Ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Akwilina: Padri Mayanga ataka aliyeua awekwe wazi, awaombe radhi Watanzania

Nimeumia sana kwa msiba wa mdogo wangu huyu, natumia nafasi hii kusali na kukushukuru Mungu Baba mwingi wa rehema, ulimleta Akwelina kama ua zuri kwetu, tunashukuru kwa waliopata kumfahamu na kuishi naye, nakuomba Baba umpokee, umsamehe dhambi zake zote, wafariji wazazi wake, wadogo zake wote, kaka hata ndugu zake. Uwasamehe na kuwahukumu wale wote walio sababisha haya kadri utakavyoona inakupendeza.
Tunashukuru kwa kutufariji kipindi hiki kigumu cha msiba wa rafiki, mdogo wetu, mtoto wetu.

Sina la kuongea zaidi, akwelina pumzika kwa amani, siku moja tutaonana tena ! Amen !!
 
Padri sio kiongozi wa serikali ni wa kidini alitakiwa ajikite hapo tu akijua kuwa huyo mpiga risasi aweza kuwa mkatoliki ambaye aweza kuja kwake kuungama dhambi ya kuua.Mihemko ya kisiasa imemtoa kwenye reli ya upadre akaongea yasiyohusiana na upadre
Falsafa aliyotumia huyo padri kufikisha ujumbe ni ngumu sana kwa wenye vichwa vya panzi kama wewe kumuelewa
 
Pumzika kwa a mani binti yetu Dunia tunapita na binadamu sote tutakufa kiburi cha uzima kitakoma inahuzunisha sana Mungu atupe moyo mkuu na ajilipizie kisasi kwa wahusika.
 
Siku mtapiga watu risasi na hakutakuwa na kiongozi wa upinzani wa kumtupia lawama.

Jitoeni akili tu. Jifanyeni hamuoni. Jifungeni macho na masikio. Jitieni mnajua sana kusimamia baadhi ya vifungu vya sheria huku vingine mkivifumbia macho.

Mtu anayekuogopa akikupiga, anakupiga kwa nguvu sana kwasababu moyoni mwake ana hofu kuwa utampiga yeye. Uwoga wenu umesababisha mtumie nguvu kubwa sana siku hadi siku.

Karma will strike.
 
Stupid logic. Eti akienda kutubu atamwanika wazi. Usichanganye mambo ya kiroho na kijamii.
 
Inakuwaje katika msiba wa yule Katibu wa CHADEMA hatukuona waziri au kiongozi yeyoye wa serikali akiwemo mkuu wa Mkoa. Leo wote wako hapo wakionyesha majonzi ya kutisha. Je damu ya Aqulina ni nzito kuliko ya Daudi?

R.I.P Aquilina na Daudi
Inawezekana wanaamini yule alistahili lakini huyu ni 'bahati mbaya'
 
Akiwekwa wazi . Na aseme ni nani alimpa amri ya kupjga risasi za moto.
 
Umeandika upuuzi mwingiii
 
NENO
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…