Ibrahim Rahbi na Azam na uchambuzi wa mgogoro wa Israel na Hamas

Ibrahim Rahbi na Azam na uchambuzi wa mgogoro wa Israel na Hamas

naijua oslo acord kuliko wewe. ila sasa jibu swali, lini palishawahi kuwepo nchi ya palestina (sio palestinian authority), taja rais wake hata mmoja tu au hata mfalme wake even one. kama huwezi, kwenda zako huko.
Mkuu hicho ndicho kinachopiganiwa sasahivu kwasababu kuna madhalimu hawataki kutii sheria na mikataba ya kimataifa ndio maana tunasema hamas wana haki ya kupigania taifa lao na kukataa any form of occupation and oppression from israel
 
Mkuu hicho ndicho kinachopiganiwa sasahivu kwasababu kuna madhalimu hawataki kutii sheria na mikataba ya kimataifa ndio maana tunasema hamas wana haki ya kupigania taifa lao na kukataa any form of occupation and oppression from israel
taifa lao lipi we mjinga? lingi palishawahi kuwepo na taifa linaitwa palestina? rais wao alikuwa nani, mfalme wao alikuwa nani? taja hata mmoja tu.
 
taifa lao lipi we mjinga? lingi palishawahi kuwepo na taifa linaitwa palestina? rais wao alikuwa nani, mfalme wao alikuwa nani? taja hata mmoja tu.
Itakuwa huna akili kama hujui huu mgogoro unahusu nini na ubishi wako wa kijiweni
 
Huyo kama ndiyo kayanena hayo, na kuna ushahidi, chombo kinachompa airtime aeneze upuuzi wake, kichukuliwe hatua haraka.

Dunia nzima, kwa kauli moja, yakiwemo mataifa ya Kiarabu, yamelaani vitendo vya Houthi vya kushambulia meli za kibiashara, halafu huyo mwehu anasema Houthi wapo sahihi; ana akili huyo? Katika kulaani vitendo vya kigaidi vya Houthi, mataifa yote kwenye UN Security council, yametoa kauli ya kulaani; na hivyo kutoa ruhusa kwa mataifa yenye nguvu kuwadhibiti. Na shambulio la jana la US na UK dhidi ya Houthi, limeungwa mkono na mataifa mengi, ikiwemo Bahrain.
Kichukuliwe hatua na nani ? Wewe sii uchukue tu hizo hatua unangoja nini?
 
Yeye ni muislam, Azam channel ya muislam imemuweka awe anachambua masuala yote yanayoigusa Israel na Hamas, pamoja na wahurthi.

1. Anasapoti wahurthi Yemen, na anasema wanafanya cha maana kuzuia meli zisiende Israel na dunia iache unafiki, ishughulikie kwanza vita ya Gaza ili wahuthi waacha kushambilia meli (ambazo hata sio za Israel).

2. Anasema Bandari ya Eliat ambayo ipo Israel, ipo kwenye ardhi ya Palestina. Amesahau kwamba Umoja wa mataifa unaitambua Israel kama nchi na hauitambui palestina kama nchi. Kama UN wameitambua Israel kama nchi, mfanyakazi mmoja wa serikali ya Tanzania anakujaje leo kusema Israel sio nchi? Na kwamba ile bandari haipo ISrael ipo palestina?

3. Yeye ni mfanyakazi wa Mwalimu Nyerere Memorial Academy, chuo cha serikali, serikali haina dini, na hata kwenye migogoro yote hii serikali haijatamka lolote kwasababu wanajua nchini kuna wafuasi wengi wanaoipenda Israel na wengi wanaoipenda Palestina, huwezi kusimamia upande mmoja labda kama haupo serikalini.

Anapokataa uwepo wa Israel wakati bado anafanya kazi serikalini, anafanya hivyo kwa kuwakilisha chuo cha mwalimu nyerere au anafikiri nini? Chuo kimwangalie kwasababu suala la dini, Israel na palestina sio laini, linaweza kuharibu mshikamano wetu.

4. Ni mtanzania wa aina gani tena mfanyakazi wa serikali anaweza kuongea mbele ya chombo cha tv kwamba wahurthi Yemen wasilaumiwe badi Israel ndio ilaumiwe?

Kwahiyo eneo lile la bahari ya wote ambalo magaidi ya Yemen yanazuia nchi zingine zisipite sio ugaidi? Na yeye tuseme sio gaidi? hivi gaidi akija nyumbani kwa IBRAHIM RAHBI hawezi kumhifadhi na akasababisha matatizo nchini kwetu kama ana mlengo huo? yeye sio gaidi? hasapoti magaidi?
Hoja zako azina mashiko jeshi la Yemeni linahaki ya kuzuia meli zipite kwenye maji yake

Pia hiyo bandari ya isirael mwanzo ilikuwa upande wa palesitina wakaikalia kwa mabavu

Unapo sema heti ni muisilamu huo ni upumbavu kwani muisilamu apaswi kusema kweli?

Nchi ya afirika kusini imeishitaka Israel kwenye mahakama ya kimataifa kosa mauji ya kimbari ndio kusema hao wanasheria ni waisilamu?
 
unajua kuna watu wanaishi wakiamini vile wanavyohisi wao kila mtu yupo hivyo, kale kagaidi kanaamini watanzania wote hawaitambui na hawatakiwi kuitambua israel kama nchi, bandari za Israel anasema ni bandari za Palestina ambazo Israel inazikalia kwa mabavu, lini wapalestina wamejenga, atasema miaka mingi. anataka watu wote tuichukie israel na azam wamemuweka hapo makusudi kwa ajili ya kusambaza hiyo sumu.
Kigezo sio kujenga hizo bandari zimejengwa kwenye aridhi ya nani?
 
Yule ni mchambuzi na anachambua kwa mtazamo wala sio msimamo wa media house ya Azam, unasumbuliwa na udini bro, na wewe chambua tuone maoni yako.
Stachumbua nini mjinga tu huyo kwanza ukiona mtu kila kitu anakihusisha na udini mtu huyo akili zake sio sawa
 
Inategemea una upeo gani lakini swala israel kuikalia palestina kwa mabavu ni uongo?
ISrael hadi leo anaendelea kuchukua maeneo ya palestina na kukiuka mikataba yote ya mipaka iliyowekwa hilo nani asiyejua
Usiwe kipofu kwa ushabiki wa dini, ni watu wachache wanaoweza kusema ukwrli kama huyo mtangazaji
Ndiyo tatizo la kukaririshwa! Sijui Mungu gani anakuwa dalali wa kiwanja/ ardhi! As if leo akija mtu toka Misri na dini yake inaitwa Kemet Orthodox akaja kumwambia Mungu wake amemuambia eneo alilopo ni mali yaie amepewa yeye na uzao wake wote! Yeye atakuwa tayar kumpisha.
 
Kwa mtu anayejielewa na msomi hawezi kuongea kwenye media kubwa hivyo huku akiunga mkono makundi kama houth na Hezbollah ambayo ni mkono WA Iran WA kueneza itikadi ya kishia.

Hajiulizi kwa Nini wasaud wameoigana nao, it's the war of idealogy the Kislam na watu wanashabikia bila kujua.

Huyu pengine amenyezwa na huo upande WA Iran na Wala sio issue ya uislam Bali itikadi ya mashia.
Houth wanahaki ya kuzuia meli za isirael zisipite kwenye maji yao daudi Saudi hawa ndio vibaraka wa israel
 
Jamaa fulani azam wamemuweka kila siku asubuhi awe anachambua masuala ya kisiasa, anaamini anajua sana kumbe hamna kitu udini tu umemjaa. hajawahi kuongea chochote ila vile vinavyopendelea dini yake.
Kwani muisilamu hapaswi kusema kweli?
 
Yeye ni muislam, Azam channel ya muislam imemuweka awe anachambua masuala yote yanayoigusa Israel na Hamas, pamoja na wahurthi.
Mfalme, kwako wewe unaumia unapoona Muislam anachambua masuala ya Mashariki ya kati? Mbona unaonesha hisia hasi kwa Watanzania wenzio kisa dini? Unataka kumaanisha kwamba vyombo vyote vya habari vinavyomilikiwa na wakristo ni marufuku mkristo kuchambua masuala na vile vinavyomilikiwa na waislam iwe marufuku muislam kuchambua? Hapa unachochea ubaguzi ambao hauna afya yoyote kwa taifa.
1. Anasapoti wahurthi Yemen, na anasema wanafanya cha maana kuzuia meli zisiende Israel na dunia iache unafiki, ishughulikie kwanza vita ya Gaza ili wahuthi waacha kushambilia meli (ambazo hata sio za Israel).

2. Anasema Bandari ya Eliat ambayo ipo Israel, ipo kwenye ardhi ya Palestina. Amesahau kwamba Umoja wa mataifa unaitambua Israel kama nchi na hauitambui palestina kama nchi.
Kwanini UN hawaitambui Palestine kama nchi? Na umoja wa mataifa ni nani? Kwa maoni yako na utashi wako unaona Palestine haistahili kuwa nchi bali inastahili kutawaliwa?
Kama UN wameitambua Israel kama nchi, mfanyakazi mmoja wa serikali ya Tanzania anakujaje leo kusema Israel sio nchi? Na kwamba ile bandari haipo ISrael ipo palestina?
Bila shaka wewe ni mfuatikiaji mzuri wa siasa za kimataifa, Katibu Mkuu wa UN alisema nini juu ya mzozo wa Isreal na Palestine? Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa ndio mfanyakazi namba moja wa serikali alikuwa na msimamo upi juu ya Palestine?
3. Yeye ni mfanyakazi wa Mwalimu Nyerere Memorial Academy, chuo cha serikali, serikali haina dini, na hata kwenye migogoro yote hii serikali haijatamka lolote kwasababu wanajua nchini kuna wafuasi wengi wanaoipenda Israel na wengi wanaoipenda Palestina, huwezi kusimamia upande mmoja labda kama haupo serikalini.
Serikali kutotamka lolote kwa wakati huu sio hoja, Mwalimu Nyerere alikuwa ni Rais wa nchi na ni Mkristo lakini haikumzuia kuweka msimamo wake dhidi ya Isreal ambapo aliona kinachofanywa na Waisrael huko Palestine sio haki. Na yeye Mwalimu alipambana na kuwatetea waliodhulumiwa ikiwemo Afrika ya Kusini dhidi ya Makaburu.
Anapokataa uwepo wa Israel wakati bado anafanya kazi serikalini, anafanya hivyo kwa kuwakilisha chuo cha mwalimu nyerere au anafikiri nini? Chuo kimwangalie kwasababu suala la dini, Israel na palestina sio laini, linaweza kuharibu mshikamano wetu.
Anakataa uwepo wa Isreal mahala gani? Vipi kuhusu mipaka ya mwaka 1967 inayotambuliwa na Umoja wa mataifa ambayo Isreal kila kukicha inaendeleza makazi ya Wayahudi na kunyang'anya ardhi ya Wapalestine, unalionaje hili Mfalme?

Afrika Kusini wala sio nchi ya kiislam na haiongozwi na muislam lakini kutokana na kinachofanywa na Isreal huko Gaza nchi imeamua kusimama dhidi ya Isreal, hapo ndugu Mfalme una maoni gani pia?

Unadhani Ramaphosa anasimama dhidi ya Isreal anatetea uislam? Ana udini? Jibu ni hapana bali anatetea UTU, UBINADAMU na kupinga dhulma, unyanyasaji, ukatili ambao kimsingi huwezi kutofautisha na UGAIDI ambacho ndicho kinachofanywa na Isreal huko Gaza.

Au Mfalme, ukiondoa dini yako na ukaamua kubaki na utu wako, kwa dhati yako kabisa unaona wale watoto, wanawake, wazee maelfu kwa maelfu wanaouwa kila siku na Isreal ni sawa?

Na unadhani nini kifanyike ili utulivu na amani ya kudumu ipatikane huko Isreal na Palestine?

Au Mfalme utaungana na wale mawaziri wawili wa Isreal waliotangaza waziwazi kwamba Wapastina wote waangamizwe na mwenzie akasema Wapalestina wote wafukuzwe na pajengwe nyumba za waisreal?
4. Ni mtanzania wa aina gani tena mfanyakazi wa serikali anaweza kuongea mbele ya chombo cha tv kwamba wahurthi Yemen wasilaumiwe badi Israel ndio ilaumiwe?
Huyu hatakuwa mfanyakazi wa kwanza kueleza sababu au kiini cha machafuko huko Isreal na Palestine. Katibu Mkuu wa UN mbele ya vyombo vya habari vya kimataifa alibainisha wazi kuwa vitendo vinavyofanywa na Isreal kwa Wapalestine ndio vinachochea matokeo hasi. Lau Isreal ingekuwa inawatreat kiutu Wapalestina, kutambua uhuru wao, utaifa wao na kila mmoja akaheshimu mipaka ya mwenzie yamkini hata jina la Hamas usingelisikia Mfalme.
Kwahiyo eneo lile la bahari ya wote ambalo magaidi ya Yemen yanazuia nchi zingine zisipite sio ugaidi? Na yeye tuseme sio gaidi? hivi gaidi akija nyumbani kwa IBRAHIM RAHBI hawezi kumhifadhi na akasababisha matatizo nchini kwetu kama ana mlengo huo? yeye sio gaidi? hasapoti magaidi?
Ndugu Mfalme unapaswa kuwa fair kwa mambo ya huko. Marekani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani wanatoa fedha na mabomu kuyapeleka Isreal ili yatupwe Gaza kuteketeza na kuchanachana mpaka miili ya watoto na wanawake kwa kisingizio cha kujilinda, huu wewe huoni kuwa ni ugaidi wa kutisha zaidi kuliko hata ugaidi wa Wahuthi?

Marekani inapotoa silaha kwa Isreal iangamize hata wasio na hatia huko Gaza na kweli imeangamiza vya kutosha huoni kama hili pia linapaswa kukemewa kama ambavyo wahuthi wanapozuia meli za Isreal na wafadhili wake kushinikiza waache kuendelea kuangamiza maisha ya wasio na hatia huko Gaza.

Mwisho; kama huyo Mchambuzi anasapoti kusimamisha mauaji ya Isreal huko Palestine na kwa sapoti hii wewe unamnasibisha na gaidi basi kufanya hivyo unaleta tafsiri kuwa hata Mwalimu Nyerere, Nelson Mandela na sasa Ramaphosa wanatetea ugaidi duniani.

Usisahau hata Mandela wakati anapigania uhuru dhidi ya ubanguzi na ukatili wa Makaburu naye aliitwa Gaidi na akafungwa jela kwa ugaidi wake. Unaamini Mandela kweli alikuwa Gaidi?

Mfalme, tumia Ufalme wako kusimamia haki, uadilifu, usawa, utu na uhuru. Ufalme huohuo utumie kupinga dhulma, ubaguzi, unyanyasaji, unyonyaji kwa wananchi wako bila kujali dini zao, makabila yao, jinsia zao.
 
Hawa watu wanasema hadi Nduli Iddi Amin dada alionewa baada ya kuvamia, kuua watanzania na kutangaza kui annex Kagera kisa dini yao moja.!! Wahouth walitaka wazungu wawatazame tu wanavyovamia meli zao.!!!!
 
Kama huyo Ni lecturer, wanafunzi wasipofahamu misimamo yake ya kiislam watafeli vibaya, usalama wao Ni kusifia Hamas, Boko Haram, isis n. k Kama vikundi vya ukombozi!!!!
 
kama yupo mchambuzi anaesema ukweli azam kuanzia kesho naanza kumfatilia asanteni azam na mbarikiwe sana na muendelee na uislamu wenu uwe na nguvu
 
Huyo Ibrahim Rahbu inawezekana ni miongoni mwa magaidi yaliyopanga na kuendesha ule ugaidi uliokuwa unafanyika kule Mkuranga na Kibiti.

Kule Kibiti na Mkuranga waliokuwepo watekelezaji lakini waandaji na wapanga mipango walikuwa Dar. Huyu yawezekana ni miongoni.

Ugaidi wa Houthi, hakuna hata nchi moja, Duniani kote inayounga mkono vitendo vyao. Na kwenye hilo Dunia nzima imeungana. Sasa huyu anayeunga mkono, hawezi kuwa binadamu wa kawaida.

Na hao Azam wameshindwa kuwapata watu wema na wenye weledi kuwa wachimbuzi hadi kuwatafuta watu wenye akili ndogo wenye elements za ugaidi kuwa wachambuzi wa masuala ya siasa.

Mataifa makubwa yamepata mandate ya UN Security council kuwashughulika Houths, wamchukue na huyu.

hata mama yako alikuwa kwenye mpango huo wa ugaidi
 
IMG_1504.jpg
 
Back
Top Bottom