Huyu Mwanajeshi aliyekuwa akihutubia leo si ndiyo yule muuza madafu wa Ikulu, au?

Huyu Mwanajeshi aliyekuwa akihutubia leo si ndiyo yule muuza madafu wa Ikulu, au?

Story nyingi za Mji husika huwa zinapatikana Kwa bodaboda as mgeni gani ameingia kwenye huo mji, amefikia Kwa Mzee gani ama nyumba ipi.

Anajihusisha na nini n.k

Kumbuka hao jamaa wanatakiwa kuripoti Kila tukio Kila Siku

Kwahiyo wakiwa wanachambua hizo taarifa ndipo ambapo hutenganishwa kusema hii taarifa si muhimu ile ni muhimu, so we have to dig deep on that


Ukipita kituo cha bodaboda unaweza kupata taarifa zote kuanzia za kisiasa/Kiuchumi ama kijamii

Nani anataka kugombea uenyekiti wa Kijiji/Udiwani ama Ubunge kwenye eneo lako.

Nani anajenga kituo cha mafuta hapo Kijijini/nani anajenga nyumba ya Kupangisha ya vyumba 20 kwenye eneo lako. Amepata wapi Mtaji wa kufanya hayo n.k isije kuwa anatumika kutakatisha fedha n.k

Kuna Kijana mgeni hawamtambui kwenye eneo lao ila anapenda sana sketi kwahiyo ili kumfahamu vizuri wanakuletea msichana wao(kutoka ofisini kwao) ili ajilengeshe kwako na achote taarifa zako kukuhusu hata kama itakuwa Kwa kukupa tunda
Ingekuwa system ya namna hii ina exist basi Tanzania isingekuwa na mambo ya hovyo kama ilivyo sasa hivi.
 
ukakamavu wake ungekuwa na legacy kama angetusaidia tukio kama la Traore, nchi ikafanyiwa factory reset a.k,a, * Renaissance *
Na akitaka direct contact na SAS hilo nitarahisisha!
 
Tanzania hakuna elite mixed martial artists.

Hata mabondia elite Tanzania hatuna.

Ila kwa viwango vya Kitanzania, si ajabu kuna posers mnaowaona ni wa maana sana ilhali hakuna kitu.

Heck, hata jeshi la Tanzania ni la 6 kwa ubora duniani 🤣.
We Nyani Ngabu maskhara mengine si ya kuandika, inakuwa kama viroja, kwamba

JESHI LA TANZANIA NI LA SITA KWA UBORA DUNIANI!!!

kwamba sasa tunaweza mpiga Iran, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Canada, Israel, Korea, Urusi, China, Marekani, Japani, nk

Je ktk orodha hiyo ukihesabu sita zako tunaweza kumpiga nani ktk zitakazosalia?
 
Mimi leo nimemuona nikasema huyu si jamaa wa madafu? Nikatafuta kama kuna thread ya yanayojiri maadhimisho ya Muungano niseme hilo nikaikosa nikakaa kimya.

Jamaa tokea namuona siku ya kwanza ile fitness haikuwa ya kawaida.
Angalia usimamaji wake ni wa ukakamavu.

Angalia pia uvaaji wake wa kofia kati ya ile ya kijeshi na ile kofia ya madafu utagundua code za jamaa
 
View attachment 2975020
Hawa ni watu wawili tofauti muuza madafu hata kiumri ni mdogo kwa Komando ingawa wamefanana
Kama una nia ya kupotosha sawa, ila ukweli nikwamba muuza madafu anaonekana mdogo kwa kuwa alilegeza sura ya upole na huruma ili malengo ya sanaa yatimie wakati muuza madafu commando amekaza uso wa mbuzi kulingana na kazi yake inavyomtaka na hapo ndipo uso wake unapoonekana wa kikubwa.
 
Lying is just taking advantage of present time (s), situation and circumstances to hide the truth. But at the same time, it is risk in the future, when those times, circumstances and situation have changed or no longer exist.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Uchunguzi wa kina nimeufanyika na kuona kuwa muuza madafu aliyeonekana katika viwanja vya ikulu na Mwanajeshi kutoka kikosi maalumu cha Makomando waliofanya maonyesho siku ya leo ya kuazimisha miaka 60 ya Muungano ni watu wawili tofauti kabisa. Na hapa chini ndio vitu nilivyotizama kwa ukaribu na kuonesha siyo mtu mmoja.

Cha kwanza ni pua zao ukitizama kwa ukaribu na kwa umakini unaona kabisa pua zao zinatofautiana na wala hazifanani hata kidogo.angalia upana na urefu wa pua zao,angalia muonekano na muundo wa pua zao kutoka chini ya macho mpaka eneo zinapotanukia na ukaaji wa matundu yote mawili ya pua kwa kila mmoja.

Pili ni mdomo tizama midomo yao ilivyo kwa ukaribu, tizama ukaaji wa lipsi zao katika picha ambazo ziliwachukua wakiwa wamefumba midomo tizama mkao wa midomo yao kutoka eneo la chini kidogo ya pua kushuka chini.

Tatu ni muonekano wa sura kuanzia mashavu,paji la nyuso zao wote wawili, ukubwa wa macho yao na ukaaji wa macho ikiwa ni pamoja na muonekano wake katika kuingia ndani.na namna wanavyoonekana katika picha zilizowachukuwa wakiwa wamefumba midomo.

Haya kwa uchache tu ukiyaangalia unagundua kuwa watu hawa ni watu wawili tofauti kabisa.na siyo kweli kwamba ni mtu mmoja.

Picha nazileta muda siyo mrefu.

Kazi iendelee,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.

MAMA ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili kutokana na uchapa kazi wake uliotukuka.
Kama alinenepa je? Maana ile baskeli, dafu zina maji na taka zake akachoka kusukuma baiskeli mpaka ndani ongezea na hofu ya ikulu lazima apungue kidogo, baadae ya futari akatulia akanenepa akijiandaa na Muungano in relaxing mode...Kwa kifupi ni huyo huyo.

Haya ni makosa makubwa msirudie 🤣🤣
 
Ndugu zangu Watanzania,

Uchunguzi wa kina nimeufanyika na kuona kuwa muuza madafu aliyeonekana katika viwanja vya ikulu na Mwanajeshi kutoka kikosi maalumu cha Makomando waliofanya maonyesho siku ya leo ya kuazimisha miaka 60 ya Muungano ni watu wawili tofauti kabisa. Na hapa chini ndio vitu nilivyotizama kwa ukaribu na kuonesha siyo mtu mmoja.

Cha kwanza ni pua zao ukitizama kwa ukaribu na kwa umakini unaona kabisa pua zao zinatofautiana na wala hazifanani hata kidogo.angalia upana na urefu wa pua zao,angalia muonekano na muundo wa pua zao kutoka chini ya macho mpaka eneo zinapotanukia na ukaaji wa matundu yote mawili ya pua kwa kila mmoja.

Pili ni mdomo tizama midomo yao ilivyo kwa ukaribu, tizama ukaaji wa lipsi zao katika picha ambazo ziliwachukua wakiwa wamefumba midomo tizama mkao wa midomo yao kutoka eneo la chini kidogo ya pua kushuka chini.

Tatu ni muonekano wa sura kuanzia mashavu,paji la nyuso zao wote wawili, ukubwa wa macho yao na ukaaji wa macho ikiwa ni pamoja na muonekano wake katika kuingia ndani.na namna wanavyoonekana katika picha zilizowachukuwa wakiwa wamefumba midomo.

Haya kwa uchache tu ukiyaangalia unagundua kuwa watu hawa ni watu wawili tofauti kabisa.na siyo kweli kwamba ni mtu mmoja.

Picha nazileta muda siyo mrefu.

Kazi iendelee,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.

MAMA ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili kutokana na uchapa kazi wake uliotukuka.
Hivi humu huna kuna mtu wa kumsikiliza huyu chawa? Ujinga ujinga huu nani huwa anausoma
 
Back
Top Bottom