IGP Sirro: Tunakichunguza Kituo cha Kutetea Haki za Binadamu baada ya kupokea fedha nyingi takriban Tsh. bilioni 6 kutoka nje

IGP Sirro: Tunakichunguza Kituo cha Kutetea Haki za Binadamu baada ya kupokea fedha nyingi takriban Tsh. bilioni 6 kutoka nje

Wewe unataka serikali ifanye kama anayotoka lisu na watu wake wakati wao hawataki kufata utaratibu wa serikali. unajua kuna vitu vingine nibora angevifanya raia wa kawaida ambaye hajui tratibu zinakuwaje lakini sio kwa wakina lissu.
Taratibu gani za Serikali hazikufuatwa???
 
Kwani Fungu la Ununuzi wa Wabunge na Madiwani kwa Jina la "Kuunga Juhudi" lilitoka wapi?
Na IHP hakuwaita CCM awahoji kuwa ,pesa ya kununua wapinzani wamezitoa wapi?
 
IGP Sirro amesema jeshi la polisi linakichunguza kituo cha Kutetea Haki za Binadamu kinachoongozwa na Ole Nguruma baada ya kituo hicho kupokea kiasi kikubwa cha fedha kutoka nje.

Sirro amesema kwa mwaka huu pekee kuanzia mwezi January kituo hicho kimepokea takribani Tsh bilioni 6 kutoka nje hivyo Jeshi linataka kujiridhisha uhalali wa fedha hizo zisijekutumika kwa nia ovu ikiwemo ugaidi na utakatishaji.

Chanzo: BBC Dira ya Dunia!

Maendeleo hayana vyama!
IGP Sirro ndo alitoa ukomo wa budget ya kituo?
 
Ina maana siku hizi donors kutuma hela kwa wadau hairuusiwi tena kwan mboga mboga mnaogopa nini
Waza nje ya box, kwa nini hela hizo ziingizwe mwaka huu wa uchaguzi? Halafu kosa la Sirro ni kutuhabarisha?

Amani ya nchi yetu inawakera sana wahuni wa kisiasa na uchumi ndani na nje. Lazima tuwe macho na makini kwenye usalama na amani yetu.

Waache polisi wafanye kazi yao wakiona hakuna tatizo si wataruhusiwa kutumia hizo fedha?
 
"vichaka" vyote vichunguzwe na hatua zichukuliwe, tunataka nchi yetu ibaki salama na amani ktk uchaguzi huu
 
Hawa Polisi wakikwambia 10 usishike hata moja. Ndiyo hawa hawa wanabambikia kesi FAKE Watanzania wengi wasio na hatia hivyo hata huu ushahidi wao pia unaweza kuwa ni FAKE. Kumbukeni kesi chungu nzima FAKE walizobambikiwa Watanzania mbali mbali ikiwemo yule Kabendera na kusababisha kifo cha mama yake mzazi.

johnthebaptist,
Mkuu
Utakufa kwa vidonda vya tumbo[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Dah hii ni Tanzania.Kaka yangu Ole Ngurumwa hata wakizuia Pesa.lazima tutawanyoosha tu kwenye sanduku la kura ije jua ije mvua.
Mrakuwa stunned na matokeo ya uchunguzi mtachoka.

Zipo taarifa za muda mrefu ndoa baina ya wanasiasa wahuni na hizi asasi ambapo sasa pesa zinapitia kwenye NGOs kuelekea mikakati mibovu inayohatarisha umoja na ustawi wa nchi yetu....
 
Sometime transfers kama hizi hutumika katika utakatishaji pesa na kufund vikundi vya kigaidi.

Siyo jambo baya kuchunguza ila tu kwa nchi yetu ilipofikia itaonekana kama vile kuna rafu inataka kuchezwa.
Hawa Polisi wakikwambia 10 usishike hata moja. Ndiyo hawa hawa wanabambikia kesi FAKE Watanzania wengi wasio na hatia hivyo hata huu ushahidi wao pia unaweza kuwa ni FAKE. Kumbukeni kesi chungu nzima FAKE walizobambikiwa Watanzania mbali mbali ikiwemo yule Kabendera na kusababisha kifo cha mama yake mzazi.

johnthebaptist,
Polisi wetu kumbe wanaweza kuchunguza matukio ya watu kupokea fedha kutoka nje,na hawana uwezo wa kuchunguza matukio ya mauaji yanayofanyika hapa hapa Tz na hata jaribio la mauaji ya Lisu?
Ama wanachanganywa na hayo maagizo kutoka juu?

Nadhani ifike wakati hawa jamaa wafanye kazi kulingana na sheria na taratibu za nchi,waache kufanya kazi za chama cha mapinduzi.
 
Sometime transfers kama hizi hutumika katika utakatishaji pesa na kufund vikundi vya kigaidi.

Siyo jambo baya kuchunguza ila tu kwa nchi yetu ilipofikia itaonekana kama vile kuna rafu inataka kuchezwa.
Kuchunguza sawa, lakini kwa nini wafunge account za asasi tena kinyume cha sheria kana kwamba kulikuwa na dharura?

Hii ni unprofessional kwa sababu kulingana na taarifa zilizopo, hiyo hesabu ya tzs.6B/- ni cummulative transactions tangu January 2019. Si wangechunguza kwanza THRDC wanafanya interventions gani, volume ya transactions in monetary terms, pesa imetoka kwa nani, pattern ya sources of fund, na, kisha, iwapo wangeona kuna mismatch, ndio wachukue hatua za kisheria?

Hawa jamaa wahuni kweli kweli. Yaani wanaamuka asubuhi tu, hao wana-dip mikono yao kwenye mifuko ya watu!

Tunaowajua. Wametanya hivyo mara nyingi kwa watu binafsi, kisha wakiisha kukomba pesa yao yote, huwaua wakisingizia ni majambazi! So sad!
 
Naona una hofu hadi unakaribia kuchanganyikiwa. Kama hujui miradi yao umezuiliwa kwenye ofisini kwao kuangalia miradi yao??? Umeshindwa hata kufungua website yao tu????

Nambie hao mabeberu wananufaikaje na hilo shirika hapa tanzania?
 
Tz simaanishi pesa ya kununua kabichi nk
Kituo kinafanya kazi Tz yote kina waajiriwa wa kutosha kina endesha mafunzo mwaka mzima,mtu anashangaa kuingiziwa pesa 6B kwa miezi zaidi ya nane?
Wanataka wote walipwe kama wao wanavyolipwa chini ya milioni moja kwa mwezi? Acheni roho mbaya.!!
Bilioni sita pesa ya mboga nchi gani?
 
Back
Top Bottom