Huyu huenda kweli akawa ni mwana wa Mungu aliye hai angalia Mayele, Dkt Biteko, Chalamila, Dkt Mwigulu, Dkt Samia, Dkt Tulia hata Paul Makonda

Huyu huenda kweli akawa ni mwana wa Mungu aliye hai angalia Mayele, Dkt Biteko, Chalamila, Dkt Mwigulu, Dkt Samia, Dkt Tulia hata Paul Makonda

View attachment 2849652View attachment 2849653View attachment 2849654
View attachment 2849655

Habari Tanzania,

Kwa muda sasa kumekuweko mijadala mbalimbali kuhusu Ndugu yetu Apostle Bonface Mwamposa almaarufu kama Bulldozer.

Apostle Bonface Mwamposa anahudumu katika madhabahu ya Arise & Shine au kwakimombo " INUKA UANGAZE" ( Isaya 60:1 ) yaliyoko Kawe jijini Dar es Salaam Tanzania.

Apostle Bonface Mwamposa amekuwa na wafuasi wengi wanaoongezeka siku baada ya siku mwezi baada ya mwezi au mwaka kwa mwaka yaani ni mamilioni kwa mamilioni ya waamini toka nje na ndani ya bara la Africa,

Apostle Bonface Mwamposa, ibada zake zote hazina Misingi ya dini au dhehebu lolote ila " IMANI KWA YESU KRISTU NA MUNGU ALIYEMTUMA "


Apostle Bonface Mwamposa, anahudumia Watu wakristo kwa Watu Waisilamu au hata wale wote wasio na dini kabisa kama akina Yeriko Nyerere nao pia wakiamini wanapokea uponyaji wa mwili na roho pamoja na haja zao kutimilizwa na Mungu wa Boniface anayejibu kwa Moto,

Apostle Bonface Mwamposa, ndiye aliyemwambia Mhe Dkt Willium Ruto kwamba "Nenda Utashinda Uchaguzi" na mishowe Ruto akashinda Urais,

Bila Mungu ilikuwa ni ngumu sana mtu kama Mhe Willium Samoi Ruto kuwashinda Mhe Raila Omolo Odinga na Kenyatta Uhuru ila Mungu wa Boniface akafanya jambo pale Kenya na dunia ikashangaa kilichotokea,

Apostle Bonface Mwamposa, Ndiye aliyemwombea pia Mhe Dkt Tulia Ackson na akashinda na kuwa Spika wa mabunge yote Duniani ( IPU ) hata Leo,

Apostle Bonface Mwamposa, ndiye aliyemwombea kaka yetu Fiston Kalala Mayele na akawa mchezaji bora wa wakati wote Nje na ndani ya Tanzania nadhani sote tunakumbuka huyu kijana anayechezea timu Pyramids FC hivi Sasa,

Orodha ya waliosaidiwa na Mungu kupitia kwenye kinywa Cha Apostle Bonface Mwamposa ni wengi na hawahesabiki,

Wengine wanakwenda kwa Siri na hawataki mtu yeyote awaone maranyingi hawashuki kwenye magari yao but wanatendewa japo ni ujinga kujificha au kuficha Matendo Makuu ya Mungu wakati kwa waganga mnakwenda tena waziwazi.

Hoja yangu hapa ni , Je? Mwamposa kwa kuzingatia mafundisho yake na Upako alionao huenda ni kweli huyu bwana akawa ni mwana wa Mungu ila sisi imani zetu zimekamatwa na shetani na hivyo tunashindwa kutofautisha kati ya kazi za Shetani na kazi za Mungu?
====

Kama hujawahi kwenda au kumsikiliza Apostle Bonface Mwamposa jipe muda wa kumfuatilia kabla hujamsema vibaya kwani ni kujitafutia laana toka kwa Mungu ALIYEMTUMA MWAMPOSA.


Mfuatilie: Azam channel No 469
Startimes channel No 117

You tube: Mwamposa Live
You tube : Arise & shine Tanzania

Instagram: Arise & shine Tanzania

Tupunguze porojo. Tatizo ni tozo na mfumuko wa Bei.
 
Mimi nililogwa sana kwa zaidi ya miaka 15,nilitembea sana kwa waganga ila nilipofika Kawe namshukuru Mungu walau kwa Sasa hata naonekana mtu, Mwamposa ni mtumishi wa Mungu
Vp ambao wameenda sana kwa Mwamposa na hadi sasa hawajakata tamaa ila matatizo yao yako palepale?
 
N
Watoto wangu walifeli sana ila baada ya kufika Kawe namshukuru Mungu wanafanya vizuri kwa sasa darasani
Nina ndugu yangu ameshampeleka sana mwanae kwa Mwamposa ili apate kazi ila wapi, wakati mwanae anasoma alimpeleka ili afaulu mitihani ila wapi. Pamoja na yote ila bado anaamini miujiza ya Mwamposa hadi sasa.
 
Wapumbavu huhamasishana waende kule mara huku kuna miujiza, ni umbumbumbu wa SGR levels.

Duniani kote Mungu hupatikana Kawe tu? nina wasiwasi na akili zetu Waafrika kiuumbwaji...
Tafsiri ya haraka hapo Mwamposa ndio hufanywa kuwa mungu mwenyewe.
 
Mke wangu alisumbuliwa na sukari kwa mwaka mzima ila Sasa iko 5.5,amepona kabisa
Mkuu watu wanapona hadi kansa kimiujiza ambayo haitumii uchawi wala kuhusishwa imani kwa Mungu.
 
Mimi sio Mkristu ila Jumapili asubuhi Insha'allah nitafika hapo Kawe asubuhi
Kwa waganga na masheikh kutibiwa ni ghari ndio maana watu wanaenda huko wanajua wanaweza wakapona matatizo yao bure tu.
 
Aiombee TANESCO isikate umeme. Akimaliza akaiombee Taifa Stars ibebe AFCON. Mleta uzi acha kuabudu binadamu mwenzako.
 
Nabii kuna huyu mama katoka katavi, anasema mume wake ajawahi ajawahi kumnunulia hata upande wa kanga, nini kimetokea? Baada ya kufika madhabahuni pako kukanyaga keki ya upako, mume wake amemtumia meseji Mke wangu nimekununulia vitenge

Makofi kwa bwana pwa pwa pwa pwa pwa.
Nani mtenda mijuza yesu.
 
View attachment 2849652View attachment 2849653View attachment 2849654
View attachment 2849655

Habari Tanzania,

Kwa muda sasa kumekuweko mijadala mbalimbali kuhusu Ndugu yetu Apostle Bonface Mwamposa almaarufu kama Bulldozer.

Apostle Bonface Mwamposa anahudumu katika madhabahu ya Arise & Shine au kwakimombo " INUKA UANGAZE" ( Isaya 60:1 ) yaliyoko Kawe jijini Dar es Salaam Tanzania.

Apostle Bonface Mwamposa amekuwa na wafuasi wengi wanaoongezeka siku baada ya siku mwezi baada ya mwezi au mwaka kwa mwaka yaani ni mamilioni kwa mamilioni ya waamini toka nje na ndani ya bara la Africa,

Apostle Bonface Mwamposa, ibada zake zote hazina Misingi ya dini au dhehebu lolote ila " IMANI KWA YESU KRISTU NA MUNGU ALIYEMTUMA "


Apostle Bonface Mwamposa, anahudumia Watu wakristo kwa Watu Waisilamu au hata wale wote wasio na dini kabisa kama akina Yeriko Nyerere nao pia wakiamini wanapokea uponyaji wa mwili na roho pamoja na haja zao kutimilizwa na Mungu wa Boniface anayejibu kwa Moto,

Apostle Bonface Mwamposa, ndiye aliyemwambia Mhe Dkt Willium Ruto kwamba "Nenda Utashinda Uchaguzi" na mishowe Ruto akashinda Urais,

Bila Mungu ilikuwa ni ngumu sana mtu kama Mhe Willium Samoi Ruto kuwashinda Mhe Raila Omolo Odinga na Kenyatta Uhuru ila Mungu wa Boniface akafanya jambo pale Kenya na dunia ikashangaa kilichotokea,

Apostle Bonface Mwamposa, Ndiye aliyemwombea pia Mhe Dkt Tulia Ackson na akashinda na kuwa Spika wa mabunge yote Duniani ( IPU ) hata Leo,

Apostle Bonface Mwamposa, ndiye aliyemwombea kaka yetu Fiston Kalala Mayele na akawa mchezaji bora wa wakati wote Nje na ndani ya Tanzania nadhani sote tunakumbuka huyu kijana anayechezea timu Pyramids FC hivi Sasa,

Orodha ya waliosaidiwa na Mungu kupitia kwenye kinywa Cha Apostle Bonface Mwamposa ni wengi na hawahesabiki,

Wengine wanakwenda kwa Siri na hawataki mtu yeyote awaone maranyingi hawashuki kwenye magari yao but wanatendewa japo ni ujinga kujificha au kuficha Matendo Makuu ya Mungu wakati kwa waganga mnakwenda tena waziwazi.

Hoja yangu hapa ni , Je? Mwamposa kwa kuzingatia mafundisho yake na Upako alionao huenda ni kweli huyu bwana akawa ni mwana wa Mungu ila sisi imani zetu zimekamatwa na shetani na hivyo tunashindwa kutofautisha kati ya kazi za Shetani na kazi za Mungu?
====

Kama hujawahi kwenda au kumsikiliza Apostle Bonface Mwamposa jipe muda wa kumfuatilia kabla hujamsema vibaya kwani ni kujitafutia laana toka kwa Mungu ALIYEMTUMA MWAMPOSA.


Mfuatilie: Azam channel No 469
Startimes channel No 117

You tube: Mwamposa Live
You tube : Arise & shine Tanzania

Instagram: Arise & shine Tanzania
Nchi Ina matatizo lukuki... Achague hata Moja mfano umeme... Kama nabii atoe unabii wake??
Yesu alienda kwa wenye shida akawaponya... Alienda bwawani na ajatenda kwa yule asiyejiweza!
Kwanini Mwamposa hafuati nyayo aende mlongazila kuponesha wagonjwa??
 
Mimi nililogwa sana kwa zaidi ya miaka 15,nilitembea sana kwa waganga ila nilipofika Kawe namshukuru Mungu walau kwa Sasa hata naonekana mtu, Mwamposa ni mtumishi wa Mungu
Wanawake walikua wakinikataa sana. Ilihitaji niimbishe sana ndio nipewe. Hata kwa kutumia hela ilikua ngumu sometimes.

Ila saa hivi uongo mbaya mi ndo nawakimbia.
 
Kwenye ukristo ukishashikia mtu anjiita "mtume" au "nabii" ujue huyo ni shetani mkubwa wa kuogopa kama ukoma.
 
Mimi nililogwa sana kwa zaidi ya miaka 15,nilitembea sana kwa waganga ila nilipofika Kawe namshukuru Mungu walau kwa Sasa hata naonekana mtu, Mwamposa ni mtumishi wa Mungu
Watu wenye Imani haba huhangaika kwa waganga na kwa mitume.
Jiulize swali na fanya utafiti kidogo;
Katika watu wanaoishi maisha ya kawaida, idadi inayoenda kwa waganga na mitume na ile isiyoenda huko, ipi ni kubwa?
Kitu Muhimu ni kumuamini Mungu wa kweli asiyekuhitaji uende kwa mganga au wanaoitwa mitume ili akubariki.
Baraka za Mungu zinakuja moja kwa moja kwako bila kupitia kwa waganga au hao manabii wa maji, chumvi, mafuta,,.....
 
Ndugu zangu wote walioenda kwa jamaa kupata uponyaji hawajasaidika.

Nimepoteza wengi kwa kudhani mwamposa angewaponya kwa maombezi
muache ujinga, imani inaanza na nyie, kama nyie hamna imani mnadhani mtumishi huyo atafanya nini?
 
Wewe Mfuatilie Mwamposa hutajuta na imani yako itapanda zaidi ya hiyo
Mkuu, usimuangalie mtumishi Mwamposya kama mtu binafsi, bali chunguza na angalia huduma yake kwa kina kama inashabihiana na ile waliyoihubiri mitume. Ni hilo tu.

WAGALATIA 1

7 Ukweli ni kwamba hakuna Injili nyingine, ila nafahamu kuwa wako watu wanaowavuruga, ambao wanataka kuipotosha Injili ya Kristo.

8 Lakini hata ikiwa ni sisi au ni malaika atokaye mbinguni, kama mtu akiwahubiria Injili ambayo ni tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo na alaaniwe.

9 Kama tulivyokwisha sema kabla, sasa nasema tena, kwamba mtu ye yote atakayewahubiria Injili tofauti na ile mliyokwishaipokea, basi mtu huyo na alaaniwe.
 
Katika kuitetea na kuisambaza Injili ya Kristo ili iwafikie watu wa mataifa yote, mitume wote walipitia taabu na mateso mengi hadi mauti. Licha ya wao hata watumishi wengine wacha
Mungu walipitia changamoto nyingi za kila namna.

Kila walichokifanya, miujiza mingi na ishara walizozifanya, kanuni kuu ni kwamba sifa, heshima, na utukufu wote unapaswa kurudishwa kwa BWANA YESU KRISTO mwenyewe, na wala si l
kwa ajili ya madhabahu ya mtumishi anayehudumu. Ni vyema tukatafakari kwa kina juu ya aina ya huduma na utumishi katika nyakati za sasa kanisa kwa kupitia nukuu ifuatayo;

UFUNUO 3

14 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.

15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na u uchi.
Sio lazima kila mtume apitie taabu au kifo ili kuhubiri injili kama wale wa kipindi kile.

Nyakati zimebadilika .
 
Back
Top Bottom