Ijue Historia ya muasisi wa TANU, Ally Kleist Sykes (1926 - 2013)

Ijue Historia ya muasisi wa TANU, Ally Kleist Sykes (1926 - 2013)

Inasikitisha namna vyombo vya habari vilivyoupuuza msiba huu, Hii ni ishara ya upofu uliogubika Historia ya Nchi yetu.

Uko sahihi kabisa,

JF pia wameupuuza msiba, members wanasoma na kuondoka bila kujadili kwa kina. Ilitakiwa akina Mohammed said kuja kutoa promo za mwisho, kwani muda wote Mohammed said and Co. walikuwa wanataka Ally amilikiwe na kundi fulani tu la imani na kusahau kuwa ni mtu wa wote.

Sijapenda hata kidogo ninapoangalia pages za kifo cha Dk. Ferdenand masau na Ally Sykes? labda watu wamechoka na historia za uhuru wanataka mambo mapya?

Naona hata kifo cha Steven Kanumba kilipata promo zaidi ya Sykes kwenye vyombo vya habari.
 
Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi......Amin.....!!
 
Pamoja nakuwa ulikusudia kuuhabarisha umma juu ya msiba huu,

Lakini upotoshaji wa aina hii usiachwe upite bila kusahihishwa!

AA imeundwa 1929 chini ya Mwalimu Cesil Matola,

1933 AA ilimkasimisha madaraka katibu wake bwana Klest Sykes, hii ni baada ya Matola kufariki,

Mwaka 1948 Klest Sykes anaasisi TAA, na mwaka huohuo anapinduliwa na Daktari kijana Vedasto Kyaruzi anashika urais wa TAA,

Katibu anakuwa Abdul Sykes kaka wa Ally Sykes,

Mwaka 1950 Dr Kyaruzi anahamishwa kikazi kwa nguvu na muingereza nakupelekwa Nzege hiyo ikiwa ni mikakati ya mkoloni kukidhoofisha chama cha TAA, baada ya hapo nafasi ya urais inakaimiwa na Abdul Sykes.

Mwaka 1953 uchaguzi unafanyika na Julius Nyerere anamshinda Abdul Sykes katika uchaguzi huo, hivyo Julius anakuwa rais wa TAA,

Mwaka unaofuata yani 1954 TAA inabadilishwa jina nakuwa TANU na uchaguzi unafanyika tena, Julius Nyerere na Abdul Sykes wanashindana katika kinyang'anyiro hicho na Julius Nyerere anaibuka kidedea hivyo kuwa rais wakwanza kwa TANU,

Hilo likaenda mpaka 1958 katika uchaguzi maarufu kama kura tatu, uliofanyikia jimbo la magharibi (Tabora) Nyerere tena akashinda,

Baada ya hapo Abdul Sykes alijitenga na siasa na kuanzisha chuki dhidi ya viongozi wa TANU hasa Julius Nyerere,

Baada ya uhuru kupatikana, kundi lililokuwa likimuunga mkono Abdul Sykes lilianzisha UASI dhidi ya serikali halali ya TANU,

Kundi hilo lilikuwa na watu wengi walitoka TAA na TANU hasa Shehe Takadir, Shehe Hassan Bin Amir, na wengine wengi!

Kundi hilo baada yakufeli mission yao kisiasa sasa liliamua kutumia misikiti kupandikiza chuki yao,

Chuki hiyo ndio inayoliathiri taifa mpaka hii leo na Ritz ukiwa ni muathirika wayo!


Kufuatia hali hiyo, mkono wa dola ukaanza kuwaandama tena kwa nguvu hii ilifuatiwa na kuunda sheria ya kuweka mtu kizuizini ya mwaka 1962,

Sasa kusema Ally Sykes ndie muasisi wa TAA na TANU ni UONGO

Ally Sykes katika uhai wake hajawahi kushika nyadhifa yoyote ya kisia, kikundi ama jumuiya!

Neno zuri lakutumia nikama ulivyoanza na kichwa cha taarifa hii kuwa MMOJA wa waasisi wa TANU na sio TAA

asante kaka kwa kuweka sawa uposhaji alioukusudia Ritz lakini si kosa lake ni matokeo ya ngano za mzee Mohamed Said
 
Last edited by a moderator:
shariff ritz,

kama kuna ndugu zetu wa aina hiyo ni uzuri kuwa nao karibu na kuwaelewesha majambo kwa kituo na utuvu.

Kwani mbona yericko nyerere,pamoja na "matata yake" yoote lakini tupo nae na tunakwenda nae taratibu kwa hila,maarifa na utuvu na sasa aelekea kunyooka,kufahamu na kukubali japo kwa shingo upande; historia anayofundishwa na maalim sheikh mohammed said.

Kwa hiyo mimi nashauri tusiwatupe au kuchoka kuwafahamisha na kuwasomesha ndugu zetu hawa historia yao ya tanganyika na zanzibar ilokua imefichwa makusudi kwa miaka mingi mno.

Waswahili tuna msemo;"tikiti bovu li shambani mwako".

Ahsanta kwa kunisikiza.

ritz; umefanya vizuri kupost hii page kwa ajili ya mzee huyu. Nashauri isiingie siasa zozote za thread nyingine

cc yericko, kadogoo
 
[h=3]MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHANI MSIBA WA ALLY SYKES JIJINI DAR[/h]
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mjane wa marehemu Ally Sykes, Zainab Ally, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa marehemu Ally Sykes, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiaga na baadhi ya wazee waliohudhuria shughuli za msiba, wakati alipokuwa akiondoka baada ya kuhani msiba wa mwasisi wa TANU, Ally Sykes, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa kuzikwa leo jioni jijini Dar es Salaam
 
Pamoja nakuwa ulikusudia kuuhabarisha umma juu ya msiba huu,

Lakini upotoshaji wa aina hii usiachwe upite bila kusahihishwa!

AA imeundwa 1929 chini ya Mwalimu Cesil Matola,

1933 AA ilimkasimisha madaraka katibu wake bwana Klest Sykes, hii ni baada ya Matola kufariki,

Mwaka 1948 Klest Sykes anaasisi TAA, na mwaka huohuo anapinduliwa na Daktari kijana Vedasto Kyaruzi anashika urais wa TAA,

Katibu anakuwa Abdul Sykes kaka wa Ally Sykes,

Mwaka 1950 Dr Kyaruzi anahamishwa kikazi kwa nguvu na muingereza nakupelekwa Nzege hiyo ikiwa ni mikakati ya mkoloni kukidhoofisha chama cha TAA, baada ya hapo nafasi ya urais inakaimiwa na Abdul Sykes.

Mwaka 1953 uchaguzi unafanyika na Julius Nyerere anamshinda Abdul Sykes katika uchaguzi huo, hivyo Julius anakuwa rais wa TAA,

Mwaka unaofuata yani 1954 TAA inabadilishwa jina nakuwa TANU na uchaguzi unafanyika tena, Julius Nyerere na Abdul Sykes wanashindana katika kinyang'anyiro hicho na Julius Nyerere anaibuka kidedea hivyo kuwa rais wakwanza kwa TANU,

Hilo likaenda mpaka 1958 katika uchaguzi maarufu kama kura tatu, uliofanyikia jimbo la magharibi (Tabora) Nyerere tena akashinda,

Baada ya hapo Abdul Sykes alijitenga na siasa na kuanzisha chuki dhidi ya viongozi wa TANU hasa Julius Nyerere,

Baada ya uhuru kupatikana, kundi lililokuwa likimuunga mkono Abdul Sykes lilianzisha UASI dhidi ya serikali halali ya TANU,

Kundi hilo lilikuwa na watu wengi walitoka TAA na TANU hasa Shehe Takadir, Shehe Hassan Bin Amir, na wengine wengi!

Kundi hilo baada yakufeli mission yao kisiasa sasa liliamua kutumia misikiti kupandikiza chuki yao,

Chuki hiyo ndio inayoliathiri taifa mpaka hii leo na Ritz ukiwa ni muathirika wayo!


Kufuatia hali hiyo, mkono wa dola ukaanza kuwaandama tena kwa nguvu hii ilifuatiwa na kuunda sheria ya kuweka mtu kizuizini ya mwaka 1962,

Sasa kusema Ally Sykes ndie muasisi wa TAA na TANU ni UONGO

Ally Sykes katika uhai wake hajawahi kushika nyadhifa yoyote ya kisia, kikundi ama jumuiya!

Neno zuri lakutumia nikama ulivyoanza na kichwa cha taarifa hii kuwa MMOJA wa waasisi wa TANU na sio TAA
du!!kaka nilidhani utamsubiri kwanza amalize arobaini ndio uje umkosoe.ninavyo mjua @Ritzhttps://www.jamiiforums.com/member.php?u=34266 akitoka tuu makaburi ya kisutu break ya kwanza ni kule kwenye mnakasha ili akujibu.RIP Mzee Ally Kleist Syke.
 
Ukitaka kuhakiki kwa kina kutengwa kwa mpigania uhuru ni lazima kuwapitia wote bila ubaguzi acha Nyerere aliyekuwa juu kwani yeye kwa nafasi yake alisikika zaidi. Utakuta si familia ya sykes tu na pengine wapo waliokuwa hali mbaya kuliko hao akina sykes.

Unajua ziliko familia za akina SECIL MATOLA na DK. VEDASTO KYARUZI. Je, umewahi hata kuzisikia? Yumkini sykes wamesikika japo kwa mbali kuliko hao?

Wazee wetu wa zamani walikuwa wanatoa maisha yao kwa taifa kuliko familia zao, dini zao au kabila zao na ndio maana wengi hujawasikia wakipaza sauti sana kulalamika. hatujasikia wajukuu wa watemi na machifu wakidai fidia za babu zao waliokufa vitani kulikomboa taifa letu. HII NAYO NI HOJA.

Very good point; there should a REASON!!!!!!!
 
Hakuna anayepinga mchango wa Nyerere kwenye TAA, TANU, CCM, kafanya mengi mazuri kwa sehemu yake mchango wake unajulikana, lakini bahati mbaya hawa wenzake historia zao zao zimewatupa.

Kuhusu machifu mbona mchango wao unajulikana katika harakati za uhuru.

Chifu Kidawa, Chifu Mariale, Chifu Makwaiya.

RITZ??????? It took you soooooooo long and a death of this Mzee to say these words. We are all human after all. Thank you.
 
Historia haiwezi kusemekana kuwa imefichwa kama haipo iliyoandikwa na kupotoshwa. Ni ipi iliandikwa ikapotoshwa?

Kimsingi, siamini kwa hakika kwamba hata historia ya Nyerere imeandikwa. kazi za nyerere zaidi ya 75% haziko kwenye maandishi na bahati mbaya hakuwahi kuweka document ya mikono yake ambayo pengine ingekuwa msingi wa yeye kutotambua mchango wa wenzake au kumlaumu kwamba hakuweka sawa au alipotosha historia ya wengine.

kinachotusumbua hapa watanzania ni dini zetu si upigania uhuru. kama ingekuwa ni upigania uhuru tungeanza kumlaumu Nyerere kwa kupuuza mchango wa watemi na machifu wetu katika mchango wao kupambana na wakoloni. wapo Watemi na machifu waliotoa uhai wao waliojinyonga au kufa katika vita hivyo lakini leo hii yule aliyetoa nyumba ya kuishi nyerere au aliyetoa mchango wa gari la kupigania uhuru ndiye anatukuzwa pekee. Hii yote mwisho wake historia ya baba na mama zetu waliopigania uhuru haina mwisho mwema.

KAZIMOTO; This is an important point. Tunakoelekea in the next 30 years kila dhehebu litakuwa na its Tanganyika History. The sure thing ni kuwa Jina la Nyerere will stay in all madhehebu "texts" either for praise or ridicule.
 
sk20.jpg
 
Ha ha ha! Nimeshauri mambo ya familia yaishie kwenye familia. Ally Sykes ni mtu mdogo sana kwenye siasa za nchi hii; huo ndio ukweli hata kama hupendi kuusikia. Tunatoa pole kwa sababu ni binadamu mwenzetu katutoka lakini sio kwa kuwa ni maarufu kihivyo. Natumaini umeelewa.

kwahiyo walikuwa wanapigania uhuru kwa ajili ya familia zao siyo!!? kuwa mwadilifu basi, nadhani kama ambavyo haikuishia kwa familia ya mama nyerere pekee kipinde kile cha umauti wa baba wa taifa basi na hili ni similitude yake. kama hutaki kunywa sumu.
 
mungu aulaze pema roho ya marehemu. INNALILAH WAINNA ILAYHI RAJIUUNA!
 
Viongozi wa Chadema msibani hawakuonekana hata salama za rambirambi hakuna Dr.W.Slaa, Zitto, John Mnyika, mnashindwa kuwaenzi wazalendo waliopigania uhuru.
 
Last edited by a moderator:
Viongozi wa Chadema msibani hawakuonekana hata salama za rambirambi hakuna Dr.W.Slaa, Zitto, John Mnyika, mnashindwa kuwaenzi wazalendo waliopigania uhuru.

Viongozi wa dini wote walikuwepo?

Viongozi wa Dini ya KirastaFari walikuwepo?

Viongozi wa Dini ya Kiyahudi walikuwepo?

Viongozi wa Dini ya Su-Yang walikuwepo?

Viongozi wa Soka walikuwepo?

Viongozi wa ..... Walikuwepo?

Umeathiriwa na udini sana, halafu ajabu sana unalaumu kuwa "wazee wako" hawaenziwi na serikali huku wewe ni mfia ccm hiyo hiyo ya Julius Nyerere unaemdhihaki kila uchao!


Nikufunde ndugu,

Chama cha siasa misiba sio nembo ya siasa zake!

Mwenye nyota ya misiba ni mwenyekiti wa chama chako ccm tu katika nchi hii!
 
Last edited by a moderator:
Kikubwa ni Mchango wa mtu kwenye taifa. Mbona hata hao wanaojiita wazaliwa wa nchi yetu lakini ndo mafisadi wakubwa?
Tony Blair ana'origination' ya Ireland, lakini alitawatala Uingereza na mpaka sasa anaheshimika!
Obama kulingana na mila za kiaaafriaka alitakiwa awe Mkenya, lakini sasa anatawala Marekani.
Watanzania kibao wapo USA kama wamarekani.
Vice-President wa Zambia ni Mzungu kabisa, lakini analitumikia taifa lake la Zambia

Siku hizi hakuna mafundisho ya uzalendo, amesahau kwamba wakati Tanganyika inapata uhuru wale wote waliozaliwa Tanganyika kabla ya uhuru hata kama wazazi wao ni wa nje walikuwa ni raia halali wa Tanganyika mpya na ndio maana tuna Watanzania wenye asili ya asia ambao tunawaita wahindi (mbona hawa hawashangai)
 
Back
Top Bottom