Huwa mnawashughulikiaje watoto wanaokuwa na tabia kama hii?

Yuko likizo anasubiri kwenda form five mwezi ujao...marafiki zake pia tumeongea nao baadhi nao wanashangaa tu hawajui kakutwa na nini
Ishu ya mchangiaji juu ya makundi possible.
Tafuteni mtu amfatilie watu hawana kazi mjini hapa ukimpa elf 10 au 20 atakuambia Huwa anashinda wapi.
Kama ni mageto ya wahuni na mkafanya uchunguzi anakaliwa kijiji na kusemwa bila kuogopa.Mtu alisemwa akisemwa itafika mahali atasikia.
 
Huo ni umri wa makundi na mapenzi.
Japo zamani ilikua ni form two ndo watu uanza kuharibika form alikua anajitambua
 
Walikuwa nae karibu kachange gia ukubwani
 
D
Dogo kapigwa tukio na demu 😅😅😅😅so muda woote anahasira mfanyie counselling
 
Msipende kuwapeleka watoto wenu police kule hawana msaada ZAIDI watakuwa sugu.
Halafu ataingiziwa maroho ya kuingia police na jela.
Kama kwenu hakujawahi mtu kwenda police au jela kwann ufungulie mlango huo uje utese familia.
Lockup na jela ni laana kama katika ukoo wenu hamna asili ya kuingia jela au police ni vigumu kuingia zile ni kuzimu ndogo Kama haliwahi kuingia possible chance ni kubwa.
 
Achane masihara basi, mnataka kupigwa makofi na kitoto Cha miaka17! Huyo ni bakora tu, kumfanya atumbue kwamba bado ni Dogo.

Mimi mwenyewe baada ya kutoka boarding school, nilikuwa nafikiria nimeshamaliza kilakitu; nilikuwa siambiliki , jeuri, kiburi na wanawake kwa sana.
Kuna siku niliingia kwenye kumi na nane za mzee, nilitandikwa bakora nyingi sana.
 
MKUU MLIKIUA

kwa kuanzia chukueni hayo maganda ya madawa mukaulize pharmacy au ata mnaweza kugoogle mkapata jawabu anaumwa na nn
Hii kazi tulishaifanya kwa ndugu yetu mmoja hivi, tulikuta hivyohivyo tukaenda pharmacy kuuliza tukapata jibu, kumbe dawa za maumivu, tukauliza kwa rafiki yake alibundwa na masela kisa demu, kumbe demu alikuwa ndumilakuwili.

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Sawa,, nimekuelewa mkuu..Asante kwa ushauri mzurii 😊🙏🏼
 
Tiba ni kipigooo unapigwaa mpaka unahisi kufaa yani.
Mwalimu Kilimanjaro kafuata ushauri wako kapiga KAUA mtoto wa darasa la kwanza kakimbia sasa hivi anatafutwa na Polisi, unajua kila TATIZO linatatuliwa kwa kupiga nani kakwambia?
 
Hii huenda ikasaidia hii😌
 
Wewe ameshawahi kukufuatilia na vibwana vyako? Sio unamfuatilia yeye tu wakati yeye hana muda wa kukufuatilia
Aisee mkuu leo umejua kunikazia jamani 😃😃😃,, sawa hajawahi kunifuatilia😃😃
 
Mwalimu Kilimanjaro kafuata ushauri wako kapiga KAUA mtoto wa darasa la kwanza kakimbia sasa hivi anatafutwa na Polisi, unajua kila TATIZO linatatuliwa kwa kupiga nani kakwambia?
hafi cha motoo anakipataaa
 
Aisee mkuu leo umejua kunikazia jamani 😃😃😃,, sawa hajawahi kunifuatilia😃😃
Basi na wewe usimfuatilie hivyo kwani kuna tatizo hapo yeye anaishi maisha yake au unalala nae Chumba kimoja?
 
wavulana wakianza kusogelea uanaume wanapenda zaidi kushinda na wanaume wenzao, huyo alikuwa mkimya kwenye uvulana ila kwa sasa anasogelea uanaume, Nyumba yenu hiyo imejaa wanawake na mshua yupo bizi, haoni cha kumfanya abaki hapo, kwa sasa anashinda kwa wanaume wenzake ama siku nyingine anashinda gesti na demu wake, nyumbani kilichobaki ni kulala na kula tu.

Kwa sasa anashinda sana na wanaume wenzake ambao wengine tayari walishaondoka kwao wanaishi kwenye mageto, huko sasa huwa wanapiga story mtoto wa kiume inabidi ashinde na wenzake ama demu wake, kama anaishi nyumbani afanye jitihada ahame na asiruhusu mama au dada zake wampande kichwa ama kumfatilia fatilia maana ashakuwa mwanaume.

huyo mdogo wako ndio anaianza safari ya uanaume, sitashangaa hata chuo achague cha mkoa wa mbali ili apate geto awe na uhuru zaidi, na hizo dawa huenda ni ugeni wa mapenzi alipiga kavu huko gesti akapata ugonjwa, kwa sasa ameshajifunza umuhimu wa condom, kuna mammbo mengi anaendelea kujifunza atarudi kuwa poa tu.

Alafu sio mtoto huyo, acheni kuingia chumbani kwake kumsafishia chumba,
 
Basi na wewe usimfuatilie hivyo kwani kuna tatizo hapo yeye anaishi maisha yake au unalala nae Chumba kimoja?
Hapana mkuu,, nimekuelewa nitamuacha na maisha yake...lakini haifurahishi kumuona ndugu yangu akiwa hayuko sawa🥹
 
Sawa mkuu nimekuelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…