Huyu raia Godwin Gondwe amepata wapi ujasiri wa kuvaa sare za JWTZ?

Huyu raia Godwin Gondwe amepata wapi ujasiri wa kuvaa sare za JWTZ?

1. DC Gondwe amepataje credential za kuvaa sare za JWTZ?
2. Nani amempa DC Gondwe sare za JWTZ?
3. Sheria inasemaje kuhusu matumizi ya sare za JWTZ?



Kama kuna katazo hili la raia kutokuvaa sare za jeshi, kwanini hili limefanyika ?

Tatizo hata jeshi letu linapata amri toka mhimili fulani
JWTZ ilikuwa zamani sio sasa
Nchi imeuzwa kwa mtu mmoja anafanya anavyotaka kwa kusaidiwa na akina bashite hapi n.k
Safari ni ndefu sana.
 
Ndio liko chini ya serkal
Tatizo hata jeshi letu linapata amri toka mhimili fulani
JWTZ ilikuwa zamani sio sasa
Nchi imeuzwa kwa mtu mmoja anafanya anavyotaka kwa kusaidiwa na akina bashite hapi n.k
Safari ni ndefu sana.
 
Hapa ni ulaya? Acha usenge
Nguo aliovaa Gondwe sio sare ya JWTZ kwasababu ni T~SHIRT na Kofia za kawaida ; nguo ambazo leo hii mtu anaweza akaenda kwenye duka la MACY's au JC PENNY huko marekani au Canada na akanunua hizo nguo bila taabu yoyote!!! Ni ushamba na lack of exposure ndio inawasumbua watu; Gondwe angevaa tepe mabegani hapo mgekuwa na jambo la kudadisi!! Hizo Nguo za mabaka mabaka ni za kawaida sana ulaya na marekani kwa wenzetu. Waulizeni mabalozi wenu.
 
Kuna kipindi nilikuwa na mazungumzo na vijana fulani wa ughaibuni, na mnene mmoja aliyetoka serikalini na kwenda kufanya kazi mashirika ya kimataifa ughaibuni.

Nikawa nalalamika habari za Magufuli kujimwambafy.

Mnene yule akasema, sasa hivi tatizo linatoka kwa Magufuli tu, huku chini vinatengenezwa vi Magufuli vingine viingi.

Sasa nilivyoona hili nikakumbuka kauli ile.

Viongozi wa serikali wanatakiwa kujua maana ya "civilian leadership of the military".

Wanatakiwa kujua "perception creates its own reality".

Magufuli ameshindwa kuongoza katika hili.

Kikwete aliyekuwa mwanajeshi, ikambidi aondoke jeshini ili kubaki kwenye siasa, alilielewa hili vizuri sana. Ndiyo maana ni nadra sana kumuona Kikwete kama kiongozi wa serikali kavaa nguo za jeshi.

Mkapa hakuvaa hivyo. Mwinyi hakuvaa hivyo.

Nyerere, rais pekee wa vita Tanzania, nje ya kuhamasisha majeshi vita vya Kagera, hakuvaa magwanda ya jeshi.

Siku hizi mpaka ma DC wanavaa magwanda.

Scratch that, mpaka wanajeshi -si wanajeshi wastaafu, walio active- wanateuliwa kuwa ma DC.

Kwa hivyo haya ya kina Gondwe sishangai.

Kwa sababu wanamuiga mkubwa wao, Magufuli.

Ukiwauliza watakwambia wao ni viongozi wa kamati za ulinzi wilayani!

Na kama umekubali Magufuli kuvaa magwanda, huna sababu ya kuwakatalia hawa.

Wanachotofautiana na Magufuli ni scope tu. Wote ni viongozi wa kiserikali. Wengine wilayani, Magufuli kitaifa.
 
Labda kwa kuwa yeye ndiyo mwenyekiti wa ulinzi na usalama basi huenda anaruhusiwa

Ila hivi kwanini huwa wanapenda kuvaa za JW tu!! za magereza au zimamoto hawazipendi??
Hata Afisa Mtendaji Kata na mwenyewe ni Mlinzi wa Amani katika kata yake!!

Sasa ikiwa kila mlinda mlinzi wa amani aruhusiwe kuvaa gwanda, si kila tunakopita tutakutana na gwanda!!!

Btw, kama ni suala la kulinda amani, wao wanalinda amani ya ndani. Sasa kama kulinda amani kunaendana na gwanda, kwanini asivae gwanda za polisi?!
 
Back
Top Bottom