Imetimia mwezi mmoja sasa tokea nimeanza kukaa na Mwanamke, natamani nimtimue

Asante sana, nimekuelewa kuwa na wanawake wa nje Sina kabisa maana hata simu yangu yupo huru kupokea,
 
Hayo ni mambo ya kawaida mkuu.

Binafsi ni mkimya mpaka nimzoee mtu sana so hiyo part ya kusocialize nimemuachia huyu mama hapa.

Kusocialize ni muhimu sana katika jamii hizi zetu za kiafrika else utakosana na hao wananchi bila sababu.

Hata kama hupendi kuwa na watu lazimisha tu kucheka nao na kupiga stori mbili tatu mradi ukae nao kwa amani.

Mimi Huwa kwenye sikukuu nachinja nagawa nyama kwa majirani we are in good terms.

Na huyu mama namuachia hicho kitengo cha kuwa karibu na jamii napiga mishe nyingine.
 
Huna adabu.
Eti ukinunua nyama, nyama kitu gani. Mpe mkeo hela ya mwezi mzima yeye ndio aamue mle nyama au tembele.
Acha uchoyo dogo. Wewe ndio mchoyo mpaka unaingilia Mambo ya jikoni.
Jikoni Ni sehemu ya kina mama kujidai. Usiingilie Mambo ya huko kabisa.
 
Hili ndilo jambo linalonisumbua kwa Sasa,nilipohamia mkoa huu kuanza kazi ndipo nilipokutana na huyu mwanamke.tulidumu ktk mahusiano kama mwaka na nusu Kila Mmoja akaanzisha maisha yake mengine. Baada ya mwaka Mmoja kupita akaanza kunitafuta kwenye simu mara kwa mara,aliomba tuktane Kuna jambo tuongee nikakubali....

Tulipokutana akaniambia kwa Sasa Hana kazi na Hana makazi hivyo anaomba hifadhi kwa muda wkt anajitafuta maana alipokua anaishi vtu vyake vimefungiwa kwa kutolipa Kodi kwa muda mrefu,kwakua nilipangisha nyumba nzima nikaona sio mbaya pia nitakua napata utelezi kwa karibu kuliko navyoenda kununua dada poa..(hapo ndipo nilipojiroga)

Nilimpa masharti yangu kuwa;

1.hapa mtaa ninapoishi hakuna anaejua nafanya kazi gani na wapi hivyo sitarajii ujio wako watu wakanifahamu.
2.sina mazoea na watu hapa mtaani kwahyo sitarajii kukuta mtu/majirani unapiga nao soga hapa kwangu.ila ukitaka kupiga stori nenda kwa mwanamke mwenzako ambaye mume wake Niko nae kazini.
3.salamu na mambo ya kijamii hapa mtaani nenda ila usijichanganye nao kupitiliza,shughuli ikiisha Rudi nyumbani.
Mambo yakaenda tofauti kbs yaani tyr ameshazoeana na watu kibao mtaani na ana marafiki kibao,kiufupi anapenda sifa+ kufahamika kimbembe Kuna siku nimerudi nimelewa akawa anaropoka kwa sauti ya juu nikampiga haswa,kumekucha kaenda kwa m/kiti kua nilitaka kumuua kwa kipigo na maneno kibao kua siogopi Cha mwenyekiti Wala nani maana hakuna wakunifanya lolote na uzushi mwingi tu.mwnykt akatupatanisha tukarudi home.
Nilipomtaka afungashe virago amegoma kabisa kua nimemtumia nilivyotaka Sasa namfukuza kwahyo haendi popote.
Hapa najipanga kumuachia Kila kitu nitafute mtaa mwingne niendeleee na maisha maana siwezi kuishi nae ni kiburi,hasikii maelekezo yangu , tukigombana kdg anaeleza majirani,ni mtu wa tamaa
 
Piga chini huyo zombie
 
Mkuu, miaka ya nyuma mzee mwenye nyumba alikuja kuangalia Mpira usiku saa 1:30 Mimi Nina Dstv yeye yuko na Azam kosa alilofanya alikuja na kijana mwingine wa mtaani Hapo (Mimi simjui) nikamtimua mzee nikamwambia usiku Huu nahitaji kupumzika alafu siwezi ruhusu wageni kwangu usiku nisiowajua, hakuamini ndivyo ilivyo maana hata muda wakiwa wananisema sipo, Sina namba ya mzee mwenye nyumba Wala mtu yoyote , mtu ndani ya Mwezi ana namba za Mama mwenye nyumba, watoto wake Majirani hapa nawaza sijui nifanyaje.
 
Shukrani mkuu nimekuelewa, Sema ninachokiona ni akili ya mwanamke Mwenyewe maana wengine wakianza mazoea saana ndio mwanzo wa kuangamia.
 
Jamaa ameshakula sasa amemkinai mapema hapa anatafuta tu sababu ya kuingia mitini.

Ila nawatahadharisha tu mtindo wa kuchezea mabinti za watu na kuwakimbia mkumbuke kuna kurogwa, ni vitu nimeshuhudia kwa macho yangu sikuhadithiwa.
Sanaa aisee hapo kwenye kurogwa dah Kuna jamaa alimpa mimba Binti alafu akaikataa jamaa kwao Tanga na Binti ni WA Tanga....alidisco engineering....ni smart kichwani ila majanga aliyonayo...analewa mpaka analala sokoni....wazazi WA yule Binti ni majirani wao kule Tanga...wanazungumza tu aje afate mwanae....lasivyo Bado sana hapo...
Kwa kifupi sio Kila mtu atachukulia poa habari za kuliwa na kuachwa..

Ila wengine fresh tu..
Sema jamaa kwenye stor yake hajakutana na mtu WA kuendana nae kwenye maisha....na mara nyingi unakutana na mtu yupo tofauuuti na wewe na yeye anaona sawa tu...Sasa pale ndo unaona akili inavurugika....
Kuna reality flani niliangalia jamaa katoka familia Bora kazoea yeye akitoka mihangaikoni Kuna wasichana WA kazi anavua nguo anaacha hovyo hivyo ...Sasa kaenda Kwa msichana wake kumtembelea akakaa siku kazaaa aiseeee....yule dada japo alikua ni single Maza ila alimshindwa jamaa jamaa ni anatupa tupa miboxer hivyo....
 
Nimesoma title tu nimecheka balaa
 
shukrani ilo ndio Huwa nalifanya, salary ikiingia namkatia kipande kikubwa na nilimwambia hata kama hesabu zikigoma asisite kuniambia.
 
Ni chance ndogo sana kukutana na mtuwenye ustaarabu na maisha unayoyapenda wewe mara nyingi unakutana na mtu ambae hamuendani....nafikiri Mungu ana balance tu equilibrium.
Japo Mimi nachoona ukimpenda mtu utamvumilia usipompenda hata AKIPUMUA utaona kero
 
Doctor hii itakuwa ni chai bila Shaka.

Ngoja nimwitempwa wako Aaliyyah aje aone hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…