Tetesi: Inadaiwa uchunguzi juu ya kupotea kwa Ben Saanane unaendelea

Tetesi: Inadaiwa uchunguzi juu ya kupotea kwa Ben Saanane unaendelea

Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo ambayo yalitokea enzi za utawala wa awamu ya tano na hakuna aliyethubutu kuanzisha uchunguzi juu ya hilo kutokana na maelekezo maalum.

Sasa nawataarifu kuwa uchunguzi juu ya kupotea kwa kijana huyo unaendelea na ni moja ya ajenda muhimu zilizojadiliwa hapo kabla. Hivi karibuni jambo hilo litawekwa wazi.

Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo yanayofanya viongozi wastaafu wa ngazi za juu kukwepa kabisa kuuzungumzia na kuujadili utawala wa hayati John Magufuli. Imefahamika kuwa yapo mambo kadhaa yasiyo ya utu yalifanyika huku yakiwa na baraka za hayati John Magufuli tena kwa maelekezo maalum.

Wekeni masikio wazi siku chache zijazo mtasikia la mgambo.
Kila nikitazama kipindi cha the last door cha kenya natamani na sisi kungekuwa na vipindi kama hivi.
Ila askari wa kenya ni mafia. Ile wiki walionyesha documentary ya kikosi maalum walivyokuwa wanaua watu wanachukua mili yao wanaimwagia acid na kuitupa mtoni ikiwa kwa magunia.
Jana wameonyesha documentary ya askari walivyomuua mtu anayewashitaki, ndugu yake na mwanasheria aliyekuwa ana simamia kesi yake kisha wakaitupa miili mtoni ikiwa kwenye magunia.
 
Watu hapa wanaropoka tu ... tujulisheni lile fufu la binadamu lililo patikana kwenye ofisi za chadema zilizo ungua lilikuwa la nani ? Acheni uhuni mbona mbowe asemagi chochote kuhusu fuvu la binadamu kwenye ofisi yao
 
Mbowe angehusika hata kama kwa size ya punje kama ya haladari basi kwa kipindi kile walivyokuwa wanamtafuta angekuwa ndani kwa kesi ya mauaji ,kwakuwa mnajua ninyi ndiyo mlikatisha miasha ya Ben ndiyo maana mnaleta utani utani.

Yakitokea mauaji yeyote kama serikali haihusiki basi ndani ya week tu wanakuwa washampata muuaji ila ukiona kimya basi ujue "kazi yao hiyo" ,Milembe na Dr wa Tarime wameuawa usiku wa maanani ,hakukuwa na mtu mwingine zaidi ya wauaji lakini serikali ishawapata waliotekeleza mauaji ila kwa Lissu ambaye alipigwa risasi ndani ya compound yenye ulinzi wa hatari mchana kweupe lakin hakuna aliyekamatwa....Yaani hapo jeshi limejipaka matope kwa udhaifu ili wawalinde kina BASHITE na MAKENZI.
Logic ni nyepesi tu mbona mbowe siku hizi kamyamaza kabisa hataki hata kusikia habari ya ben saa8 ...tena ukimtajia tu ilo jina anaweza kukupasua na chupa ya konyagi
 
Yaani katika mambo ambayo BASHITE na MAKENZI waliyofanya moja wapo baya ni hili la KUMPOTEZA Ben saanane na la pili la Kumchapa Lissu risasi hadharani mchana kweupe....Wameacha Traces waziwazi ambayo ni MBAYA sana.
Kama wameacha traces kweli basi tuwaone wakishughulikiwa Otherwise ni porojo tu kama porojo za pesa za China 🇨🇳 😅🙏
 
Waliotumwa kwa Lema walikuwa na hofu ya Mungu
 
Jambo lolote ukilifanya mbele ya macho ya watu wengine haliwezi kuwa siri tena.
Magufuli kama alitenda hayo basi yatajulikana wazi tuu.
Ninachoumia ni kuwa kama alifanya mambo mabaya kwa maisha ya mtu/watu halafu mpaka leo familia inakula pension ya kodi zetu sio sawa kabisa. Ilipaswa hata familia yake ijute kwa kuwa na baba asiye na utu pamoja na kupewa heshima kubwa na wananchi
Katika kila Tawala zilizopita yapo mabaya na mazuri yaliyotokea kwa watu !!
 
Katika kila Tawala zilizopita yapo mabaya na mazuri yaliyotokea kwa watu !!
Mabaya yametendwa mengi sana, lakini hili la mwenye dhamana mwenyewe, anayeheshimika kama kiongozi wa watu na mlinzi wa wote kutoa machine na kummwagia njugu raia wake? Hili ni zaidi ya wote.
Sidhani kama tokea Julius hadi Jakaya kama tulifikia huko
 
UONGO
Mshauri mkuu wa rais ni makamu wake. Hata leo Mpango hawezi kukwepa anayoyafanya Samia kwa kuteua watu wa dinni moja. Rejea mawaziri watano toka mkoa mmoja wa Tanga huku mawaziri wawili toka mikoa ya Mwanza Mara Simiyu Shinyanga na Kagera.

Vivyo hivyo aliyekuwa makamu kipindi cha JPM ashughulikiwe.

Sijui alikuwa nani na ni nani sasa hivi
 
Sisi jpm tulimpa go ya hata kuua kwa sababu alikuwa mzalendo na mzalendo ana ua wahuni tu wa taifa ...sasa mtu kama msoga angeuliwa wote tunge furahi sana ....siyo kila mtu ana stailik kuishi.
Na kwa vile hakuwa na AKILI basi akawa anaua watu hovyo. Sishangai kwa nini naye leo hayupo hai. Magufuli alikuwa ni shetani mwenye jicho moja na pembe kichwani
 
Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo ambayo yalitokea enzi za utawala wa awamu ya tano na hakuna aliyethubutu kuanzisha uchunguzi juu ya hilo kutokana na maelekezo maalum.

Sasa nawataarifu kuwa uchunguzi juu ya kupotea kwa kijana huyo unaendelea na ni moja ya ajenda muhimu zilizojadiliwa hapo kabla. Hivi karibuni jambo hilo litawekwa wazi.

Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo yanayofanya viongozi wastaafu wa ngazi za juu kukwepa kabisa kuuzungumzia na kuujadili utawala wa hayati John Magufuli. Imefahamika kuwa yapo mambo kadhaa yasiyo ya utu yalifanyika huku yakiwa na baraka za hayati John Magufuli tena kwa maelekezo maalum.

Wekeni masikio wazi siku chache zijazo mtasikia la mgambo.
Sasa kama mwenyewe unasema ben saanane alipotea kwa baraka za jpm unataka uchunguzi wa nini?
Binafsi nasema ben saanane lolote lililomtokea alijitakia mwenyewe.
Kwanza alijipa kazi au kupewa kazi cdm ya kumtukana magufuli, kumchafua kwa kutumia maneno yasiyofaa. Awamu ya 5 wangetaka kumshitaki wangeweza maana alikua anavunja sheria kumkejeji na kumdhalilisha rais wa jamhuri. Alijikita kueleza kadamnasi kwamba jpm aligushi cheti chake cha Phd huku bila kuonyesha ushahidi wowote. Licha ya kuonywa kuhusu uongo wake dhidi ya binafsi ya rais alikaza shingo kujitia ushujaa.
Huenda dola wanajua nani kampoteza ben ila wananyamaza kumlinda mtu huko upinzani maana akitajwa nyie mnaotaka uchunguzi hamtoamini.
 
Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo ambayo yalitokea enzi za utawala wa awamu ya tano na hakuna aliyethubutu kuanzisha uchunguzi juu ya hilo kutokana na maelekezo maalum.

Sasa nawataarifu kuwa uchunguzi juu ya kupotea kwa kijana huyo unaendelea na ni moja ya ajenda muhimu zilizojadiliwa hapo kabla. Hivi karibuni jambo hilo litawekwa wazi.

Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo yanayofanya viongozi wastaafu wa ngazi za juu kukwepa kabisa kuuzungumzia na kuujadili utawala wa hayati John Magufuli. Imefahamika kuwa yapo mambo kadhaa yasiyo ya utu yalifanyika huku yakiwa na baraka za hayati John Magufuli tena kwa maelekezo maalum.

Wekeni masikio wazi siku chache zijazo mtasikia la mgambo.
Marehemu naye alikuwa na ujasiri,wewe unamuona kabisa huyu mtawala siyo wa mchezomchezo unaenda kumpekua,sasa alitarajia kinachofuata ni nini?

Hakuna serikali isiyo ua Duniani,ukipambana na serikali ni mawili aidha uwe kilema au ufe,simple.

Ata Asange alivyoleta uhuni wake kwa serikali ya Marekani,kilichofuata wote tunajua!

"Democracy is written on papers but not in actions"
 
Kuna kipindi Mwigulu alikua waziri wa Mambo ya ndani. Ikapatikana miili ya watu mto Ruvu maeneo ya bagamoyo. Waziri yule bila uchunguzi Wala nini alituambia miili Ile Ni wahamiaji haramu. Labda Kuna kitu anakijua kuhusu miili iliyokua inaokotwa in those dark days.
Hapa kwa Mwigulu Naungana Na Wewe.
Baba Ana Roho Mbaya Sana Yule.
 
Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo ambayo yalitokea enzi za utawala wa awamu ya tano na hakuna aliyethubutu kuanzisha uchunguzi juu ya hilo kutokana na maelekezo maalum.

Sasa nawataarifu kuwa uchunguzi juu ya kupotea kwa kijana huyo unaendelea na ni moja ya ajenda muhimu zilizojadiliwa hapo kabla. Hivi karibuni jambo hilo litawekwa wazi.

Kupotea kwa Ben Saanane ni moja ya mambo yanayofanya viongozi wastaafu wa ngazi za juu kukwepa kabisa kuuzungumzia na kuujadili utawala wa hayati John Magufuli. Imefahamika kuwa yapo mambo kadhaa yasiyo ya utu yalifanyika huku yakiwa na baraka za hayati John Magufuli tena kwa maelekezo maalum.

Wekeni masikio wazi siku chache zijazo mtasikia la mgambo.
Itakuwa ni jambo la kheri,huenda hata chuki,visa,na visasi na tofauti za kiitikadi,kikanda na kikabila vikaisha kabisa kama sio kupungua mambo,🤔
 
Back
Top Bottom