IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

Sawa.

Nitajie mtu mmoja ambaye angeteuliwa na Rais Magufuli kuwa katibu mkuu kiongozi mpya ambaye wewe ungemkubali na ambaye angekubaliwa na wanaJF wote na wananchi wote kwa ujumla.
Kwani nimesema kuna mtu anayekubaliwa na wote?

Angemchagua El Chapo kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, halafu watu wakalalamika, ungesema uteuzi wa El Chapo ni sahihi kwa sababu hakuna mtu ambaye atakubalika na wote?
 
Akishateuliwa Balozi anapatiwa Diplomatic Passport ili katika misele yake ya Ng'ambo apite expressway...bila hivyo he doesn't qualify to hold one.

..kwa nafasi yake ya Chief Secretary bila kuwa balozi lazima apewe diplomatic passport.

..nadhani hata WABUNGE huwa wanapewa diplomatic passports. hata wake wa mabalozi wanapewa diplomatic passports.

..wengine watanirekebisha kama nimekosea.

cc MALCOM LUMUMBA, Richard
 
Bashiru ni moja ya wahaya wachache wasiojua kuvaa kabisa. Hii nafasi hatoiweza
 
Kwa hiyo anakuwa Katibu Mkuu wa Chama na Katibu Mkuu Kiongozi kwa wakati mmoja au anaacha kuwa katibu mkuu wa CCM?

Vipi kuhusu muongozo wa utumishi serikalini unaotenganisha mambo ya chama na utumishi wa umma serikalini?

Hata kama atajiuzulu Ukatibu Mkuu CCM, huu uteuzi unaonesha kwamba utumishi serikalini unaenda kupelekwa kichama chama zaidi.

Katibu mkuu wa chama( General Secretary) sio nafasi ya kisiasa, ni nafasi ya utendaji ndani ya chama husika

Kumbuka kabla ya kuteuliwa na NEC ya halmashauri kuu ya CCM taifa kuwa katibu mkuu wa CCM, Dr Bashiru Ally alikuwa ni mwalimu mwandamizi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam ( mtumishi wa umma)
 
Katibu mkuu kiongozi ndo sawa na White House Chief of Staff?

Kama ni sawa, tatizo liko wapi endapo Rais aliyepo madarakani atamteua mtu kutoka kwenye chama chake?
Hapana, sio sawa. Kulingana na website yake, Chief Secretary ni Kiongozi Mkuu wa Civil Service yote ( zamani ajira zote za watumishi wa umma wa kudumu zilikuwa chini yake) na anasimamia utendaji wa TISS na PCCB. Aidha, ni Katibu wa Baraza la Mawaziri, yeye ndie Mtendaji Mkuu wa Baraza la Mawaziri. Ni zaidi ya Chief of Staff wa White House. Kwetu sisi Chief of Staff ni kama Private Secretary to the President.

Amandla...
 
Kwani nimesema kuna mtu anayekubaliwa na wote?

Angemchagua El Chapo kuwa KATIBU mKUU Kiongozi, halafu watu wakalalamika, ungesema uteuzi wa El Chapo ni sahihi kwa sababu hakuna mtu ambaye atakubalika na wote?
El Chapo ni muuza madawa ya kulevya.

El Chapo si Mtanzania. Ni raia wa Mexico.

El Chapo yupo gerezani Marekani. Ni mfungwa.

El Chapo hana sifa za kuwa katibu mkuu kiongozi wa serikali iliyopo madarakani Tanzania.

Stick to the facts.
 
Hongera sana Dr. Bashiru hakika unastahili.
Sisi wananchi tunakuamini sana, naamini utakuwa msaada mkubwa kufanikisha azma na dhamira ya Mh. Rais.
Hongera na Mungu akulinde ktk majukumu yako mapya.
 
Hapana, sio sawa. Kulingana na website yake, Chief Secretary ni Kiongozi Mkuu wa Civil Service yote ( zamani ajira zote za watumishi wa umma wa kudumu zilikuwa chini yake) na anasimamia utendaji wa TISS na PCCB. Aidha, ni Katibu wa Baraza la Mawaziri, yeye ndie Mtendaji Mkuu wa Baraza la Mawaziri. Ni zaidi ya Chief of Staff wa White House. Kwetu sisi Chief of Staff ni kama Private Secretary to the President.

Amandla...
Hongera kwa Bashiru...

Kuna baadhi ya Teuzi zitaamua mparangano wa 2025.
 
Mpeni pole kwani huko anakokwenda atakayokutana nayo ni ya kuhuzunisha muda si mrefu!!!
Bashiru anajua figisu, anajua kubadilisha maneno halafu anajua kuusoma mchezo kwenda na bosi wake. Hivyo sitegemei apate shida sana.

Hususan kwa sababu kaamua kujitoa akili na kuweka usomi wake pembeni, kwenda ki Makaveli.
 
..hapo amemsokomeza Dr.Bashiru kuwa civil servant na foreign service office kwa wakati mmoja.

..Magufuli amekaa serikalini muda mrefu lakini inaelekea hajui jinsi civil service inavyoongozwa na miiko yake.

..Ndio maana tulikuwa tunashuhudia wanajeshi wanateuliwa makatibu wakuu wa wizara mbalimbali.
Hata mimi zamani nilifikiri hajui, si kwamba hajui, hajali na anapanga mkakati wake bila kufuata miongozo.

Alishasema atafanya teuzi kutegemea na atakavyoamka siku hiyo.

Si kwa kuangalia katiba, si kwa kuangalia ilani, si kwa kuangalia muongozo, si kwa maslahi ya umma.

Kwa kutegemea atakavyoamka siku hiyo.

Sasa huyo unaona ni mtu wa kujali utaratibu wowote uliowekwa?
 
Back
Top Bottom