IKULU: Utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Stiegler's Gorge

IKULU: Utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Stiegler's Gorge

Awamu ya 4 (kikwete) ilituaminisha kuwa umeme wa Gas ndio rahisi na utashusha bei ya umeme na bidhaa kwa ujumla! matokeo yake umekuwa na umeme uliotumia mabilioni ya shilingi na tulichoaminishwa hakuna.

Awamu hii ya 5 inatuaminisha kuwa umeme huu wa maji utakuwa ndio rahisi zaidi na utashusha bei ya bidhaa na tutatembea kifua mbele.

Awamu ya 6 huenda tukaja kuambiwa umeme wa majenereta ndio mzuri, wenye unafuu kuliko hiyo mingine!
Huo wa majenereta ndio unawaumiza nigeria mpaka sasa
 
Hydro ni cheap Sawa maana si unatumia maji kwenda kusukuma yale mamitambo mafuta hutumi kwa kiasi kikubwa sana mafuta inatumia ku lubricant mamashine...
Sema mradi utachukua miaka si chini ya 10 au zaidi kuisha....si umeona wa Ethiopia mpk leo wanajenga
Changamoto tu uaribu wa Mazingira,mambo ya global warming......
Ila waombee sana mvua zinyeshe mvua ikijanyesha syo kwa wingi italeta mushkeli

Hapo chacha....

Ova

Climate change is real and it is happening right now..!!
Ni mara ngapi tunaambiwa kuwa maji yamepungua kwenye mito na mabwawa yetu??
Anyway; hata wanaopotea njia wanakuwa na kiongozi wao!
 
1544687235591.png


Rais DKT Magufuli pamoja na waziri mkuu wa misri DKT Mostafa Madbouly washuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme megawadi 2100 katika mto Rufiji,Ikulu jijini Dar es salaa.
 
Mimi kinachonisumbu ni uwongo, hili bwawa ni kubwa kuliko lile la ethiopia, ambalo limeamza kujengwa 2014 na mpaka leo ni 60% done na litachukua miaka minane kulijaza, leo naambiwa bwawa kubwa zaidi litajengwa kwa miezi 36 na kujaa miezi sita huu uwongo utaisha lini?
Kinachosababisha ujenzi kuchelewa ni mambo mengi lakini vitu vikubwa ni accessibility ya eneo pamoja na fund. Shida ya Ethiopia hasa linakojegwa Bwawa la Grand Rennaissance ni milima mingi sana. Kama unaifahamu Wilaya ya Makete, mkoani Njombe basi hapo ni cha mtoto. Ethiopia ndiyo Nchi yenye milima mingi kuliko zote barani Afrika na ukiweka na umasikini wa miundombinu yake, imesababisha ujenzi nao kwenda kwa kusuasua.
Hata hivyo, chanzo kikuu cha kusimama ujenzi ni kuuawa kwa Meneja wa Mradi ambaye ndiye aliyekuwa mastermind wa Mradi. Kuna tuhuma kuwa, Misri ndiyo iliyomuua kutokana na kutotaka ujenzi wa Bwawa hilo kwa hofu kuwa litapunguza maji yanayoenda Mto wa Blue Nile ambao ndio unaochangia asilimia 60% ya maji ya Mto Nile.
Kwa kuwa, ujenzi unahusisha teknolojia, Wamisri walijua wakimuua huyo, itawachukua muda mrefu Waethiopia kuumaliza mradi huo na ndicho kilichotokea.

Hapa Tanzania, Bwawa liko katika ukanda wa Pwani na hata ujenzi wa miundombinu yote muhimu - umeme na barabara, vimekamilika mapema Kwa kuwa hakukuwepo changamoto kubwa. So, kikwazo kikubwa kwa Tanzania, kitakua ni fund basi. Fedha ikiwepo Bwawa litaisha mapema.
 
Ujiandae kukatwa kwenye luku hadi hiyo hela ya watu irudi.
Usiniulize kwa nini.
Naomba kuishia hapo.
Kulipia gharama za mradi unaoleta tija mimi sioni hasara.

Tatizo ni ile miradi ambayo imekaa kimaghumashi, sijui unaambiwa capacity charges, mara hela ni ya Habinder Singh na Rugmalira, alimradi tunaibiwa, ni mwiko kuwaibia waTanzania.
 
Kijana unajua maana ya stake?
Unajua vigezo vya kushinda zabuni?
Eti mradi umeuzwa, unatia huruma ujue!
Jaribu kuuliza maana ya stake ukishajua maana ya hilo neno utaelewa content nzima.
Mradi huu set up yake haipishani na dowans, symbion na wengine waliotupiga balaa, yaaani kwanza batuwezi jua unatugharimu kiasi gani, pili ule ujanja wa capacity charges ndiyo utawatajirisha watu hapa nchini , ndiyo maana nawaona wataalamu wa mambo haya rostam, na lowassa wamekuwa wapenzi wa muda huu, tumeliwa na sasa tunapigwa openly
 
Mradi wa umeme wa Stieglers Gorge utaipaisha Tanzania ya viwanda kwa kiwango ambacho si rahisi kuona hivi sasa.
Lakini ni kwa kiwango kikubwa.

Mradi ukikamilika Tanzaniabutakuwa imeongeza 2100MW katika gridi ya Taifa.
Hapa na mimi nitatembea kifua mbele, kama atuhimizavyo mh. Magufuli.

Sasa miradi kama ya kuchenjua madini itawezekana kutekelezwa nchini.

Mfano tu, Akosombo Dam huko Ghana ina installed capacity ya 1038MW(NUSU ya stiegler), lakini Ghana ilifanikiwa kuwa na moja ya smelter kubwa Afrika ya kuchenjua Aluminium.

Hapa nasema, Mh John Pombe Magufuli kalamba dume.
Kwenye umeme wa ''Gas'' Mikataba yake ni mibovu ''Maradhara ya mikataba ya siri'' Cost of electricity by source - Wikipedia
 
Ukitaka kupiga pesa ya serikali jihusishe na ujenzi tu. Miradi ndio pesa zipigwapo huko.
 
Mradi huu set up yake haipishani na dowans, symbion na wengine waliotupiga balaa, yaaani kwanza batuwezi jua unatugharimu kiasi gani, pili ule ujanja wa capacity charges ndiyo utawatajirisha watu hapa nchini , ndiyo maana nawaona wataalamu wa mambo haya rostam, na lowassa wamekuwa wapenzi wa muda huu, tumeliwa na sasa tunapigwa openly
haujajibu nimekuuliza unajua maana ya stake? kama hujui sema nikuelimishe maana naona umeanza kupotosha watu.
Kwa kukusaidia tu, unajua kwanini hadi leo kuna wakandarasi wanaidai serikali?
Unajua PSPF walistake kiasi gani kwenye ujenzi wa Nyerere bridge?
Je mmliki na mwendeshaji wa Nyerere bridge ni nani?
Haya maswali yatakusaidia kujua maana ya stake.
 
chadema itajifia taratibu sana tena kifo cha maumivu makali kama mgonjwa wa kansa. Magufuli oyee
 
haujajibu nimekuuliza unajua maana ya stake? kama hujui sema nikuelimishe maana naona umeanza kupotosha watu.
Kwa kukusaidia tu, unajua kwanini hadi leo kuna wakandarasi wanaidai serikali?
Unajua PSPF walistake kiasi gani kwenye ujenzi wa Nyerere bridge?
Je mmliki na mwendeshaji wa Nyerere bridge ni nani?
Haya maswali yatakusaidia kujua maana ya stake.
Niondolee upuuzi wako, you know nothing
 
Back
Top Bottom