If it is government funds, why call it Samia scholarships?

If it is government funds, why call it Samia scholarships?

Anatumia muda na kipindi chake kwa haraka sana kuweka legacy yake hata mkimtupa kwenye next term tayari ameacha sijui mtaika nini huko mbele!.

Wanajua kucheza na akili zetu hawa!.
 
Maswali ya kijinga. Heshima ya mtu usiichezee kisiasa kwa vile tu CUF na CHADEMA bado hamjapara Rais. Kwani Ziwa Victoria alitoa ndoo ngapi za maji kulijaza? Duke of York alijenga tofali ngapi New York? Ni heshima ya mtu, akisema NO itakuwa NO kwa sababu tulimpa madaraka hayo tulipomchangua, akamshinda tundulissu 87%/13%. Kama ingekuwa the other way round tungekuwa na Makanikia Bridge
Wewe ndo kiazi kabisa.kama uwezo mdogo sio lazima uchangie ndugu.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Huu ndio ujinga uliokubuhu! pesa za umma zinapewa jina la mtu! Hivi tumekosa akili kiasi hicho!
 
Amepata wapi hela? Alfred Nobel kwa mfano, anatoa Nobel prize kwa pesa zake ambazo zinatokana na ugunduzi wake wa dynamite... pesa tele maana patent yake bado inatumika dunia nzima. sasa yeye ana nini pa kutoa hela? kutumia
Jamaa mjinga.
 
Kuna mambo mengi sana ya kurekebisha kwenye nchi yetu tatizo ni kila ukiangalia huoni mtu sahihi wa kuyafanya.

Hizi pesa zingewekwa kwenye mfuko wa bodi ya mikopo, watoto wengi sana wa masikini wangenufaika nazo.

Tunaendelea kubuni vitu nje ya mfumo wa kisheria wakati vile vilivyo kwenye mfumo wa kisheria tumeshindwa kuvitekeleza kwa japo 70%.

Kwa vigezo vya hiyo inayoitwa scholarship, wenye sifa karibu 98% ni watoto ambao wazazi wao wanaweza kuwasomesha bila mikopo. Hapa naomba isitafsiriwe kuwa watoto wa wenye nacho hawapaswi kutazamwa lakini tuangalie hali ya wanaopitia watoto wanaosoma shule ambazo haya sehemu ya kukaa ni ya kugombania. Je wanaweza kushindana na wale wanaofika shuleni na kukuta kila kitu huko?

Kila siku ukikaa na kujiuliza hii nchi ina matatizo gani, sidhani kama utaweza kupata afya.
"Kila siku ukikaa na kujiuliza hii nchi ina matatizo gani, sidhani kama utaweza kupata afya."
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Demokrasia ni kichaka cha ufujaji wa pesa za wananchi kwa ajili ya kutafuta sifa binafsi na kujitangaza kisiasa kwa watu wa tabaka tofauti.

Chama pekee ambacho kama kitaondoa undumila kuwili wake kwa kujipendekeza kwa serikali kinachoweza kusemea machungu ya wananchi ni CHADEMA na DP vingine vyote ni vikaragosi vya chama tawala.

Haiwezekani pesa zinapatikana kwa jasho la wananchi halafu zinaitwa pesa za SAMIA ni aibu na dharau kubwa. Kama ni zake binafsi kazitoa wapi kufadhili elimu ya juu kwenda nchi za nje ambako ni aghari sana

Kuna pahala hapako sawa

Chadema ya Dr. Slaa na DP ya Mtikila ndio walikuwa kiboko cha viongozi wa CCM
 
Hili swala nimekuwa nikijiuliza peke angu na nikokza majibu kbsa
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?

Ukijibiwa usiache kunijuza tafadhali saaaana.
 
Nafikiri ilitakiwa iitwe Tanzania scholarship kwa sababu nahisi ni Kodi za wananchi Hizo!! Ukitaja jina la mtu maana yake yeye ndiye katoa hela mfukoni mwake!!
Hii ni sawa kabisa.
 
Amepata wapi hela? Alfred Nobel kwa mfano, anatoa Nobel prize kwa pesa zake ambazo zinatokana na ugunduzi wake wa dynamite... pesa tele maana patent yake bado inatumika dunia nzima. sasa yeye ana nini pa kutoa hela? kutumia
Itakuwa mafao yake ya Umakamu,kaamua kuwasomesha watoto wenyewe ufaulu mzuri.
 
Royal Tour tuliambiwa wataweka wazi nani alichangia ila kimya mpaka sasa.

Na hili nalo usitegemee kujua source of funds.

Awamu hii hakuna uwazi katika lolote kama wanavyotaka tuamini.
Mimi shida yangu hasa, malengo ya mfuko huu ni nini? Serikali haijaweza kutoa mikopo kwa maelfu ya watoto wa maskini wanaohitaji, leo wanaelekea kwa watoto wa matajari waliofanya vizuri kwakuwa baba na mama zao walikuwa na uwezo wa kiwatengenezea mazingira. Can you imagine wazazi wengi walipoteza rasilimali zao kwa ajili ya mtoto kufika tu sekondari. Chuo ndio usiseme. Hii nchi ni ya ajabu sana. Hizi fedha zilipaswa kuelekezwa kwa bodi ya mikopo. Wakope huko, wajekurejesha baadae
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Hizo ni pesa za serikali,tungekuwa tunafsta utawala wa sheria,ilibidi ziende kwenye bodi ya mikopo,lakini kwa vile huyu mama umaarufu wake umekwisha kabisa,sasa hv mawaziri machawa wanatsfuta mbinu za bei rahisi Ili kumpa umaarufu,utasikia pochi la mama,shangazi wa east Afrika,sasa hv ni hii schorahship .
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Nakubaliana kabisa na hoja yako. Hata kama wazo alilitoa yeye, bado hatupaswi kusema Samia scholarship kwa kuwa ni hela ya Serikali. Kufanya kazi vizuri ndiko anachopaswa kufanya akiwa katika madaraka hayo ya urais. La sivyo avurumishwe kwa kushindwa kutimiza wajibu aliopewa. Ni tofauti na scholarship ya Mwalimu Nyerere Foundation kwa kuwa hela hizo siyo za serikali. Watu wanaelemewa na mizigo ya tozo. Mwigulu anasema mapato ya hizo tozo tunayaelekeza kwenye elimu, afya na kadhalika. Hapo hapo tunasema Samia scholarship! Huku ni kuchezea akili za Watanzania.
 
Back
Top Bottom