Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Wadau huu uzi comments zaidi ya 225 na una views 2000. Tumchangie mwenzetu hata buku buku tu.
 
Jaribu kufanya hivi inaweza kukusaidia kiasi chake.

Hapo ulipoibiwa ni Songea mjini, sasa hapo mbele ya hiyo bank ya Nmb kuna jengo la watawa wa mission ya Abasia Hanga monastery kabla hujafika mbele Nbc bank na jengo lao linatazamana na soko kuu, nafikiri wewe ndo umetapeliwa maeneo hayo. Kuna sister mmoja wa mission ya chipole ana sifa hizo za kitapeli alishawahi kumtapeli dogo mmoja wa Mpesa laki 4, issue nzima ilikuwa hivi:

Hawa watawa wana kawaida ya kutembeleana maana wapo wa mashirika mengi, mfano wa benedictine Ndanda wakawatembelea wachipole, wa peramiho wakaenda Bukoba... Kama hivyo.

Sasa huyo sister alitoka akaenda Hanga monastery, alivyofika akawa ana survey mitaa ya kijijini.... Akafika Mpesa flani kwa huyo dogo akamwambia amuwekee hela kwenye cm ndo hiyo 400k. Dogo kamaliza kuweka anamuomba hela....sister anajifanya kutafuta kwenye mkoba mara anamwambia nimesahau utawani ngoja nikachukue, sasa sijui mavazi yalimchanganya akamuamini ndo ikawa imeenda kihivyo. Dogo kwenda utawani anaambiwa mbona hapa wanakuja na kuondoka masister wengi! Huyo tutamjuaje? Basi ikabidi aondoke tu.

NIMETOA HIKO KISA ILI WATU WAJUE KUNA BAADHI YA WATUMISHI WA MUNGU SIO WA KWELI.


Nirudi sasa kumshauri mtoa mada, ila ikiwa bado hujasamehe laki 6 yako.

1. Ukiweza nenda kwenye hilo jengo la watawa ukifika ingia lile duka la vitabu halafu jitambulishe halafu useme hiyo siku ulipita ulikuwa unawahi bank ila kuna gari uliliona limepack hapo kulikuwa na Sr ndani yake limeandikwa sijui st Joseph nini vile... Sasa ulivyotoka bank hukulikuta, kwahiyo lengo la kuja hapo ni kuulizia pengine wanalijua labda la shule kati ya primary au secondary kwa sababu mpaka sasa bado unatafuta shule kwaajili ya kijana wako, hivyo ulivyoliona hilo gari (kama unakumbuka rangi na model yake litaje) ukahamasika kutaka kupata taarifa zake ni la shule gani.

Kama akikuuliza sasa imekuwaje umekuja kuulizia hapa? Simple mjibu nimekuja hapa sababu ni kwa wa mission halafu nilivyomuona yule sister nikajua haya mashirika huwa yanafahamiana kwahiyo naweza nikapata pa kuanzia ili nipate shule bora kwa kijana wangu. HEBU JARIBU HII UNAWEZA KUPATA PA KUANZIA KUMPATA MWIZI WAKO, (kibongo bongo jiwe 6 si mchezo!)



2. Nenda kwenye may bank yote na Mpesa hizi kubwa kubwa, wale huwa wanabandika sehemu maalumu majina ya shule nyingi tu na taasisi mbali mbali kama za dini kwaajili ya michango mbali mbali. Hapo we chukua majina ya st. Joseph yote! Yawe ya shule au taasisi then ingia Google ingia jina moja baada ya lingine, zaidi we deal na images tu... Huwezi jua pengine unaweza kuliona gari linalofanana na hao matapeli ukaenda sehemu hukika ukajikuta unakaribishwa na wezi wako 😂😁. (japo hii njia hai make sense kivile ila siku ukiyatimba! Kila njia utaona inafaa kujaribu).


Nb: hiyo hela ni nyingi jamani! Kwahiyo mpango mkakati ni muhimu. Ila kama mtoa mada umeamua kusamehe basi achana nazo, maana process zote hizo zina consume time!
Kusamehe hapo sio rahisi mkuu,.

Hiyo ya kwanza nadhani inaweza ikafanya kitu mana siko maeneo ya mbali sana,.
Hawawezi kunizingua nikiwa mwenyewe Au nitafute mtu mzima niende nae,.
 
Ni mtu ambaye tulikuwa tunafanya nae biashara afu tukawa na ukaribu hadi katika familia, polisi niliona nitapoteza muda na pesa.

Nilishauriwa nikamsuribishe kwa mtaalamu, na kwa hasira nilizokuwa nazo ilikuwa ni rahisi sana kwenda sema huwa siamini katika revenge, MUDA ni mwalimu kuliko yote aisee nilimuacha kama alivyo, nikajifunza kupitia upumbavu wangu maisha yakaendelea.
Una moyo wa ujasiri sana aisee,. Kuishi unamwangalia mwizi wako sio mchezo ujue
 
Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
Pole sana
 
Kusamehe hapo sio rahisi mkuu,.

Hiyo ya kwanza nadhani inaweza ikafanya kitu mana siko maeneo ya mbali sana,.
Hawawezi kunizingua nikiwa mwenyewe Au nitafute mtu mzima niende nae,.
Hapana hawawezi we kuwa comfortable tu ukifika, we unachofanya ni kuulizia kama watakuwa wanazifahamu shule hizo za st st watakwambia tu. Ila hata ukitaka kwenda na mtu mzima then yeye ndo akauliza kwa niaba yako pia imekaa njema
 
Daah kwakweli siwezi kujudge mpaka yanikute ila kwa kusimuliwa unaweza kuona simple sana. Mimi sijui ila ningetafuta namna nyingine niwafirimbe washenzi hawa.

We listen we don't judge. Pole sana ndugu
 
IMG-20250104-WA0028.jpg

Leejay49 done
 
Hapana hawawezi we kuwa comfortable tu ukifika, we unachofanya ni kuulizia kama watakuwa wanazifahamu shule hizo za st st watakwambia tu. Ila hata ukitaka kwenda na mtu mzima then yeye ndo akauliza kwa niaba yako pia imekaa njema
Yeah ngoja nijaribu huenda nitapata kitu,. Zilipo shule zao na kituo chao cha watoto wa mazingira magumu napafahamu, ila kwenda mwenyewe nisije kuharibu wacha niende na mtu mzima
 
Mmh!aisee pole sana
Mjinga kumpa pole haimsaidii! Iko hivi; mtu yeyote hata kama ni mzazi wako au mwanao; whoever no matter the relationship akianza kuomba, kutaka kujua, au hata kutajataja taarifa zako binafisi - jina, namba ya simu, unapoishi, etc etc etc as long as ni taarifa zako specific na huna business yoyote naye huyo huhitaji kuendelea na mazungumzo naye.

Just ignore him/her sembuse mtu umemkuta barabarani! Watu wengine sijui wana akili za aina gani.
 
Back
Top Bottom