Huu umati ni kielelezo cha jamii iliyokata tamaa, inayotegemea miujiza ya mafuta itoboe!

Huu umati ni kielelezo cha jamii iliyokata tamaa, inayotegemea miujiza ya mafuta itoboe!

ingekuwa ni nyomi ya ZUCHU na Mondi hapo ungetoa sifa kedekede we jingalao!

These people did not commit any crime you Son of a beach!

Let God be God we are healing our problems through him
What kind of problems have you been healed through him?

Wakati hao watu wakitoka hapo hata hela ya nauli hawana wametoa zote sadaka ya kujimaliza?

Wajinga ndio waliwao.
 
ila wakienda kutafuta msaada wa kutatuliwa shida zao kwingine mnaona nongwa.
Shida gani Wewe ni Akili tu, Mwoposa ana Akili anatumia Akili kwa wasio na Akili unaambiwa kuna karatasi 2 moja ni plain una pewa bure Ila ya pili Ina maombi 12 sema sio bure Wewe unachagua ipi? Unauziwa karatasi yenye maombi 12

Km kweli wewe una Akili unachagua plain au yenye maombi 12 na kumbuka hayo maombi 12 sio ya kwako ni maombi ya Mwoposa kwa hio kila mtu ana maombi yake kwa Mungu wake Ila wote mnajumuishwa kwenye OMBI 1 ambalo limeandaliwa na Mwoposa Jamaa ana Akili sana, hapo bado hajawauzia mafuta Chupa ndogo 1000 yaan Chupa ni ndogo ukipaka siku 2 imekata ukalipe tena 1000 upewe mengine aisee Jamaa Akili kubwa Mc mapesa
 
ingekuwa ni nyomi ya ZUCHU na Mondi hapo ungetoa sifa kedekede we jingalao!

These people did not commit any crime you Son of a beach!

Let God be God we are healing our problems through him
Hapana. Hili la Mwamposa ni kielelezo cha jamii yenye matatizo na haijui yanasababishwa na nani/nini au wafanye nini kuyatatua. Maskini hawa wanadhani huyu tapeli ana uwezo wa kuyatatua. Mungu hatatui matatizo kwa njia hii. Mbona Ulaya watu hawaendi nyumba za ibada lakini wana maisha mazuri?
 
Watu wana matatizo ya kimwili na kiroho ambayo wamehangaika kwingi bila mafanikio.

Wewe ukiona watu wamejaa baa, kwa sangoma, viwanja vya mpira au matamasha ya wasanii mnaona sawa, ila wakienda kutafuta msaada wa kutatuliwa shida zao kwingine mnaona nongwa.

Watu wana shida, acha watafute ufumbuzi kwa njia rafiki. Wakufanikiwa atafanikiwa ambaye muda wake bado ataendelea kuwa na subra
Hapo ulipoandika; "wakufanikiwa atafanikiwa, ambaye muda wake bado aendelee kuwa na subra" ndipo mnapowaumizia ndugu, jamaa na marafiki zetu, wanaendelea kumiminika tu wakiamini siku yao ya miujiza iko njiani huku nyie mnakula tu sadaka.
 
Hapana. Hili la Mwamposa ni kielelezo cha jamii yenye matatizo na haijui yanasababishwa na nani/nini au wafanye nini kuyatatua. Maskini hawa wanadhani huyu tapeli ana uwezo wa kuyatatua. Mungu hatatui matatizo kwa njia hii. Mbona Ulaya watu hawaendi nyumba za ibada lakini wana maisha mazuri?
Jamaa kawawin sana Ila ndio ishakua hivyo utafanyaje ni suala zima la sayansi ya hesabu za Algebra MJINI kati pale wale wanaolala nje wote Jana walilala matanga kwa Mwoposa aligawa na Pilau bure au ndio aliwauzia Maneno matupu?
 
Wapuuzi kufanya kazi watoboe hawataki wanataka kukanyaga mafuta watajirike.
Hawa wachina walioishika dunia kwa uchumi wanachapa kazi hatari.
Waafrika wapumbavu wako kwenye mikesha ya kuomba utajiri.
Yes Mkuu watu wanataka tu miujiza watu wanataka waokote nyumba waokote Gari waokote viwanja waokote mke/Mume yaan iwe tu mseleleko vuuvwaaa wamepona Gono Sugu miujiza
 
Jamaa kawawin sana Ila ndio ishakua hivyo utafanyaje ni suala zima la sayansi ya hesabu za Algebra MJINI kati pale wale wanaolala nje wote Jana walilala matanga kwa Mwoposa aligawa na Pilau bure au ndio aliwauzia Maneno matupu?
Mkuu mimi sina cha kufanya bali ni kushangaa jinsi nchi ilivyojaa wajinga. Huyu jamaa ni tapeli wa kutupwa na kuweza kuvuta umati wa watu wengi namna hiyo eti wanafuata miujiza ya kuondoa shida zao na kuponywa magonjwa ni uhayani usiosemekana.
 
Kwa akili hizi no way tutafika mbali kama taifa. Kuna wakati naamini hata wanasiasa wanafurahi kuona watu wakijiingiza kwenye imani namna hii, they'll rule us as they are pleased, wanatuambia tuwe watu wa imani, tutii mamlaka ili mamlaka ziwe huru kuiba, kupora, kufisadi na kufanya kile wanachotaka kututawala.

In this case usotegemee kuwa na taifa la watu wanaohoji, wanaodadisi coz tunajengwa kwenye misingi ya MIUJIZA. Yaani ili ccm itoke madarakani ni lazima itendeke MIUJIZA, wenzetu wanaingia front kuikabili serikali sisi tunasubiri MIUJIZA.

Watu wamechoka balaa, akili zimeshikwa na mafuta, maji na sadaka za kujimaliza.
 
Back
Top Bottom