Huwa mnawashughulikiaje watoto wanaokuwa na tabia kama hii?

Huwa mnawashughulikiaje watoto wanaokuwa na tabia kama hii?

Tafuta mshkaji mmoja mtaani. Kila mtaa kuna mwana mwenye taarifa za kila mtu. Mpe pesa huyo mtu kama 10,000 tu akuletee taarifa za dogo. Haitamaliza hata wiki utajua mishe zote za dogo lako.
Kwakweli itabidi tufanye hivyo mkuu
 
Yupo hatua ya kubalehe; katika hatua hii anaweza kujiunga na makundi ambayo si mazuri kama hakupewa tahadhari katika umri huo.
 
Yupo hatua ya kubalehe; katika hatua hii anaweza kujiunga na makundi ambayo si mazuri kama hakupewa tahadhari katika umri huo.
Kwahiyo tunatakiwa kufanya nini ili kumsaidia asiangukie huko kwenye hayo makundi yasiyo mazuri
 
Kwakweli itabidi tufanye hivyo mkuu
Yaani hii mbinu ni kama unafanya diagnosis...majibu utakayoyapata hapo utajua pa kuanzia yaani polisi, kuzungumza naye, hospital kupima magonjwa au kwa mwana saikolojia. Kumbuka unaweza kumuitia polisi ndo ukamkosa kabisaa. Cha kwanza ni kujua unadili na nini? Fanya hivi kwanza kabla hujachukua hatua yoyote ya kivitendo.
 
Yaani hii mbinu ni kama unafanya diagnosis...majibu utakayoyapata hapo utajua pa kuanzia yaani polisi, kuzungumza naye, hospital kupima magonjwa au kwa mwana saikolojia. Kumbuka unaweza kumuitia polisi ndo ukamkosa kabisaa. Cha kwanza ni kujua unadili na nini? Fanya hivi kwanza kabla hujachukua hatua yoyote ya kivitendo.
Sawa, nmekuelewa mkuu Asante kwa ushauri mzurii 😊🙏🏼
 
tatizo ni kwamba baba tumemshirikisha na hafanyi lolote anasema tumuache tu kama alivyosema mwenyewe..na bad luck nyumbani hatuna mwanaume mwingne zaidi ya yeye na baba tu
Inawezekana dingi ana plan zake pia na hiyo kitu pia inamvuruga ila anajaribu kuitafutia ufumbuz sema labda hatak kwenda naye resi ndio maana anasema mwacheni.
Je ni mtoto wa kiume peke yake?
 
Kwahiyo tunatakiwa kufanya nini ili kumsaidia asiangukie huko kwenye hayo makundi yasiyo mazuri
Mzee ndio anatakiwa awape ushirikiano, ikishindikana, fuatilieni mienendo yake pamoja na marafiki anaokutana nao, alafu mkabizini kwa ndugu yenu wakiume, wajomba n.k wamrekebishe, iwe kwa viboko au kwa ushauri.
Kwa nyie wenyewe, itakuwa ngumu; na kama alishaanza kutumia bangi/dawa za kulevya ndio tatizo zaidi.​
 
Habari wanajamvi...

Nina imani humu kuna wazazi ambao walishawahi kua na watoto wenye tabia kama hizi naombeni msaada wenu wa mawazo na ushauri unisaidie na mimi.

Binafsi nina mdogo wangu aliyenifuata wa kiume, ana miaka 17...huyu mdogo wangu alikua ni mpole Sanaa, akiwa nyumbani ni mtu wa kushinda ndani mda wote ni kusoma kula na kulala, mara chache sana unaweza kumkuta anaangalia movie hata marafiki zake ni mpaka waje nyumbani kutembelea ndo apige nao story bila hivyo hatoi mguu nyumbani labda aagizwe mahali..

Shida kwamba sikuizi( yani miezi hii hapa miwili) amebadilika sana hadi tunaogopa,, amekua ni mtu wa kuondoka nyumbani bila kuaga na akiondoka asubuhi harudi nyumbani msipompigia simu anaweza asionekane kabisa hadi usiku,, sometimes tukimpigia simu anaweza akapokea halafu akajibu kwa ukali kua tusimfatilie na maisha yake, hataki kula chakula nyumbani, amekua ni mtu wa kufokafoka tu mda wote hadi mama akimuuliza kitu anajibu kwa kufoka tu sio kama alivyokua zamani.

Saizi amefikia hatua kwenda kanisani pamoja na sisi hataki anasema tumuache., alikua anaumwa hakutoa taarifa mpaka anapona na hatuelewi alikua anaumwa nini yani tumefanya tu kustukia kumwona anakunywa dawa, kuna mda alivyoondoka mama akaingia chumbani kwake kukagua akakuta dawa nyingi sana, hata hatuelewi zinatibu ugonjwa gani., baada ya mama kumuuliza alikua mkali sana na ametupigia marufuku kuingia chumbani kwake hata kama ni kufanya usafi.

Ajabu ni kwamba tukimuelezea baba tabia za huyu dogo sikuizi wala hata hatilii maanani anasema tu muacheni kama alivyowaambia mumuache...hasa tatizo ni lipo kwa mama amekua na wasiwasi sana na mabadiliko ya huyu mdogo wangu yani pressure inampanda mda wote, akijaribu hata kukaa nae chini kuongea nae dogo hataki kumskiliza yeyote zaidi ni anakua mkali ukimsogelea jirani anaweza akupige makofi...

Naombeni msaada wenu wa mawazo ili niweze kumsaidia huyu mdogo wangu maana napata shida sana kumuona mama akiwa na wasiwasi mda wote 🙏🏼
Leteni mabinti cousins wakae hapo nyumbani atatulia huyo.

Wakishindwa hao kumfanya akae nyumbani muelewe kuwa ana kampani mbaya huko nje.
 
Pole sana huyo anapitia stress kali sana,uenda kushindana kwake ndani kukamnyima fursa ya kujifunza vitu vipya.
So uenda alivamia madege yasiyoliwa.
Kujua ugonjwa gani tuma picha za dawa alizotumia tutakuambia ni ugonjwa upi
 
Inawezekana dingi ana plan zake pia na hiyo kitu pia inamvuruga ila anajaribu kuitafutia ufumbuz sema labda hatak kwenda naye resi ndio maana anasema mwacheni.
Je ni mtoto wa kiume peke yake?
Ndio wakiume yupo pekeyake tu
 
Mzee ndio anatakiwa awape ushirikiano, ikishindikana, fuatilieni mienendo yake pamoja na marafiki anaokutana nao, alafu mkabizini kwa ndugu yenu wakiume, wajomba n.k wamrekebishe, iwe kwa viboko au kwa ushauri.
Kwa nyie wenyewe, itakuwa ngumu; na kama alishaanza kutumia bangi/dawa za kulevya ndio tatizo zaidi.​
Sawa nmekuelewa mkuu
 
Pole sana huyo anapitia stress kali sana,uenda kushindana kwake ndani kukamnyima fursa ya kujifunza vitu vipya.
So uenda alivamia madege yasiyoliwa.
Kujua ugonjwa gani tuma picha za dawa alizotumia tutakuambia ni ugonjwa upi
Sawa Asante kwa ushauri
 
Tafuteni rafiki yake wa karibu atakuambieni ana shinda wapi au anashida gani.
Kujua rafiki yake nenda shule anayosoma omba ushirikiano na Mwalimu atakuambia swahiba wake ni nani,mtie ten swahiba wake atafunguka kuhusu maisha binafsi ya shule huyo ni mtu wa aina gani shuleni
Usikute ashavurugwa na mapenzi.
Umri wa 17 yupo kwenye stage ya ujuaji.
 
Akizingua wekeni hidden cctv camera mtap maongezi yake kwa phone mtapa jibu.
Umri huo Zaid ya stress za mapenzi hakuna zingine
 
Tafuteni rafiki yake wa karibu atakuambieni ana shinda wapi au anashida gani.
Kujua rafiki yake nenda shule anayosoma omba ushirikiano na Mwalimu atakuambia swahiba wake ni nani,mtie ten swahiba wake atafunguka kuhusu maisha binafsi ya shule huyo ni mtu wa aina gani shuleni
Usikute ashavurugwa na mapenzi.
Umri wa 17 yupo kwenye stage ya ujuaji.
Yuko likizo anasubiri kwenda form five mwezi ujao...marafiki zake pia tumeongea nao baadhi nao wanashangaa tu hawajui kakutwa na nini
 
Back
Top Bottom