Ifikapo 2030 hizi nyimbo za kipuuzi za bongo flava zitaiharibu jamii nzima

Ifikapo 2030 hizi nyimbo za kipuuzi za bongo flava zitaiharibu jamii nzima

Hata mbuyu ulianza kama mchicha, ndivyo unavyoweza kusema. Nipo kwenye basi natokea Songea kwenda Mwanza, safari nzima tunasikilizishwa nyimbo na video za kihuni za bongo flava mwanzo mwisho. Baadhi ya nyimbo zinazopigwa humu ni hizi:

1. Kila demu ana matako.
2. Nataka kunya
3. Nitongoze
4. Nipe tamu yangu

Wewe fikiria nyimbo za kipumbavu na kipuuzi kama hizi zinapigwa na kuchezwa hadharani kwenye video. Maadili ya jamii yatabaki salama? Ukija kwenye video ndiko kwenye balaa zaidi. Mabinti wanacheza uchi huku wakishikwashikwa matiti na makalio hadi kero. Tukienda na mwendo huu hadi 2030, jamii itakuwa imeharibiwa sana na nyimbo hizi za ajabu ajabu.

Watu hadi tunashindwa kusafiri na watoto pamoja na wakwe zetu kwa sababu ya kuogopa kuaibika kutazamishwa video za kingono zinazochezwa kwenye mabasi haya. Chanzo kimojawapo cha kusambaza uharibifu wa maadili potovu yaliyomo kwenye nyimbo za bongo flava ni kupitia mabasi ya daladala na haya ya mikoani

Ifike wakati serikali ipige marufuku nyimbo na video hizi za kihuni kupigwa kwenye mabasi ili kuepuka kusambaza sumu ya uharibifu wa maadili katika jamii. Mwisho wa siku serikali itakuja kuwalaumu wazazi wakati yenyewe ndiyo imeshindwa kusimamia utaratibu wa kistaarabu na kimaadili ktk jamii.

Tujifunze kutokana na makosa ya wengine. Wazungu waliruhusu mfumo wa maisha huria kwa raia wa nchi zao lakini sasa wanalia baada ya maadili ya jamii kumomonyoka kwa kiwango kisichorekebika.

Hata kama vyama vya siasa vimekuwa vikiwatumia wasanii kuimba nyimbo hizi za ovyo kwenye kampeni za kisiasa, wakati umefika sasa serikali iache kuharibu maadili ya jamii kwa kisingizio chochote kile. Tusipiziba ufa ipo siku tutajenga ukuta.​
Unayo haki ya kuzuia kupigwa nyimbo hizo, ulitakiwa umwambie mhudumu wa ndani ya basi badala ya sisi.
 
Unayo haki ya kuzuia kupigwa nyimbo hizo, ulitakiwa umwambie mhudumu wa ndani ya basi badala ya sisi.
Mkuu ningeweza kumuambia lakini niliogopa reaction ya abiria. Kuna baadhi ya aboria wamepinda sana wangenitukana kwa kuwanyima 'burudani'.
 
Moja ya sababu kwa nini sipendi safari za basi ni huo upumbavu, hua wanaona kama vile abiria wote ni wahuni wenzao, ni bora watu wasafiri kibubu kama kwenye treni kuliko kuweka huo upumbavu
 
Hakuna jipya chini ya Jua haya yote unayoyaona yalikuwepo enzi na enzi

Wapi Sodoma na Gomola
Wapi yule kahaba aliyemfuta Yesu vumbi la miguu kwa kutumia machozi.
 
Mkuu ningeweza kumuambia lakini niliogopa reaction ya abiria. Kuna baadhi ya aboria wamepinda sana wangenitukana kwa kuwanyima 'burudani'.
Muite mhudumu kwenye kiti chako kisha mueleze kwa sauti ya kawaida bila kupayuka.
 
Hali ni tete sana, enzi za kina msondo na bendi nyingine za zamani miziki ilikuwa ya kuelimisha na ilipigwa kiutu uzima, siku hizi ni matusi tupu hadi watoto wa chekechea wanaitikia vibwagizo.
 
Ila kwa kweli, wenye mabasi wangepewa muongozo wa aina ya vitu vya kuonyesha..tuna vivutio vya utalii kibao..tungeonyesha hivyo vitu kuliko kuonyeshana matusi. Ukisafiri na wakwe, wazazi au watoto inabidi mjifanye mmelala msisikie na kutazama yanayoendelea.

Kuna siku waliweka wimbo wa Mr Mwanya, aisee ilibidi wautoe. Ulikuwa Kama pono vile. Nikajiuliza BASATA wameruhusuje kitu Kama hiki.
 
Uje uangalie hata hadhi ya wahudumu wa mabasi hayo,utagundua na wenyewe yale yale tu.
Ila jambo la kujiuliza: zipigwe zipi? Za kilokole, si kwamba watu wote watapenda. Za kihuni hizo,si kwamba wote wanapenda. Mawaiza,si kwamba wote watapenda. Miaka ya nyuma walikua wakiweka muvi mwanzo mwisho,niliona kulikua na ahueni tofauti na sasa. Bila namkatia vibuno hawajafurahia. Hawaangalii wamebeba watoto na watu wazima. Ini shoti, wanaonaga abilia kama wahuni wenzao. Teh teh teh teh teh

Kuna siku tupo kwenye basi wakawa wameweka movie, Sasa movie imekolea yule konda akaitoa na kuweka bongofleva za kijinga. Aliniboa Sana. Kwa masaa Saba tuanaangalia vichupi.
 
Bottom line watasema wanaimba kwaajili ya maokoto. Cha kushangaza wanachoingiza ni kidogo sana hakiendani na athari ya maadili wanayoyaaribu.

Watu wachache wasituaribie vizazi.

Na hiyo ndio sababu. Wanasingizia kuwa watu wanataka nyimbo za hivyo.
 
Back
Top Bottom