Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hebu tofautisha Fedha na kitu? Kitu lazima kipewe Jina ndio maana madaraja, airport yanapewa majina...ila fedha kama fedha iliyo katika mfumo wa karatasi huwezi ipa Jina lako labda uwe wewe ndio ume izalisha.Daraja la Kijazi ama Mfugale ni fedha za Umma why yanaitwa hivyo?
Airport je?
Hostel ya JPM je?
Mkicomment narudi
Unahangaika bure,umewahi sikia kitu inaitwa Obamacare? Pesa zilikuwa za Obama? Muachage ujinga basi..Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Hakuna swali la msingi,umewahi sikia Mabilioni ya JK? Umewahi Sikia ObamaCare?Umeuliza swali la msingi sana!
Ongezea na Stand ya MagufuliMkuu ongezea na uwanja wa Benjamin Mkapa.
Umeonyesha ujinga wako hadharani! Huna unachojua!Daraja la Kijazi ama Mfugale ni fedha za Umma why yanaitwa hivyo?
Airport je?
Hostel ya JPM je?
Mkicomment narudi
Labda kama ana NGO yake lkn sijui mtu kama rais anaruhusiwa kufanya vile akiwa madarakani?wajibu wa sheria watusaidieSamia ndio katoa ufadhili.
Wengine tuliishaliona kitambo kuwa sasa wanaanza kuwagawa watoto wa maskini na wa matajiri halafu mmoja kaandika humu jf kuwa hela hizo zinaenda kuwanufaisha watoto wa maskini.nchi hii ngumu sana na kizazi kilichopo sasa ni cha ajabu sana.Kuna mambo mengi sana ya kurekebisha kwenye nchi yetu tatizo ni kila ukiangalia huoni mtu sahihi wa kuyafanya.
Hizi pesa zingewekwa kwenye mfuko wa bodi ya mikopo, watoto wengi sana wa masikini wangenufaika nazo.
Tunaendelea kubuni vitu nje ya mfumo wa kisheria wakati vile vilivyo kwenye mfumo wa kisheria tumeshindwa kuvitekeleza kwa japo 70%.
Kwa vigezo vya hiyo inayoitwa scholarship, wenye sifa karibu 98% ni watoto ambao wazazi wao wanaweza kuwasomesha bila mikopo. Hapa naomba isitafsiriwe kuwa watoto wa wenye nacho hawapaswi kutazamwa lakini tuangalie hali ya wanaopitia watoto wanaosoma shule ambazo haya sehemu ya kukaa ni ya kugombania. Je wanaweza kushindana na wale wanaofika shuleni na kukuta kila kitu huko?
Kila siku ukikaa na kujiuliza hii nchi ina matatizo gani, sidhani kama utaweza kupata afya.
Ni kweli government funds, lakini aliye elekeza hizo funds ziende kwa ajili ya scholarship ni Madamme Samia , angetaka kuzielekeza kwenye matumizi mengine kusingekuwa na hiyo scholarship.Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Wangeziongezea tu Loan Board.Mbona tayari Mwigulu alieleza kwamba ni kutokana na tozo? Mtanzania abebeshwe tozo; hongera zielekezwe kwa Samia.
Kama ni Government funds sio sahihi kutumia jina lake while ni wananchi wanachangia 100% kwa pesa zao.Ni kweli government funds, lakini aliye elekeza hizo funds ziende kwa ajili ya scholarship ni Madamme Samia , angetaka kuzielekeza kwenye matumizi mengine kusingekuwa na hiyo scholarship.
Ndio maana ukipewa mkopo na benki husemi nimepewa mkopo na depositors wa benki , kwa sababu benki kama benki hawana pesa zao bali unasema nimepewa mkopo na benki.
ExactlyHuyo mama alishapoteza mwelekeo kitambo. Aende akalee wajukuu.
Ili aweze kugawa anaowataka yeye kwa upendeleo.Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Hao ni wafadhili, au ndio wanufaika wa mali za waTanzania?Pesa za wafadhili kupitia jina lake...
Hakuna taasisi inayoshughulikia mambo hayo, bali inabidi yeye ndiye awe mhusika?Amepotezaje mwelekeo wakati anatoa scholarship? Au mwenzetu hufahamu maana ya scholarship?
Nchi ambayo CHAWA anaalikwa bungeni kama mgeni wa heshima na watunga sheria wanamshangilia kama shujaaKila siku ukikaa na kujiuliza hii nchi ina matatizo gani, sidhani kama utaweza kupata afya.