Huwezi kuchukua nchi bila SYSTEM kuwa upande wako

Unasema mfumo mbovu wa taifa wakati upinzani wenyewe ndo mbovu kuliko hata huo mfumo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
we unaona hao watu wa system walifanya maamuzi sahihi kumweka magu?
 
Ccm ndio system na system ndio Ccm,

kuwaambia wapinzani wajenge ushawishi kwa Ccm ili washinde ni kuwajaza ujinga.
 
we unaona hao watu wa system walifanya maamuzi sahihi kumweka magu?
Walikuwa sahihi nchi kulikuwa na ufisadi nchi angeshika KIONGOZI WA MAFISADI na aliyetaka kuwekwa na Mafisadi Lowasa tungekwisha na nchi kuirudisha mikononi mwa wanyonge ingetuchukua maelfu ya miaka tena kwa kumwaga damu

Walikuwa sahihi nchi ilishaangukia mikononi mwa mafisadi wachache ambao kutwa ilikuwa kukwapua tu kwa njia mbali mbali mwananchi wa kawaida alikuwa akidharaulika mno na kuonekana takataka tu

Ona sasa hivi kiongozi gani wa serikali aweza chezea mtu wa kawaida.Heshima ya utumishi wa umma kutumikia wananchi imerudi .YALE YA KUJITIA UNANIJUA MIMI NANI MTAANI YAMEISHA!!!

Zamani mfanyakazi wa serikali hakuwa wa mtumishi wa umma alikuwa mtumishi wa bosi wake tu wengine wote anawaona takataka tu

CHAMA CHA MAPINDUZI NI CHA MAPINDUZI KAMA YA KIJESHI ILA HUPINDUANA NDANI KWA NDANI

Kilichofanyika 2015 ni wanyonge wa CCM kuangusha na kupindua utawala wa mafisadi ndani ya CCM na ndani ya serikali na kuutupilia mbali
 

Hili nalo ni neno....

Lakini ungeenda mbele kidogo kwa kuwashauri wafanye nini ili wawe karibu na vyombo hivi...

Anyway, let me try say something as ushauri kwa wanaotaka kuiondoa CCM barabarani...

Jambo kubwa kabisa kulifahamu ni kuwa, ni ukweli usiopingika kuwa "SYSTEM IKIWA UPANDE WAKO", there's no way kuwa utashindwa kuchukua nchi....

Kinyume chake, " The SYSTEM" ikiwa against you, hata kama umeongoza kwa kura 90%, there's no way kuwa watakupa nafasi ya kuongoza nchi....

Kwa maoni yangu, nadhani kuna umuhimu wa kina Freeman Mbowe, Zito Kabwe na Maalim Seif Shariff Hamad kuona namna ya kuingia special agreements na "SYSTEM" ili kuwakikishia usalama wao mara watakapowapa nchi kwa kuzingatia maeneo yote muhimu watakayo yaweka mezani kama msingi (basis) ya makubaliano....

Ni ukweli usiopingika kuwa, watu wa SYSTEM na WATAWALA kwa umoja wao wametenda mengi ya ovyo na maovu kiasi ambacho hawatakuwa tayari kuona mtawala aliyepo chini ya CCM anaondoka maana likitokea hili wao pia wako hatarini.

Yaani wanaona ni bora zaidi wafe na shetani waliyenaye sasa kuliko kumkaribisha mwingine wasiyejua agenda zake kwao especially ktk kuwakikishia maisha yao baada ya mabadiliko hayo....!!

Kila mtu anaogopa mabadiliko. System nayo inaogopa mabadiliko yenye athari hasi kwao. Ni lazima kama hujaeleweka, wakuzuie kwa namna yoyote kupenya...

For sure, this is a difficult task to be done, but it is possible..

Kwa sababu, binafsi deep inside my heart, natambua kuwa hii kitu tunayoiita "SYSTEM" kwa maana ya vyombo vya ulinzi na usalama (polisi, JWTZ &TISS) hawaridhishwi na hawapendi kabisa jinsi mambo yanavyopelekwa ktk nchi hii kwa sasa chini ya uongozi wa serikali iliyoundwa na CCM....

Hii mtu apende kusikia au asipende, lakini ukweli ndiyo huu maana walio ndani ya system wengine ni rafiki zetu, tunaongea nao kwa njia zetu, wanasema haya waziwazi, hawafichi kitu....

Na pia nafahamu kuwa, ili kuzuia haya kutokea, watawala wa sasa wanajaribu kuwapa kila aina ya INCENTIVES wakuu wa taasisi hizi pamoja na affiliates wao ili kuwazuia na kuwashawishi wasije kuwageuka....

Mathalani; wafanyakazi wa taasisi hizi (polisi, JWTZ na TISS) kuanzia wakuu wao hadi wafanyakazi wa kada ya chini kabisa, wana marupu rupu bora na mazuri sana kuliko wafanyakazi wengine wa umma wote...

Aidha, wengi wa watu toka taasisi hizi (hasa wanajeshi wa JWTZ na wale toka TISS) wamepewa kushika nyadhifa nyeti serikalini kuanzia wizara mbalimbali, ma-RC, DCs, DEDs na kuwa wakuu wa idara/taasisi nyeti kama PCCB, BoT, NEC nk

Si hivyo, kwa jinsi utawala uliopo unavyohakikisha umeikamata vyema "SYSTEM", sasa mpaka ngazi ya kata na tarafa unafanya recruitment ya vijana wa kike na kiume wenye element na mtazamo huu na kuwaweka huko wasimamie mambo yao...!!

Sasa tujiulize, hawa kina Tundu Lissu , Zito Kabwe, Maalim Seif Shariff Hamad, Freeman Mbowe na wengine watapitia wapi?.. Ni lazima kuwe na njia zenye ubunifu wa ziada kubadili mambo haya ili yawe upande wao, na INAWEZEKANA....!!

Sasa tunaweza kuona kuwa hii pekee inaifanya SYSTEM iwe na utiifu kwa utawala uliopo madarakani kwa viwango vyote na hivyo kuwa vigumu sana kuusalitiana wao kwa wao japo INAWEZEKANA hili kutokea if something special has to be done.......

Therefore, NOTHING IS IMPOSSIBLE ON EARTH...

Why? Kwa sbb hawa ni watu kama alivyo mtu yeyote. Wana familia na ndugu zao wengi kwa maelfu na malaki wanateseka dhidi ya utawala huu mwovu..

Hii pekee pamoja na mengine mengi yaliyo dhaifu kabisa yanaweza kutumika kama fursa ya kubadilisha mwelekeo wa mambo...

Tukumbuke kuwa, nyama na wali na makando kando yake ndiyo chakula kinachopendwa na chenye hadhi ktk maeneo ya jamii nyingi...

Lakini, ukila hicho tu kila siku unakikinai na MTU angependa siku nyingine ale hata "mchembe" ama chakula cha aina nyingine...

Vivyo hivyo hata kwa "SYSTEM" yetu, inawezekana wanapata chochote watakacho, lakini ukinaifu na kuchoka kupo tu na lazima wanahitaji mabadiliko fulani ambayo watawala waliopo hawawezi kuwapatia...

Tumie fursa hiyo, take advantage na zungumzeni nao. IT'S POSSIBLE to change the direction...!!
 
Umeongea mengi ila mwishoni ukarudia ujinga uleule!

Yani eti siasa zetu tufanye kwa kumlaumu Magufuli ila siyo vyombo vya usalama.

Kweli ujinga mzigo.

Hivi kwa akili yako unafikiri leo Magufuli kama Magufuli yuko pale kwa matakwa yake na si system?

Yani chadema walivyo wajinga wanafikiri hata Magufuli akifa leo wao ndio wataingia ikulu! Hawajui kuwa ccm/system inawawekea chuma kingine na ngonjera zilezile zinaendelea.

Ndio maana watu wanaposema leteni hoja na sera zenu nyie hamuelewi bali mnataka mpewe nchi kwa kumtukana Magufuli! Sasa hiyo nchi mkipewa mtatawala kwa matusi mliyomtukana Magu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo system ya Tanzania ya Nyerere ndo wapinzani hawapewi nchi hata wakishinda?..

Mbona Malawi na Zambia ni kawaida kuheshimu matakwa ya wananchi?Au tuseme kina Kaunda na Kamuzu Banda walikuwa na akili kumzidi Nyerere?
Hapa kwetu system siyo shida,! Shida ipo kwa hao wanaotaka wawe mbadala wa ccm ni kwamba hawajielewi.
Yani eti tufanye siasa kwa kumshambulia Magufuli [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]akili za bata hizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama system ndio kila kitu huoni hata kama ukipewa nchi ukijaribu kuwazingua wanakufyekelea mbali?

Kuna kitu mnakikosa wapinzani na hicho mtaendelea kuitwa wapimzani hadi mnaingia kaburini, labda mjitambue.

Hebu fikiria leo Msigwa anamuomba radhi kinana,! Yani Dr. Slaa huko aliko atakuwa anaumia sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msingi wa nguvu ya kushika madaraka ni kukubalika na wananchi na sio vyombo vya ulinzi.Hakuna chombo chochote cha ulinzi duniani kiliwahi shida nguvu ya umma ikiamua kufanya mabadiliko.Sema tu ccm imewekeza kwenye ujinga wa watu ili iendelee kutawala wanatumia kanuni ya wafanye wawe masikini ili uwatawale.
Siku Jamii ikichoka itafanya mabadiliko na hayatoweza zuilika.
 
Vyombo vya ulinzi huwa vipo neutral upima nguvu ya umma ikiwa kubwa usimama na wananchi tumeshuudia nchi nyingi.Ili kulinda amani ya nchi.
 
Huitaji kuwa hivyo, wakati wao wapo kwenye urais ninyi badilini system ya nchi kwa wabunge,
Hakuna agreement ya kuingia na mtu hapo na halitawezekana

Kikubwa tupate wabunge wanamabadiliko si wapinzani bali wanaotaka tuhame hapa tulipo kwani hasta wapinzani wanapenda system hii mbovu nao wang'ae na vizazi vyao

Hijo system itapanguliwa na sheria tajwa kule juu

Jokakuu na kalamu 1
Wabunge wengi 2015 hawakuja na lowasa bali Ukawa

Mbinu ya kuaminiana kati ya personnel kutoka ccm, na vyama pinzani kisha kuachiana majimbo , pamoja na kuhakikisha wanapitishwa na vyama vyao ili waende General election ambako watapita

Ukipata wabunge waaminifu 250 mchanganyiko, serikali inakuwa yenu kupitia waziri mkuu hivyo Rais anakuwa mali ya wabunge, inarahisisha kazi za bunge na serikali hivyo ninyi mnakuwa na nchi kwa kivuli cha baraza la mawaziri na hapo ccm na rais wataamini mfumo huo haufai na watabadilika na nchi itabadilika

Bila wabunge waaminifu ktk mabadiliko hakuna Tanzania mpya kwani hata chadema nao wakipata watakuwa mabwanyenye kama ccm

Vita yao ni madaraka si maendeleo
 
Hii ndio Jamiiforums ya enzi zile za JamboForums. Nimeimiss sana.
Hongera sana mkuu,umeutendea haki uzi. Sina cha kuongeza wal kupunguza.
 
Endelea kujidanganya tu,hakuna siku system itakuja kuwakubali upinzani,hao police,tiss lazima wasemwe kama wanakwamisha harakati za kujikomboa,kwa mfano ulitaka kusema chadema wasiseme kwamba mdude alitekwa nao police/tiss? ulitaka kusema kwamba wanaharakati/upinzani wasiseme kwamba aliyemteka ulimboka ni mtu wa tiss?

Kama Police /Tiss wakifanya kazi kwa weledi hawatosemwa ila wakiendelea kufanya utopolo watasemwa na wataendelea kupigwa spana mpaka 2050 na wataachia tu nchi siku moja,kaachia mugabe ndio itakuwa kwetu? Ipo siku uoga watu utawaisha tu amini hivyo kwa kadri tiss/police wanavyotekeleza amri za SISIEMU ndio wanazidi kurahisisha hiyo siku.
 
Kweli huwezi kutenganisha Tiss na ccm
Huwezi kutenganisha tiss na ccm ndo mfumo ulivyo. Wengi wao hao maafisa na wenyewe ni wafia chama tu. Umeshawahi kusikia ccm wanashida na wasiojulikana?! Never! Kwasababu ni hao hao tu. Ni kitengo.
 
..jina lake ni Lt.Gen.Imran Kombe.

..vitani aliitwa kamanda mbogo.

..brigade yake ndiyo iliwachakaza askari wa Uganda, Libya, na Wapalestina, ktk eneo linaitwa Lukaya.
Nashukuru sana ndugu kwa masahihisho. Pia alipatwa na kadhia ile kwa kushirikiana na Mrema.
 
Nadhani mfumo uliopo, dola yote inaitumikia ccm. Polisi ni waziwazi. Hao wengine ndo kwa style ya kutokujulikana. Wote ni wale wale. Utaanzia wapi kukubaliwa na kufanya kazi na tiss hii ya ccm na usiitwe msaliti ama unataka kupindua nchi? Ccm wenyewe wenye mahusiano na upinzani wanadhibitiwa! Achilia mbali maafisa wa serikali na viongozi kama wakuu wa wilaya, mikoa nk.

Nguruvi3
 
Siku zingine acha Kukurupuka Kuyataja Majina ya Watu kama unajua huyajui vizuri au hujajiridhisha nayo. Umejichoresha sana!
Siyo kihivyo. Wewe tu. Naenda kurekebisha kwasababu mwenye busara JokaKuu amenikumbusha na kunisahihisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…