IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

I am lost ... I have decided to rest my mind for a while... May be I will understand someday
Kuna kipindi nilikuwa nafikiri Magufuli anaharibu mambo kwa ushamba tu, kwa ujinga, kwa kutojua, kwa ubishi, na kwa kutosikiliza watu.

Granted, hizo sifa nyingi kama si zote anazo.

Lakini kuna mambo mengi anafanya deliberately, kwa manipulation, Machievallian machinations, calculations etc.

Hapa naona kuna mkakati wa kukisimika chama deep kabisa kwenye civil service huko.
 
Tatizo la Bashiru ni kuacha itikadi alizokuwa anazisimamia akiwa mwalimu pale udsm na kugeuzwa mfuasi wa kuvunja Haki za binadamu kwa maslahi ya CCM.
Huoni kuwa amefanikiwa sawa na yule Benson Bana maana nayeye alikuwa mhadhiri pale mlimani lkn akijitoa sifa zilizo mfanya awe pale na mwisho wake leo hii ni balozi
 
Kwa hiyo anakuwa Katibu Mkuu wa Chama na Katibu Mkuu Kiongozi kwa wakati mmoja au anaacha kuwa katibu mkuu wa CCM?

Vipi kuhusu muongozo wa utumishi serikalini unaotenganisha mambo ya chama na utumishi wa umma serikalini?

Hata kama atajiuzulu Ukatibu Mkuu CCM, huu uteuzi unaonesha kwamba utumishi serikalini unaenda kupelekwa kichama chama zaidi.
Huyu bado ni mwalimu wa udsm

Akiacha siasa anarudi udsm, Wanamsubiri
 
Hata kama atajiuzulu Ukatibu Mkuu CCM, huu uteuzi unaonesha kwamba utumishi serikalini unaenda kupelekwa kichama chama zaidi.

Kwa hiyo siku zooote hizo hujuagi kama shughuli za kiserikali zinaendeshagwa kichama chama (Ki-CCM) zaidi?
Hilo lipo tangu enzi za Nyerere.
 
Tatizo la Bashiru ni kuacha itikadi alizokuwa anazisimamia akiwa mwalimu pale udsm na kugeuzwa mfuasi wa kuvunja Haki za binadamu kwa maslahi ya CCM.
Acha kulalama kijana,yeyote anayekuwa kinyume nanyi lazima awe adui yenu,hivi kuna mtu mwenye akili timamu anaweza kuwa na misimamo ya wafuasi wa chadema?

Kodumu chama cha mapinduzi!
 
Kwenye sheria kuna msemo, justice must not only be done, it must also seem to be done.

Rais alikuwa na watu wengi sana wa kuwateua katika nafasi hii ya kiserikali isiyotakiwaa kuongozwa kisiasa, akachagua katibu mkuu wa chama chake ambaye ni mtu wa kisiasa.

Katibu Mku huyu ana historia tayari, historia mabayo hawezi kuikana na itamfuata tu huko kwenye civil servant.

Hivi Katibu Mkuu Kiongozi ambaye ashatoa matamko kibao ya kishabiki kwa kuishabikia CCM leo akiwaambia wafanyakazi wa serikali, watumishi wa umma, wasiendekeze siasa sehemu za kazi atachukuliwa serious?

Hivi, watu wakisema Magufuli ana mkakati wa kuingiza siasa za vyama kwenye civil service, atakuwa na point za kujitetea?

Hivi, hakuna watu wengine ambao hawana historia ya chama ambao wangefaa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi?

Umeongelea Katiba. Ukweli kwamba kitu hakikatazwi kikatiba haumaanishi kwamba kukifanya ni busara na jambo zuri.

Magufuli kama last custodian of the land hakatazwi kikatiba kuiuza nchi nzima iwe shamba la Emir of Qatar.

Hakuna sehemu ambapo katiba inamkataza kufanya hivyo.

Lakini je, kufanya hivyo itakuwa haki? Itakuwa sawa? Itakuwa busara?
Yale yale ya kulalamikia kila kitu!

Yeyote yule ambaye angeteuliwa na Magufuli mngemtafutia kasoro tu!

Angemteua Freeman Mbowe kuwa ndo katibu mkuu kiongozi, mngesema Mbowe kanunuliwa.

Sioni tatizo la Bashiru kuwa katibu mkuu kiongozi.

Kateuliwa kihalali na Rais aliyepo madarakani. Hata kwenye nchi zenye demokrasia zilizopevuka, viongozi wake huteua watu wa mirengo na itikadi zinazofanana na za kwao kwenye nafasi mbalimbali, zikiwemo mahakama, vyombo vya usalama, nk.

Apewe nafasi ya kufanya kazi tuone utendaji wake ukoje kabla hatujaanza kumtafutia kasoro.
 
Hongera sana mh Raisi kwakutupa mtu sahihi katika utumishi wa uma #hongera sana mh bashiru ulifanya makubwa sana ndani ya chama chetu kwakuangusha upinzani wote
 
Kwa hiyo siku zooote hizo hujuagi kama shughuli za kiserikali zinaendeshagwa kichama chama (Ki-CCM) zaidi?
Hilo lipo tangu enzi za Nyerere.
Kama ilikuwa hivyo, hakujawahi kuwapo na rais aliyefanya hilo kwa wazi kabisa kwa ngazi ya kumteua Katibu Mkuu wa Chama kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Hii ndiyo mara ya kwanza mnaambiwa wazi kabisa kwamba "utumishi wa umma unaenda kuongozwa na kada wa juu kabisa wa chama sasa"
 
Yale yale ya kulalamikia kila kitu!

Yeyote yule ambaye angeteuliwa na Magufuli mngemtafutia kasoro tu!

Angemteua Freeman Mbowe kuwa ndo katibu mkuu kiongozi, mngesema Mbowe kanunuliwa.

Sioni tatizo la Bashiru kuwa katibu mkuu kiongozi.

Kateuliwa kihalali na Rais aliyepo madarakani. Hata kwenye nchi zenye demokrasia zilizopevuka, viongozi wake huteua watu wa mirengo na itikadi zinazofanana na za kwao kwenye nafasi mbalimbali, zikiwemo mahakama, vyombo vya usalama, nk.

Apewe nafasi ya kufanya kazi tuone utendaji wake ukoje kabla hatujaanza kumtafutia kasoro.
Mkuu,

Unalalamika kwamba mimi nalalamika sana.

Lakini wewe unanizidi kulalamika.

Unalalamika kwamba nitalalamika kuhusu vitu ambavyo sijalalamikia bado!

Kama vile umekuwa time traveler uliyeenda katika alternate universe na kuona nalalamika halafu ukarudi hapa kutoa ripoti.

Stick to the facts please.
 
Back
Top Bottom