Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Huyu ndiye Christopher Kasanga Tumbo (RIP) - Mwanasiasa Machachari

Juzi nilipita pale alipopumzika Simba wa Tabora...jamani ni huzuni kubwa....hebu JF hata sisi tumjengee na tumhigadhi hiyu Nguri na muasisi wa siasa za Upinzani miaka kablanya TANU. ..

Mtu aliyekuwa na vision kubwa kitaifa; Taifa halimkimbuki hata sisi JF? Nipo tayari kushirikiana nanyi kwa hili.
 
Wakurugenzi,

Nilibahatika kuzaliwa kijiji kimoja na Chritopher Kasangatumbo, alikuwa si mbinafsi mjamaa wa kweli, nilibahatika kumjua nikiwa kijana mdogo sana pale kijijini kwetu ipole, alikuwa mzee mpole na kwenye hekma sana; kwenye misiba alikuwa anatumia muda mwingi kutuelimisha, nakumbuka alituambia mambo ya demokrasia na dhana nzima ya vyama vingi kipindi nipo darasa la tatu; sikuielewa philosophy yake hadi nilipofika kidato cha sita na kukutana na kitu kinaitwa vyama vingi (1995) hapo ndipo nikafungua macho na kujua ni nini hasa Kasangatumbo alimaanisha those days.

Kuna tetesi kwamba wale wote waliohoji au kwenda tofauti na mawazo ya mwalimu walipata ban; yule mzee Kasangatumbo alifanyiwa visa vingi sana hadi kufikia kuibiwa ngombe zake zote, Pamoja na kuishi uingeleza lakini hakuwa na mali yoyote ile mbali ya ngombe zisizozidi therathin alizorithi kutoka kwa wazazi wake. Nilibahatika kusoma na watoto wake, nakumbuka hata viatu hawakuwa navyo; tulienda shuleni pekupeku pamoja ingawa wenzangu waliyaonja maisha ya Uingeleza.

Mzee alikuwa mjamaa wa kweli na hilo halina ubishi, tatizo ni kwamba je alikorofishana vipi na mwalimu? Mimi na wewe hatujui, kuishi kijijini ilikuwa ni moja ya adhabu alizopewa toka juu. Kuna kipindi pale Tabora mjini Bendera ya taifa ilikuwa inashushwa, yeye hakusimama, akakamatwa kupelekwa kituo kikuu, pale kituoni akawaambia mapolice kwamba hawezi kuongea ya yeyote yule pale isipokuwa mwalimu tu. Police hawakumpa nafasi hiyo bali wakamsweka ndani - habari zikamfikia mwalimu ikulu na mara moja akawaambia wamfungulie aende zake - hizo zilikuwa moja ya story zake tukiwa kwenye misiba pale kijijini kwetu.

Kuna siku nilikuwa nimepanga foleni kwa ajiri ya kupata vitu adimu (sukari, sabuni), kwa wale mnaokumbuka yale maduka ya RTC basi watoto tuliambiwa twende mapema ili wakati duka linafunguliwa saa 9 basi tupate vitu hivyo; mida ya saa kumi duka linafunguliwa foleni ikiwa ndefu sana, nikamwona Kasangatumbo anafika eneo la duka, akatuambia tumsikilze dk tano, pale nakumbuka alituambia tutapanga foleni hizo hadi tutakapoamua kuwa na demokrasia ya vyama vingi - pale sikuelewa kitu kwamba hiyo demokrasia ndiyo italeta maduka mengi? I was young by age anyway. (9)

Inaendelea post #2 chini...

cc Ngongo, JingalaFalsafa, Mzee Mwanakijiji, Ogah, Mohamed Said, Nguruvi3, Mchambuzi, WOWOWO, Mkandara, Jasusi, Gembe, Phillemon Mikael, Mwanagenzi, Rutashubanyuma, Augustine Moshi, Pasco,
Fuso,
Naomba nami nikueleze machache kuhusu Christopher Kassanga Tumbo.

Mtaa wa Kanoni Isevya, Tabora mwanzo wa mtaa kwa mkono wa kushoto kama unaelekea Kachoma, kuna nyumba ya babu yangu Salum Abdallah maarufu kwa jina la Baba Popo.

Huyu Popo ni mwanae wa kwanza ambae kwangu mimi ni baba yangu mkubwa.

Jina lake hasa ni Humud lakini hili halikushika alijulikana kwa jina la Popo hadi mwisho wa maisha yake.

Jina lake kamili lilitakiwa liwe Mwekapopo jina la babu yake aliyeingia Tanganyika kutoka Belgian Congo kama askari katika jeshi la Wajerumani miaka ya mwisho 1880 lakini kwa ufupisho akawa wanamwita Popo.

Hapo mwanzo wa mtaa mkono wa kushoto ndipo ilipokuwa nyumba ya babu yangu Salum Abdallah Mwekapopo Samitungo Muyukwa.

Yote haya majina ya Kimanyema.

Nyumba ya babu yangu ilikuwa maarufu kwa kuwa katika miaka ile ya 1950 wakati harakati za kudai uhuru zimepamba moto yeye alikuwa mstari wa mbele dhidi ya Waingereza kwanza akiwa katika TAA, TANU na TRAU.

Mwisho wa mtaa wa Kanoni kabla hujafika Kachoma ilikuwapo nyumba nyingine ya babu yangu na mkabala wa nyumba hii ilikuwapo nyumba ya Christopher Kassanga Tumbo na zote mbili ni nyumba kwa wakati ule zilizokuwa nzuri mtaa mzima.

hii Kachoma ni sehemu maarufu kwa kuwa kulikuwa na kilabu cha pombe za kienyeji.

Mwaka wa 1955 mara tu baada ya kuundwa kwa TANU babu yangu na Kassanga Tumbo waliasisi chama cha wafanyakazi wa reli Tanganyika, kikijulikana kama Tanganyika Railway African Union (TRAU) babu yangu akiwa Rais na Kassanga Tumbo Katibu.

Wakati wa likizo mwaka wa 1964 nikiwa darasa la sita nililifika Tabora kumtembelea babu yangu lakini hakuwapo nyumbani na kwa akili za kitoto hili halikunishughulisha na baada ya likizo kwisha nikarudi Dar es Salaam bila ya kumuona.

Lakini kilichotokea kwa babu yangu kutokuwa nyumbani ni kuwa alikuwa amewekwa kizuizini jela ya Uyui kufuatia maasi ya wanajeshi tarehe 20 Januari,1964 na baada ya Jeshi la Kiingereza kumaliza maasi yale, serikali iliwakamata viongozi wote wa vyama vya wafanyakazi na kuwaweka kizuizini.

Kassanga Tumbo alipata taarifa za msako wa viongozi wa vyama vya wafanyakazi mapema na akawahi kutoroka akaenda Mombasa lakini alikamatwa baadae na akarejeshwa Tanzania na kuwekwa kizuizini.

Babu yangu pia alitoweka akawa haonekani mjini na makachero wakawa wanamsaka bila mafaniko hadi alipojitokeza mwenyewe kituo cha polisi na hapo ndipo alipokamatwa.

TRAU wakati wa uhai wake TANU ilipokuwa inapigania uhuru wa Tanganyika chama hiki kilikuwa na nguvu kubwa kwani viongozi hawa wawili waliunganisha nguvu ya TRAU na TANU kupambana na Waingereza na hili lilitoa uwanja mpana sana kwa TRAU kufanya siasa za mapambano.

Mwaka wa 1960 TRAU ilifanya mgomo uliodumu siku 82 mgomo huu ulivunja rekodi ya mgomo wa Kenya chini ya kiongozi Makhan Singh wa siku 62 ambao kabla ya huu mgomo wa TRAU ndiyo uliochukua muda mrefu zaidi kumalizika.

Inasemekana ilikuwa mgomo huu ndiyo uliomtia Mwalimu Nyerere hofu kwani kwa miezi mitatu wafanyakazi wa reli waligoma na kufanya treni, meli na mabasi yasimame.

Ikamdhihirikia Nyerere kuwa hawa ndiyo viongozi wa wafanyakazi ambao atakuja kukabiliananao katika Tanganyika huru.

Hii ndiyo ikawa sababu ya yeye kuwakamata viongozi wa vyama huru vya wafanyakazi baada ya maasi na kuwaweka kizuizini na kuunda NUTA chama kipya cha wafanyakazi na kukiweka chini ya TANU.

Wakati Kassanga Tumbo anaondoka kwenda Uingereza kuchukua nafasi yake kama Balozi alikwenda kumuaga babu yangu na alimwambia kuwa Nyerere kaamua kumpeleka Uingereza kuwa balozi ili apunguze nguvu ya TRAU.

Yapo mengi sana ambayo Kassanga Tumbo na babu yangu walifanya pamoja na kushauriana.

Katika picha kulia ni Christopher Kassanga Tumbo na pembeni yake aliyevaa mgolole ni babu yangu Salum Abdallah.

Unaweza kumsoma zaidi Salum Abdallah hapo chini:
 

Attachments

  • SALUM ABDALLAH NA KASSANGA TUMBO.jpg
    SALUM ABDALLAH NA KASSANGA TUMBO.jpg
    76.8 KB · Views: 20
Asante sana chief; ndiyo tunasema harakati za kudai Uhuru wetu kuna baadhi ya mambo yamenyofolewa!! Ni lazima tuhakikishe tunayadai yarejeshwe kabla hatujatoka hapa duniani.
 
Nakumbuka nikiwa mdogo Mwalimu alituma wapambe wake kijijini na 109 Landrover kumpa tena KasangaTumbo shirika la Reli; Kasanga aligoma kabisa akasema Shirika umeliua wewe mimi leo unanipa maiti nikaizike...

Haya aliyasema mara kwa mara kwenye misiba ambapo ndipo ilikiwa room yake kuyasema; nikiwa mdogo sana tuliona kwamba kachanganyikiwa baadaye sana nikajua kumbe the guy was bright and intelligent .

Si kila kitu unachoambiwa na kiongizi wako kinakuwa sawa; hapana. Kiongozi bora ni lazima awe na focus & vision yake.

Viongozi wa sasa ni wa ndiyo Mzee...hapa ndipo tunapoiua Tanzania yetu kifo cha wima.
 
Kuna kipindi cha miaka ya themanini magari 3 aina ya Land-rover 109 yalikuja kijijini kwetu na kwenda moja kwa moja hadi kwake, watu wale wakaingia ndani wakaongea mambo mengi, sisi by the time tukiona gari linaingia kijijini lazima itakuwa ni msiba, lakini haikuwa hivyo; gari zile zikaondoka. Mara msiba ulipotekea tena mzee akafunguka akatuambia aliitwa na Mwalimu ili aende kupewa kazi ya kuongoza shirika la Reli - yeye akasema Shirika wameliua wao then wananipatia mimi - siwezi. Mimi kipindi hicho pamoja na utoto wangu sikumwelewa huyu mzee; kuna wakati mimi na marafiki zangu tukimwona amekaa nje ya nyumba yake akisikiliza radio (BBC) tulikuwa tunahisi kasoma hadi kachanganyikiwa - tulikuwa watoto hatukujua mambo mengi.

Christopher Kasanga Tumbo na Chief Addullah Fundikira ndiyo walikuwa watu wa kwanza kabisa kuunda chama 1992 (UMD) Union for Multi-Party Democracy baada tu ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi nchini. Chama kilikuwa kwa nguvu sana hasa kanda ya ziwa na Tabora wa ujumla!! lakini cha ajabu hakikufika hata 1995 kwenye uchaguzi mkuu wa kwanza kikawa kimesambaratika vibaya sana nafikiri ikikuwa kazi ya ki-itifaki.

Kijiji alichozaliwa Kasangatumbo (Ipole) kimekuwa na mizizi ya upinzani toka miaka hiyo, CUF wamekuwa wakitawala wakibadilishana na CCM, lakini uchaguzi mdogo juzi juzi CDM imechukua kata hiyo; si toka mbinguni lakini ni mizizi ambayo mzee kasangatumbo aliitengeneza. wazee na hata vijana /watoto wa wakati huo nikiwemo mimi tunakumbuka mchango wa Christopher kasangatumbo - ingawa hakuna historia yoyote iliyoandikwa juu ya maisha yake.

Ameondoka akiwa maskini ingawa alitoa mchango mkubwa kwa taifa hili - Kuhusu ungomvi na mwalimu hakuna anayejua ila aliishi Kijiji cha Ipole akiwa amekuwa-grounded na system, hakuwa na ruhusa kutoka mkoani Tabora bila kibali toka kwa mwalimu na pass ya kusafiria ilibebwa - pia hakuruhusiwa kufanya mikutano yoyote ile -- kwa ujanja wake alitumia misiba pale kijijini kutueleza falsafa ya demokrasia

sisi wanakijiji wa ipole hatuwezi kumchukia mwalimu kwa namna yoyote ile, lakini kama ungebahatika kuona maisha ya mwanasiasa huyu live basi ungeungana na mimi kusikitika kwamba hakuna hata kipande cha historia kilichoandikwa juu yake kwa vizazi vijavyo.

Kuna mdogo wake aliingia kwenye siasa, nafikiri kuna kipindi alikuwa CDM sijui yupo wapi siku hizi? ile miaka hiyo ya themanini kuna pia mdogo wake mweingine alikuwa anafanya shirika la viatu BORA, hata yeye sina habari zake, huu ni ukoo wa ki-chief kwa pale IPOLE na ndiyo maana ukimuuliza mtu yeyote aliyezaliwa hapo anaweza kukupa mengi juu ya hii familia.

kwa sasa ukoo huu ni kama umesambaratika, hata ile nyumba ya udongo iliyoezekwa kwa bati ambayo Kasangatumbo aliishi pamoja na familia yake akiwemo marehemu mama yake mzazi ilishaanguka kitambo. huwa nikienda likizo nyumbani nikiangalia masalia ya ile nyumba nakumbuka yote haya niliyowajuza leo, kweli yanasikitisha.

Wenye Kumbukumbu nzuri mwanasiasa huyu baada ya mambo kuwa magumu kimaisha na hali ya afya yake kuzolota basi alifuatwa na watu wa system na kweli for the first time akarudi CCM. hakudumu sana CCM mauti yakamkuta. Kipindi kile sikuweza kuhudhuria mazishi yake kwani nilikuwa chuo.

Sisi wana Ipole tutamkumbuka milele, kwani huu ukoo ni wa ki-chief na yeye alikuwa ni kamanda kweli kweli.


"Hakuna dola ambayo ilipambana na raia wake dola hiyo ikashinda" Mh. Christopher Kasanga Tumbo: (RIP)
Tunashukurubkuona kuwa bado wapo watanzania wanapata nafasi ya kufahamu ukweli juu ya historia ya taifa letu. Napenda pia kuwahimiza waandishi na wanahistoria mbalimbali kuandika upya historia ya nchi yetu ingali mapema kwani bado vyanzo vya taarifa vinapatikana kabla hatujasahau tulipotoka kabisa.
 
Fuso,
Naomba nami nikueleze machache kuhusu Christopher Kassanga Tumbo.

Mtaa wa Kanoni Isevya, Tabora mwanzo wa mtaa kwa mkono wa kushoto kama unaelekea Kachoma, kuna nyumba ya babu yangu Salum Abdallah maarufu kwa jina la Baba Popo.

Huyu Popo ni mwanae wa kwanza ambae kwangu mimi ni baba yangu mkubwa.

Jina lake hasa ni Humud lakini hili halikushika alijulikana kwa jina la Popo hadi mwisho wa maisha yake.

Jina lake kamili lilitakiwa liwe Mwekapopo jina la babu yake aliyeingia Tanganyika kutoka Belgian Congo kama askari katika jeshi la Wajerumani miaka ya mwisho 1880 lakini kwa ufupisho akawa wanamwita Popo.

Hapo mwanzo wa mtaa mkono wa kushoto ndipo ilipokuwa nyumba ya babu yangu Salum Abdallah Mwekapopo Samitungo Muyukwa.

Yote haya majina ya Kimanyema.

Nyumba ya babu yangu ilikuwa maarufu kwa kuwa katika miaka ile ya 1950 wakati harakati za kudai uhuru zimepamba moto yeye alikuwa mstari wa mbele dhidi ya Waingereza kwanza akiwa katika TAA, TANU na TRAU.

Mwisho wa mtaa wa Kanoni kabla hujafika Kachoma ilikuwapo nyumba nyingine ya babu yangu na mkabala wa nyumba hii ilikuwapo nyumba ya Christopher Kassanga Tumbo na zote mbili ni nyumba kwa wakati ule zlizokuwa nzuri mtaa mzima.

hii Kachoma ni sehemu maarufu kwa kuwa kulikuwa na kilabu cha pombe za kienyeji.

Mwaka wa 1955 mara tu baada ya kuundwa kwa TANU babu yangu na Kassanga Tumbo waliasisi chama cha wafanyakazi wa reli Tanganyika, kikijulikana kama Tanganyika Railway African Union (TRAU) babu yangu akiwa Rais na Kassanga Tumbo Katibu.

Wakati wa likizo mwaka wa 1964 nikiwa darasa la nne nililifika Tabora kumtembelea babu yangu lakini hakuwapo nyumbani na kwa akili za kitoto hili halikunishughulisha na baada ya likizo kwisha nikarudi Dar es Salaam bila ya kumuona.

Lakini kilichotokea kwa babu yangu kutokuwa nyumbani ni kuwa alikuwa amewekwa kizuizini jela ya Uyui kufuatia maasi ya wanajeshi tarehe 20 Januari,1964 na baada ya Jeshi la Kiingereza kumaliza maasi yale, serikali iliwakamata viongozi wote wa vyama vya wafanyakazi na kuwaweka kizuizini.

Kassanga Tumbo alipata taarifa za msako wa viongozi wa vyama vya wafanyakazi mapema na akawahi kutoroka akaenda Mombasa lakini alikamatwa baadae na akarejeshwa Tanzania na kuwekwa kizuizini.

Babu yangu pia alitoweka akawa haonekani mjini na makachero wakawa wanamsaka bila mafaniko hadi alipojitokeza mwenyewe kituo cha polisi na hapo ndipo alipokamatwa.

TRAU wakati wa uhai wake TANU ilipokuwa inapigania uhuru wa Tanganyika chama hiki kilikuwa na nguvu kubwa kwani viongozi hawa wawili waliunganisha nguvu ya TRAU na TANU kupambana na Waingereza na hili lilitoa uwanja mpana sana kwa TRAU kufanya siasa za mapambano.

Mwaka wa 1960 TRAU ilifanya mgomo uliodumu siku 82 mgomo huu ulivunja rekodi ya mgomo wa Kenya chini ya kiongozi Makhan Singh wa siku 62 ambao kabla ya huu mgomo wa TRAU ndiyo uliochukua muda mrefu zaidi kumalizika.

Inasemekana ilikuwa mgomo huu ndiyo uliomtia Mwalimu Nyerere hofu kwani kwa miezi mitatu wafanyakazi wa reli waligoma na kufanya treni, meli na mabasi yasimame.

Ikamdhihirikia Nyerere kuwa hawa ndiyo viongozi wa wafanyakazi ambao atakuja kukabiliananao katika Tanganyika huru.

Hii ndiyo ikawa sababu ya yeye kuwakamata viongozi wa vyama huru vya wafanyakazi baada ya maasi na kuwaweka kizuizini na kuunda NUTA chama kipya cha wafanyakazi na kukiweka chini ya TANU.

Wakati Kassanga Tumbo anaondoka kwenda Uingereza kuchukua nafasi yake kama Balozi alikwenda kumuaga babu yangu na alimwambia kuwa Nyerere kaamua kumpeleka Uingereza kuwa balozi ili apunguze nguvu ya TRAU.

Yapo mengi sana ambayo Kassanga Tumbo na babu yangu walifanya pamoja na kushauriana.

Katika picha kulia ni Christopher Kassanga Tumbo na pembeni yake aliyevaa mgolole ni babu yangu Salum Abdallah.

Unaweza kumsoma zaidi Salum Abdallah hapo chini:
Ahsante kwa histori kama hiz.
 
Ahsante kwa histori kama hiz.
London 1,
Historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ina mengi ya kusisimua.

Mimi nilijukuta kama vile niliyeingia dunia nyingine ambayo sikuwa hapa kabla najua kuwa ipo.

Fikiria nilikuwa hali gani siku Ahmed Rashad Ali ananifahamisha kuwa 1950 mashindano ya Kombe la Gossage yalikuwa yanafanyika Nairobi.

Haya yalikuwa mashindano ya mpira ya nchi nne za Afrika ya Mashariki yakifanyika kila mwaka.

Ahmed Rashad alikuwa nahodha wa timu ya Zanzibar.

Ananambia Abdul Sykes kaja Nairobi na akamweleza kuwa kaja kukutana na Jomo Kenyatta na viongozi wenzake wa Kenya African Union (KAU).

Abdul alikuwa ndiye katibu wa TAA baada ya mapinduzi yaliyowatoa madarakani Thomas Plantan President na Clement Mtamila Katibu.

Ahmed Rashad kwa jicho lake ananambia nimemsindikiza Abdul na nimemuona Kenyatta katoka nje ya nyumba ambayo walikuwa wanakutania na kamwita Abdul kwa jina kumkaribisha ndani.

Ahmed Rashad ananieleza yeye alibaki nje kusubiri akiwa na walinzi.

Baada ya zaidi ya miaka 30 rafiki zangu Uingereza wananiletea Tanganyika Intelliegence Summary taarifa za siri za kikachero za Waingereza wakithibitisha mkutano huu wa Abdul Sykes na Jomo Kenyatta, Peter Mbiu Koinange, Bildad Kaggia na timu nzima iliyokuja kujulikana kama Kapenguria Six.

Abdul alikuwa kijana mdogo wa miaka 26.
 

Attachments

  • KAPENGURIA SIX.jpg
    KAPENGURIA SIX.jpg
    38.4 KB · Views: 18
Informer,
Naikumbuka hii sana. Tuliposoma kwenye magazeti kuwa Kassanga Tumbo amesema amelipwa hela na Uingereza kumpindua Nyerere tulijua huyu jamaa ataishia detention. Na kweli muda haukupita akawekwa detention. Mimi nadhani tatizo la watu kama marehemu Tumbo ni kwamba alikuwa na akili sana na alijiona kuwa na akili sana na watu aina hii mara nyingi wana matatizo ya kutojua kitu cha kusema hadharani. Kuna mwingine yule aliyemfuata Mwalimu baada ya masomo na kusema kazi anayostahili kupewa ni ile aliyo nayo Mwalimu, sasa mtu kama huyu kweli utasema ana akili timamu?
Huyu atakuwa yule jamaa wa MAKETE mwenye degree saba
 
Nyerere asingewafanyia hayo waliompa changamoto madaraka yake yangekumbwa na misukosuko sana
 
Kuna kipindi cha miaka ya themanini magari 3 aina ya Land-rover 109 yalikuja kijijini kwetu na kwenda moja kwa moja hadi kwake, watu wale wakaingia ndani wakaongea mambo mengi, sisi by the time tukiona gari linaingia kijijini lazima itakuwa ni msiba, lakini haikuwa hivyo; gari zile zikaondoka. Mara msiba ulipotekea tena mzee akafunguka akatuambia aliitwa na Mwalimu ili aende kupewa kazi ya kuongoza shirika la Reli - yeye akasema Shirika wameliua wao then wananipatia mimi - siwezi. Mimi kipindi hicho pamoja na utoto wangu sikumwelewa huyu mzee; kuna wakati mimi na marafiki zangu tukimwona amekaa nje ya nyumba yake akisikiliza radio (BBC) tulikuwa tunahisi kasoma hadi kachanganyikiwa - tulikuwa watoto hatukujua mambo mengi.

Christopher Kasanga Tumbo na Chief Addullah Fundikira ndiyo walikuwa watu wa kwanza kabisa kuunda chama 1992 (UMD) Union for Multi-Party Democracy baada tu ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi nchini. Chama kilikuwa kwa nguvu sana hasa kanda ya ziwa na Tabora wa ujumla!! lakini cha ajabu hakikufika hata 1995 kwenye uchaguzi mkuu wa kwanza kikawa kimesambaratika vibaya sana nafikiri ikikuwa kazi ya ki-itifaki.

Kijiji alichozaliwa Kasangatumbo (Ipole) kimekuwa na mizizi ya upinzani toka miaka hiyo, CUF wamekuwa wakitawala wakibadilishana na CCM, lakini uchaguzi mdogo juzi juzi CDM imechukua kata hiyo; si toka mbinguni lakini ni mizizi ambayo mzee kasangatumbo aliitengeneza. wazee na hata vijana /watoto wa wakati huo nikiwemo mimi tunakumbuka mchango wa Christopher kasangatumbo - ingawa hakuna historia yoyote iliyoandikwa juu ya maisha yake.

Ameondoka akiwa maskini ingawa alitoa mchango mkubwa kwa taifa hili - Kuhusu ungomvi na mwalimu hakuna anayejua ila aliishi Kijiji cha Ipole akiwa amekuwa-grounded na system, hakuwa na ruhusa kutoka mkoani Tabora bila kibali toka kwa mwalimu na pass ya kusafiria ilibebwa - pia hakuruhusiwa kufanya mikutano yoyote ile -- kwa ujanja wake alitumia misiba pale kijijini kutueleza falsafa ya demokrasia

sisi wanakijiji wa ipole hatuwezi kumchukia mwalimu kwa namna yoyote ile, lakini kama ungebahatika kuona maisha ya mwanasiasa huyu live basi ungeungana na mimi kusikitika kwamba hakuna hata kipande cha historia kilichoandikwa juu yake kwa vizazi vijavyo.

Kuna mdogo wake aliingia kwenye siasa, nafikiri kuna kipindi alikuwa CDM sijui yupo wapi siku hizi? ile miaka hiyo ya themanini kuna pia mdogo wake mweingine alikuwa anafanya shirika la viatu BORA, hata yeye sina habari zake, huu ni ukoo wa ki-chief kwa pale IPOLE na ndiyo maana ukimuuliza mtu yeyote aliyezaliwa hapo anaweza kukupa mengi juu ya hii familia.

kwa sasa ukoo huu ni kama umesambaratika, hata ile nyumba ya udongo iliyoezekwa kwa bati ambayo Kasangatumbo aliishi pamoja na familia yake akiwemo marehemu mama yake mzazi ilishaanguka kitambo. huwa nikienda likizo nyumbani nikiangalia masalia ya ile nyumba nakumbuka yote haya niliyowajuza leo, kweli yanasikitisha.

Wenye Kumbukumbu nzuri mwanasiasa huyu baada ya mambo kuwa magumu kimaisha na hali ya afya yake kuzolota basi alifuatwa na watu wa system na kweli for the first time akarudi CCM. hakudumu sana CCM mauti yakamkuta. Kipindi kile sikuweza kuhudhuria mazishi yake kwani nilikuwa chuo.

Sisi wana Ipole tutamkumbuka milele, kwani huu ukoo ni wa ki-chief na yeye alikuwa ni kamanda kweli kweli.


"Hakuna dola ambayo ilipambana na raia wake dola hiyo ikashinda" Mh. Christopher Kasanga Tumbo: (RIP)
RIP Kasanga Tumbo rafiki yangu pia
 
Daaa kweli
Kuna kipindi cha miaka ya themanini magari 3 aina ya Land-rover 109 yalikuja kijijini kwetu na kwenda moja kwa moja hadi kwake, watu wale wakaingia ndani wakaongea mambo mengi, sisi by the time tukiona gari linaingia kijijini lazima itakuwa ni msiba, lakini haikuwa hivyo; gari zile zikaondoka. Mara msiba ulipotekea tena mzee akafunguka akatuambia aliitwa na Mwalimu ili aende kupewa kazi ya kuongoza shirika la Reli - yeye akasema Shirika wameliua wao then wananipatia mimi - siwezi. Mimi kipindi hicho pamoja na utoto wangu sikumwelewa huyu mzee; kuna wakati mimi na marafiki zangu tukimwona amekaa nje ya nyumba yake akisikiliza radio (BBC) tulikuwa tunahisi kasoma hadi kachanganyikiwa - tulikuwa watoto hatukujua mambo mengi.

Christopher Kasanga Tumbo na Chief Addullah Fundikira ndiyo walikuwa watu wa kwanza kabisa kuunda chama 1992 (UMD) Union for Multi-Party Democracy baada tu ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi nchini. Chama kilikuwa kwa nguvu sana hasa kanda ya ziwa na Tabora wa ujumla!! lakini cha ajabu hakikufika hata 1995 kwenye uchaguzi mkuu wa kwanza kikawa kimesambaratika vibaya sana nafikiri ikikuwa kazi ya ki-itifaki.

Kijiji alichozaliwa Kasangatumbo (Ipole) kimekuwa na mizizi ya upinzani toka miaka hiyo, CUF wamekuwa wakitawala wakibadilishana na CCM, lakini uchaguzi mdogo juzi juzi CDM imechukua kata hiyo; si toka mbinguni lakini ni mizizi ambayo mzee kasangatumbo aliitengeneza. wazee na hata vijana /watoto wa wakati huo nikiwemo mimi tunakumbuka mchango wa Christopher kasangatumbo - ingawa hakuna historia yoyote iliyoandikwa juu ya maisha yake.

Ameondoka akiwa maskini ingawa alitoa mchango mkubwa kwa taifa hili - Kuhusu ungomvi na mwalimu hakuna anayejua ila aliishi Kijiji cha Ipole akiwa amekuwa-grounded na system, hakuwa na ruhusa kutoka mkoani Tabora bila kibali toka kwa mwalimu na pass ya kusafiria ilibebwa - pia hakuruhusiwa kufanya mikutano yoyote ile -- kwa ujanja wake alitumia misiba pale kijijini kutueleza falsafa ya demokrasia

sisi wanakijiji wa ipole hatuwezi kumchukia mwalimu kwa namna yoyote ile, lakini kama ungebahatika kuona maisha ya mwanasiasa huyu live basi ungeungana na mimi kusikitika kwamba hakuna hata kipande cha historia kilichoandikwa juu yake kwa vizazi vijavyo.

Kuna mdogo wake aliingia kwenye siasa, nafikiri kuna kipindi alikuwa CDM sijui yupo wapi siku hizi? ile miaka hiyo ya themanini kuna pia mdogo wake mweingine alikuwa anafanya shirika la viatu BORA, hata yeye sina habari zake, huu ni ukoo wa ki-chief kwa pale IPOLE na ndiyo maana ukimuuliza mtu yeyote aliyezaliwa hapo anaweza kukupa mengi juu ya hii familia.

kwa sasa ukoo huu ni kama umesambaratika, hata ile nyumba ya udongo iliyoezekwa kwa bati ambayo Kasangatumbo aliishi pamoja na familia yake akiwemo marehemu mama yake mzazi ilishaanguka kitambo. huwa nikienda likizo nyumbani nikiangalia masalia ya ile nyumba nakumbuka yote haya niliyowajuza leo, kweli yanasikitisha.

Wenye Kumbukumbu nzuri mwanasiasa huyu baada ya mambo kuwa magumu kimaisha na hali ya afya yake kuzolota basi alifuatwa na watu wa system na kweli for the first time akarudi CCM. hakudumu sana CCM mauti yakamkuta. Kipindi kile sikuweza kuhudhuria mazishi yake kwani nilikuwa chuo.

Sisi wana Ipole tutamkumbuka milele, kwani huu ukoo ni wa ki-chief na yeye alikuwa ni kamanda kweli kweli.


"Hakuna dola ambayo ilipambana na raia wake dola hiyo ikashinda"
Mh. Christopher Kasanga Tumbo: (RIP)
 
Historia adimu sana kwenye Uzi huu. Nilisoma kwenye kitabu cha Sir Andy Chande, A Knight in Africa, anaeleza kuwa mgogoro wa Africanization uliwafanya Nyerere na Tumbo kugombana.

Afrikanization ilikuwa ni vuguvugu lilokuwa ndani ya TANU ambalo lilipigania kuona watanganyika 'weusi'-wakidaiwa ndio watanganyika halisi-pekee ndio wanashika nafasi zote za utawala nchini. Nyerere alipinga sera hii akiamini utanganyika sio rangi bali uzalendo. Nyerere aliacha uwaziri mkuu na kumkabidhi Kawawa, yeye akazunguka nchi nzima akihubiri dhidi ya afrikanaizesheni. Sasa vyama vya wafanyakazi mfano cha mkonge cha Kassanga Tumbo kilikuwa mstari wa mbele juu ya afrikanaizesheni. Hii ikamlazimu Nyerere kuja na sheria iliyoipa mamlaka serikali kuweka mtu kizuizini pasi na kupelekwa mahakamani (Preventive Detention Act). Tumbo alikumbwa na gharika hili. Na ndio sababu vyama na jumuiya za kijamii kuwa 'chini' ya serikali.
 
Huyu mzee alipotoka kizuizini, alikuwa anaishi maeneo ya Ubungo kwa mdogo wake. Alikuwa akisikia watu wanaongea siasa tu alikuwa anatoka nduki. Hivi walimfanya nini?
Anaona mnamletea nyoka amgonge kwa Mara ya pili tena tena kinga za mwili zimeshachoka hazihimili sumu ya nyoka huyo
 
Karanga Tumbo alianza siasa alisoma shule ya Tabora boys secondary school na alimaliza katika miaka ya katikati ya 50 akiwa na Edwin Mtei alianza siasa tangu akiwa shule Tabora school kwa kukataa kuitwa Christopher Samuel Tumbo na kujiita Kasanga Tumbo (jina lake la kiafrika) ilipelekea kuta kufukuzwa shule lakini alifanikiwa kumalizia shule na kuchaguliwa kujiunga na chuo kikuu cha Makerere huko uganda lakini hakwenda na aliamua kuanza kazi katika shirika la Railways co.na hapa ndipo alipoanza Siasa baada ya kuchaguliwa kuwa katibu mkuu wa chama cha wafanyakazi cha Railways na mwaka 58 (akiwa na umri wa miaka 24) alianzisha mgomo uliodumu kwa siku tisini (huu ndio ulikuwa mgomo wa mwisho wa kupinga ukandamizaji wa wazungu ambao uliwaogopesha wazungu na kupelekea kuachia nchi) baada ya uhuru akiwa na miaka 26 aliteuliwa kuwa Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Uingereza baada ya muda aliacha ubalozi na kurudi Tanzania na alianzisha chama cha siasa PDP ambacho kilikubarika sana nadhani ndio kilicho mletea shida mpaka ukapelekwa kukimbia nchi na kupata hifadhi nchini Somalia na baadaye Kenya huko ndiko alipokamatwa na kurejeshwa Tanzania na alishtakiwa kwa kesi ya uhaini akaukumiwa kunyongwa kwa bahati nzuri inashindikana (haikuwa kunyongwa mpaka kufa) ivyo akafungwa miaka 27 (miaka3 jela) . Mwaka 92 wakaanzisha kamati ya kushinikiza katiba (NCCR) yeye akiwa masterplan baadae akataka kiwe chama wengine wakaogopa yeye na Chief s Fundikira wakaanzisha UMD ndicho chama cha kwanza cha upinzani lakini kikasambaratika bàada ya hapo akajiunga na vyama mbalimbali na atimaye Chadema likiwa bado akatembee nchi nzima na aliweka matawi nchi nzima lakini aliona baada ya kufanyiwa figisu figisu zilizo mfanya aende CUF napo pia alifungua matawi mengi sana na alipata umaarufu sana ( washabiki walimwita Mandela) napo figisu zimuondoa ndio akajiunga na CCM lakini hakudumu na alifariki dunia
 
Paundi 60,000 ili kuweza kumpindua Mwalimu Nyerere, nahisi hapa ndipo alipochemsha na kujikuta hawezi kukwepa mkono wa dola.
Je zilibainishwa sababu ni nini hasa za kulipwa ili ampindue Mwalimu.
 
Back
Top Bottom