IGP Sirro: CHADEMA wanamuona Mbowe Malaika hawezi kosea, ushahidi tunao

IGP Sirro: CHADEMA wanamuona Mbowe Malaika hawezi kosea, ushahidi tunao

IGP Sirro anadhani Watanzania wamesahau kutekwa kwa MO? Kwa makusudi mjadala wa nani alimteka MO na kukaa naye ndani ya siku 9 umeamka tena baada ya IGP Sirro kujigeuza mahakama na kumhukumu Mbowe kuwa anao ushahidi kuwa Mbowe ni gaidi.

IGP Sirro nataka ujue kuwa, jinai huwa haizeeki, unachokifanya kuna siku utasimama mbele ya Mahakama. Usidhani ilivyo leo ndivyo na kesho itakuwa hivyo.

Kwa sababu ugaidi wa Mbowe unaujua, tunataka kujua ni nani alimteka MO? Na ile picha ya gari la watekaji wa MO uliitoa wapi?

Na ulijuaje kama walikuwa ni wazungu,na waliwezaje kutoroka mipaka ya Tanzania?
Siyo hivyo tu, tunataka utuambie Ben Saanane yuko wapi?

Na Tuambie pia Azory Gwanda yuko wapi?
Na ni kina nani walimpiga risasi Tundu Lissu?

Na tuambie pia yuko wapi Police aliyefyatua risasi iliyomuua Aquilina? Kwa sababu risasi ya kutuliza ghasia hufyatuliwa juu,sasa ilikuwaje Police kufyatua risasi kuelekea kwenye Daladala?

IGP Sirro, hujui gharama ya kukabiliana na Dhambi,siku ukianza kulipa maovu yako na wenzako, usije sema umeonewa.

MUNGU si wa mchezo,walikuwepo kina Samuel Doe,yaliyowakuta ni majonzi na vilio siku walipolipa matendo yao.

MUNGU hawahi wala hachelewi.

Siku inakuja mtalipa tu sawa sawa na matendo yenu.

Amina...!
 
Hapa issue ni kupata katiba mpya mkuu itakayoleta mgawanyo sawa wa mamlaka, tume huru ya uchaguzi, na uhuru wa mahakama. Majibu ya maswali mengi ya Watanzania yatajibiwa Mahakamani na kwenye sanduku la kura.
 
Wasalaam.
Napenda kukupa hongera kamanda kwa kazi nzuri ya intelligence hadi kufanikiwa kumkamata Mbowe na kundi lake.

Ama baada ya pongezi nakusihi utoke hadharani kama ulivyotoka leo kuutangazia ulimwengu umekamata gaidi uwatangazie watanzania wanasubiri kujua hadi leo ni kundi gani lilitaka kumuua mh Tundu Lissu.

Ni wakati muafaka Jeshi letu la Polisi mkawafahamisha watanganyika juu ya watu wasiojulika, ni kina nani watu wasiojulika mpaka leo hawajulikani, hata Jeshi letu na kamanda Sirro eti hawana hata intelence ya kuwakamata watu wasiojulika ila mmepata ya kumkamata gaidi mbowe.

Hitimisho: Polisi mjitafakari tendeni haki kwa watanzania wote tuwajue ni nani walitaka kumuua mh Lissu? Kweli mmeshindwa kazi ndogo hii kuwajua wasiojulikana? Au ndo huyo huyo gaidi Mbowe?
 
IGP Sirro anadhani Watanzania wamesahau kutekwa kwa MO? Kwa makusudi mjadala wa nani alimteka MO na kukaa naye ndani ya siku 9 umeamka tena baada ya IGP Sirro kujigeuza mahakama na kumhukumu Mbowe kuwa anao ushahidi kuwa Mbowe ni gaidi...
instagram.jpg
 
Akistaafu kahaidiwa ubunge hivyo ni lzm alinde chama kisife
 
Bado nawaza niunge vipi Dots,

Lakini RPC wake alisema Rais kaagiza Mbowe akamatwe, ilikaaje hapo au Sirro hajalifafanua why?
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
"If wishes were horses, beggars would ride" is a proverb and nursery rhyme, first recorded about 1628 in a collection of Scottish proverbs, which suggests if wishing could make things happen, then even the most destitute people would have everything they wanted.

natamani andiko lako litokee kama ulivyoomba
 
Huyu hapa akishirikiana na dhalimu mwendazake. Inasemekana $3 millions “zilichukuliwa” kutoka bank account yake wakati akiwa ametekwa.
IGP Sirro anadhani Watanzania wamesahau kutekwa kwa MO? Kwa makusudi mjadala wa nani alimteka MO na kukaa naye ndani ya siku 9 umeamka tena baada ya IGP Sirro kujigeuza mahakama na kumhukumu Mbowe kuwa anao ushahidi kuwa Mbowe ni gaidi.

IGP Sirro nataka ujue kuwa,jinai huwa haizeeki,unachokifanya kuna siku utasimama mbele ya Mahakama.
Usidhani ilivyo leo ndivyo na kesho itakuwa hivyo.
Kwa sababu ugaidi wa Mbowe unaujua,tunataka kujua ni nani alimteka MO? Na ile picha ya gari la watekaji wa MO uliitoa wapi?
Na ulijuaje kama walikuwa ni wazungu,na waliwezaje kutoroka mipaka ya Tanzania?
Siyo hivyo tu, tunataka utuambie Ben Saanane yuko wapi?
Na Tuambie pia Azory Gwanda yuko wapi?
Na ni kina nani walimpiga risasi Tundu Lissu?
Na tuambie pia yuko wapi Police aliyefyatua risasi iliyomuua Aquilina? Kwa sababu risasi ya kutuliza ghasia hufyatuliwa juu,sasa ilikuwaje Police kufyatua risasi kuelekea kwenye Daladala?
IGP Sirro, hujui gharama ya kukabiliana na Dhambi,siku ukianza kulipa maovu yako na wenzako,usije sema umeonewa.
MUNGU si wa mchezo,walikuwepo kina Samuel Doe,yaliyowakuta ni majonzi na vilio siku walipolipa matendo yao.
MUNGU hawahi wala hachelewi.
Siku inakuja mtalipa tu sawa sawa na matendo yenu.
Amina...!
 
SIRRO amekuwa IGP wa ajabu bila kutegemewa kabisa.

Analaumu aliyetaka kuuliwa kwa kushindwa kwake kufanya uchunguzi juu ya jaribio hilo.

Anatisha raia wasidai haki zao ndani ya sheria zilizopo "akilinda usalama" wa wanaomshibisha yeye.
 
Sirro tuletee aliempiga risasi Mh mbunge saa saba mchana pale area D Dodoma Mungu anakuona
 
SIRRO amekuwa IGP wa ajabu bila kutegemewa kabisa.

Analaumu aliyetaka kuuliwa kwa kushindwa kwake kufanya uchunguzi juu ya jaribio hilo.

Anatisha raia wasidai haki zao ndani ya sheria zilizopo "akilinda usalama" wa wanaomshibisha yeye.

Hivi Jeshi la Polisi halina wanasheria? Inakuwaje IGP anaongea hadharani kwamba kuandamana ni kuvunja sheria za nchi ni kifungu gani hicho kama si kulidhalilisha Jeshi zima la Polisi?
 
Back
Top Bottom