Ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Akwilina: Padri Mayanga ataka aliyeua awekwe wazi, awaombe radhi Watanzania

Ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Akwilina: Padri Mayanga ataka aliyeua awekwe wazi, awaombe radhi Watanzania



Baba Paroko uko vizuri sana! Kwa utulivu mkubwa umeongea ujumbe mkubwa sana! Mungu akubariki sana!
 
Kaeni mbali isije ikatokea hii kitu
d874ff475664afa6197c2800f8d47237.jpg
[emoji87] [emoji87] [emoji85] [emoji15]
 
Anhaaa... basi nchi yetu sio shithole bali baadhi ya viongozi wetu... hapo vipi?
teh...teh..bora babu umetoa draw nilikuwa nampango wa kukusemea kwa bibi kuwa wanakuchuna huku! lakini kwa hili nimekubali
 
Kwenu,

Katika muda wote ambao nchi inaomboleza kimya kimya kifo cha mwanafunzi wa NIT, Akwilina, Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako ameonekana kuwa mstari wa mbele katika kufariji, kuhakikisha maziko yanafanyika kama Serikali ilivyoahidi na kuhimiza uchunguzi unaharakishwe ili muuaji afikishwe mbele ya sheria.Sijamsikia Waziri wa Mambo ya Ndani, Mh. Mwigulu.

Inatia uchungu na kusikitisha binti mdogo kuuawa bila hatia. Mauaji kabla, wakati na baada ya chaguzi ndogo ni kitu kilichozoeleka. Imezoeleka si kwa kuwa ni kawaida, la hasha, ni kwa sababu dola haijawahi kuhangaika kutafuta au kushughulikia muuaji/wauaji.

Ni jambo la kusikitisha pia, kwamba mauaji haya huwalenga viongozi na wanachama wa CHADEMA. Baada ya mauaji ya Akwilina, polisi walitangaza kumsaka Mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe ingawa hakuwa amejificha. Polisi pamoja na mashabiki wengi wa CCM wanamnyooshea kidole Mh. Mbowe kama mhusika mkuu ingawa hakufyatua risasi. Ni sahihi kufyatua risasi za moto kwa kulenga ili kutawanya waandamanaji?

Inaelekea kuna mtu alilengwa lakini risasi haikumpata. Ingempata kusingekuwa na kauli za kukanganya toka kwa polisi. Kufyatua risasi kwa kulenga raia hakuna maana ya kutawanya, kuna makusudi ya kuua. Ukikusudia kuua unashindwaje kumjua muuaji?

Waliomuua Alfonce Mawazo,waliowachinja viongozi wa CDM Kata ya Usa River Arumeru Mashariki wakati wa uchaguzi mdogo,waliomteka kisha kumuua katibu wa CHADEMA kata ya Hananasif Kinondoni ni watu wa aina moja na lengo moja, kupata faida za kisiasa kwa gharama ya uhai wa watu wengine(ambao hawastahili kupewa uongozi japo wa kata).

Kugharamia mazishi kwa milioni 80 kwa mtu aliyeuwawa kwenye maandamano(ingawa alikuwa mpita njia)ni huruma ya ajabu sana ambayo haijapata kutokea. Serikali itawajibu nini ndugu wa raia watakaodai gharama za mazishi kwa kuuawa wapendwa wao katika mazingira yaleyale ya Akwilina?

Ni vema kufanya uchunguzi na kuwabaini wauaji wote waliohusika kwenye mauaji kabla, wakati na baada ya chaguzi ndogo/chaguzi za marudio. Kila mtu ana haki ya kuishi, hata kama humpendi.

RIP Akwilina.
 
Anayedhani yuko salama asikilize vizuri clip ya mama Aquilina akimwambia prof Ndalichako kwamba alikuwa akisikia kwenye vyombo vya habari watu wanauawa na polisi lakini hakutegemea hata siku moja kwamba hilo litatokea kwa mmoja Wa wanafamilia wake. AJIDHANIAYE AMESIMAMA AANGALIE ASIANGUKE.
Maneno ya mzee wa sheria yanatimia,alisema msidhani kuwa,mko salama kila wakati
 
Anayedhani yuko salama asikilize vizuri clip ya mama Aquilina akimwambia prof Ndalichako kwamba alikuwa akisikia kwenye vyombo vya habari watu wanauawa na polisi lakini hakutegemea hata siku moja kwamba hilo litatokea kwa mmoja Wa wanafamilia wake. AJIDHANIAYE AMESIMAMA AANGALIE ASIANGUKE.
Maneno ya mzee wa sheria yanatimia,alisema msidhani kuwa,mko salama kila wakati
 
Padre wangu amesahau kuwa msamaha haulazimishwi. Tatizo si msamaha bali ni zaidi ya aliyepiga risasi. Kama ni msamaha Uongozi wa juu wa serikali ndio unaotakiwa kufanya hivyo siyo waliyempa risasi za moto kwenda nazo site.
 
hivi kwanini tusiungane jf kumchangia huyu mzee rambirambi za kumjengea nyumba iwe ndo pole yetu na rambi rambi zetu
 
Nshatoa ushauri ni bora upinzani waunde kikosi kazi chao kwaajili ya kudeal na polisisiem pamoja na viongozi wanajifanya kulewa madaraka......hire snippers and serial kill3rs...haya magamba yatanyooka tu.
 
Amani iwe nanyi, cku zote msema kweli ni mpenzi wa mungu nami nasema kweli ya kwamba police ndio waliofanya vurugu tarehe 16/02/2018 na hatimae kusababisha kifo cha dada yangu akwilina. Maana naona zinafanyika jitihada kubwa kupotosha ukweli.

Umma wote wa Tanzania wanafahamu ukweli huu kwamba police wa Leo kazi yao kubwa ni kulinda chama cha mapinduzi na sio RAIA kama ilivyo msingi mkuu wa kuanzishwa kwake. Tufahamu kua hata jambazi ana haki ya kuishi sio kuuawa sembuse wafuasi vya vyama vya upinzani na RAIA?
Ova.
 
hivi kwanini tusiungane jf kumchangia huyu mzee rambirambi za kumjengea nyumba iwe ndo pole yetu na rambi rambi zetu
Kwani analala nje, au barabarani, una maana gani, kabla ya hapo aliishi wapi?
 
Hata yule Abdul Nondo wa ngome ya vijana sijamsikia akisema lolote kama huu ndio mwisho rasmi wa kufuatilia haki za Akwilina.

Ila kiukweli wanasiasa ni kama wala rushwa tu wamepofushwa macho, fikiria katika hitimisho la kesi kama hii mbwembwe za kulipiana faini zinatoka wapi?.......haikuwezekana kulipiana kimya kimya huku tukitafakari damu isiyo na hatia ya mtoto Akwilina iliyomwagika?

Tuzidi sana kumuomba Mungu atuletee amani ile atoayo yeye ya mbinguni.

Nawatakia Kwaresma yenye baraka!
 
Back
Top Bottom