Ilikuwaje mara ya kwanza ulipokutana na mtu mliyechati mtandaoni kwa nia ya kuwa wapenzi?

Ilikuwaje mara ya kwanza ulipokutana na mtu mliyechati mtandaoni kwa nia ya kuwa wapenzi?

Iliwahi kunitokea mimi pia. Zamani hizo hapahapa JF niliandika nataka mtoto wa kufanya nae mambo ya kikubwa tu. No serious relation.

Dada mmoja akanisakua kwenye mawasiliano niliyoweka. Tukabadilishana phone no. Tukaanza kuchati. Nilikuwa chuo kipindi hiko. Ikatokea nae kumbe alikuwa chuo cha kati mkoa uleule niliokuwa mimi.

Tulichati visiku kadhaa kwa mahaba yote. Hatimaye siku ya siku ikampendeza mola tukutane.

Nilipanda gari hadi kwenye chuo alichokuwa anasoma. Njiani tulivokuwa tunawasiliana alionekana yupo very exited kuniona, ila nilivofika duh!.

Sawa hakunichana, ila unaona tu kabisa mtu huyu kakutana na mtu ambaye hakumtarajia. Tulipiga story mbili tatu mi mwenyewe tu nikaona huu ugeni umeenda ndivyosivyo nikaaga nikaondoka.

iLa baadae usiku nilivojaribu ku initiate contact nae ndo akanichana sasa. Kwamba hakutarajia mtu kama mimi ndiye alikuwa anamngoja. So lets end it here na tufanye kama hamna kitu kimetokea.

Kutokana na haya ma sosho media, juzijuzi nimemfuma anatangaza biashara yake Facebook. Si unajua tena wadada siku hizi na tubiashara biashara. Kaweka na namba yake Tena yupo mkoa huu huu ninaoishi. Sijapata tu muda, ila i hope ntamtimbia siku moja japo tukapige tu story.
 
"Samahani sana ninavyokuona sio kama nilivyotegemea, HATUENDANI"... baada ya kusema hivyo jamaa aliyekuwa naye kwenye Toyota Hiace nyeupe akaniangalia na kutabasamu kisha akaondoa gari. Mimi nikaachwa nimesimama. Kubaya zaidi hata kwenye gari hakushuka. Sikuweza kujua yule kijana alikuwa nani yake hadi leo. Ilitokea Arusha maeneo ya Njiro nje tu ya Njiro Complex (Bugaluu).

Mwaka 2007 kupitia mtandao wa marafiki.com niliweza kupata mchuchu mwenye asili ya kiasia na kuanza kuchat naye. Chats zilikuwa nzuri sana za kuvutia utadhani tumejuana kitambo sana. Siku tunakutana kwa mara ya kwanza nje ya Njiro Complex ndo akakata tamaa na kunijibu kama nilivyoandika kwenye aya ya kwanza. Ilikuwa ni aibu kubwa sana kwenye haya maisha yangu. Bahati nzuri hakukuwa na mtu niliyeenda naye eneo la tukio kwahiyo aibu ilikuwa ni yangu binafsi.

Ila sikumchukia wala kumlaumu yule binti wa kishua kwa sababu kwa wakati ule kweli nilikuwa nimepigika haswa. Yaani nilikuwa mwembamba ila ule wembamba wa lishe duni. Kiufupi nilikuwa nimekonda. Kama unavyojua mtu mwenye njaa ndo mwenye sura mbaya kwahiyo hata mimi nilikuwa mtu mwenye sura mbaya sana kwa hisani ya NJAA. Zilikuwa nyakati ambazo kutembea kwa mguu kutoka Mianzini hadi Mbauda ni kitu cha kawaida sana. Au wakati mwingine Clock Tower - Njiro ilikuwa jambo dogo. Akitembea tajiri huwa ni matembezi ya hisani ila mimi sijui ilikuwa matembezi ya kuchochea umaskini?

Nakumbuka mwaka 2010 ndo nilipata matumaini makubwa sana baada ya manzi mmoja wa Chalinze kuniambia mimi ni handsome. Huyo manzi nilikutana naye nilipokuwa natoka Iringa kuchukua cheti cha form six.

Kimsingi baada ya tukio la 2007 nikaanza kuogopa sana kutongoza demu mtandaoni. Hadi leo nikiona manzi mtandaoni huwa hadi nifuatilie sana kumjua kiasi na sio kukurupuka.
Nina scenario 2 kama ifuatavyo,

Scenario 1
"Mhhh mbona katoto, ndo huyu kweli?" Alisema mwenzie aliyekuwa nae pembeni kwenye gari. Binafsi nilipoteza confidence na nikazuga tu kuwa nitawachek muda kidogo kuna assignment nafanya hiyo ni miaka fulani nikiwa napiga shule IFM, kwa kweli nilidharirika sana, uzuri tu ilikuwa usk hakuna aliyeshuhudia.

Scenario 2
Anapiga simu mdada mwenye sauti nyororo anajitambulisha kwa jina X, nampokea kwa bashasha ananiambia mm ni yule tunawasiliana sana kwenye messenger nadhani ni hotmail by then. Basi kidume bahati ilioje nikawa nipo kikazi Moro so nikamwambia namaliza session then napanda gar saa 8 kumfuata Dar, akaniambia poa tukakubaliana achukue lodge pale ubungo ili iwe rahisi mm asbh kudaka gar kurudi zangu Chugastan.

Nikaelekezwa lodge hadi room Number, chap nikafika nikagonga mlango mtu huyo...nikawa najaribu kumtazama aisee nikawa najarb kuinama nimuangalie vzr lkn kiukweli ni wale wadada wa mdomo wa sungura dah ilini-stress sana nishaingia ndani na natokaje sasa...anyway tuishie hapo.
 
Umenikumbusha nyimbo ya Rupert Holmes inaitwa Escape,(Pina Colada)

Rupert alikua kachoshwa na mke wake,akaamua atafute mwanamke MWINGINE amuoe,time hiyo hakukua na Simu Wala fb,so akanunua Gazeti kaficha utambulisho wake,akaweka tangazo kua anatafuta mwanamke,sifa asiwe smart sana awe na half brain,asiwe mlevi,hata kama anapenda yoga sio mbaya,Cha mwisho awe anapenda Pina colada (aina ya chakula)..

Akatokea mwanamke ambae ana sifa kama zile,nae kachoshwa na gume gume lake,wakapanga date kukutana,siku ya kukutana kaenda kukutana na mke wake.. wakachukuana wakarudi home..
 
demu anayekaa Masaki ni mrembo kulingana na nguo na vipodozi anavyotumia.

demu anayekaa Chalinze ndani ndani ni Mzuri wa asili.

kwani huyo demu anayekaa Masaki anazaliwa na Malaika au Eliens?
Ndugu Kitombise urembo huanza kwanza na lishe bora. Watoto wa Masaki na Oysterbay ni wazuri kuliko wa uswazi kwa sababu ya lishe. Virutubisho ni muhimu sana. Njaa ni kitu kibaya sana. Inaharibu hata sura za watu. Mtu mwenye njaa ana sura mbaya ambayo pia huchangia kuwa na roho mbaya.
 
Iliwahi kunitokea mimi pia. Zamani hizo hapahapa JF niliandika nataka mtoto wa kufanya nae mambo ya kikubwa tu. No serious relation.

Dada mmoja akanisakua kwenye mawasiliano niliyoweka. Tukabadilishana phone no. Tukaanza kuchati. Nilikuwa chuo kipindi hiko. Ikatokea nae kumbe alikuwa chuo cha kati mkoa uleule niliokuwa mimi.

Tulichati visiku kadhaa kwa mahaba yote. Hatimaye siku ya siku ikampendeza mola tukutane.

Nilipanda gari hadi kwenye chuo alichokuwa anasoma. Njiani tulivokuwa tunawasiliana alionekana yupo very exited kuniona, ila nilivofika duh!.

Sawa hakunichana, ila unaona tu kabisa mtu huyu kakutana na mtu ambaye hakumtarajia. Tulipiga story mbili tatu mi mwenyewe tu nikaona huu ugeni umeenda ndivyosivyo nikaaga nikaondoka.

iLa baadae usiku nilivojaribu ku initiate contact nae ndo akanichana sasa. Kwamba hakutarajia mtu kama mimi ndiye alikuwa anamngoja. So lets end it here na tufanye kama hamna kitu kimetokea.

Kutokana na haya ma sosho media, juzijuzi nimemfuma anatangaza biashara yake Facebook. Si unajua tena wadada siku hizi na tubiashara biashara. Kaweka na namba yake Tena yupo mkoa huu huu ninaoishi. Sijapata tu muda, ila i hope ntamtimbia siku moja japo tukapige tu story.
Ulikuwa una sura mbaya?
 
Ndugu Kitombise urembo huanza kwanza na lishe bora. Watoto wa Masaki na Oysterbay ni wazuri kuliko wa uswazi kwa sababu ya lishe. Virutubisho ni muhimu sana. Njaa ni kitu kibaya sana. Inaharibu hata sura za watu. Mtu mwenye njaa ana sura mbaya ambayo pia huchangia kuwa na roho mbaya.
sawa sawa
 
Mimi scenario yangu ilikuwa tofauti kidogo maana niliiba number ya demu Kwenye simu ya rafiki yangu mmoja.

Ipo hivi, siku Moja tulikuwa kijiweni tunacheza draft then rafiki yangu mmoja akanipa simu yake nimfanyie settings ilikuwa inamzingua.Simu yenyewe ilikuwa ya buttons ya Itel,Sasa baada ya kufanya settings chap nikakimbia Kwenye inbox ya jamaa nikaanza kusoma messages😂

Kwenye charts nikaona jina la mtoto mmoja anaitwa Sharon.
Nikaiba number yake nikaisave Kwenye simu yangu nikasema ngoja nimjaribu huyu.
Nilipofika nyumbani nikaa nyuma ya keyboards za simu yangu nikaanza kuchart na mtoto Sharon.
Nilitongoza mtoto akajaa mazima ikabaki ishu ya kukutana tu.Kumbe mtoto kwao na kwetu sio mbali kihivyo.

FAST FORWARDING: Mtoto alinipa location nikaenda nikakutana naye nikakuta Ni mtoto mzuri balaa.Sura nzuri na nyuma kajazia vizuri.

Picha linaisha nilikula Sana yule mtoto ila rafiki yangu hakuwahi kustukia mchezo wetu.
Tulidate almost for 1 year then tukaachana jumla kila mtu akashika njia yake😂

I hereby rest my case.
 
😅😅Nilikuwa nimechokachoka tu, hata dress code yangu mi mwenyewe ilinisaliti baada ya kukutana nae. Nilikuwa mwanafunzi obviously sikuwa na hela.
Kupigika kifedha = kuwa na sura mbaya. Demu akishaona umechoka anakuona kama sokwe mbele yake. Hata mimi siku nakutana na huyo manzi nilikuwa nimevaa suruali ya kitambaa na shati kama la mwanakwaya wa kijijini kwa kina Lucas Mwashambwa. Hata kukutania pale Njiro Complex ilikuwa ni kufosi mambo.
 
Moja ya vitu sipendi basi ni kukonda aisee.
Ukikonda kwa njaa unaonekana tu.

Nimeishi Mbeya, Iringa, Shinyanga, Tanga na Dsm. Kati ya mikoa yote hiyo Dsm ndo inaongoza kwa vijana kukonda kwa lishe duni.
Unamkuta mwanachuo kapendeza ila sura haina nuru, mwili umekongoroka mno, tumbo limeingia ndani mpaka imekua kama ana kibiyongo.

Mavazi ni muhimu ila wanachuo mzingatie chakula sio kuwaza mavazi tu.
 
Kupigika kifedha = kuwa na sura mbaya. Demu akishaona umechoka anakuona kama sokwe mbele yake. Hata mimi siku nakutana na huyo manzi nilikuwa nimevaa suruali ya kitambaa na shati kama la mwanakwaya wa kijijini kwa kina Lucas Mwashambwa. Hata kukutania pale Njiro Complex ilikuwa ni kufosi mambo.
Hebu tuache kidogo basi 😂😂😂😂
 
Na
Mimi nilipokutana nae kama aliniona wa kuja sijui, ila haku react alikuwa humble sana. Binfsi nilivyomdhania haikuwa hivyo.
Alkuwa mzuri na myenyekevu sana, naami hakuwa anaigiza ila ndio uhalisia wake, ilikuwa siku ya furaha kwangu kiasi sijaweza kuisahau.

Abarikiwe tu.
Na mkaachana?
 
Bwana bwana , huyu alieleta mambo ya kuedit mapicha na mafilter kwa ujumla hakuwa na nia njema kabisa.

Hizi tamaa acha tu, nishawai ingia dating site moja huko nikaiimbisha Manzi ikaja Wasap Inbox huko ikatuma mapicha weee, bwana wee nikajisemea mtoto si ndiyo huyuu sasa na kwa jinsi alivyo basi nitamtuliza na kumfanya bibie wangu permanent na nitaacha kupapalika na mamanzi wengine[emoji3].

Toto toto kweli, jiuso zurii, ilo lirangi sasa[emoji3], shape fulani hivi isiyoumiza macho wala kukera watizamaji, kiufupi Toto HD Utra.

Basi bwana, nikaliimbisha toto tukakubaliana kutoka date, siku ilipofika muhuni niliipania siku nzima maandalizi ya kutosha sana nikijua nakwenda kumpokea mwali wangu ambaye kila mwanaume fisi hiyo ni ndoto kuwa na mpenzi wa sifa hizo.

Niishie kwa kusikitika tu, niliyoyakuta si yale niliyoyatarajia wala niliyoyaona katika picha na video zake.

Kiufupi walikuwa watu wawili tofauti kabisa isingelikuwa ile tabia ya kuongea nae kwa Voice call basi ningehitimisha kuwa yule mrembo wangu si huyo kigagura niliyeonana nae[emoji3][emoji3].

Serikali ingilieni kati haya mambo wanaume tunadanganywa sana.
Hujakoma tu au bado unaendelea kukutana nao
 
Back
Top Bottom