Ibada za wakiristo mbona siku hizi zipo hivi?

Ibada za wakiristo mbona siku hizi zipo hivi?

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
1. Utakuta baadhi ya makanisa saa 11 alfajiri yanaanza ibada kwa kutumia maspika makubwa yanayotoa sauti kubwa . kama unaishi Mitaa ya Mbabaga basi hadi Kongowe utasikia. na sio kama sauti ya mchungaji bali ni nyimbo na mziki wenye kurindima na kutikisha nyumba

2. Ukiwa kanisa lipo karibu na msikiti- mziki wote unangia msikitini
Kama kanisa lipo karibu na chuo kikuu au Taasisi ya Taaluma siku hio huwezi kusoma

3. Baadhi ya makanisa hasa walokole wanasali usiku kwa kutumia maspika yenye sauti kubwa na kusababisha hata watoto na wagonjwa washindwe kulala

BIBLIA INATAKA IBADA KWA SIRI
Mathayo 6:6 (Biblia Habari Njema):
  • "Lakini wewe, ukiomba, ingia chumbani kwako, ukafunge mlango wako, na omba kwa Baba yako aliye siri; na Baba yako aonae siri atakujalia wazi."
  • Katika kifungu hiki, Yesu anasisitiza umuhimu wa sala kwa siri na kwa uaminifu wa moyo, badala ya kufanya ibada kwa ajili ya kuonekana na watu.
  • Marko 12:30 (Biblia Habari Njema):
    • "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote."
    • Ingawa kifungu hiki hakizungumzii ibada kwa siri moja kwa moja, inasisitiza mapenzi ya kweli ya moyo na roho kwa Mungu, jambo ambalo linaweza kujumuisha kufanya ibada kwa hali ya siri na kwa uaminifu wa ndani.
  • Mathayo 6:5 (Biblia Habari Njema):
    • "Wakati mnapokuwa mnawomba, msifanye hivyo kama wanafiki, kwa sababu wanapenda kusimama wakiomba mashuleni na kwenye kona za mitaa ili waonekane na watu. Kweli nawaambieni, wameshapokea thawabu yao."
    • Katika aya hii, Yesu anasisitiza kwamba kufanya ibada kwa lengo la kuonekana na watu ni kupoteza malipo. Hii inahusu zaidi kuhusu nia ya moyo kuliko sauti inayotumika.

IBDA ZA WAISLAM
Waislam wao sauti inatoka kwenye adhana tu ambayo dakika 2 au ili kuamsha watu, na hii inawasadia hata wasiokuwa waisam kuwahi makazini, mashuleni na masokoni.

TANBIH
Maada hii haina nia ya kukebehi dini, ni maada ya kuelimishana katika hii dunia.
Uislam inawapenda watu wa dini nyengine wao wanavyowapenda waislam. ushahidi wa haya ni hi:
Surah Al-Mumtahanah (60:8):

  • "Mwenyezi Mungu hakukatazi wale wanaokutendeeni mema na hawakukufuru kwa dini yenu kuwa na urafiki nao. Hakika Mwenyezi Mungu anapenda wenye haki."
  • Aya hii inaonyesha kuwa Waislamu wanapaswa kuwa na urafiki na heshima kwa wale wanaoishi kwa amani na waislamu na hawawapingi katika dini yao.
Pia wakati wa Mtume kulikuwa na Makafiri wakubwa wakimpiga vita Mtume wazi wazi wengine kupanga kumuua, lakini baadae wakasilimu wakawa ndio Maswahaba wakubwa. Pia Mtume wakati alipopigwa mawe akatakiwa aombe dua kwa wale waliomshambulia, yeye akaomba Allah awajaalie watoto waliomshambulia wawe watoto wema
KWA MFANO WATU WAOVU BAADAE KUWA WEMA WAKUBWA
  • Abu Sufyan ibn Harb (RA):
  • Abu Sufyan alikuwa kiongozi wa Quraysh na adui mkubwa wa Mtume Muhammad (SAW) kabla ya kubadili imani na kukubali Kiislamu. Alikuwa na nafasi muhimu katika vita vya Badr, Uhud, na Hudaibiya, lakini baadaye aligeuka kuwa muislamu baada ya Mkataba wa Hudaibiya na aliungana na Waislamu.

  • Ikrimah ibn Abi Jahl (RA):
  • Ikrimah alikuwa mwana wa Abu Jahl, mmoja wa maadui wakuu wa Mtume Muhammad (SAW). Alikuwa na uadui mkali dhidi ya Waislamu lakini alikubali Kiislamu baadaye na kuwa mmoja wa waislamu wa kweli.
  • Khalid ibn al-Walid (RA):
    • Khalid alikuwa kiongozi maarufu wa jeshi la Quraysh na aliongoza vita dhidi ya Waislamu. Alikuwa na uadui mkubwa na Mtume Muhammad (SAW) lakini alikubali Kiislamu baada ya vita vya Uhud na kuwa mmoja wa mashujaa wa Kiislamu katika vita vya Khyber na vita vingine.
  • Amr ibn al-As (RA):
    • Amr alikuwa mmoja wa viongozi wa Quraysh na alikuwa na upinzani dhidi ya Waislamu. Alikubali Kiislamu baada ya Mkataba wa Hudaibiya na alichangia kwa kiasi kikubwa katika kueneza dini ya Kiislamu.
  • Hind bint Utbah (RA):
    • Hind alikuwa mke wa Abu Sufyan na aliongoza kampeni dhidi ya Waislamu. Baada ya kukubali Kiislamu, aligeuka kuwa mcha Mungu na aliunga mkono dini kwa nguvu.WAPO WAISLAM WALIOASI KWA MFANO
  • Abdullah ibn Ubayy (RA):
    • Abdullah ibn Ubayy alikuwa kiongozi wa makabila ya Khazraj na alikuwa miongoni mwa Waislamu waliokubali dini mapema. Hata hivyo, alikuwa na matendo ya unafiki na alijaribu kudhoofisha jamii ya Kiislamu kwa kutoa maoni yenye mashaka na kuongoza watu kwa uasi.
Ndio maana waislam kila wakati tunatakiwa tuombe Allah atuondoshe katika dunia hali ya kuwa ameturidhia

SOMA KWA UTULIVU KABLA KUKOMENTS USIJE KUCOMENTS KITU USICHOKIJUA
 
1. Utakuta baadhi ya makanisa saa 11 alfajiri yanaanza ibada kwa kutumia maspika makubwa yanayotoa sauti kubwa . kama unaishi Mitaa ya Mbabaga basi hadi Kongowe utasikia. na sio kama sauti ya mchungaji bali ni nyimbo na mziki wenye kurindima na kutikisha nyumba

2. Ukiwa kanisa lipo karibu na msikiti- mziki wote unangia msikitini
Kama kanisa lipo karibu na chuo kikuu au Taasisi ya Taaluma siku hio huwezi kusoma

3. Baadhi ya makanisa hasa walokole wanasali usiku kwa kutumia maspika yenye sauti kubwa na kusababisha hata watoto na wagonjwa washindwe kulala
Kuna kiongozi wa NEMC alianza kulifanyia kazi jambo hili watu walimshambulia sana kwa maneno
 
UMESOMA? AU UNARUKIA TU? TULIA USOME ACHA JAZBA. HII SIO CCM VS CHADEMA ULIZOEA JUKWAA LA SIASA
Hili nakubaliana na wewe. N makanisa ya kilokole. Serikali ndiyo ya kulaumiwa. Jiji la Dar lina noise pollution mbaya sana. Bar, makanisa, honi za magari na wapiga debe wanaotumia speaker.
 
Hili nakubaliana na wewe. N makanisa ya kilokole. Serikali ndiyo ya kulaumiwa. Jiji la Dar lina noise pollution mbaya sana. Bar, makanisa, honi za magari na wapiga debe wanaotumia speaker.
noo. sio kuwathibiti. huwezi kumtibti mtu mwenye imani, muelimishe ili aelimike mwisho wa siku atafahamu
 
noo. sio kuwathibiti. huwezi kumtibti mtu mwenye imani, muelimishe ili aelimike mwisho wa siku atafahamu
Niko sahihi. Kudhibiti. Namaanisha hivyo. Imani ya jambo lolote siyo tiketi ya kuvunja sheria. Sheria ya kukataza uchafuzi wa sauti ipo. Mamlaka zinazohusika zinatakiwa kuitumia. Najuwa wewe pengine unaona kama itakuwa tishio kwa waislam na adhana zao. Adhana kutoka misikitini kwangu siyo issue kubkwa kwa sababu inafanywa kwa muda mfupi na haikeri kama maspika ya mahubiri kutoka makanisani yanayoungurumishwa karibu siku nzima. Au muziki wa bar kutwa kuchwa.
 
Umeileta hii mada kwa mtazamo wa kidini! Kama ungeileta mada kwa mtazamo wa kuchafua mazingira ungeeleweka!
Hata hivyo mamlaka husika zichukue hatua!
 
Niko sahihi. Kudhibiti. Namaanisha hivyo. Imani ya jambo lolote siyo tiketi ya kuvunja sheria. Sheria ya kukataza uchafuzi wa sauti ipo. Mamlaka zinazohusika zinatakiwa kuitumia. Najuwa wewe pengine unaona kama itakuwa tishio kwa waislam na adhana zao. Adhana kutoka misikitini kwangu siyo issue kubkwa kwa sababu inafanywa kwa muda mfupi na haikeri kama maspika ya mahubiri kutoka makanisani yanayoungurumishwa karibu siku nzima. Au muziki wa bar kutwa kuchwa.
adhana dakika 2 zinakukera? kuna waislam wapo chini ya msikitini hawasikii adhana, ukiwauliza anakwambia sikusikia adhana kwa sabau nilichoka. Hapa tunakusudia Mziki
 
Umeileta hii mada kwa mtazamo wa kidini! Kama ungeileta mada kwa mtazamo wa kuchafua mazingira ungeeleweka!
Hata hivyo mamlaka husika zichukue hatua!
ningaliandika vipi? Makanisani taka zipo nyingi?
 
adhana dakika 2 zinakukera? kuna waislam wapo chini ya msikitini hawasikii adhana, ukiwauliza anakwambia sikusikia adhana kwa sabau nilichoka. Hapa tunakusudia Mziki
Nimeandika nini na umejibu nini? Rudia kusoma uelewe nilichoandika. Usiongozwe na jazba.
 
Ujinga Ujinga tu maelezo mengi yote eti una tetea Uislamu 🤣🤣 Dini zote ni mambo ya kufikirika tu sasa io adhana yenu nani aliwambia kua anataka kuamshwa uo mda
 
Mjinga nani sasa? anaebishana na mjinga yeye huwa mjinga zaidi - MANDELA SPEECH
Nenda kabishane Facebook sio humu JF....au rudi shule wewe MEMKWA usiyejua tofauti ya "Mada" na "Maada" 😆😆
 
Back
Top Bottom