Uchaguzi 2020 Ikiwa Dkt. Magufuli atafanikiwa kushinda, aachane na agenda za kuminya Upinzani

Uchaguzi 2020 Ikiwa Dkt. Magufuli atafanikiwa kushinda, aachane na agenda za kuminya Upinzani

Upo sahihi mkuu.
Pamoja na mapungufu yote ya aliye madarakani ambayo yameumiza na yanaendelea kuumiza watu wengi sana . Watanzania tungependa mabadiliko ya kweli yenye uelekeo wa kuchukua dola lakini km ulivyosema, upinzani wa Tanzania bado haujajipanga na mwaka huu pia hali ni Ile Ile ya miaka yote. Pamoja na kubanwa kwa vyama vya upinzani bado kuna mwanya wa kukiwezesha chama tawala kuendelea kushika Dola Kwa sababu zifuatazo:

- Kukosa umoja na maelewano kati ya vyama vya upinzani (Rejea UKAWA 2015). Chama tawala ni mbuyu na una mizizi mirefu bila muungano wa kweli haiwezekani kukitoa madarakani.

- Baadhi ya vyama vya upinzani havijitambui vina malengo gani. (Rejea kauli za baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kutaka kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni na kingine kumpitisha kiongozi wa chama tawala unayempinga kuwa mgombea urais wa chama cha upinzani.) Aidha vyama vingine vya upinzani huonekana wakati wa uchaguzi mkuu tu. Hivi vyama vinafanya mzaha na taasisi ya Urais ama vina malengo gani.

- Watanzani hatutabiriki, wapiga kura ni wachache mno kulingana na takwimu zilizotolewa na Tume ya Uchaguzi juzi. Hata hao waliojiandikisha bado si wote watakaopiga kura. Elimu / uelewa duni, elimu ya uraia ni duni pia. Zaidi ya 70% ya watanzania ni waathirika wa haya na wengi wao wapo maeneo ya vijijini na ndiyo wapiga kura wanaotegemewa na chama tawala. Bado tuna safari ndefu.

Lazima vyama vya upinzani vifanye jitihada za makusudi kuondoa ubinafsi wa viongozi wao, kuwa na mikakati na agenda endelevu ya kutaka kuchukua dola siyo kusubiri mikakati ya papo kwa papo kuelekea uchaguzi mkuu na kwa bahati mbaya sana tunaelekea uchaguzi mkuu bila Tume Huru ya Uchaguzi.

Kinachowezekana sasa ni kuweka nguvu kubwa kwenye ubunge na udiwani. Kwa mtazamo wangu, bado ni ngumu kukiondoa chama tawala madarakani. Huu ndiyo ukweli japo ni mchungu.

Ni hayo tu
Kura tunapiga lakini zinaibiwa. Sasa kwakuwa imezoeleka hivyo tunataka kinuke ili watu wafukuze nzi wa kijani ikulu. Damu ikimwagika ndio ukombozi bila hilo hatutaweza.
 
Kwa akili za hivyo vichwa viwili inawezekana.
Ndio hao hao maana mmoja alikuwa mambo ya ndani, mwingine alikuwa na ushawishi mkubwa kwa rais. Kumbuka kauli za nchemba bungeni huitaji kujua nini anamaanisha.
 
Kura tunapiga lakini zinaibiwa. Sasa kwakuwa imezoeleka hivyo tunataka kinuke ili watu wafukuze nzi wa kijani ikulu. Damu ikimwagika ndio ukombozi bila hilo hatutaweza.
Kupiga kura siyo tatizo, loss ni vyama vya upinzani kukosa umoja ( Rejea nilichoandika ) Ni vigumu sana kukiondoa chama tawala madarakani kwa aina ya upinzani tulionao. Vyama vipo zaidi ya 13, km kweli vingeungana na kudai kuwepo Kwa Tume Huru ya Uchaguzi ama kugoma kuingia kwenye uchaguzi mkuu kwa kukosa tume huru. Hapo mabadiliko ni lazima kwa sababu pamoja na chama tawala kuwa mbuyu, kingesalimu amri tu. Sasa shuhudia sarakasi za hivyo vyama, utashangaa kwanini vinaitwa vyama vya upinzani na siyo CCM B!

Kukinukisha siyo suluhisho. Wananchi wenyewe tuna nafasi ya kuvikataa vyama vya upinzani visivyotambua lengo lao ni nini na vyama vinavyojitambua vijipange na kuwa na mikakati ya pamoja ya kuchukua dola kwa uchaguzi unaofuata na siyo kuwa na mikakati ya zimamoto.
 
Huwezi ukawaacha wapinzani waishi watakavyo sababu hawa ni zaidi ya wapinzani..ni watu wanaopenda chokochoko, fitina, uongo na matusi.. muulize kikwete.
 
..huwezi kuwatupia lawama wasaidizi.

..kama unamfuatilia kwa umakini Magufuli wakati akiwa Waziri ungeona viashiria kwamba akipata mamlaka makubwa atakuwa na tabia hizi tunazozishuhudia sasa hivi.

..Raisi wa Tanzania ana mamlaka makubwa ya Kikatiba, wasaidizi basically wanampeleke Raisi kule anakotaka kuelekea.

..Kama ni mtu MKATILI, basi wasaidizi watamuwezesha awe mkatili kwelikweli. Kama ni mtu wa HAKI wasaidizi watamuwezesha awe mtenda haki wa kweli.

..Lingine linalomharibu ni chama chake kuwa na WABUNGE wengi kiasi kwamba hawahitaji kushirikiana na wabunge wa vyama vingine.

..Na la mwisho ni kwamba yeye ndiye MWENYEKITI wa chama, kwa hiyo yuko juu ya kila mtu.

Ni vizuri kuangalia kila hatua inayosemekana ni unyanyasaji wa upinzani kwa kina, na kufanya hivyo tutaona michango ya upinzani ina manufaa au laa na wapi.

Hatua yeyote ile lazima tujenge uwezo wa kuangalia kwa muono na utafakarishi wa Hypothesis na synthesis analysis.

Kwa kufuata hali hiyo ndio kila kisemwacho au kifanywacho na pande zote ama upinzani au uongozi wa Magufuli utaweza kupata picha halisi kuwa yafanywayo ni sawa au hapana.

Wakosefu au wauwaji wanapo hukumiwa au kifungo kirefu au kifo haipendezi, lakini kufanyika huko kunaweza kuwa ku- deter kurudiwa rudiwa kwa makosa yasio pendeza.

Mkuu Joka kuu, tupo ambao telikuwa waumini wa upinzani wa kweli kwa miaka kadhaa na tukawa viongozi katika ngazi zetu mbali mbali kichama.

Tukitaka kutapika tuna weza ikaonekana kama tunahalalisha matendo ya Magufuli- lakini sisi pia upinzani lazima tujitahidi kutengeneza matendo ya heshima na tabia ambazo CCM wanaweza kutuona katika sura ya utuu. Ikitiliwa maanani demokrasia yetu bado changa.

kWA MFANO: Nakiri bila kushawishiwa serikali ya awamu ya tano kuna vitu vingi vizuri na vya kimaendeleo wamefanya kwa taifa hili.

Tunaposema hawafanya kitu chochote au tunabadilisha maneno kuonyesha kila wafanyayo hayana thamani kwa watu wetu, jee unategemea Magufuli akushangilie kwa kubalisha ukweli wakati umesema uongo?

Kwa maamuzi ya haraka haraka kwa kubadilisha au kudhihaki kila afanyalo Magufuli anaona bora atunyanyase kwa kuwa analipa tunacho mfanyia. Kumdhihaki hata anapofanya kizuri.

Lazima tuabadilike pia ili nao tuwashawishi wabadilike. CROSS CUTTING.
 
Ni vizuri kuangalia kila hatua inayosemekana ni unyanyasaji wa upinzani kwa kina, na kufanya hivyo tutaona michango ya upinzani ina manufaa au laa na wapi.

Hatua yeyote ile lazima tujenge uwezo wa kuangalia kwa muono na utafakarishi wa Hypothesis na synthesis analysis.

Kwa kufuata hali hiyo ndio kila kisemwacho au kifanywacho na pande zote ama upinzani au uongozi wa Magufuli utaweza kupata picha halisi kuwa yafanywayo ni sawa au hapana.

Wakosefu au wauwaji wanapo hukumiwa au kifungo kirefu au kifo haipendezi, lakini kufanyika huko kunaweza kuwa ku- deter kurudiwa rudiwa kwa makosa yasio pendeza.

Mkuu Joka kuu, tupo ambao telikuwa waumini wa upinzani wa kweli kwa miaka kadhaa na tukawa viongozi katika ngazi zetu mbali mbali kichama.

Tukitaka kutapika tuna weza ikaonekana kama tunahalalisha matendo ya Magufuli- lakini sisi pia upinzani lazima tujitahidi kutengeneza matendo ya heshima na tabia ambazo CCM wanaweza kutuona katika sura ya utuu. Ikitiliwa maanani demokrasia yetu bado changa.

kWA MFANO: Nakiri bila kushawishiwa serikali ya awamu ya tano kuna vitu vingi vizuri na vya kimaendeleo wamefanya kwa taifa hili.

Tunaposema hawafanya kitu chochote au tunabadilisha maneno kuonyesha kila wafanyayo hayana thamani kwa watu wetu, jee unategemea Magufuli akushangilie kwa kubalisha ukweli wakati umesema uongo?

Kwa maamuzi ya haraka haraka kwa kubadilisha au kudhihaki kila afanyalo Magufuli anaona bora atunyanyase kwa kuwa analipa tunacho mfanyia. Kumdhihaki hata anapofanya kizuri.

Lazima tuabadilike pia ili nao tuwashawishi wabadilike. CROSS CUTTING.

..imepita miaka 4+ tangu Jpm aingie madarakani.

..nadhani tunaweza ku-conclude kwamba Jpm si kiongozi anayeweza ku-co-exist na vyama vya upinzani.

..nimeeleza kwamba binafsi nilianza kuona viashiria vya Jpm kutokukubaliana na demokrasia ya vyama vingi tangu alipokuwa waziri ktk serikali ya Jpm.

..Yapo matamko yake ktk nyakati mbalimbali ambayo yalikuwa yana viashiria vya mambo mabaya ambayo tunayashuhudia leo hii yakiwatokea wapinzani.

..jambo lingine unalopaswa kuangalia ni aina ya kampeni za uchaguzi ambazo Jpm alifanya mwaka 2015. kampeni zile zilijaa MATUSI makubwa-makubwa dhidi ya mpinzani wake, na kwa msingi huo ziliacha MADONDA/MAJERAHA kwa wadau wa uchaguzi ule.

..mshindi mwenye busara, na ukomavu wa kisiasa, alipaswa kuhakikisha kwamba anatibu madonda/majeraha ya kipindi cha kampeni za uchaguzi. Jpm hakushughulika na jambo hilo badala yake alitangaza VITA dhidi ya vyama vya upinzani nchini.

Kuhusu Wapinzani kumsifia / kutomsifia Jpm:

..mimi nadhani wapinzani wakitoa kasoro na mapungufu ya kila aina ndipo tutakapopata nafasi ya kum-appreciate Jpm genuinely.

..wapinzani wasipokuwa "gado" au vigilant, au wakaingia ktk mkumbo wa kusifia na kuabudu, mambo yakiharibika wataingia ktk lawama, kwasababu ni wajibu wao kuikagua na kuikosoa serikali wakati wote.

..Kukosoa maana yake kuna mambo yamefanyika. Jpm angekuwa hajafanya jambo lolote hakuna ambaye angemkosoa.
 
Akifanikiwa kupewa urais awasikilize wananchi wanataka nini asilazimishe wananchi kukubali na kusifia anavyotaka yeye.
Mwalimu Nyerere alisema ukiisha onja nyama ya mtu hutaacha. Hata JPM hataacha. Hiyo iko kwa DNA yake!
 
Tabia ni kama ngozi mkuu ni ngumu sana jamaa kubadilika
 
Mimi kama mwana CCM moja ya matamanio yangu ni kuona CCM ikiendelea kushika dola ya Tanzania.

Ila kati ya jambo ninalotamani litokee kwenye muhula wa pili wa Rais Magufuli endapo akifanikiwa kushinda, ni kuacha kabisa kuwachokonoa wapinzani.

Wapinzani waachwe na kuishi maisha yao na ku play part yao kama kusudi la kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi.

Binafsi pamoja na kuegemea upande wa CCM ila sijafurahishwa kabisa na baadhi ya matukio ndani ya miaka mitano iliyopita ya kukandamiza upinzani.

Tukio la kupigwa risasi Lisu, hila za kununua viongozi wa upinzani, vitabaki kama doa lisilofutika kwa utawala wa kwanza wa Magufuli. Ni moja wapo ya mbinu chafu za kisiasa karne hii ya utandawazi.

Kwa hizi wiki chache za ujio wa Lissu na mapokeo yake, ni kama vile upinzani umekuwa na nguvu maradufu pamoja na hila zote hizo chafu.

Najua wanadamu hukosea, Magufuli rais wangu kweli hapo ni mahali alikosea, lakini ana uwezo wa kuparekebisha endapo akichaguliwa tena.

Awaache upinzani waishi maisha yao kama maana ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini.
Mkuu hivi umewahi kuona mwalimu incompetent akiingia darasani bila fimbo au akampa nafasi mwanafunzi kuuliza swali?
 
Shida sio Magufuli, ila ni wshauri wake. Hivi leo una weza kuzuia redio na tv kweli? Zisitangaze habari fulani? Su wao Ccm ndio wana jidanganya hizo habari hazionekani?? Mambo ya utopolo kabisa

Kama mshauri wangu akifanya mambo yasiyonipendezea namuonya au kumfuta kazi. Kama anakubaliana na washauri wake maana yake anayapenda yale wanayomwambia.
 
Shida sio Magufuli, ila ni wshauri wake. Hivi leo una weza kuzuia redio na tv kweli? Zisitangaze habari fulani? Su wao Ccm ndio wana jidanganya hizo habari hazionekani?? Mambo ya utopolo kabisa
Shida sio washauri shida ni yeye mwenyewe, tusifiche. Huyu jamaa ni hovyo na hafai kabisa.
 
Shida sio Magufuli, ila ni wshauri wake. Hivi leo una weza kuzuia redio na tv kweli? Zisitangaze habari fulani? Su wao Ccm ndio wana jidanganya hizo habari hazionekani?? Mambo ya utopolo kabisa

Akifanya kazi nzuri sifa zinaenda kwake ila akiharibu lawama zinakua ni za wasaidizi wake,tuacheni unafiki.
 
Tukio la kupigwa risasi Lissu, hila za kununua viongozi wa upinzani, vitabaki kama doa lisilofutika kwa utawala wa kwanza wa Magufuli. Ni moja wapo ya mbinu chafu za kisiasa karne hii ya utandawazi.


Jr[emoji769]
Hali inaweza kuwa mbaya zaidi 2020. He has nothing to lose.
 
Sikilza wewe mwana CCM. Magufuli hashindi uraisi mwaka huu. Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025 ni Tundu Antipas Lissu!

Kama wewe unasoma Biblia nenda kasome hadithi ya Mfalme Saul na Mfalme Daudi alafu Njoo hapa niambie kama umeona tofauti yeyote kati ya yanayoendelea baina ya Magufuli na Tundu Lissu!
Magufuli akishinda urais utafanya nini?
 
Namaanisha upinzani bado sana kishinda Urais wa Tanzania huo ndo ukweli mchungu japo hamtaki kuusikia ! Bado upinzani haujajipanga kimkakati kushinda Urais ndugu!
nkutoe wasi wasi toka 1995 upinzani unashinda
 
Back
Top Bottom