Uchaguzi 2020 Huyu siyo Abood ninayemjua. Huwezi kuwa mwema utotoni ukawa shetani uzeeni

Mimi Morogoro ipo moyoni,sisi watoto wa Morogoro tumekulia Morogoro kuishi tunakuja kuishi Dar maana Morogoro hakuna ajira,kwa hiyo Morogoro wapo wazee wetu tu,hili jambo linauma kwa kila aliyekulia Morogoro maana tukiwa wadogo Miaka ya 1980's tulikuwa tunaona viwanda vikiajiri maelfu ya watu,wakichukuliwa na bus asubuhi na kurudishwa jioni,Viwanda vya Vyombo vya Udongo (Ceramics) Moro Shoes,Polyster,Canvas,Moproco,Viwanda vya dawa za Kilimo,kiwanda Cha nyuzi za mkonge,Kiwanda cha ngozi.
 
Kwenye kura za maoni nilienda chooni nikakuta mtu anagawa 10,000 akanipa elfu kumi kaniambia nenda kampigie,nilivyorudi nikawaambia wenzangu kuna mtu anagawa hela,tukasema kwa Viongozi wa Uchaguzi wakapiga marufuku kwenda chooni,tukasikia tena supu inagawiwa bure duuh
 
Huyo Mbunge kichwani hamna halafu kakutana na Mwenyekiti wa Wilaya ambae anachukua Uenyekiti wa Mkoa,kichwani nae hamna,kwenye ufunguzi wa soko Rais alipomsifia Mwenyekiti wa Wilaya anampa dole anamwambia unaona halafu wanacheka kipesa pesa,pale kwa body language anamwambia ongeza pesa basi nimefanya hadi Rais anakusifia,
 
Abood sio level yako kaa kwa kutulia....wewe so far umefanya nini hapo Morogoro?
 
LOooo, umeyasema mengi ya moyoni!

Sasa elewa hiyo ndiyo CCM, Chama Cha Mapinduzi, kilichoasisiwa na mpenda haki; mpiganiaji wa dhati wa wanyonge.

Lakini tunapoyasema yote haya, inatulazimu pia tujiulize: hivi hawa wananchi wanaotumiwa kwa nini hawayaoni haya na kuyakataa?

Sasa nimekumbuka jambo: watu wa Morogoro (mkoa), inasemekana ndio waliotoa kura zao nyingi 96% kumchagua kiranja!

Kuna uhusiano wowote wa kura hizo na mchango mkubwa alioufanya Abood katika upatikanaji wa kura hizo nyingi?
 
Unafiki unawasumbua wana ccm,mbona hukuwahi kusema sasa?zaidi zaidi mlikuwa mnashangilia ushindi wa kishindo cha wizi?
 
Huna jipya Morogoro ina wenyewe....
Ukweli mchungu, Morogoro ina wenyewe!
Wengine tumetoka huko tukaja kutafuta maisha Morogoro.
Baada ya kura za maoni walioshindwa wote waliamriwa na wakakubali kufanyia kampeni wateuliwa.

Wakasherehekea kwa pamoja ushindi wa kishindo. Kumbe walikuwa na vinyongo. Unafiki, fitina, vijiba vya roho havijawahi kumuacha mtu salama. 😂 😂

Everyday is Saturday................................😎
 
Hata shetani Alikuwa malaika(kwa mujibu wa biblia ...Abood Ni Nani ?
Asibadilike?
 
Kufa kwa moro ndio kuneemeka kwa Kariakoo kwa bidhaa (feki zikiwemo) za kutoka nje ya nchi
 
cyo Siri ule mji ulipambwa kwa viwanda kwakweli lakini sasa duuuuuh umesahau komoa na bado hii awamu ya moto mzee kakimalizia na kiwanda cha tumbaku
 
tajiri anaijua sana akili na udhaifu wa maskini. Maskini daima anapumbazwa na vitu vidogo vidogo visivyoweza mnasua kwenye shida zake. Kwa jamii iliyoorganised, huhitaji mpigia kura mtu kwa kigezo cha kusaidia msiba.

ndio yale ya mgodi kuondoka na mabilion huku maskini wakipewa vyandarua.
 
Lakini tujiulize wema huo mnaousema alikuwa nao tangu akiwa si mbunge? Je wema huo alikuwa nao hata kwenye taasisi zake zinazoajiri watu. Isije ikawa ni wema wa Mamba wa kukulilia wakati amekukosa kukutafuna au anataka kukutafuna. Abood anaonekana mpole na mtu mcha Mung ukimuanagalia usoni, sijui watu walio karibu nae wanasemaje. Kwa kweli aliyoyafanya safari hii kwenye mchakato wa uchaguzi yanatia ukakasi hadhi yake na mbaya zaidi leo andhalilishwa na Rais mbele ya wapiga kura wake. Hii ndi kazi ya shetani, kukutumia halafu anakuanika uadhirike. Alitakiwa asome alama za nyakati kwani huyu huyu Rais alishamzodoa siku moja pale stand ya mabasi Msamvu, ingawa kwa ajili ya mchuan kuwa mkali kwenye uchaguzi huu walimwacha kwa sababu ya uezo wake wa pesa.
 
Mkuu Beatrice Kamugisha, unaposhirikiana na mchawi,ipo siku nawe utawanga tuu.
CCM ni genge la kihalifu. Ukiingia humo ndani yake, lazima nawe ufuate ibada zao.
Hakuna shetani mzuri,shetani ni shetani tu.
 
tutajie sisiemu mmoja ambaye kichwani zimo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…