Uchaguzi 2020 Ikungi: Magufuli amuahidi Lissu kazi, amuambia aachane na Urais ambao hatashinda

Uchaguzi 2020 Ikungi: Magufuli amuahidi Lissu kazi, amuambia aachane na Urais ambao hatashinda

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo Magufuli aliweka kituo kidogo Ikungi wakati anatoka Dodoma ambapo wananchi walisimama barabarani kumsubiri akiwa anaelekea kwenye mkutano wa kampeni Singida. Pamoja na ahadi nyingine pomoni, pia amemuahidi mgombea mwenzake anaetokea Singida nafasi ndogo ya kazi kwa madai kwamba hii anayopambania hatoiweza.

"Mmoja wa wagombea nafikiri anatoka hapa (Singida) nishaurieni tu kwamba mimi mnipe kura nyingi yeye nitamtafutia kikazi kidogo dogo huko serikalini. Ni mtoto wetu tunampenda, wala hatuna tatizo na mimi ndugu zangu sina tatizo na mtu yoyote, kwani kazi lazima uwe Rais. Muachie Rais Magufuli wewe tutakupa kikazi unachoweza kufanya (Ikungi oyee)

Kwa sababu sisi wote ni wamoja, akija mwambieni kwamba Magufuli amesema atakupa kazi, kwa nini unahangaikia hii kazi ambayo hutashinda." Mwisho wa kunukuu.
 
Kuliko udhalilishaji kwa umaskini na maisha yako bora unyanyaswe kwa mambo mengine, Mzee leo kawaambia Singida kuwa atawapa kazi ndogondogo maana hawana nguvu ya kuwa na mgombea wakuingia Ikulu.

Kwanini tumepaniki kiasi hiki? Hatukujipanga kufanya kampeni? Eleza sera zako acha wananchi wachague siyo ueleze Mambo binafsi.
 
Jamaa eti hizi ndio sera zake kwa Sasa duh...

IMG_20200901_125901.jpg
 
Leo Magufuli aliweka kituo kidogo Ikungi wakati anatoka Dodoma ambapo wananchi walisimama barabarani kumsubiri akiwa anaelekea kwenye mkutano wa kampeni Singida. Pamoja na ahadi nyingine pomoni, pia amemuahidi mgombea mwenzake anaetokea Singida nafasi ndogo ya kazi kwa madai kwamba hii anayopambania hatoiweza.
Ndio ukweli wenyewe
 
Kuliko udhalilishaji kwa umaskini na maisha yako bora unyanyaswe kwa mambo mengine, Mzee leo kawaambia Singida kuwa atawapa kazi ndogondogo maana hawana nguvu ya kuwa na mgombea wakuingia Ikulu.

Kwanini tumepaniki kiasi hiki? Hatukujipanga kufanya kampeni? Eleza sera zako acha wananchi wachague siyo ueleze Mambo binafsi.

Jiwe huwa anapanic ile mbaya, awape kazi wanaccm maana ndio huwa wanamtemekea. Na kina Mbatia, Lipumba ndio wenye shida na kazi za jiwe.
 
Back
Top Bottom