Huu ndo Ushahidi wa Nchi za Magharibi zinavyotusaidia. Anayewatukana na kuwasimanga muonee huruma sana!

Ni kweli nchi za magharibi zimekuwa zikitoa misaada, lakini hiyo missada inatolewa na msharti ambayo mwisho mnufaika mkubwa anakuwa ni mtoaji msaada. Kumbuka nchi kama Kenya ilipata uhuru 1962. Tanzania ilipata uhuru 1961. Mwaka 1962 uchumi wa Kenya ulikuwa unalingana na wa Korea ya kusini. Uchumi wa TZ uliukaribia ule wa Vietnam (kabla haijachakazwa na Maarekani). Leo nchi hizo mbili zina uchumi wa juu sisi bado maskini wa kutupwa. Misaada mingi ililenga kututia ganzi tuendelee kuwa tegemezi. Na tumerudi huko na sasa tunapewa mikopo left and right bila kukumbuka tunakiwa kuilipa.
Tunapopata mikopo toka magharibi au mashariki tunawakaribisha kchimba madini yetu bure, kwa sababu tunakubali mikataba mibovu ambayo ukifurukuta unafirisiwa. Kwanza unatupiwa chambo (msaada), alafu wanakuja kuchimba madini kwa mkataba waliyoandika wao. Misaada mingi tunaipokea bila kufikiria, hela ya msaada itakapokoma kilichoanzishwa kitaendelezwa vipi. Je kuna mpango mzuri wa takeover toka msaada. Kama huna njia ya kuendesha mradi baada ya hela ya msaada kukauka, itakuwa sawa na bure. Lakini mwenye msaada alishapata mgodi atakaochimba kwa masharti yake kwa miaka 50. Baada ya miaka 50 unaachiwa shimo, michanga, na kemikali (enironmental hazards)
 
 
Haifiki hata Trilioni 3 Kwa mwaka
 
Inafikirisha sana kumkoromea anayekusaidia kila siku, tena mtu ambaye anajaribu kukukumbusha kuwa unachofanya sio sahihi. Inatakiwa tuwakoromee tukiwa tunajitegemea 100% kama China.
Mzungu hakusaidii chochote mzee.
Tena huyu mzungu ndio kakuzuia wewe kuendelea.
Wewe bora umshukuru Mchina ambaye kakubali kufanya biashara na wewe ndio maana una miundombinu na maendeleo mengine.
Nenda kafuatilie sakata la SAP-Structured adjustment Program.
Nchi nyingi Afrika hususan sub Saharan Afrika ndio zilimalizwa kwa mtego huu wa SAP.
Halafu walivyo washenzi wakawa wanawaletea msaada wa vyandarua na madawa mkiwa hafifu kwa miundombinu na kila kitu.
Aliyewasaidia angalau Mchina kwa kukubali kuwafungulia hata hivyo viwanda vya kushona Chandarua.

Mzungu huwa anataka sisi tuonekane tegemezi kwake siku zote.
Mtu kama huyo hakusaidii bali anakutawala kikoloni mambo leo.
 
Hilo kibaraka ni jinga ni la kufurushwa 🇹🇿
 
Serikali ya Canada ina haki ya kusitisha misaada yake kwa yeyote, kwa sababu yoyote, au hata bila sababu.

Kwa sababu yenyewe ndiyo inatoa misaada hiyo.

Unataka kuilazimisha jinsi ya kutoa misaada yake?

Tengeneza uchumi wako usihitaji msaada. Laumu viongozi wako kwa kufanya nchi yako yenye utajiri mwingi kutegemea misaada.

Kwa nini unailaumu serikali ya Canada kwa kujipangia yenyewe itoe misaada kwa nani na kwa sababu gani? Hiyo ni haki ya serikali ya Canada.
 
Mkuu mtu akija kwako anachuma mchicha wa 500 anauza halafu baadae anakuletea 200 jioni hakusaidii, hao wanahitaji Africa zaidi kuliko Africa inavyowahitaji wao. Mentality zenu hizo ndio za Kutojitegemea ndio zinafanya kila siku bara lipo gizani.
Kwa hio suluhisho ni kuwafurumusha wote na tufunge balozi zote kisa tu wamesema ule uuaji na utekaji ufanyiwe uchunguzi wenye majibu yanayoeleweka kisha somebody nanii anawaambia wasimwambie wala wasimuelekeze cha kufanya yeye mboni kwao kukiungua huko hata rais wao akiapishwa huko hasogezi pua yake na hajawahi kukanyaga kwao hata wanaowawakilisha wasimzingue wao wanapokua na mambo yao huko yanaendelea hawaingilii anawaacha wafanye wanavyoona wao kwanini yeye wanamuingilia yaan wasimuingilie muingilie nyumbani kwake wamuache na nyumba yake
 
Kwani anayepereka bakuri si ni wewe? We tulia uone kama watakufuata, walidanganya uchaguzi Zanzibar wakasitisha REA karibu miaka 5, ilirejea tena baada ya kupiga magoti.
Aliyepiga magoti si huyu mama yenu kizimkazi??
Mbonga hiyo REA ilipositishwa hakukuwa na shida tukawa tunajimudu!?
 
Haifiki hata Trilioni 3 Kwa mwaka
Naona unauona ukweli ila unajifariji kwa unazi tu🤣🤣🤣

Hao jamaa hapo hazijawekwa hela wanazoingiza ili watoto wenu wa shule za msingi wapate chakula mashuleni.

Kwa ufupi wakikata misaada tumeisha. Na anawasimanga hatumii akili zake vizuri.
 
Hapa kwa bandari natofautiana na wewe......ila twende mbele na hao wanaowasema vibaya nchi za magharibi. Hakika hawajitambui......na kwa hili bandiko umewaacha midomo wazi 😀
Ninyi mnaowasifia wazungu ndio hamjitambui.
Pia inaonesha mnapimia mambo kiutoto sana aisee.
Hata history inaonekana mlifeli darasani.
Hao wazungu kwa mwamvuli wa msaada wa kifedha ndio wamewafikisha hapa.
Embu nitajie,kuna kipi kikubwa ambacho mzungu amekufanyia ambacho ni potential hadi sasa??
Kwani alishindwa kuzindua kiwanda cha chandarua hadi aje akuletee msaada wa vyandarua??
Hapo tu akili yako haiamki??
 
Kwani hata mkipewa viwanda mnaweza kuviendesha? Kiwanda cha dawa cha kibaha kimefikia wapi?

Nyie ni wajinga tu! Hata kujiongoza kwenyewe hamuwezi
 
Hayo ni maneno tu hata kwenye kanga yapo. Weka ushahidi wa wanachopata. Acha maneno matupu
Ulisoma mikataba aliyoivunja ama kuisitisha Magufuli!??
Pia uliwahi jiuliza kwanini Magufuli alisisitiza uranium kutokuchimbwa sasa hivi??
 
Ulisoma mikataba aliyoivunja ama kuisitisha Magufuli!??
Pia uliwahi jiuliza kwanini Magufuli alisisitiza uranium kutokuchimbwa sasa hivi??
Huyo mzee wako ndo alikuwa mjinga wa mwisho. Ndo mana wakamshughulikia
 
Sijui mpaka lini tutakuwa hivi?
Huku kila kiongozi anaengia madarakani anasema sisi ni tajiri
Ila kusema la haki kujisifia umasikini ni Laana pia
hivi unafikiri sisi ni masikini wa mali ama masikini wa akili..??
 
Kwani hata mkipewa viwanda mnaweza kuviendesha? Kiwanda cha dawa cha kibaha kimefikia wapi?

Nyie ni wajinga tu! Hata kujiongoza kwenyewe hamuwezi
Mbona mambo kibao yanaenda kwa ushirikiano wa China na mambo yanasonga??
Kwanini wamagharibi wasifanye kama China we do business with mutual benefit??
Shida yako akili kisoda.
Una akili mgando.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…