana yake ni kusanyiko.la kishetani ...mungu hana madhehebu kwa sababu yeye ni mmoja nafsi moja
 
Hujalazimishwa kwenda kwake njoo hapa Mtoro kuna wahadhiri wengi tu akina Mazinge watakupa majibu
Thubutu mazingi huyu huyu chenga ndiyo anijibu maswali yangu kama yupo hapa JF muiteni tena nitachagua marefa waislamu wenzake.......wewe ujagundua kuwa waislamu hata wa humu jf unikwepa ? Mimi siyo wakristo wajinga jinga wanao danganywa na wapumbavu kina mwamposa na gamanywa na gwajima boy....
 
Hujalazimishwa kwenda kwake njoo hapa Mtoro kuna wahadhiri wengi tu akina Mazinge watakupa majibu
Wewe ni muislamu au la...kama ni muislamu niambie nikupe swali moja ukamuulize shekh wako alafu uje utupe majibu hapa
 
Thubutu mazingi huyu huyu chenga ndiyo anijibu maswali yangu kama yupo hapa JF muiteni tena nitachagua marefa waislamu wenzake.......wewe ujagundua kuwa waislamu hata wa humu jf unikwepa ? Mimi siyo wakristo wajinga jinga wanao danganywa na wapumbavu kina mwamposa na gamanywa na gwajima boy....
Wewe ndiye hata ukristo huujuwi kabisa ,umoumo na ubishi usio mashiko
 
Hana majibu yoyote huyo .....maswali yangu nikiyauliza hadi huyo niliye muuliza huanza kutilia shaka alicho kiamini toka mdogo na kupoteza amani ya dini yake mwenyewe
unaingia mitini, uganda, kenya watu wameuliza maswali - majibu mi mpaka swali liulizwe, ila wewe unatengeneza mazingira ya kuingia mitini. Unafeli sana maana yeye anasema anapenda maswali mazito na wewe unasema una maswali mazito. Kikichobaki ni wewe kufika mkuu
 
Wewe ni muislamu au la...kama ni muislamu niambie nikupe swali moja ukamuulize shekh wako alafu uje utupe majibu hapa

Anza wewe kunijibu ,kama ni mkristo, lete aya ni wapi yesu alimfufua mtu
 
Wewe ndiye hata ukristo huujuwi kabisa ,umoumo na ubishi usio mashiko
Siujui ukiristo 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 kuna jamaa hapa hapa jf alianzisha uzi kuelezea 666 mbona qliukacha uzi hadi watu wakawa wanashangaa au niutafute ule uzi uone mkristo mwenzako alivyo toka mbio
 
unaingia mitini, uganda, kenya watu wameuliza maswali - majibu mi mpaka swali liulizwe, ila wewe unatengeneza mazingira ya kuingia mitini. Unafeli sana maana yeye anasema anapenda maswali mazito na wewe unasema una maswali mazito. Kikichobaki ni wewe kufika mkuu

Mnaanza kuharisha hapa JF , kiingilio ni bure mnapapatika kitu gani ??
 
Back
Top Bottom