Huwezi lazimisha Mwanamke akuheshimu, Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda

Huwezi lazimisha Mwanamke akuheshimu, Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda

Mwanamke anapenda kama ilivyo mwanaume. Tena anapenda zaidi ya mwanaume ndio maana huwa mtiifu.
Huwezi kumtii mtu usiyempenda.

Pesa haibadili moyo wa mtu akiwepo hiyo Mwanamke.
Pesa inampa uhuru mtu wa kuonyesha hulka yake halisi.

Mwanamke kama alikuwa hakupendi akiwa na pesa ndio wakati wa kuonyesha kile ambacho ulikuwa hukioni.

Pia elewa, hata ukizeeka au ukiishiwa au kufilisika ndio wakati ambao Mwanamke atakuwa huru kuonyesha yaliyomoyoni mwake. Kama alikuwa hakupendi ndio utajua lakini kuna kulipa kisasi.

Hata wanaume sisi tulipata hizo pesa mbona wengi tunaanzisha mahusiano mengine na kuwa na MICHEPUKO au kuoa kabisa wanawake wengine?
Sio kwamba pesa ndio zimetubadilisha, ila pesa zimetupa uhuru wa kujionyesha dhahiri sisi ni watu wa aina gani.

Mwanamke anapenda. Sema wengi hawapati bahari ya kuolewa na wanaume wanaowapenda ndio maana unasema ulichokisema
Hii ndo ilitakiwa iwe pale juu.
Pata pesa tujue tabia yako. Mimi ndiomana naanzisha mahusiano na mwanaume mwenye pesa sababu anakuwa yuko halisi haigizi..!!
 
Mapenzi ya dhati yanaendana na kutimiza majukumu ipasavyo, mwanamke asipokuwa na stress upendo wake kwako utaongezeka, na hata kama ikitokea mara moja moja umekosa hawezi kuwa na shida.

Tatizo linakuja pale utaposhindwa kutimiza majukumu ipasavyo, akachoka kukuvumilia hata kama alikuwa anakuoenda kwa dhati, ukamlazimu mwanamke aanze kujichanganya kwa ajili ya kuihudumia familia, akishaanza kukutana na watu tofauti huku akiwa na akili ya kutafuta, penda usipende upendo wake kwako na heshima vitaanza kupungua.

Umeandika uzi wako kama vile upendo na heshima vya mwanamke kwa mwanaume ampendae ni constant, havipungui, no way, hivyo vyote lazima ujue namna ya kuvitunza kwa ajili ya manufaa yako.
Nimeipenda hii
 
Hili neno "nakuvumilia -namvumilia " ni neno la kisiasa Sana.

Hakuna binadamu anayemvumilia mwenzake ikiwa unamuhudumia mwanamke au yeye anakuhudumia hakuna anayemvumilia mwenzake hapo.

Ni tafsiri mbaya Sana kusema nakuvumilia .
Asili ya mwanadamu huvumilia pale tu amehahidiwa au kuna kitu chenye benefit kwake hapo yupo tayari kuvumilia.
 
Rubbish heshima ya mwanaume ni pesa hizo nyingine ni fasihi simulizi na fasihi andishi.
 
Hapa nakuunga mkono ila kwenye ile mada ya kumruhusu mwanamke aende semina ya wiki3 kisa yuko kazini hapana siwezi kuunga mkono!
Sikufichi huku semina Wanawake wanaliwa sio kidogo.Mie nilikuja tu kuhitimisha kwa hawa wanawake zetu wa kiafrika hakuna Mwanamke wa peke yako cha kuomba usifanikiwe kumfania
 
Hapa nakuunga mkono ila kwenye ile mada ya kumruhusu mwanamke aende semina ya wiki3 kisa yuko kazini hapana siwezi kuunga mkono!
Sikufichi huku semina Wanawake wanaliwa sio kidogo.Mie nilikuja tu kuhitimisha kwa hawa wanawake zetu wa kiafrika hakuna Mwanamke wa peke yako cha kuomba usifanikiwe kumfania
 
Upendo ni matarajio ya kupata kitu toka kwa mtu pesa au mwili wake au heshima yake.
 
Hakuna mwanamke mwenye tabia mbovu kwa mwanaume ampae pesa.
Ukitaka kujua tabia ya mke wake filisika,fukuzwa kazi au staafu then pesa ziishe ndo utajua miaka ya 40 ya ndoa ulipendwa wewe au kile alichopata toka kwako.
 
Ukitaka kupendwa inatakiwa kile alichokupendea mwanzoni ndicho ukimaintaine milele
 
HUWEZI LAZIMISHA MWANAMKE AKUHESHIMU, MWANAMKE ANAMHESHIMU MWANAUME ANAYEMPENDA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Wanaume wengi hudhani kĂşmpiga Mwanamke ndio humfanya Mwanamke awe mtiifu na mwenye heshima. Wengine huwafokea na kuwatukana na kuwatolea maneno makali kwa kudhani kufanya hivyo ndio humfanya Mwanamke amheshimu.
Elewa Mwanamke sio mtoto mpaka umpige. Elewa, Mwanamke ni kiumbe pekee chenye kisasi. Elewa Mwanamke hawezi kusahau jambo baya lolote hata moja ambalo umemfanyia hasa ukimpiga Ă u kumfanyia ushenzi wowote.

Wazee wetu wengi wakifikisha miaka kuanzia hamsini (50+yrs) huanza kupewa kiinua mgongo chao kwa yale yote waliyofanyia Wake zao kipindi cha nyuma.
Sasa kijana anapompiga mkewe, au kumfokea kwa maneno ya kudhalilisha, alafu akaona Mwanamke wake amekaa kimya wanadhani ndio heshima imerudi. Kumbe hawa viumbe wamejiweka kiporo ambacho wanauhakika watakinywea na chai ya moto yenye tangawizi na mdalasini. Wakati huo kiporo ambaye ni wewe utakuwa wabaridi umepoa unakaribia kuchacha.

Asije akakudanganya mtu kuwa kukusanya pesa pekee kutakuondoa na kadhia ya mkeo uliyemnyanyasa. Njia pekee labda ni kupeana talaka. Vinginevyo hata uwe nani, nasema hata uwe nani. Lazima upasuke.

Wengine hufikiria heshima wataipata kwa kutoa pesa, na hiyo hupelekea kutafuta pesa kwa nguvu zote na kuwapa wake zao lakini mwisho wa siku heshima hawapewi.

Taikon Master kama mtaalamu wa saikolojia, falsafa, na mwanasosholojia ninakuambia kuwa kwenye hii dunia Mwanamke hawezi kukuheshîmu kisa unampa pesa, au kukuheshîmu kisa unampiga. Huwezi force heshima ya Mwanamke kwako.

Mwanamke anamheshimu mwanaume anayempenda bila kujali mwanaume huyo yupo katika nafasi ipi,

Hata uwe Rais, hata uwe mfalme, hata uwe mkuu majeshi, hata uwe nani. Mwanamke ambaye utamuita mkeo au ambaye utalala naye uchi mkakutana kimwili hawezi kukuheshîmu kisa hicho cheo chako au mapesa yako.

Mwanamke huogopa zaidi kumsaliti mwanaume anayempenda kuliko kitu chochote.
Kuwa mkuu wa majeshi, au Rais au jambazi hakumuogopeshi Mwanamke asiku-cheat.

Elewa Mwanamke woga wake upo katika hisia zake. Mwanamke anaogopa zaidi kupoteza kile kinachompa furaha.
Elewa, Mwanamke anaheshimu kile kinachompa furaha. Na mtu anayempenda raha ndiye anayempa raha.

Ukiona upo kwenye kundi la wale wanaume wanaodhani wanawake hawatoi pesa zao kwa wanaume jua huyo Mwanamke uliyenaye hakupendi. Na kama hakundi automatically hakuheshimu wala kukutii ila anakuigizia.

Ukiona upo na mwanamke ambaye chake ni chake lakini chako ni Chenu be aware, huyo hakupendi na automatically hakuheshimu ila anachokifanya ni unafiki.

Mtu anayesema Mwanamke hapendi lakini anapaswa awe mtiifu anashindwa kuelewa kuwa Utiifu ni matokeo ya upendo uliopitiliza.
Kumaanisha Mwanamke anatakiwa akupende sana ili awe mtiifu kwako. Huwezi mtii mtu usiyempenda. Kama unamtii mtu usiyempenda tafsiri yake ni kuwa unamwogopa.
Kuna heshima au Utiifu na kuja hofu au Woga.

Elewa kuwa hakuna pesa yoyote ya kununua upendo wa Mwanamke, asije akakudanganya mtu yeyote.
Utapigwa na kitu kizito. Upendo haununuliwi.

Elewa, Wanawake huipata pesa kipaombele baada ya ku - disappontiwa, kuumizwa na kusalitiwa na wanaume wanaowapenda.
Mwanamke yeyote aliyeumizwa na mwanaume aliyempenda sana hubadilika kwa kiwango cha juu.

Elewa huwezi fanya lolote kumpa furaha Mwanamke ambaye hana furaha. Furaha ya Mwanamke ipo kwa mwanaume anayempenda.

Usijesema sikukwambia. Hivyo ndivyo utakavyoishi ña Wanawake Mwanangu

Robèrt Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
kuna sehemu unasoma inayosema Adamu hakumshimu Hawa, au kuna sehemu unasoma kwamba Samsoni alimkosea Delila hadi amsaliti
Recently mke wa mchezaji Kaka anadai alimuacha Kaka because he was so nice to her
Mkuu tuliza komwe, huwezi kuwaelewa, ishi nao kwa akili, while your eyes open
 
Ni wapi Mungu alilazimisha upendo kiongozi?

By the way
Kuna mwanamke nilikuwa nae tukawa tunaishi maisha ya ligi sana kutukanana
Siku moja nikamkusanya.

longtime nilishajua huyu sitawezana nae na mwisho wangu na yeye utakuwa ni wa visasi ni yule mwanamke ukikaa nae anazungumzis yale mabaya tu hana nzuri analoweza kuzungumza
nilizaa nae mtoto mmoja.

Niliona bora tu tuachane.
mkuu umezalisha single maza
 
Heshima na utii ni matokeo ya malezi.
Malezi ni program ambayo mzazi anaiplant kwa mtoto ili hawezi ishi vyema.
Pana watu wanadharau za asili huwezi badili sababu wana vinasababu vya dharau toka kwa wazazi wao.
 
Back
Top Bottom