Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hongera sana Ruto na pole sana Raila. Kugombea x5 unaangukia pua, imetosha sasa!Tume ya Uchaguzi Huru na Mipaka (IEBC) imemtangaza aliyekuwa Naibu Rais, William Ruto (55) kuwa Rais Mteule wa Awamu ya Tano kwa tiketi ya Chama cha UDA kufuatia Uchaguzi Mkuu uliofanyika Agosti 9, 2022
Tume imesema Ruto amepata Kura 7,176,141 sawa na asilimia 50.49 huku akifuatiwa na Raila Odinga kutoka Chama cha Azimio la Umoja
Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati ametangaza matokeo hayo baada ya siku sita za kuyasubiri tangu siku iliyopigwa kura, Agosti 9, 2022.
Ruto amewashinda wagombea wenzake ambao ni Raila Odinga, mgombea wa Chama cha Agano, David Waihiga ambaye Agosti 14 alitangaza kushindwa, pamoja na Profesa George Wajackoyah wa Chama cha Roots.
William Ruto (UDA)
50.49%
7,176,121 Votes
Raila Odinga (AZIMIO)
48.85%
6,942,930 Votes
George Wajackoyah (RPK)
0.44%
61,969 Votes
David Waihiga (AGANO)
0.23%
31,987 Votes
Nawe umeanza vitendawili kama Mzee wa Kitendawili?Mzee Lee Kinyanjui alisema katika uwindaji pori ukiongozana na mbwa wako kuwa makini. Kwani porini utakuwa pekee yako pamoja na mbwa, mbweha na mbwa mwitu. Sasa hawa wanyama watatu binamu wakiamua kukugeuka wakati upo nao pekee yako utapona ?
Sidhani ,siyo kweli. Mpasuko wa IEBC dhahiri ngoma bado mbichi.Yule Mzee kigegeu, alishindwa kuwasoma hao watoto wa mjini, wakamjaza akajaa mazima kama mjamzito
Ni kawaida ya yule mzee kufanya hivyo, hata hivyo nadhani kuna kundi lilimchukia kwa kufanya u turnSidhani ,siyo kweli. Mpasuko wa IEBC dhahiri ngoma bado mbichi.
Wazee wa Katiba Mpya wanasemaje maana nako huko kwa 'wenzetu' Nako kuna madai ya wizi wa kura
Kinyanganyiro kinahamia supreme court of Kenya. Karua twit-it is not over until it is over. Mahakama inayo siku 14 kusikiza malalamiko na kutoa maamuzi. Iwapo mahakama itaafiki uchaguzi ulikuwa na dosari,uchaguzia wa
Kumpeleka Ruto supreme court ni sawa na kumsukumia chura majini! Mabepari wote wa Kenya wako nyuma ya Ruto!marudio muda usiozidi siku 14
Apumzike Ukweli Hastahiri Tena Kupanda Jukwaani, Vocal Yenyewe ShidaOdinga apumzike kwa amani sasa, imetosha.
Punguza makasiriko.Dikteta bado anakubutua hata baada ya kufa!
Nani ajuaye? Huenda akienda mahakamani atapewa Urais.Daah raila ndo basi tena
Hoja pekee kubwa waliyo nayo (kama ni hoja kweli), ni kwamba eti hawakuwa-previewed matokeo kabla ya kutangazwa. Kwamba walipaswa kwanza kuyajua matokeo ndipo yatangazwe. Nonsense!Sidhani ,siyo kweli. Mpasuko wa IEBC dhahiri ngoma bado mbichi.
ila uchaguzi ilikuwa wa wazi japo raila sidhani kama atakubali hii ngoma iishe hivihiviNani ajuaye? Huenda akienda mahakamani atapewa Urais.
Mbona Raila alisema yuko kwenye serikali, deep state, na kwa wazoefu na manguli wa siasa? Nini kimetokea tena huko? Au ameamua kumwachia mdogo wake?Wakuu nakuja kuwapa habari kamili.
Kama taarifa inavyoeleza pichani, mkongwe na mzoefu wa siasa za Kenya mh Raila Odinga ameangukia tena pua kwa mara nyingine...
Mwaka 2017 alisema kulikuwepo na VIFARANGA VYA KOMPYUTA kwenye matokeo ya uchaguzi. Ngoja tuone safari hii sijui vitakuwa vifaranga vya ndege yupi?ila uchaguzi ilikuwa wa wazi japo raila sidhani kama atakubali hii ngoma iishe hivihivi