If it is government funds, why call it Samia scholarships?

If it is government funds, why call it Samia scholarships?

Unabakije kuwa kiongozi au mzazi/mlezi kama unakuja na mipango ya kibaguzi ya aina hii? Kwa hiyo watoto wasiofanya vizuri kwenye masomo lakini Mola amewajalia vipaji kwenye mambo mengine wao hawastahili ufadhili wake? Ni sawa na mzazi ana watoto watatu wanasoma darasa moja, wawili hawafanyi vizuri kwenye masomo, mmoja ndiye anafanya vizuri..kwa hiyo ni sahihi mzazi kumsomesha huyo mmoja anayefanya vizuri na kumgharimia vyote atakavyo na hawa wawili wao hata waache shule wakachunge ni sawa, nadhani mzazi mwenye kujua wajibu wake atatumia rasilimali kadiri awezavyo kusaidia hawa wawili zaidi kuliko huyo mmoja!
Lakini pia, utaanzishaje scholarship bila kutaja vyanzo vya resources za huo ufadhili? Kiongozi mwema ni yule anayelenga kusaidia zaidi wenye uwezo mdogo kuliko wanaojiweza..WENYE AFYA HAWAHITAJI DAKTARI BALI WALIO WAGONJWA..na kutaja vyanzo vya funding ili wengine wenye nafasi washiriki kuchanga ili wanufaika wawe wengi kwa kuangalia uhitaji zaidi na sio ufaulu tu!
 
Waliobuni hiki kitu si wazima upstairs.

Huwezi kuita Samia scholarship wakati ni pesa ya Serikali.

Ingewezekana, kuita Samia Scholarship, labda akawa amestaafu, akatoa sehemu ya pesa zake halafu akafanya mobilization kutoka kwa watu au kampuni mbalimbali (maana yake wanchamgia yeye il8 atoe scholarahip). Lakini huwezi kutoa pesa ya Serikali halafu uiite kuwa ni scholarship ya Samia.

Matumizi ya pesa ya Serikali huidhinishwa Bungeni. Japo tunalo bunge bandia, mnaosikikiza, hiyo bajeti ya Samia scholarship ilipitishwa kwenye fungu gani?
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?


Kwanini tunaita stendi Magufuli wakati ni pesa ya umma au nyerere road wakati ni barabara ya umma
 
Nalo tuendelee kulitizamia. Science subjects Division One Scholarships, Eti Samia scholarships daah nchi hii iko hoi sana. Tozo scholarships
 
Huku sijui mama nani scholaship huku sijui pochi la mama,sijui tushike lipi
 
Samia scholarships maana yake ni wazo la Samia kaja na wazo la ufadhili Kwa vipanga wa paper ya kidato Cha SITA Kwa masomo ya science
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Kuna watu wanataka kujifanya Rockfeller wa USA .Prof Mkenda anayo maswali ya kujibu. Hizi ni pesa za watanzania zinatoa impact kwa watoto wa kitanzania. Kuiita samia si sawa maana watoto wetu wanatoka na mind set kuwa wamefadhiriwa na.samia .its not right
 
Kuna watu wanataka kujifanya Rockfeller wa USA .Prof Mkenda anayo maswali ya kujibu. Hizi ni pesa za watanzania zinatoa impact kwa watoto wa kitanzania. Kuiita samia si sawa maana watoto wetu wanatoka na mind set kuwa wamefadhiriwa na.samia .its not right
Kwa hio kwa hisani ya watu Marekani mnaona sawa ila Samia nongwaa hehe
 
Nchi ambayo CHAWA anaalikwa bungeni kama mgeni wa heshima na watunga sheria wanamshangilia kama shujaa
Mara sijui ...Karibu Mandonga, Manara, msanii fulani kaalikwa bungeni.. etc.. hivi kweli bunge la watz mko serious mkitumia kodi za wananchi,badala ya kujadili maswala ya msingi yenye tija na kutatua matatizo lukuki ya nchi, ili kupata maendeleo ????. Jamani punguzeni ' commedy ili Kazi iendelee.
 
Maswali ya kijinga. Heshima ya mtu usiichezee kisiasa kwa vile tu CUF na CHADEMA bado hamjapara Rais. Kwani Ziwa Victoria alitoa ndoo ngapi za maji kulijaza? Duke of York alijenga tofali ngapi New York? Ni heshima ya mtu, akisema NO itakuwa NO kwa sababu tulimpa madaraka hayo tulipomchangua, akamshinda tundulissu 87%/13%. Kama ingekuwa the other way round tungekuwa na Makanikia Bridge
Ungekaa kimya mkuu... sasa umeongea tumejua ukoje kichwani.
 
Kwa hio kwa hisani ya watu Marekani mnaona sawa ila Samia nongwaa hehe
Hisani ya marekani ni kwa hisani kweli siyo gangwe mmoja anarukia public fund na kupachika jina we vipi. Watawala wa kiafrica haya mkiyaacha mtakuja kulilia chooni hata huko marekani huwezikurukia public fund wakakuacha.
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
It's how we operate. How we treat our leaders. Godlike. It's as if every cent they approve it's coming from the pockets!
Try watching TBC just for 1 hr. I dare you!
If not wanting to smash your TV you will be depressed the whole day!😭🤒😡😠
 
Samia scholarships maana yake ni wazo la Samia kaja na wazo la ufadhili Kwa vipanga wa paper ya kidato Cha SITA Kwa masomo ya science
Atumie fedha zake sio za umma kwenye kufund idea yake.
 
Kwanini tunaita stendi Magufuli wakati ni pesa ya umma au nyerere road wakati ni barabara ya umma
Hizo ni fedha zilizopitishwa na kuidhininishwa na Bunge , ingeweza kuitwa jina lolote lile.

Ila huu ni mradi binafsi ambao chanzo cha pesa ni pesa za umma.

Bunge linapaswa kuidhinisha hili jambo.
Else source of funds iwe raised privately.
 
Back
Top Bottom