Idadi ya watoto ndani ya ndoa: Nani huamua?

Idadi ya watoto ndani ya ndoa: Nani huamua?

Jugado

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2021
Posts
1,446
Reaction score
3,184
Habari.

Miaka ya wazazi wetu mwanamke akiolewa ni kuzaa mpaka kizazi kiishe. Huku watoto wakipishana miaka miwili.

Ndiyo maana si ajabu kuona familia zenye watoto nane, tisa mpaka kumi. Lakini Karne hii mambo ni tofauti. Wanawake hawataki kuzaa watoto wengi. Utasikia wawili wanatosha. Akienda sana watatu au wanne.

Swali langu kwa wana JF nani wakuamua idadi ya watoto? Ikiwa hakuna makubaliano? Mama hataki watoto wengi na baba anataka! Naelewa kile wanachokipitia wamama wakati wa kubeba mimba, kunyonyesha na hata malezi. Lakini ndivyo ilivyo. Naelewa hivyo kwani mimi na mke wangu tuna watoto watatu.

Kilichonifanya kuandika huu uzi ni mke wangu kupata mimba ambayo hatukuitarajia/hatukupanga. Hivyo kuleta gumzo japo hatimaye Mungu mkubwa kakubali kuzaa kwa sharti lazima afunge kizazi baada ya kujifungua! Kwa upande wangu naona nahitaji watoto zaidi. Sipo tayari wife afunge kizazi. Hii imekaaje? Je, ni kweli watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu?

Au ni maamuzi ya wanandoa wote au mmoja wao. Nawasilisha kwa michango ya jumla kuhusu mada na specifically kuhusu mimi na wife tutatoboaje?
 
Mfuko ndio uamue unamudu wangapi!

Usikubali kuamuliwa na mihemko ya kichwani kwamba watoto ndio utajiri wako kesho, utateseka na utawatesa watoti.

Kama unamudu mmoja basi huyo anatosha mpaka uwe na uwezo wa kuhudumia mwingine, hatushindanishi nguvu za kiume aisee

Na hii kauli ya "Mungu akileta mtoto analeta na sahani yake" kua nayo makini, ndio maana huyohuyo alisema "watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa"
 
Asante. Miaka pia inaenda kasi. Mimi pia ni muumini wa kila mtoto huja na sahani yake. Nilipompata mtoto wa pili maisha yetu yalibadilika kwa kasi sana... Naamini hata sasa mambo mengi yatakuja upande wetu.
 
Maamuzi ni ya wote lakini mwanaume nakupa kipaumbele chakuamua. Kama mkeo ameamua akizaa anafunga kizazi usimkatalie mwache azae akifunga kizazi oa mwingine akiuliza mwambie unahitaji watoto zaidi. Kama ni wakristo na mmefunga ndoa kanisani basi jina la bwana lihimidiwe
 
Ushauri wangu watoto wawili tu wanatosha, kukua kwa uchumi wa watanzania hakuendani kabisa na ongezeko letu, Tanzania 🇹🇿 tuna eneo lenye ukubwa zaidi ya 900k+ na idadi ya watu 60M +,Botswana wana eneo 500k+na idadi ya watu 3M,hii ni hatari kubwa kwa nchi yetu, kuzaa au kutokuzaa ni uamuzi wa wote ILA mwenye FINAL SAY NI MWANAMKE, maana ndiye anayebeba mimba sio Mwanaume.
 
Habari. Miaka ya wazazi wetu mwanamke akiolewa ni kuzaa mpaka kizazi kiishe. Huku watoto wakipishana miaka miwili. Ndiyo maana si ajabu kuona familia zenye watoto nane, tisa mpaka kumi. Lakini Karne hii mambo ni tofauti. Wanawake hawataki kuzaa watoto wengi. Utasikia wawili wanatosha. Akienda sana watatu au wanne. Swali langu kwa wana JF nani wakuamua idadi ya watoto? Ikiwa hakuna makubaliano? Mama hataki watoto wengi na baba anataka! Naelewa kile wanachokipitia wamama wakati wa kubeba mimba, kunyonyesha na hata malezi. Lakini ndivyo ilivyo... Naelewa hivyo kwani mimi na mke wangu tuna watoto watatu.
Kilichonifanya kuandika huu uzi ni mke wangu kupata mimba ambayo hatukuitarajia/hatukupanga. Hivyo kuleta gumzo japo hatimaye Mungu mkubwa kakubali kuzaa kwa sharti lazima afunge kizazi baada ya kujifungua! Kwa upande wangu naona nahitaji watoto zaidi. Sipo tayari wife afunge kizazi. Hii imekaaje? Je ni kweli watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu? Au ni maamuzi ya wanandoa wote au mmoja wao...
Nawasilisha kwa michango ya jumla kuhusu mada na specifically kuhusu mimi na wife tutatoboaje?
Mkuu, huoni jinsi gani vitu vimepanda bei?
Unawaza kuzaa zaa tu, utawalisha nini hao watoto? Mpumzishe mkeo bhana na yeye aifaidi dunia! Huyu mtoto awe wa mwisho mkuu!
 
Watoto kuwa nao uwe na mipango mizuri tu kiuchumi. Vinginevyo ni hawa bodaboda na wauza nguchiro tunawaona humu njiani.
Binafsi nnao wa5.
Kati yao kiukweli ni wa2 tu nilizalisha kwa kudhamiria pamoja na mama zao.
Wa3 waliobaki ni mimba zisizotarajiwa,kutegesheana,na kubambikiana.
Watoto wapo ni wakwangu haikwepeki.mama zao vimekua vizee haswa watoto ndo hao wanashamiri na kuonyesha baba yao nani.
Kizazi chetu tumezaliwa wa4 full stop.
Watajua wazazi walichofanya, ila bibi ukoo upande wa mama alizaa 10,
Bibi ukoo upande wa baba aligonga 6.
Hao wote walikua mama wa nyumbani.
Na walikua ngangari mpk wanakufa.
Kwasasa wanawake tunaoa wanataka wachakarike watengeneze vyao utamzalisha vipi watoto 10?
Hiyo sio mashine,watoto 10+ halafu ukute lijitu anazaa nalo km ww mleta mada unamuona mwanamke ni kumtumia tu.
Unataka watoto kagonge nje huko km we mwamba.
Hao wa3 wanatosha sana wape huduma na mahitaji ya muhimu bila kupungua na mpe afya ya kutosha mzazi mwenzio arudishe nuru yake.
Nna wa5 na kila mmoja na mama yake.
So i talk from experience
 
Ushauri wangu watoto wawili tu wanatosha, kukua kwa uchumi wa watanzania hakuendani kabisa na ongezeko letu, Tanzania [emoji1241] tuna eneo lenye ukubwa zaidi ya 900k+ na idadi ya watu 60M +,Botswana wana eneo 500k+na idadi ya watu 3M,hii ni hatari kubwa kwa nchi yetu, kuzaa au kutokuzaa ni uamuzi wa wote ILA mwenye FINAL SAY NI MWANAMKE, maana ndiye anayebeba mimba sio Mwanaume.
Botswana [emoji1052] eneo kubwa ni inhabitable, kumbuka pale kuna Kalahari desert ndio maana wana eneo kubwa na population ndogo.

Sisi sehemu kariba zote no fertile sana.
 
Botswana [emoji1052] eneo kubwa ni inhabitable, kumbuka pale kuna Kalahari desert ndio maana wana eneo kubwa na population ndogo.

Sisi sehemu kariba zote no fertile sana.
Mkuu with all my respect kwako, ni vema mambo mengine ukajiridhia kwa kuthibitisha, pls tembelea Botswana 🇧🇼 na uje na mrejesho hapa, desert ni sehemu ndogo tu ya nchi, wenzetu wamefanikiwa mno to keep on check ongozeko la watu ili Lilian na la uchumi, kwa sasa 1lt of diesel ni 17P,sisi ni 3,500tsh!
 
Mkuu with all my respect kwako, ni vema mambo mengine ukajiridhia kwa kuthibitisha, pls tembelea Botswana 🇧🇼 na uje na mrejesho hapa, desert ni sehemu ndogo tu ya nchi, wenzetu wamefanikiwa mno to keep on check ongozeko la watu ili Lilian na la uchumi, kwa sasa 1lt of diesel ni 17P,sisi ni 3,500tsh!
Mkuu,
1P ni sawa na 193Tsh, hivyo 17P haina tofauti sana na sisi, ni almost 3,300Tsh wakati hapa Dar tunanunua 2,996Tsh.

Sijafika huko Botswana mkuu, ila nasoma tu kuwa most of the land is inhabitable. Kama only 0.65% of the land ndio inalimwa, unategemea population growth ya aina gani mkuu? Najua hiyo nchi ni tajiri kwa viwango vya Africa, lakini kuruhusu ongezeko kubwa la kuzaana kwao ni ngumu.

Kama umeishi huko nipe practical experience yako.

 
watu mnazaa....duuh...

una watoto watatu ila bado hawakutoshi.... mtoto mmoja anatosha wa pili labda ukipitiwa.

binafsi nina mmoja na hapati kaka wala dada.
Uko serious? Hebu ongeza mwingine apate ndugu/rafiki wa kukua nae hata kesho mkiondoka ajue anaendugu yake wa damu itamtolea upweke.
Watoto wa ma uncle na aunties wapo lakini kuna raha ya kua na kaka/dada wa baba/mama mmoja.
 
Habari. Miaka ya wazazi wetu mwanamke akiolewa ni kuzaa mpaka kizazi kiishe. Huku watoto wakipishana miaka miwili. Ndiyo maana si ajabu kuona familia zenye watoto nane, tisa mpaka kumi. Lakini Karne hii mambo ni tofauti. Wanawake hawataki kuzaa watoto wengi. Utasikia wawili wanatosha. Akienda sana watatu au wanne. Swali langu kwa wana JF nani wakuamua idadi ya watoto? Ikiwa hakuna makubaliano? Mama hataki watoto wengi na baba anataka! Naelewa kile wanachokipitia wamama wakati wa kubeba mimba, kunyonyesha na hata malezi. Lakini ndivyo ilivyo... Naelewa hivyo kwani mimi na mke wangu tuna watoto watatu.
Kilichonifanya kuandika huu uzi ni mke wangu kupata mimba ambayo hatukuitarajia/hatukupanga. Hivyo kuleta gumzo japo hatimaye Mungu mkubwa kakubali kuzaa kwa sharti lazima afunge kizazi baada ya kujifungua! Kwa upande wangu naona nahitaji watoto zaidi. Sipo tayari wife afunge kizazi. Hii imekaaje? Je ni kweli watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu? Au ni maamuzi ya wanandoa wote au mmoja wao...
Nawasilisha kwa michango ya jumla kuhusu mada na specifically kuhusu mimi na wife tutatoboaje?
Mnapaswa kushauriana wote na kuamua kwa pamoja . Ila jambo la msingi ni kuangalia afya ya mama kama inaruhusu idadi ya watoto mnaopanga kuzaa ila pia kuangalia uchumi wenu kama utaweza kuhudumia watoto mnaopanga kuwazaa comfortably...hata ikitokea mmoja wenu ametangulia (Mungu atupe maisha marefu tulee watoto wetu) anaebaki aweze kuhudumia watoto na sio kuwagawa kwa ndugu.
 
Back
Top Bottom